MSEZA MKULU
JF-Expert Member
- Jul 22, 2011
- 3,752
- 5,497
Habarini za jioni wanaintellijensia na watu wa kufikiri katika nyuzi 360 kwa kila jambo.
Kama kuna kosa kubwa tunafanya ni kushika imani bila kujua japo historia kiduchu ya tulikotoka.
Dunia ya Imani imegawanyika katika makundi mawili makubwa yasiyoingiliana yaani Waislamu na Wakristo.
Paul (SAUL wa Tarso):
Historia inaonyesha Komandoo wa imani ya kikristo na mpambanaji aliyepitia kila aina ya changamoto ni PAULO aliyeitwa Sauli. Hakuna kuanzia matendo ya Mitume hadi Ufunuo hadi kesho aliyeonyesha viwango vya Paul.
Muda mwingi utamkuta kwenye boti akisafiri huku na kule, asia,ulaya,afrika kaskazini, mashariki ya kati kueneza injiri kwa ushawishi mkubwa usio na mfano.
Hakuna kama paul katika Ukristo.
Alikuwa msomi aliyetukuka linapokuja suala la elimu dunia, Hakuwa mtu wa majivuno.
Huyu kwa kazi aliyoifanya, na maandiko aliyoandika sio tu wapinzani wa ukristo yamewachanganya bali hadi wakristo wenyewe wakijikuta ktka makundi makundi kiasi cha mtu aliyekuwa mwanafunzi wa yesu PETRO kuwataadhalisha wasomaji wa maandiko yake kuwa kuna watu wasio na uelewa huyachanganya na kujichanyanya.
Mwisho wa paul, Baada ya kazi kubwa ya kusambaza Ukristo maeneo yote yenye ushawishi enzi hizo. Anakamatwa na kukatwa kichwa kama ng'ombe machinjioni. Tofauti na Ng'ombe,Mbuzi,Kitimoto au tunaowaona wakichinjwa na ISIS kwenye habari alionekana mtu mwenye furaha, kama vile Bwanaharusi anakwenda kumpokea bibi harusi.
Kifo kwake hakikuwa Tishio tena bali ni zawadi kwa kazi kubwa aliyoifanya mpiganaji huyu tayari kwa Kusubiri Taji na Medali siku ile ya Hukumu.
Haya ndio maneno yake ya Mwisho mwisho akimuandikia barua kijana shupavu Timotheo katika Usiku ule ambao wanahistoria wanasema asubuhi yake alipokea zawadi ya Kifo kwa kukatwa kichwa na shoka...
2timotheo 4:5-7
Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
UMAR Ibn Al-Khattab mtume alimuita Farouq(Distinguisher of truth and Falsehood )
Baada ya kifo cha Mtume Momammed SAW, Hakuna mtume mwingine aliyetakiwa kuwepo isipokuwa ukawepo mpango mkubwa wa muda mrefu wa kuwa na kingozi wa kidini atakayesimamia mambo ya imani na kuwa kiongozi wa dola la kiislam maarufu kama Islamic Calphate. Kiongozi wa Dora hii alijulikana kama Caliph. Katika historia Kumewahi kuwepo macaliph wanne tu tangu mtume kufariki na baada ya hapo imani iliendelea kuwepo bila ya umoja wa enzi hizo.
1:Abu Bakr.
2:Umar ibn al-Khattab.
3:Uthman ibn Affan.
4:Ali ibn Abi Talib.
Hapa tunamzungumzia Caliph wa pili kuwahi kuwepo duniani maarufu kwa jina la Umar. ZTV na nadhan Azam media wanavipidi wanaonyesha juu ya jemedali huyu na kiongozi shupavu ambae wanazuoni wanafananyisha kazi aliyoifanya katika uislam inaweza kufananishwa na PAULO kwa kazi aliyoifanya kwenye Ukristo miaka zaidi ta 500 kabla yake. Alipokea Uislam mwaka 616ACE kama SAUL Umar alikuwa katika harakati ya Kutafuta kumuua Mohammad kabla ya kukutana na watu wake wa karibu ambao tayari walikuwa wameshakuwa waislam. alishawishiwa na maneno ya quran na akajikuta nia yake ovu akiijutia na Kusilimu...
-Alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa katika mazungumzo (Public speaking), alikuwa na uwezo mkubwa sana wa ushawishi na usuluhishi,Wanahistoria wanamtaja kama mtu wa 52 kwa umaarufu duniani tangu mwanzo wa history...
Alikuwa mtu hodari kwa kusambaza Uslam. Ukiona leo waislam wamesambaa karibu dunia nzima huwezi kuwatenga na kazi ya huyu jamaa aliyejiita commander of the faithful” (amīr al-muʾminīn). Ndiye aliyebadili taswira ya Uislam kutoka kwa waarabu tu na kusambaa dunia nzima.Leo kuna waislam wachina,wahindi,wazungu,weusi n.k
Anaheshimika duniani kote kwa kutawala kwa kufuata haki. Alianzisha mifumo thabiti ya kidini na kiutawala.
Tofauti na wengi wanavyodhani, Siku walipoiteka Jerusalem, kulikuwemo na wayahudi na wakristo. Umar aliingia jijini hapo siku kadhaa baadae kwa staili ya aina yake ya kujinyenyekeza. Yaani aliingia akiwa amembeba mfayakazi wake kwenye punda huku yeye akivuta kamba ya punda yule. Kwa kiongozi kama yule watu hawakutegemea. Alipofika alitoa fundisho ambalo kwangu ni naliona kama ni la muhimu sana. Aliwaagiza waislamu wote wasimlazimishe mtu yoyote kuwa muislamu kwa lazima. bali waishi maisha mema ya mfano ili wakristo na mayahudi wawe waislamu kwa mvuto wa maisha ya waislamu wanaozunguka. aliagiza kuwe na haki sawa kwenye ardhi kwa watu wote. Aliwatoza kodi ya chini wakazi wa Jerusalem kuliko hata wakoloni waliokuwepo hapo.
Hiztoria za kuyahudi zinasema Umar japo yerusalem yote ilikuwa chini yake lakini aliwaruhusu wayahudi na wakristo kuendelea na ibada zao.
HIVI NI BAADHI YA VITU ALIVYOFANYA VYA KUKUMBUKWA
1: Historia zinasema ndiye aliyetoa wazo(kuna wananzuoni wengine wanasema yeye aliweka sheria tu lakini utaratibu ulikuwepo) la kutenganisha kwa wanawake na wanaume katika ibada ili kusiwe na matamanio na watu wajielekeze kwenye ibada tu.
2: Ni Umar aliyeifuta kabisa kazi nzuri aliyoifanya Paul middle east na maeneo ya karibu kwa kusambaza uislam kote huko.
3:wanahistoria wanasema wakati wa mwanzo waislamu walikuwa wanaabudu kwa siri, Umar ndiye aliyetoa wazo wafanye mambo yao wazi, na kuwatishia wote ambao wangewaingilia katika kusali kitu kilichosababisha mtume kuuita "AL-Farouq".
4:Umar ndie aliyeanzisha Kalenda ya Kiislam mwaka 639AD inayotumika hadi leo,
5:Kipindi cha njaa kubwa kuwa ubunifu mkubwa na akili nyingi akiwa kiongozi wa dola la kiislam aliokoa maisha ya mamillioni na watu.
6:Alikataa kuwakata mikono wezi, kwa sababu aliamini mtu aliiba kutokana na yeye kushindwa kutoa ajira kwa jamii.Kwenye utawala wake alikuwa na maono katika dola yake mtu asilale usiku akiwa hajashiba...
KIFO
kama inavyotokea mara nyingi Mashujaa wengi hufa vifo vya kawaida. Siku moja akiwa anasoma sala ya asubuhi alivamiwa na mtumwa wa kiajemi na kumchoma kisu/Jambia mara sita tumboni (vyanzo vingine vinasema mgongoni) na kumuacha damu zikibubujika ardhini na hapo ndio ukawa mwisho wa shujaa huyu katikati ya utawala. Umar sio mtu wa kawaida kwa maana ya uongozi
kuna mengi alifanya hapa wataalam zaidi wanaweza kuchambua.
karibuni,
mashehe,wachungaji, wananzuoni na maulamaa tujadili watu mashuhuri hawa katika imani hizi kinzani bila jazba, ugomvi,fitna na maneno ya kejeli.
naweza kuwa sijaweka mzigo wote ila yaliyobaki yanabaki kama changamoto na mianya kwa wachangiaji.
