Umalaika wa CHADEMA Utaiua

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kama mtoto anayedekezwa alivyo ndivyo taasisi yoyote ile isiyokosolewa au kukubali kukosolewa ndivyo inavyoharibika. Taasisi zote duniani zinaongozwa na wanadamu na si malaika.

Kwa kipindi kirefu sana humu ndani ya JF au CHADEMA kwenyewe inaonekana kukosoa mambo mabaya yanayofanywa na chama hicho kama ni kupinga mabadiliko. Mtu akimkosoa Mbowe anaitwa kibaraka wa mafisadi.

Watu wakihoji busara ya kutajataja watu kwa kuwatuhumu (bila sababu za msingi, siyo mafisadi) anaitwa mbumbumbu au fisadi. CHADEMA lazima ikubali kwamba hata wao kama binadamu wanaoongoza taasisi kubwa na inayokubalika kwa jamii na katika kuongoza kwao wakati mwingine huwa wanakosea.

Mwalimu Nyerere wengi tunamkubali kama alikuwa ni Genius lakini hata yeye aliwahi kuandika kitabu kinaitwa "tujisahihishe" lengo likiwa ni kuwazindua viongozi kwamba hata wao wanakosea. CHADEMA ijisahihishe.
 
Ya Chadema waachie Chadema na ya CCM waachie CCM.

Ila kwenye mambo ya SERIKALI na TAIFA kwa ujumla, tutabanana bila kujali wewe ni chama gani.
 
Itakufa sisi m kwanza maana iko ICU inaishi kwa mirija na drip, hayo uliyosema yataikuta sisi m tu.
Si wameanza kufukuzana kule Shy?
 
Kama mtoto anayedekezwa alivyo ndivyo taasisi yoyote ile isiyokosolewa au kukubali kukosolewa ndivyo inavyoharibika. Taasisi zote duniani zinaongozwa na wanadamu na si malaika.

Kwa kipindi kirefu sana humu ndani ya JF au CHADEMA kwenyewe inaonekana kukosoa mambo mabaya yanayofanywa na chama hicho kama ni kupinga mabadiliko. Mtu akimkosoa Mbowe anaitwa kibaraka wa mafisadi.

Watu wakihoji busara ya kutajataja watu kwa kuwatuhumu (bila sababu za msingi, siyo mafisadi) anaitwa mbumbumbu au fisadi. CHADEMA lazima ikubali kwamba hata wao kama binadamu wanaoongoza taasisi kubwa na inayokubalika kwa jamii na katika kuongoza kwao wakati mwingine huwa wanakosea.

Mwalimu Nyerere wengi tunamkubali kama alikuwa ni Genius lakini hata yeye aliwahi kuandika kitabu kinaitwa "tujisahihishe" lengo likiwa ni kuwazindua viongozi kwamba hata wao wanakosea. CHADEMA ijisahihishe.

Kama wewe si CHADEMA endelea na yale unayoyakubali. wasio kubali nao wana nafasi yao.
 
Ndugu yangu CHADEMA kama chama cha upinzani kimeelekeza nguvu zake kwenye kupambana na uzembe, utendaji mbovu na ufisadi uliotamalaki serikalini (unaweza sema serikali ya CCM). Tatizo la wengi wa wakosoajii wa CHADEMA huelekea kutetea mapungufu hayo serikalini pamoja na watuhumiwa wake. Kama unakosa raha watuhumiwa wakitajwa kwa majina basi jiulize kwa nini hawajaenda mahakamani kudai "haki" yao? Wewe kweli unaamini kwamba viongozi wa CHADEMA ni wajinga kiasi cha kutaja mafisadi bila sababu za msingi? Hapa tulipofikishwa na serikali isiyotaka kusimamia maadili kwenye utumishi wa umma basi "naming and shaming" ni hatua muafaka tu kwa upinzani. And it works! Wananchi wanazidi kuuona ukweli. I tell you CCM and its govt have to wake up and smell ze coffee. Nchi inabadilika!
 
Ya Chadema waachie Chadema na ya CCM waachie CCM.

Ila kwenye mambo ya SERIKALI na TAIFA kwa ujumla, tutabanana bila kujali wewe ni chama gani.

