CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,985
- 4,083
UMACHINGA SIO KIPAJI, SIO SIFA, SIO CHEO, SIO KIPAWA | UMACHINGA NI HATUA YA KUFIKIA NDOTO YA KUWA MFANYABIASHARA MKUBWA NDANI|NJE YA TANZANIA
________________________________________
Nguli wa Uchumi mfaransa Jean Baptiste mwanzilishi wa neno ujasiriamali|Umachinga alisema " Umachinga ni hatua ya kutoka katika uchumi mdogo kwenda uchumi wakati na baadae uchumi wa juu " Jean-Baptiste,
Hata hivyo, niserikali ya kishamba tu ndio inaweza kujisikia fahari mtu kujiita Machinga miaka nenda rudi uje na nimshamba pekee ndio anaweza kujisifia yeye ni mmachinga mzoefu,Umachinga sio sifa wala kipaji ni hatua|daraja la kupita kwenda hatua ya juu zaidi katika kumiliki na kuendesha biashara kubwa,Kila anayetamani machinga aendelee kuwa machinga huyo ni muuwaji wa ndoto za watu hao nani mtu hatari sana kwa Ustawi wa Taifa na Watu wake hasa hao machinga,Akitokea mtu anayetafuta nafuu kwenye Siasa akakwambia wewe Machinga endelea kuwa machinga nitakulinda huyo ni hatari kuliko mchawi na hafai kuwa kiongozi kama anashindwa kukuongoza kwenda kuwa mfanyabiashara mkubwa na anafurahia namna jua linavyoishia mwilini mwako siku kwa siku ili tu siku moja umpigie kura huyo hakufai wewe wala Mungu,
Tanzania inajumla ya Wamachinga 2,335,711 wenye vitambulisho huku wafanyabiashara wakifikia 3.8M,Hii ni sawa nakusema idadi ya wamachinga Tanzania ni 62% ya walipa kodi wote wa nchi hii,Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza wamachinga wapangwe vizuri maana yake watolewe Juani wapeleke kwenye maeneo ambayo watatambulika ( Permanent premises) ili kutimiza ndoto yao ya kuwa wafanyabiashara wakubwa,hapa lazima tumpongeze sana Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan ,Moja ya Sharti kubwa la kupata mkopo toka benki yoyote ya Biashara ni kuwa na eneo sahihi na kufanyia biashara ( business premise ).Nahapa natamani wamachinga mnielewe vizuri nimesema umachinga sio kipaji ni hatua ya ukuaji katika biashara hivyo ni lazima ifike siku Muhitimu huo Umachinga ila kamwe hamuwezi kuuhitimu Umachinga mkiwa Chini pembeni ya Barabara,
Wamachinga wa nchi hii wamefanyiwa sana siasa na imefika wakati wamejiona kama wao ndio wenye turufu ya Siasa na Wanasiasa wa Tanzania badala ya kuwaza zaidi kesho yao katika biashara zao,Leo Machinga akihamishwa kupelekwa mahali patakapoamua kesho yake iliyonjema anahisi kaonewa kwakuwa tu uchaguzi umekwisha,Tunataka viongozi kama Rais Samia wasiojali kesho yao kisiasa ila Kesho ya wamachinga na watoto wao na watoto wa watoto wao,Kama Rais Samia atafanikiwa kuwahitimisha Umachinga hao watu 2.34M maana yake by 2024|25 Tanzania itakuwa na walipakodi zaidi ya 6M na itakuwa rekodi nyingine kwake kwani tangu Uhuru walipakodi wamefikia 3.8M kwenye nchi ya watu 60M,kwa akili za kawaida Watu wanaweza wakadhani machinga wanaonewa kumbe wanasaidiwa kufikia ndoto zao kirahisi, Mwenye masikio naasikie haya,
.........Kazi iendelee .........
VIVA TANZANIA | VIVA SAMIA | VIVA CCM
________________________________________
Nguli wa Uchumi mfaransa Jean Baptiste mwanzilishi wa neno ujasiriamali|Umachinga alisema " Umachinga ni hatua ya kutoka katika uchumi mdogo kwenda uchumi wakati na baadae uchumi wa juu " Jean-Baptiste,
Hata hivyo, niserikali ya kishamba tu ndio inaweza kujisikia fahari mtu kujiita Machinga miaka nenda rudi uje na nimshamba pekee ndio anaweza kujisifia yeye ni mmachinga mzoefu,Umachinga sio sifa wala kipaji ni hatua|daraja la kupita kwenda hatua ya juu zaidi katika kumiliki na kuendesha biashara kubwa,Kila anayetamani machinga aendelee kuwa machinga huyo ni muuwaji wa ndoto za watu hao nani mtu hatari sana kwa Ustawi wa Taifa na Watu wake hasa hao machinga,Akitokea mtu anayetafuta nafuu kwenye Siasa akakwambia wewe Machinga endelea kuwa machinga nitakulinda huyo ni hatari kuliko mchawi na hafai kuwa kiongozi kama anashindwa kukuongoza kwenda kuwa mfanyabiashara mkubwa na anafurahia namna jua linavyoishia mwilini mwako siku kwa siku ili tu siku moja umpigie kura huyo hakufai wewe wala Mungu,
Tanzania inajumla ya Wamachinga 2,335,711 wenye vitambulisho huku wafanyabiashara wakifikia 3.8M,Hii ni sawa nakusema idadi ya wamachinga Tanzania ni 62% ya walipa kodi wote wa nchi hii,Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza wamachinga wapangwe vizuri maana yake watolewe Juani wapeleke kwenye maeneo ambayo watatambulika ( Permanent premises) ili kutimiza ndoto yao ya kuwa wafanyabiashara wakubwa,hapa lazima tumpongeze sana Rais wetu Mhe Samia Suluhu Hassan ,Moja ya Sharti kubwa la kupata mkopo toka benki yoyote ya Biashara ni kuwa na eneo sahihi na kufanyia biashara ( business premise ).Nahapa natamani wamachinga mnielewe vizuri nimesema umachinga sio kipaji ni hatua ya ukuaji katika biashara hivyo ni lazima ifike siku Muhitimu huo Umachinga ila kamwe hamuwezi kuuhitimu Umachinga mkiwa Chini pembeni ya Barabara,
Wamachinga wa nchi hii wamefanyiwa sana siasa na imefika wakati wamejiona kama wao ndio wenye turufu ya Siasa na Wanasiasa wa Tanzania badala ya kuwaza zaidi kesho yao katika biashara zao,Leo Machinga akihamishwa kupelekwa mahali patakapoamua kesho yake iliyonjema anahisi kaonewa kwakuwa tu uchaguzi umekwisha,Tunataka viongozi kama Rais Samia wasiojali kesho yao kisiasa ila Kesho ya wamachinga na watoto wao na watoto wa watoto wao,Kama Rais Samia atafanikiwa kuwahitimisha Umachinga hao watu 2.34M maana yake by 2024|25 Tanzania itakuwa na walipakodi zaidi ya 6M na itakuwa rekodi nyingine kwake kwani tangu Uhuru walipakodi wamefikia 3.8M kwenye nchi ya watu 60M,kwa akili za kawaida Watu wanaweza wakadhani machinga wanaonewa kumbe wanasaidiwa kufikia ndoto zao kirahisi, Mwenye masikio naasikie haya,
.........Kazi iendelee .........