Umasikini Magonjwa na Vita

Sura-ya-Kwanza

JF-Expert Member
Nov 17, 2007
566
10
Je Umoja wa Nchi za Afrika lazima?

Bara letu hili la Afrika ambalo linajulikana Ulimwenguni kama jeusi, limejaa UMASIKINI MAGONJWA na VITA na wakati huhuo ni bara ambalo limejaa Rasilimali- mapori,wanyama,utamaduni,madini na kadha wa kadha...na bado tuna hayo yote.
Walakini?

Tanzania ina bahati ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko nchi nyingi barani humu lakini bado ni MASIKINI ina MAGONJWA na imeshapigana VITA...
1. Je Kujiunga na Umoja wa Kiafrika utamkomboa Mtanzania kujikinga na hayo hapo juu?

Au itachangia hayo hapo juu?

2. Ni lipi katika haya (UMASIKINI MAGONJWA na VITA)litatufanya tusiungane na Umoja huo

Kwa mtazamo wangu hii ni lazima...tujadiliane
 
Nchi za Africa sio masikini ila viongozi wa ulimwengu ndo wanasababisha hizi nchi ziwe masikini, mataifa ya magharibi kwa kushirikiana na viongozi wetu na ukoloni mpya unaoitwa utandawazi ndo unatumika kuamisha rasirimali za Africa na kuzipeleka nchi za nje, mkoa wa shinyanga una reserve kubwa sana ya dhahabu lakini una km 12 tu za rami ukiondoa main road ya mwanza nzega, rasirimali haziwasaidii wananchi wake bali zinanufaisha viongozi walioko madarakani na mabwana zao wa magharibi.
mkapa ana lundo la mali, Chenge ana $1000000 ofshore account lakini tuna shule za msingi ambazo hawana hata darasa moja la kudumu isipokuwa full suit (juu majani chini majani).
hipo siku watu waregret kuzaliwa Africa unless the state should be changed
 
Bado haya yanajadiliwa hapa Tanzania...hii nimetoa kwenye article moja ippmedia.com. I quote,
"Wanavijiji bado hawajaweza kutambua, kutumia fursa zilizopo kiuchumi" na Lusekelo Philemon

"...Umaskini ni gonjwa ndugu ambalo linaendelea kuwatafuna Watanzania siku hadi siku..."

"Matatizo mengi ya kijamii hapa nchini yanatokana na umaskini uliokithiri ukasababishwa na Ukimwi na magonjwa mengine yanayofanana na hayo..."


Sasa huu umaskini ni wa kujiletea au ndio tunakubali kuwa sie masikini?:confused:
 
Nimeona Thread moja Is Tanzania Rich or Poor?

Sikuwa nataka kuingiliana nayo ila kutaka kuchambua Umasikini Magonjwa na hata Vita kwa Afrika kwa Ujumla na siyo tanzania peke yake naona mengi niliyo quote yapo kwenye thread hiyo hapo juu... I shall edit
 
Back
Top Bottom