Umakini wa bunge letu chini ya spika Makinda ni wakutiliwa shaka.

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Tangu kuzinduliwa kwa bunge hili la kumi wananchi wengi wamekuwa wakionyesha kutoridhishwa na utendaji kazi wake. Chazo cha kutokuwa na imani na bunge hilo hasa kinatokana na hisia zilizojengeka miongoni mwa watu wengi ya kwamba spika wa sasa wa bunge hilo alipandikizwa na mafisadi na hivyo yuko pale kulinda maslahi yao na siyo ya wananchi. Wasiwasi huo wa wananchi juu ya utendaji kazi wa bunge la sasa umezidi kuongezeka kutokana na namna linavyoshughulikia huu muswada wa mabadiriko ya katiba; kwa maoni ya watu wengi kwa bunge makini huu muswada wa mabadiriko ya katiba haukustahili kupelekwa kwa wananchi kwaajili ya kupata maoni yao kwakuwa kwa vigezo vyovyote vile bado haukidhi haja. hivyo ulistahili kurejeshwa serikalini katika ngazi ya kamati ili uandikwe upya. Nasema haukidhi haja kwanza kwasababu unazungumzia suala la marekebisho ya katiba iliyopo wakati kinachodaiwa na wananchi ni katiba mpya, na vile vile maudhui ya muswada huo yanakiuka msingi wa utungaji wa katiba ambao unataka wananchi wenyewe ndio waongoze mchakato huo na wala siyo rais.
 
sio kua ni hisia ziznazowafanya wananchi kutilia shaka utendaji wa spika huyu bali ni uwezo wake kikazi akilinganishwa na yule aliyekuepo hawa ikizingatiwa kua yule aliekuepo bado alikua wlling kuendelea na kazi yake.
Pili ni mchakato mzima uliomwezesha yeye spika aliyepo kuwepo. Upendeleo wa kigezo cha gender na wala sio uwezo.hivi ndivyo vigezo vinatufanya tuamini kua ni mamluki wa mafisadi.
anyway, ni sisis wananchi ndo tunaotaka nchi iwe namna fulani wao kamwe hawataweza kutupindisha.
 
Katiba, nyie wabunge ccm sio jambo la mchezo. endapo mtaipitisha hivyo hivyo kwa sababu ya wingi wenu MUNGU atawalaani milele. msitegemee mtatawala milele nchi hii. 2015 sio mbali na mtakuja kulalamika nyinyi wenyewe wakati chama mbadala kimeingia madarakani. kumbukeni watznian wa sasa wako tayari kufa kuliko kuona wanaletewa sheria mbovu ya uundwaji wa katiba yao.
 
Back
Top Bottom