Umefaidika nini na JF tangu ulipojiunga?

Mimi niliipata jamiiforum kupitia kugoogle huko, sehemu ya kwanza kabisa kuingia ilikuwa ni jukwaa la Jamii Photos, hapo ndo ikawa mwanzo!
 
Kama wanavyosema kuishi Dar es salaam tu ni elimu ya form six. Kwangu JF is another degree. Kama unataka kujua what is happening in Tz just google Jamii Forums and you will get everything on your finger tips.
 
JF imenielimisha mambo mengi sana lakini ambacho kiko kichwani mwangu kwa sasa ni kuhusu hiki chama Cha Majambazi na Magamba - CCM.Na kuwa ni chama kibaya sana kwa karne hii,nitaeleza.

1.Vijana tunakosa ajira za kutosha kwa sababu CCM wamefilisi viwanda vyetu.

2.Miaka 50 ya uhuru bado tu wajinga kwa sababu CCM wamefanikisha majengo mabovu kujengwa kukiwa hakuna walimu,vitabu wala maabara wao wakiziita shule.

3.Tunaendelea kufa kwa sababu hakuna hospitali wala zahanati za kutosha na hata hizo zilizopo hazina dawa,lakini wao kila siku wanapanga foleni kwa safari za nje kuangalia afya zao.

4.Rasiliamali zetu zinawaneemesha wao,tukilalamika wanasema tumevamia migodi,wanatuua kwa kutumia bunduki tulizowapa ili watulinde.

5.Wameanza kueneza udini na chokochoko ili wananchi tusambaratike kwa sababu wameshaona muda wao wa kukaa madarakani umekwisha.

Through JF nimejifunza mambo mengi sanaaaana....yaani sana tu!
 
Acheni utani, JF imekuwa ya msaada sana kwangu.
Nakumbuka zilikuwa zimebaki siku chache sana nifunge ndoa. Bestman wangu akawa haeleweki. Nikiwasiliana naye kuhusu mipango ya kwenda kufanya manunuzi (tena kwa ghalama zangu) ananikwepa. Nilipomkumbusha siku ya kwenda rehearsal na kubaini hatuko ukurasa mmoja nikachanganyikiwa. Haraka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyewahi kuniomba mchango wa harusi kwa PM hapa JF. Huyu mtu japo nilimchangia, hatukuwa tumewahi kukutana na wala hatukuwa tunajuana. Roho ikanituma kuwasiliana naye. Jibu lilikuwa, USIPATE SHIDA. Hivyo ndivyo ilivyokuwa JF ikawa imenipa Bestman and Best-friend. Asante sana JF, Udumu Milele


Kumbe inawezekana...
 
Ninapoteza muda kujadiliana na ghost names hapa! Sijawahi onana na MjF hata mmoja...ngoja nisepe
 
kikubwa nilichojifunza ni whats going in our country (tz) na technology ndo makubwa niliyojifunza zaidi tokea nimejiregister...
 
Mimi naona jf imenizidishia hasira zangu kwa lichama la magamba,
nape anavyojibu, wanaccm hawako sirius ni wachache wenye hekima,
actually nimeinjoy kisiasa zaidi sababu napenda siasa.
 
ukitaka kushiriki na kuchangia ndani ya JF hususan kwenye majukwaa ya siasa nk, lazima uitume akil yako kufikiri na kutafakari suala lililo mjadalani. hiyo ni sifa ya ziada ya JF. sio wengi wetu walipata fursa ya kufundishwa namna ya kutafakari na kuingia kwenye hoja. asante JF kwa taarifa na changamoto nyingi uzitoazo. zote zinaboresha akili na taaluma za Watz na hicho ni kitu bora zaidi kuliko hata kuwajaza mapesa mifukoni!
 
Jamani nisipo fungua jf kwa siku sijui kama siku itaenda nimekuwa addicted na jf. Kikubwa nimejua mbivu na mbichi kwenye nchi yangu nafurahi any time nikitaka kupitia jf. Nimepata kuchat na watu wakubwa nchini kama Dr wa ukweli Slaa Regia Mtema na wanasiasa kibao. Kiukweli jf idumu milele. Hii web ndio nafungua muda mwengi kuliko zote dunia sitaicha.
 
Back
Top Bottom