Lakini mbona ya CCM hayaachwi! Yameng'ang'aniwa tu!
 
Ya Chadema waachie Chadema na ya CCM waachie CCM.

Ila kwenye mambo ya SERIKALI na TAIFA kwa ujumla, tutabanana bila kujali wewe ni chama gani.
Well said, kama ana mawazo mazuri awapelekee kina Makamba waache kuiendesha CCM kifamilia.
 
Kitu kikubwa nataka kukiona from Chadema ni jinsi gani wataweza kuwa na hoja za msingi bungeni. Nataka kujua wanaplan gani, au Muswaada gani watakaouleta bungeni wa kuwapatia kazi WTZ.
Pili, wanampango gani bungeni kuhusu kuwasadia Wanafunzi kuweza kupata Mikopo ya shule, au Grants.
Tatu, nataka kujua kama watapeleka bengeni muswaada gani kuhusu viwango vya kodi, ushuru. Maana yake TZ ina viwango vikubwa sana vya kodi.
Nk.
 
Wanademokrasi lazima tukubali ukosoaji unaokuza demokrasi ndani ya vyama vetu. Demokrasi ndani ya vyama ni muhimu sana ila pia lazima tuwe makini na watu wanaotumia upande unaoshindwa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi ndani ya vyama vetu kutugawa. Kwa wale wanaong'ang'ania kufanya vyama vetu vionekane kama havina demokrasi au kutusingizia udini na ukabila kwa nia ya kutudhoofisha hivo kudhoofisha kwa makusudi au kwa kutoelewa lazima tujihadhari nao.
BRAVO CHADEMA
 
Hiyo sasa ndugu yangu kamata ilani yao ina kila kitu. Lakini kwa kifupi nadhani yale mambo yote unayoona ccm hawafanyi vizuri kama vile matumizi mabaya ya pesa za umma, Mikataba mibovu ya madini, huduma duni za afya, elimu ndo vitu ambavyo watangangana navyo
 
Kama mtoto anayedekezwa alivyo ndivyo taasisi yoyote ile isiyokosolewa au kukubali kukosolewa ndivyo inavyoharibika. Taasisi zote duniani zinaongozwa na wanadamu na si malaika.

Kwa kipindi kirefu sana humu ndani ya JF au CHADEMA kwenyewe inaonekana kukosoa mambo mabaya yanayofanywa na chama hicho kama ni kupinga mabadiliko. Mtu akimkosoa Mbowe anaitwa kibaraka wa mafisadi.

Watu wakihoji busara ya kutajataja watu kwa kuwatuhumu (bila sababu za msingi, siyo mafisadi) anaitwa mbumbumbu au fisadi. CHADEMA lazima ikubali kwamba hata wao kama binadamu wanaoongoza taasisi kubwa na inayokubalika kwa jamii na katika kuongoza kwao wakati mwingine huwa wanakosea.

Mwalimu Nyerere wengi tunamkubali kama alikuwa ni Genius lakini hata yeye aliwahi kuandika kitabu kinaitwa "tujisahihishe" lengo likiwa ni kuwazindua viongozi kwamba hata wao wanakosea. CHADEMA ijisahihishe.

Unadhani kwa mtazamo wako huo mwenye kuchemsha Bongo atakuelewa ? Wape Sisi m ushauri huo
 
I think what our friend fails to understand is this: Constructive criticsm is always welcome, but destructive critisim must be shunned. Sio kila kukosoa ni kukosoa, kukosoa kunakojenga. Kipimo cha constructive criticism ni usahihi wa hoja zake, na shabaha zake.
 
Well said, kama ana mawazo mazuri awapelekee kina Makamba waache kuiendesha CCM kifamilia.

Wallah wewe u mbali ningekupiga na Castle Lite bee, hayo anayoona ni mawazo mazuri ayawasilishe kwenye Chama Dume fake aone atakavyotolewa baruti na Riz 1 achilia mbali Makamba.Hapo ndo utajua hakuna kitu wala udume wowote isipokuwa ni JAMARI Group of Company.Note JAMARI (Jakaya, January, Makamba,Riz 1)
 
Back
Top Bottom