Kama kuna kosa kubwa tunafanya ni kushika imani bila kujua japo historia kiduchu ya tulikotoka.
Dunia ya Imani imegawanyika katika makundi mawili makubwa yasiyoingiliana yaani Waislamu na Wakristo.
Paul (SAUL wa Tarso):
Historia inaonyesha Komandoo wa imani ya kikristo na mpambanaji aliyepitia kila aina ya changamoto ni PAULO aliyeitwa Sauli. Hakuna kuanzia matendo ya Mitume hadi Ufunuo hadi kesho aliyeonyesha viwango vya Paul.
Muda mwingi utamkuta kwenye boti akisafiri huku na kule, asia,ulaya,afrika kaskazini, mashariki ya kati kueneza injiri kwa ushawishi mkubwa usio na mfano.
Hakuna kama paul katika Ukristo.
Alikuwa msomi aliyetukuka linapokuja suala la elimu dunia, Hakuwa mtu wa majivuno.
Huyu kwa kazi aliyoifanya, na maandiko aliyoandika sio tu wapinzani wa ukristo yamewachanganya bali hadi wakristo wenyewe wakijikuta ktka makundi makundi kiasi cha mtu aliyekuwa mwanafunzi wa yesu PETRO kuwataadhalisha wasomaji wa maandiko yake kuwa kuna watu wasio na uelewa huyachanganya na kujichanyanya.
Mwisho wa paul, Baada ya kazi kubwa ya kusambaza Ukristo maeneo yote yenye ushawishi enzi hizo. Anakamatwa na kukatwa kichwa kama ng'ombe machinjioni. Tofauti na Ng'ombe,Mbuzi,Kitimoto au tunaowaona wakichinjwa na ISIS kwenye habari alionekana mtu mwenye furaha, kama vile Bwanaharusi anakwenda kumpokea bibi harusi.
Kifo kwake hakikuwa Tishio tena bali ni zawadi kwa kazi kubwa aliyoifanya mpiganaji huyu tayari kwa Kusubiri Taji na Medali siku ile ya Hukumu.
Haya ndio maneno yake ya Mwisho mwisho akimuandikia barua kijana shupavu Timotheo katika Usiku ule ambao wanahistoria wanasema asubuhi yake alipokea zawadi ya Kifo kwa kukatwa kichwa na shoka...
2timotheo 4:5-7
Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
UMAR Ibn Al-Khattab mtume alimuita Farouq(Distinguisher of truth and Falsehood )
Baada ya kifo cha Mtume Momammed SAW, Hakuna mtume mwingine aliyetakiwa kuwepo isipokuwa ukawepo mpango mkubwa wa muda mrefu wa kuwa na kingozi wa kidini atakayesimamia mambo ya imani na kuwa kiongozi wa dola la kiislam maarufu kama Islamic Calphate. Kiongozi wa Dora hii alijulikana kama Caliph. Katika historia Kumewahi kuwepo macaliph wanne tu tangu mtume kufariki na baada ya hapo imani iliendelea kuwepo bila ya umoja wa enzi hizo.
1:Abu Bakr.
2:Umar ibn al-Khattab.
3:Uthman ibn Affan.
4:Ali ibn Abi Talib.
Hapa tunamzungumzia Caliph wa pili kuwahi kuwepo duniani maarufu kwa jina la Umar. ZTV na nadhan Azam media wanavipidi wanaonyesha juu ya jemedali huyu na kiongozi shupavu ambae wanazuoni wanafananyisha kazi aliyoifanya katika uislam inaweza kufananishwa na PAULO kwa kazi aliyoifanya kwenye Ukristo miaka zaidi ta 500 kabla yake. Alipokea Uislam mwaka 616ACE kama SAUL Umar alikuwa katika harakati ya Kutafuta kumuua Mohammad kabla ya kukutana na watu wake wa karibu ambao tayari walikuwa wameshakuwa waislam. alishawishiwa na maneno ya quran na akajikuta nia yake ovu akiijutia na Kusilimu...
-Alikuwa ni mtu mwenye uwezo mkubwa katika mazungumzo (Public speaking), alikuwa na uwezo mkubwa sana wa ushawishi na usuluhishi,Wanahistoria wanamtaja kama mtu wa 52 kwa umaarufu duniani tangu mwanzo wa history...
Alikuwa mtu hodari kwa kusambaza Uslam. Ukiona leo waislam wamesambaa karibu dunia nzima huwezi kuwatenga na kazi ya huyu jamaa aliyejiita commander of the faithful” (amīr al-muʾminīn). Ndiye aliyebadili taswira ya Uislam kutoka kwa waarabu tu na kusambaa dunia nzima.Leo kuna waislam wachina,wahindi,wazungu,weusi n.k
Anaheshimika duniani kote kwa kutawala kwa kufuata haki. Alianzisha mifumo thabiti ya kidini na kiutawala.
Tofauti na wengi wanavyodhani, Siku walipoiteka Jerusalem, kulikuwemo na wayahudi na wakristo. Umar aliingia jijini hapo siku kadhaa baadae kwa staili ya aina yake ya kujinyenyekeza. Yaani aliingia akiwa amembeba mfayakazi wake kwenye punda huku yeye akivuta kamba ya punda yule. Kwa kiongozi kama yule watu hawakutegemea. Alipofika alitoa fundisho ambalo kwangu ni naliona kama ni la muhimu sana. Aliwaagiza waislamu wote wasimlazimishe mtu yoyote kuwa muislamu kwa lazima. bali waishi maisha mema ya mfano ili wakristo na mayahudi wawe waislamu kwa mvuto wa maisha ya waislamu wanaozunguka. aliagiza kuwe na haki sawa kwenye ardhi kwa watu wote. Aliwatoza kodi ya chini wakazi wa Jerusalem kuliko hata wakoloni waliokuwepo hapo.
Hiztoria za kuyahudi zinasema Umar japo yerusalem yote ilikuwa chini yake lakini aliwaruhusu wayahudi na wakristo kuendelea na ibada zao.
HIVI NI BAADHI YA VITU ALIVYOFANYA VYA KUKUMBUKWA
1: Historia zinasema ndiye aliyetoa wazo(kuna wananzuoni wengine wanasema yeye aliweka sheria tu lakini utaratibu ulikuwepo) la kutenganisha kwa wanawake na wanaume katika ibada ili kusiwe na matamanio na watu wajielekeze kwenye ibada tu.
2: Ni Umar aliyeifuta kabisa kazi nzuri aliyoifanya Paul middle east na maeneo ya karibu kwa kusambaza uislam kote huko.
3:wanahistoria wanasema wakati wa mwanzo waislamu walikuwa wanaabudu kwa siri, Umar ndiye aliyetoa wazo wafanye mambo yao wazi, na kuwatishia wote ambao wangewaingilia katika kusali kitu kilichosababisha mtume kuuita "AL-Farouq".
4:Umar ndie aliyeanzisha Kalenda ya Kiislam mwaka 639AD inayotumika hadi leo,
5:Kipindi cha njaa kubwa kuwa ubunifu mkubwa na akili nyingi akiwa kiongozi wa dola la kiislam aliokoa maisha ya mamillioni na watu.
6:Alikataa kuwakata mikono wezi, kwa sababu aliamini mtu aliiba kutokana na yeye kushindwa kutoa ajira kwa jamii.Kwenye utawala wake alikuwa na maono katika dola yake mtu asilale usiku akiwa hajashiba...
KIFO
kama inavyotokea mara nyingi Mashujaa wengi hufa vifo vya kawaida. Siku moja akiwa anasoma sala ya asubuhi alivamiwa na mtumwa wa kiajemi na kumchoma kisu/Jambia mara sita tumboni (vyanzo vingine vinasema mgongoni) na kumuacha damu zikibubujika ardhini na hapo ndio ukawa mwisho wa shujaa huyu katikati ya utawala. Umar sio mtu wa kawaida kwa maana ya uongozi
kuna mengi alifanya hapa wataalam zaidi wanaweza kuchambua.
karibuni,
mashehe,wachungaji, wananzuoni na maulamaa tujadili watu mashuhuri hawa katika imani hizi kinzani bila jazba, ugomvi,fitna na maneno ya kejeli.
naweza kuwa sijaweka mzigo wote ila yaliyobaki yanabaki kama changamoto na mianya kwa wachangiaji.