Umaarufu!

Nilikuwa bize na harakati zangu sipendi mazoea yakifala.

Wenzangu wakiwa mstarini Mimi Niko jikoni.. wakiwa wanasali Mimi Niko kwenye bustani ya shule.....

muda wa prepo mi ndio naoga .......

wakilala Mimi ndio nazurura kila chumba na kupiga chabo hosteli za mademu...

Daily Mimi ni mtu wa adhabu za mashambani manake class siiuwahi paelewa. Adhabu yenyewe kulima dakika 20 nimeshamaliza nakuwa na ticket ya kutoenda class.....

Nilikuwa na dili na mpishi wa skuli kwenye biashara ya mazao ya shule na bangi (kwa wateja wangu) niliwahi kamatwa ila niliitoka kesi kibabilon....

Nilikuwa sioni umuhimu wa ratiba manake Kama Ni class nilikuwa vizuri. Na nimemaliza na Division One Tena nzuri tuuu..

tukipewa kazi ya shamba ndio dakika mbili nimeshamaliza nawadere watoto wa mama.......

Cjawahi kuwa msafi kupindukia ule usarobaro wa O-level hata siku moja kwanza mashati nilikuwa naiba daily ya watoto wa mama, nikikuta nguo imefuliwa ikakauka ndio naitupia mwilini ikichafuka narudisha nilipotoa.....

Nilikuwa nakula sio utani aisee Yani mademu wakienda kumwaga msosi si unajua Toto za kishua Mimi natia nanga msosi. Kama wote kwangu.....

Ila nilikuwa mkimya watu wananijua ila Sasa kuanza kunisemesha ndio msala kwaiyo sikuwa na marafiki wa shule na hata Sasa (wale sijui best friend wa kufatana kila mahali)


Nilianza kupunguza udismainda baada ya kwenda advance...ila swala la kufata ratiba za watu zisizo muhimu siwezi hata siku moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilifanikiwa kumwekea mwalim kioo chini katikati ya mguu na mguu tukaona kila kutu ila kuanzia ule mstari wanaume wote tuliokuwepo tulikula stick zaidi ya 40 kila mmoja maana walim wa kiume walikuwa 18 na kila mwalim alichapa zaidi ya viboko 6
Ni kitu gani kilikupa umaarufu shuleni?
mimi ni good handwriting!
 
Headmaster alikuwa cha pombe,nikikutana naye mtaani nampiga bia mbili,nilifanya matukio ya kila aina ila siyo kujeruhi,hutoona hata suspension,wengine hata wakicheka hovyo anaenda kupumzika wiki kadhaa,darasani nilikuwa kati tu siyo genius sana wala siyo kilaza,yaani zile za B,C kwenye ufaulu harafu smart kupindukia,suruali tano,shati tano nikivaa hizi leo mpaka next week,nanukia body spray mpka walimu wanaulizia.
Acha tu niishie hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa msafi sana tabia nzuri,mtaratibu,napenda kufuata taratibu za shule husika. ivo nikawa kiranja mkuu, nikafanya vizuri sana haijawahi tokea,ktk shule ile, nikafaulu kwa msaada wa mwalimu kwa sababu walinifundisha sana kwa mara ya kwanza nilimaliza sylubus masomo yote na nika zirudia tena baadhi, maisha yakawa rahisi mno, nikaishi kwa huyo mwalimu mkuu anajulikana kwa jina la KAJUMLO.mhaya,
Nikaenda A level,shule jirani na pale,kila likizo narudi kwa kajumlo, mpaka chuo kikuu mwalimu akanipenda sanapamoja namke wake wakasema ni lazima niunganishe damu na binti yake ambaye tulizoeana sana bila kula tunda kwa muda mrefu, jambo lilimfurahisha sana kajumlo,basi kama kawaida mzee mzima nikakubali, na huko nyuma wazazi wangu hasa hasa baba alioa mke mwingine hivo hakunifuatilia sana alijua sina akili za kufaulu mitihani bila msaada wake sababu alikuwa na pesa, hata akiambiwa mwanao kafaulu alidhani natafuta sifa tu, nilipo graduate ndo kaona kumbeee.sawa akamwambia mama akili zangu hizoo! nimejizaa mimi, unaona nimekupa mwenye akili.
Binti Kajumlo ndo mke wangu mpaka leo tuna vitoto 2. na baba mkwe alinipa PEUGEOT 54 niitumie Nayo mpaka leo.ila wachache wanafunzi wanajua hili jambo kuwa nimeoa mtoto wa Head master wangu.kwa jinsi binti alivo pendeza walio wengi wanamsahau. hilo nalo kalipenda baba mkwe wangu.nikenda Bukoba baba heeee! wale watu wanajua kutunza na kulinga wacha tu ukipata nafasi oa muhaya uta enjoy kuliko kawaida uwe na tabia nzuri, mie kwangu ni burudani tosha wameshaniambukiza.Sababu mimi tu ni sehemu ya majidai yao kwa vile nimetulia
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom