#COVID19 Umakini kwenye matumizi ya Feni katika nyakati zenye tahadhari ya kuwepo kwa maambukizi ya virusi vya Corona

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
20210302_083424_0000.png


Matumizi ya feni nyumbani ni salama kwa mzunguko wa hewa kati ya wanafamilia wanaoishi pamoja ambao hawajaambukizwa na virusi vya Korona

Lakini, feni zinapaswa kuepukwa wakati ambapo watu ambao sio sehemu ya familia ya karibu wanapotembelea

Hii ni kwa sababu upepo unaovuma kutoka kwa mtu aliyeambukizwa kwenye sehemu zilizofungwa kama ndani unaweza kuongeza maambukizi ya virusi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine

Nyumbani, ofisini au shuleni, ikiwa matumizi ya feni ni lazima ni muhimu kuongeza mzunguko wa hewa kwa kufungua madirisha na kuruhusu upepo wa njee kuingia ndani na hewa ya ndani kwenda nje badala ya kuzunguka humo ndani
 
Feni ukanda wa Pwani haswa Dar ukizuia watu hawawezi kulala usiku
Labda tusimbishie sana mtoa mada kwamba feni linaweza kusaidia kuenea kwa ugonjwa. Kwa chumbani hakuna haja kuzuia kwani mnakowapo watu wa palepale tu. Hata mkiwa sebuleni watu wa familia moja hamuwezi kushinda mmevaa barakoa. Hizo tahadhari ni kwa pale wanapokusanyika watu wengi wanaotoka mahali tofauti. Kwa mfano shuleni wanafunzi wanatoka mahali mbalimbali na kama mmoja ana ugonjwa huo feni inaweza kusaidia kuueneza. Kwa hiyo feni zisitumike mashuleni, makanisani na pengine po pote penye mikusanyiko ya watu wengi. Nyumbani zinaweza kutumika si chumbani tu bali hata sebuleni.
 
View attachment 1715242

Matumizi ya feni nyumbani ni salama kwa mzunguko wa hewa kati ya wanafamilia wanaoishi pamoja ambao hawajaambukizwa na virusi vya Korona

Lakini, feni zinapaswa kuepukwa wakati ambapo watu ambao sio sehemu ya familia ya karibu wanapotembelea

Hii ni kwa sababu upepo unaovuma kutoka kwa mtu aliyeambukizwa kwenye sehemu zilizofungwa kama ndani unaweza kuongeza maambukizi ya virusi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine

Nyumbani, ofisini au shuleni, ikiwa matumizi ya feni ni lazima ni muhimu kuongeza mzunguko wa hewa kwa kufungua madirisha na kuruhusu upepo wa njee kuingia ndani na hewa ya ndani kwenda nje badala ya kuzunguka humo ndani
Bora kutumia AC kuliko feni
 
Bora kutumia AC kuliko feni
Tangu haya maradhi yaanze wameshakufa wengi wanaotumia Ac na hawagusani na mtu.Wamebaki wengi wazee kwa vijana wanaosongamana masokoni na wanaokoholeana uso kwa uso.Ni mtihani mkubwa huu kutoka kwa Allah. Tuzinduke
 
Ni kuchukua tahadhari tu maana hali ni tete iwe unatumia feni ama hutumii cha msingi kufuata maelekezo na ushauri unaotolewa mara kwa mara na wataalam wa afya.
 
Kwani Corona inaambukiza kwa njia ya hewa ?
NI kwa njia ya kupiga chafya.Twataraji hii hewa tunayovuta ni safi sana na tunaihitaji kwa wingi kila wakati.Tukianza kuitilia shaka na kuiogopa tutashindwa kuishi.
 
Bora kutumia AC kuliko feni
View attachment 1715242

Matumizi ya feni nyumbani ni salama kwa mzunguko wa hewa kati ya wanafamilia wanaoishi pamoja ambao hawajaambukizwa na virusi vya Korona

Lakini, feni zinapaswa kuepukwa wakati ambapo watu ambao sio sehemu ya familia ya karibu wanapotembelea

Hii ni kwa sababu upepo unaovuma kutoka kwa mtu aliyeambukizwa kwenye sehemu zilizofungwa kama ndani unaweza kuongeza maambukizi ya virusi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine

Nyumbani, ofisini au shuleni, ikiwa matumizi ya feni ni lazima ni muhimu kuongeza mzunguko wa hewa kwa kufungua madirisha na kuruhusu upepo wa njee kuingia ndani na hewa ya ndani kwenda nje badala ya kuzunguka humo ndani
CORONA VIRUS DISEASE 2019 haimbukizwi kwa njia ya hewa bali ni maji maji au mate yatokayo mdomoni kwa muathirika! Na hawa wenye kutumia sana Air conditioner kuwa na maaambukizi ni kutokana na ubaridi kupita kiasi na virusi hawa wanastawi sana kwenye hali ya ubaridi.
Nimejibu kwa uzoefu wangu ila mie sio mtaalam wa afya.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom