Shoctopus
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 3,434
- 1,985
Asalam-alaekoum Wana-JF
Nianze kwa kurudia 'mantra' yangu kuhusu maamuzi ya wanasiasa na watawala wetu katika MFUMO tulionao:
THE HALLMARKS OF BAD GOVERNANCE:
1. Ambiguity
2. Arbitrariness
3. Capriciousness
Maana ya mantra hii ni kwamba huwezi kuwa na Utawala Bora kwa maamuzi:
1. YA KUKINZANA, [Ambiguity]
2. YA KIHOLELA, [Arbitrariness]
2. YA HILA. (mizengwe) [Caprice]
Lengo la andiko hili ni kujadili sera na maamuzi ya wanasiasa na watawala wetu katika masuala ya maendeleo na ustawi wa jamii hasahasa katika masuala ya siasa na sera za CCM za social engineering na mipangomiji, pamoja na usafi wa mazingira na ujasiriamali kwa ujumla wake katika muktadha wa (in the context of) mantra yangu hapa juu kuhusu haki za binadamu na UTAWALA BORA.
Tamko la UN kuhusu ajira ni kwamba ajira ni haki ya kila mtu. Kama ilivyo haki ya kuishi. Na kwenye Tamko hilo hakuna ambiguity kuhusu tafsiri ya neno AJIRA.
Sera ya CCM ni kwamba ajira ni "kujiajiri mwenyewe" au "ujasiriamali". Kujikanganya kwa sera kunaanzia hapo. Kwasababu kauli hii ni ya kisiasa tu na haiendani na tamko la UN kuhusu ajira. Kwasababu jukumu la serikali ni kuzalisha nafasi za ajira. Hii maana yake siyo kwamba serikali iajiri raia, hapana. Bali ni jukumu la serikali Kubuni sera zitakazozaa VYANZO VYA AJIRA. Serikali yetu badala ya kubuni vyanzo vya ajira kila siku inabuni vyanzo vya kodi!
Sera hii ndiyo iliyotufikisha katika kero au tatizo la machinga nchi nzima, pamoja na bodaboda, mamantilie, daladala, bajaji nk. Haya ni makundi ya vijana, wanawake, wazee nk wanaotumiwa na CCM kwenye kura wakati wa kampeni za uchaguzi na upigaji kura.
Kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020 Hayati JPM alianzisha vitambulisho rasmi vya ujasiriamali. Nimeshasema mahali pengine humu kwamba CCM walilifungua chupa la jini. Lakini JPM akaenda mbali zaidi kwa kulitoa ndani ya chupa na kuliweka 'SEBULENI' kwao.
Ulikuwa uamuzi holela, usiozingatia kanuni za mipangomiji usafi wa mazingira na njia za kiuchumi au kisayansi (social economic policies) za ubunifu wa AJIRA katika misingi ya tamko la UN kuhusu haki ya ajira.
Ulikuwa uamuzi wa hila pia (wa mizengwe) kwa madhumuni ya kuwatumia wahusika kisiasa dhidi ya upinzani kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.
Machinga ni kaa la moto hawagusiki. Bodaboda nao kupitia siasa za CCM wamepewa kiburi cha kukiuka sheria za usalama barabarani!
Hulka au tabia asili ya makundi haya (croud behavior) ni kutumia status kama makundi ya wapigakura wa CHAMA TAWALA na wingi wao kulinda maslahi yao. Wingi wao unaotumiwa kisiasa umewapa nguvu ya ajabu mbele ya local government na traffic policing.
Halafu kuna phenomenon katika town planning inaitwa "attractive nuisance" (kero mtego) ukiitengeneza au kuiruhusu iwepo, ni ngumu sana kuiondoa.
Jalala au dampo ni kero mtego wenye chambo (an attractive nuisance) unaovutia uzembe.
Kwamfano ukirihusu watu watupe takataka eneo fulani kwa muda fulani, utakuwa umeanzisha jalala au dampo, an attractive nuisance. Kila mwenye taka zake ataziweka hapo. Na wengine watakuja kushinda hapo wakisakula.
Si rahisi baada ya muda fulani kuzuia watu wasitupe taka hapo au kuwaondoa wasakulaji. Utakuwa umebadili social behavior ya jamii husika ambayo ni ngumu kuibadili. Binadamu wanakuwa kama nzi wanaovutiwa na uchafu!
Kwa mantiki hiyo umachinga ni social behavior. Ni hulka ya jamii au kundi la jamii. Hata bodaboda ni kundi la watu waliozoezwa kuvunja sheria za usalama barabarani na usafi wa mazingira. Huwezi kuwabadili tabia yao kirahisi, haswa unapowatumia kisiasa. Unawapa nguvu dhidi ya mamlaka zinazosimamia mipangomiji na mazingira nk.
Kitu cha tatu katika mantra yangu ni AMBIGUITY.
Huwezi kuwa na Utawala Bora hata kama lengo ni kubuni vyanzo vya ajira, kwa maamuzi yanayokinzana.
Unaajiri wataalamu wa mipangomiji, wa afya ya jamii, wataalamu wa mazingira nk.; Halafu unawapa wajasiriamali vitambulisho rasmi vya kufanya biashara POPOTE'!
Ukweli hapa bni kwamba hujabuni ajira wala VYANZO VYA AJIRA endelevu kwa misingi ya tamko la UN kuhusu ajira.
Rais SSH alipokiwa Mwanza alisema anajua kwamba baadhi ya machinga huwauzia wafanyabiashara wakubwa mbele ya maduka yao, akawaonya kwamba wanaziba njia za waenda kwa miguu na kuleta msongamano barabarani!
Zoezi hili linaonyesha kwamba siri ya wajasiriamali hawa ni wafanyabiashara wenye MITAJI MIKUBWA wanaowapa "AJIRA" baadhi ya wamachinga (kwa mlago wa nyuma) na kufanya watawala kudai kwamba wamezalisha ajira!
Kwa fikra za kawaida serikali ingeboresha mazingira ya wafanyabiashara wenye MITAJI MIKUBWA ili wawape ajira hao wanaopanga bidhaa barabarani nayo serikali ipate kodi zaidi. Badala yake sera za CCM zinawaumiza wafanyabiashara wakubwa wanaolipakodi kwa EFD kwasababu hawaupendi mfumo wenyewe, na wengine humfanya mbinu za kuuhujumu. Halafu pia serikali haipati kodi inayostahili toka kwa machinga hata kama baadhi yao wana mitaji mikubwa. Ilimradi wamepata vitambulisho rasmi na kuvivaa shingoni. Hawagusiki!
Huko Morogoro DC na Mkurugenzi wa Jiji wamefutwa kazi kwa suala la machinga; tena kupitia tamko la hadharani kule Mwanza! Mimi bado sijaelewa kama Rais SSH alishauriwa na waziri yupi katika serikali yake?
Kwasababu suala la kubuni au kuhamisha maeneo ya biashara za machinga ni la mamlaka za miji na wizara mtambuka. Lakini uamuzi wake ulifanywa papo kwa papo siku chache tu baada ya vurugu kati ya Mgambo na machinga huko Morogoro! Ni mfano nzuri wa 'arbitrary decision' uamuzi wa holela.
Tumefika mahali hata bungeni Mbunge wa CCM anasema kwamfano kwamba: Mtukufu Rais ameamua katika bajeti ya mwaka huu "kuongeza kodi ya vifurushi vya simu" au"kuwapandisha vyeo na mishahara walimu". Yaani mbunge anasahau kwamba yuko bungeni kusemea wananchi na kuiwahibisha serikali katika kutumikia wananchi wote kwa usawa. Na kwamba mapato na matumizi ya Serikali (budget) yanaidhinishwa na bunge.
Nimalizie kwa kusema kwamba sera ya CCM ya ELIMU ni kuwezesha kijana kujiajiri, si kuajiriwa. Hapo hapo sera ya CCM ya UCHUMI ni kuvutia wawekezaji kuanzisha viwanda.
Swali gumu ni kwamba ni nani watakaoajiriwa kwenye viwanda hivyo? Ajira katika dunia ya sasa na baadae inahitaji elimu ya kimataifa pamoja na lugha, katika nyanja mbalimbali za uchumi. Hii sera ya elimu ya kujiajiri ni potofu, inakinzana na lengo la kupeleka nchi kwenye UCHUMI WA JUU.
Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
Nianze kwa kurudia 'mantra' yangu kuhusu maamuzi ya wanasiasa na watawala wetu katika MFUMO tulionao:
THE HALLMARKS OF BAD GOVERNANCE:
1. Ambiguity
2. Arbitrariness
3. Capriciousness
Maana ya mantra hii ni kwamba huwezi kuwa na Utawala Bora kwa maamuzi:
1. YA KUKINZANA, [Ambiguity]
2. YA KIHOLELA, [Arbitrariness]
2. YA HILA. (mizengwe) [Caprice]
Lengo la andiko hili ni kujadili sera na maamuzi ya wanasiasa na watawala wetu katika masuala ya maendeleo na ustawi wa jamii hasahasa katika masuala ya siasa na sera za CCM za social engineering na mipangomiji, pamoja na usafi wa mazingira na ujasiriamali kwa ujumla wake katika muktadha wa (in the context of) mantra yangu hapa juu kuhusu haki za binadamu na UTAWALA BORA.
Tamko la UN kuhusu ajira ni kwamba ajira ni haki ya kila mtu. Kama ilivyo haki ya kuishi. Na kwenye Tamko hilo hakuna ambiguity kuhusu tafsiri ya neno AJIRA.
Sera ya CCM ni kwamba ajira ni "kujiajiri mwenyewe" au "ujasiriamali". Kujikanganya kwa sera kunaanzia hapo. Kwasababu kauli hii ni ya kisiasa tu na haiendani na tamko la UN kuhusu ajira. Kwasababu jukumu la serikali ni kuzalisha nafasi za ajira. Hii maana yake siyo kwamba serikali iajiri raia, hapana. Bali ni jukumu la serikali Kubuni sera zitakazozaa VYANZO VYA AJIRA. Serikali yetu badala ya kubuni vyanzo vya ajira kila siku inabuni vyanzo vya kodi!
Sera hii ndiyo iliyotufikisha katika kero au tatizo la machinga nchi nzima, pamoja na bodaboda, mamantilie, daladala, bajaji nk. Haya ni makundi ya vijana, wanawake, wazee nk wanaotumiwa na CCM kwenye kura wakati wa kampeni za uchaguzi na upigaji kura.
Kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2020 Hayati JPM alianzisha vitambulisho rasmi vya ujasiriamali. Nimeshasema mahali pengine humu kwamba CCM walilifungua chupa la jini. Lakini JPM akaenda mbali zaidi kwa kulitoa ndani ya chupa na kuliweka 'SEBULENI' kwao.
Ulikuwa uamuzi holela, usiozingatia kanuni za mipangomiji usafi wa mazingira na njia za kiuchumi au kisayansi (social economic policies) za ubunifu wa AJIRA katika misingi ya tamko la UN kuhusu haki ya ajira.
Ulikuwa uamuzi wa hila pia (wa mizengwe) kwa madhumuni ya kuwatumia wahusika kisiasa dhidi ya upinzani kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.
Machinga ni kaa la moto hawagusiki. Bodaboda nao kupitia siasa za CCM wamepewa kiburi cha kukiuka sheria za usalama barabarani!
Hulka au tabia asili ya makundi haya (croud behavior) ni kutumia status kama makundi ya wapigakura wa CHAMA TAWALA na wingi wao kulinda maslahi yao. Wingi wao unaotumiwa kisiasa umewapa nguvu ya ajabu mbele ya local government na traffic policing.
Halafu kuna phenomenon katika town planning inaitwa "attractive nuisance" (kero mtego) ukiitengeneza au kuiruhusu iwepo, ni ngumu sana kuiondoa.
Jalala au dampo ni kero mtego wenye chambo (an attractive nuisance) unaovutia uzembe.
Kwamfano ukirihusu watu watupe takataka eneo fulani kwa muda fulani, utakuwa umeanzisha jalala au dampo, an attractive nuisance. Kila mwenye taka zake ataziweka hapo. Na wengine watakuja kushinda hapo wakisakula.
Si rahisi baada ya muda fulani kuzuia watu wasitupe taka hapo au kuwaondoa wasakulaji. Utakuwa umebadili social behavior ya jamii husika ambayo ni ngumu kuibadili. Binadamu wanakuwa kama nzi wanaovutiwa na uchafu!
Kwa mantiki hiyo umachinga ni social behavior. Ni hulka ya jamii au kundi la jamii. Hata bodaboda ni kundi la watu waliozoezwa kuvunja sheria za usalama barabarani na usafi wa mazingira. Huwezi kuwabadili tabia yao kirahisi, haswa unapowatumia kisiasa. Unawapa nguvu dhidi ya mamlaka zinazosimamia mipangomiji na mazingira nk.
Kitu cha tatu katika mantra yangu ni AMBIGUITY.
Huwezi kuwa na Utawala Bora hata kama lengo ni kubuni vyanzo vya ajira, kwa maamuzi yanayokinzana.
Unaajiri wataalamu wa mipangomiji, wa afya ya jamii, wataalamu wa mazingira nk.; Halafu unawapa wajasiriamali vitambulisho rasmi vya kufanya biashara POPOTE'!
Ukweli hapa bni kwamba hujabuni ajira wala VYANZO VYA AJIRA endelevu kwa misingi ya tamko la UN kuhusu ajira.
Rais SSH alipokiwa Mwanza alisema anajua kwamba baadhi ya machinga huwauzia wafanyabiashara wakubwa mbele ya maduka yao, akawaonya kwamba wanaziba njia za waenda kwa miguu na kuleta msongamano barabarani!
Zoezi hili linaonyesha kwamba siri ya wajasiriamali hawa ni wafanyabiashara wenye MITAJI MIKUBWA wanaowapa "AJIRA" baadhi ya wamachinga (kwa mlago wa nyuma) na kufanya watawala kudai kwamba wamezalisha ajira!
Kwa fikra za kawaida serikali ingeboresha mazingira ya wafanyabiashara wenye MITAJI MIKUBWA ili wawape ajira hao wanaopanga bidhaa barabarani nayo serikali ipate kodi zaidi. Badala yake sera za CCM zinawaumiza wafanyabiashara wakubwa wanaolipakodi kwa EFD kwasababu hawaupendi mfumo wenyewe, na wengine humfanya mbinu za kuuhujumu. Halafu pia serikali haipati kodi inayostahili toka kwa machinga hata kama baadhi yao wana mitaji mikubwa. Ilimradi wamepata vitambulisho rasmi na kuvivaa shingoni. Hawagusiki!
Huko Morogoro DC na Mkurugenzi wa Jiji wamefutwa kazi kwa suala la machinga; tena kupitia tamko la hadharani kule Mwanza! Mimi bado sijaelewa kama Rais SSH alishauriwa na waziri yupi katika serikali yake?
Kwasababu suala la kubuni au kuhamisha maeneo ya biashara za machinga ni la mamlaka za miji na wizara mtambuka. Lakini uamuzi wake ulifanywa papo kwa papo siku chache tu baada ya vurugu kati ya Mgambo na machinga huko Morogoro! Ni mfano nzuri wa 'arbitrary decision' uamuzi wa holela.
Tumefika mahali hata bungeni Mbunge wa CCM anasema kwamfano kwamba: Mtukufu Rais ameamua katika bajeti ya mwaka huu "kuongeza kodi ya vifurushi vya simu" au"kuwapandisha vyeo na mishahara walimu". Yaani mbunge anasahau kwamba yuko bungeni kusemea wananchi na kuiwahibisha serikali katika kutumikia wananchi wote kwa usawa. Na kwamba mapato na matumizi ya Serikali (budget) yanaidhinishwa na bunge.
Nimalizie kwa kusema kwamba sera ya CCM ya ELIMU ni kuwezesha kijana kujiajiri, si kuajiriwa. Hapo hapo sera ya CCM ya UCHUMI ni kuvutia wawekezaji kuanzisha viwanda.
Swali gumu ni kwamba ni nani watakaoajiriwa kwenye viwanda hivyo? Ajira katika dunia ya sasa na baadae inahitaji elimu ya kimataifa pamoja na lugha, katika nyanja mbalimbali za uchumi. Hii sera ya elimu ya kujiajiri ni potofu, inakinzana na lengo la kupeleka nchi kwenye UCHUMI WA JUU.
Sent from my G80 using JamiiForums mobile app