Umaarufu/Umashuhuri wa Mandela uliotengenezwa na Magharibi na Wazungu!

YouTube

JF-Expert Member
Jul 24, 2012
936
361
nilkuwa najiuliza sana kafanya nini haswa cha kuwashinda viongozi wengine waafrika waliopata kutokea na waliofanya mengi ya kuwahusu waafrika, nikawa nahisi si bure ni zawadi ya wa Magharibi walioyompatia baada ya kuwardhisha. na wengi wetu waafrika tumekwuwa "brain washed" na hata kuwasahau viongozi wetu mashuhuri waliopita e.g kwame Nkurumah

na leo saa 3usiku nimesikia maoni ya mchambuzi mmoja alikuwa kwenye kipindi cha bbc swahili kinachorushwa na star tv akichagiza kwamba Mandela alikuwa ni maarufu zaidi Magharibi kuliko hata Afrika, sababu baada ya kutoka gerezani aliwapa wazungu kilie walichokitaka. akaongeza na kuna kipindi alipotoka gerezani ANC iligawanyika wale waliotaka mabadiliko makubwa na wale waliokuwa laini kwa wazungu akina Mandela, Thabo Mbeki n.k

huyo mchambuzi akaongeza;

......Mandela ameondoka na ametutoka na lakini mfumo wa ubaguzi aliouacha ni uleule wa ubaguzi

.......umaskini afrika kusini kwa waafrika kusini ni uleule na bado sana kuuondoa.

.......waliofaidika ni wa wale wa chama chake cha ANC waliokuwa na msimamo laini dhidi ya mabadiliko ya kweli na ambao wamekuwa matajiri wa kutupwa sana na waafrika kusini wengi wakiwa maskini.

wazungu/makaburu ni kama waliingia naye mkataba wamuachie huru, then wampe urais , lakini kusameheana ni lazima.

watakuja watu na mapovu yao hapa na kusema hakuna kama Madiba na wala hawana point za kusema anawazidi akina Kwame Nkuruma, Jk Nyerere n.k

watashupalia ooh Mdiba kafanya Menigi sana;-

eti kafuta ubaguzi wa rangi..... hivi ni kweli kafuta ubaguzi wa rangi au makaburu waliona tu waachane na sera ya apartheid baada ya kusoma alama za nyakati??

......kingine alichofanya ni kuwasemhe wazungu,,,,, hivyo viwili ndio alivyofanya vya kuwa praise kiasi hiki???

......au kukaa jela kwa miaka 27 ndio ishu kubwa sana,,,,,,

Mtu ukimfanyia makosa makubwa harafu akasamehe utampenda zaidi, lakn mapenzi hayo sio ya dhati ni majikombo kwa muhusika ili asije kumbushia madhira na madhara ulompatia hapo awali. Kwenye biblia imeandikwa mtu anayesahemewa deni kubwa huwa karibu zaidi na msamehe deni kuliko aliyesamehewa hela ya mboga.

Mandela ni mvumilivu kwel kweli, alisamehe deni kubwa na kusahau madhara yaliyosababishwa na watesi wa waafrika. Pengine ndo ilikuwa njia sahihi kwa wanyonge kutoweka ligi na wenye mabavu, atakumbukwa kwa hilo mchana ama usiku. Kweli mandela hakutaka kuwaoesha wazungu makosa yao, aliwafundisha kuwa wanaweza kupuuzwa kwa yale waliofanya. Alisamehe wazungu kirahisi kuliko hata weusi, alishindwa kumsamehe Winnie ambaye kama binadamu n baada ya Mzee kuwa jela miaka 27 alibanjuka na Dali Mpofu, ambaye alikuwa Mwanasheria wao.

Swali linalobaki kuwa nyeti sana na ambalo ningependa kuliongelea ni umaarufu ambao mandela alitunukiwa baada ya kushindwa kutoa hukumu ya haki kwa wazungu kwa makosa waliyoyafanya kwa makusudi, maana hawajafanya mara moja wala mbili, wala hakufanya mzungu mmoja wala wawili tuseme ilitokea bahati mbaya ktk maisha. Ghafla kama ilivyo ktk mikakati ya wazungu ktk kutoa kile kinaitwa elimu, walimbeba Mandela juu ya vongozi wote wa afrika juu ya kila mtu kama kwamba mandela alisaidia ukombozi wa Africa, kushinda aliyestahili tuzo hiyo Mwalimu Nyerere, Nyerere hakupendwa sana na wazungu maana aliwapinga waziwazi na kukemea vitendo vyao, aliyekosa nyerere kinyume na mandela amlipa adhabu yake. Mandela ukiacha S. Africa ambako kwa dhati kabisa anahitajika kuitwababa wa taifa, hakuna tena nchi ya afrika ambayo alitoa mchango wake.

Ukiwapinga wazungu unakuwa adui, kama ilivyo kwa Nyerere, Mugabe tunaona anapendwa sana ispokuwa ghafla anakuwa mbaya saaana baada tu ya kupinga wazungu kumiliki ardhi kubwa mno Zimbabwe. Gadafi alipotaka kuonesha nji kwa waafrika aliuawa na hawa hawa wazungu, tena juzi tu, kama kusamehe ni dili mbona hajaachwa, OSAMA mbona hakusamehewa? Kusamehe asamehewe mzungu sifa kibao.

Wasiwasi wangu Heshima anayopewa Mandela isije kuwa ni hongo kwa vile alivyosaliti weusi kwa kutotoa adhabu kwa makosa makubwa ya wazungu, sijui kama kutotoa adhabu ni sahihi, dunia inaangamia kwa watu wema kushindwa kuwakataza watu waovu, kushindwa kutoa adhabu stahiki kwa makosa kunawezajenga picha mbaya sana. kwa hili japo mandela ni baba afrika kusini sio baba afrika wala kwamaoni yangu hakaribii hata kwa nusu mchango wa Nyerere ambaye anasthili kuitwa baba wa afrika.

Mitego iko mingi huu nao ni mtego kwa mwafrika, lazima tuung'amue. Tumehongwa pesa, madaraka leo hata sifa tunahongwa tunafumbia macho ukweli. Kama ilivyo kwa elimu, pesa na wakati/muda hakuna mwafrika anayejua vyote hivyo zimetoka wapi, lakn tunatumia tu, madhara ya kuwa watumiaji tu ni kutambulika kama wajinga mbele ya mzungu (Biology, Chemistry Physics, Maths nani aliamua ziwe zilivyo), kutambulika kama masikini mbele ya mzungu maana ndo mwenyehela (kumbuka hoja za Muhongo jana Nkrumah Hall), kutambulika kama watu wasijali muda there is no hurry in Africa. Ukweli hatujui nani alileta vitu hivi kwa faida ya nani?

Japo sio vema sana kuwalinganisha marafiki hawa lakni ifahamike, Nyerere kakopwa sifa zake na kupewa Mandela kwa faida ya Wazungu.

Nawasilisha
 
issue hapo mimi naona kukaa jela miaka yote hiyo, na si vinginevyo , kama ni umaarufu wa umoja ambao wazungu hawaupendi basi nyerere na nkurumah wangeongoza , lakini huyu bwana kwa kukaa kwake magereza ametia fora, wacha tumsifie kwa uvumilivu wake
 
meza ukweli mchungu.
au sema ni lipi haswaa amelifanya kustaili praise zoote hizo kuwazidi hao mahsuhuri wengine viongozi wa Afrika.
Mleta maada shenzi zako tunaomboleza unaleta siasa
 
mtoa mada ulianza darasa la kwanza mwaka gani..???na ulikua na miaka mingapi?
 
Mleta maada shenzi zako tunaomboleza unaleta siasa

Nilipata wasaa wa kutembelea gereza la Robben Island, na arrangement tu zilikuwa zinatoa picha kuwa Mandela hakuwa threat kubwa kwa Makaburu na kuna uwezekano mkubwa kuwa umaarufu wa Mandela ulitengenezwa ili kuwafunika weusi wenye misimamo mikali kupata umaarufu zaidi miongoni mwa umma wa Afrika Kusini.

Wakati Mandela alikuwa kwenye bweni pamoja na viongozi wenzake na akiwa na nafasi ya kuonana na wafungwa wengine wa kisiasa waliokuwepo gerezani hapo na kuongea,kufundishana na kubadilishana mawazo, Prof Robert Mangaliso Sobukwe aliwekwa kwenye nyumba maalumu iliyotengwa mbali kabisa na walipowekwa wafungwa wengine,peke yake chini ya ulinzi mkali na wa kipekee gerezani pale ili asipate chance ya kuonana na mfungwa mwingine yeyote.

Lengo kuu likiwa ni kuzuia itikadi zake kali zisiwaingie wafungwa wengine,wakiamini kuwa akionana nao ataweza kuwashawishi wafungwa wengine wafuate itikadi zake,hasa wakihofia hatima yao (weupe) ndani ya Afrika Kusini.

Hivyo yawezekana umaarufu wa Mandela ulikuwa overrated sio kwa sababu ni kibaraka bali kwa sababu alikuwa mlaini sana kwa Wazungu,na walijua hana impact kwao.

RIP Mandela,RIP My Hero Robert Mangaliso Sobukwe.
 
mtoa mada ulianza darasa la kwanza mwaka gani..???na ulikua na miaka mingapi?

Kwanini unang'ang'ania kufikiri ndani boksi? hebu toka nje kwanza, eenh vizuri dogo! haya sasa upo nje ya boksi fikiri upya naamini utakuja na komenti sahihi. Mimi naungana na mleta mada kuna uwezekano mkubwa Mzee Madiba aliingia mkataba wa siri kati yake na wazungu wachache ili wamtoe gerezani then akiupata urais wasamehane, uwezekano huo ni mkubwa sana.
 
issue hapo mimi naona kukaa jela miaka yote hiyo, na si vinginevyo , kama ni umaarufu wa umoja ambao wazungu hawaupendi basi nyerere na nkurumah wangeongoza , lakini huyu bwana kwa kukaa kwake magereza ametia fora, wacha tumsifie kwa uvumilivu wake

Waliokaa jela ni wengi na hawajapewa heshima. Mbona Mugabe kakaa sana jela pia lakini hakuna watu wengi Africa wanaomshabikia? Kataa usikatae, lakini Madiba ni wa aina yake na siamini kuwa tutamuona tena mtu wa aina yake
 
Nilipata wasaa wa kutembelea gereza la Robben Island, na arrangement tu zilikuwa zinatoa picha kuwa Mandela hakuwa threat kubwa kwa Makaburu na kuna uwezekano mkubwa kuwa umaarufu wa Mandela ulitengenezwa ili kumfunika Robert Mangaliso Sobukwe aliyekuwa mwiba mkali sana kwa makaburi enzi hizo.


Wakati Mandela alikuwa kwenye bweni pamoja na viongozi wenzake na akiwa na nafasi ya kuonana na wafungwa wengine wa kisiasa waliokuwepo gerezani hapo na kuongea,kufundishana na kubadilishana mawazo, Robert Mangaliso Sobukwe aliwekwa kwenye nyuba maalumu iliyotengwa mbali kabisa na walipowekwa wafungwa wengine,peke yake ili asipate chance ya kuonana na mfungwa yeyote.Lengo kuu likiwa ni kuzuia itikadi zake kali zisiwaingie wafungwa wengine,kwa hofu kuwa ingekuwa ni hatari kwa hatima za weupe Afrika Kusini.

RIP Mandela,RIP My Hero Robert Mangaliso Sobukwe.

wale waliokuwa hatari walikuwa asasinated, akina steve biko etc

habari zinasema kabla ya Mandela kuachiwa alihamishwa gereza la Robbin na kupelekwa gereza la pollsmoor akapewa sehemu yenye nafasi zaid, kama vile nyumba ya peke yake, hadi sehemu ya kupokelea wageni ilikuwepo. hapo ndipo walizidi kumalainisha zaidi.
 
Waliokaa jela ni wengi na hawajapewa heshima. Mbona Mugabe kakaa sana jela pia lakini hakuna watu wengi Africa wanaomshabikia? Kataa usikatae, lakini Madiba ni wa aina yake na siamini kuwa tutamuona tena mtu wa aina yake
kafanya nini hicho cha aina yake alichostahili kuwa juu hivi kuliko akina Nkurumah???? ebu tujuze!! au upo brainwashed tu na vyombo vya habari vya magharibi??
 
kuna ukweli uliyosema sababu ata mi numeshangaa waliokuwa wanamuita gaidi sasa hivi wanamuita shujaa. nimeweka nakala nzuri jukwaa la kimataifa kuhusiana na mandela kuitwa gaidi
 
Interiors zinasema alikuwa na nia kubwa ya kutaifisha assets kubwa zilizokuwa zikimilikiwa na makaburu wakamwabmia ajaribu aone kama hawajatimka wakaharibu uchumi kama walivyomfanyia Mugabe.

wengine wanasema kutoka kwake gerezani ni influence kubwa ya kugomea bidhaa nyingi na huduma kama za barclays bank kwa wananchi wengi ndipo wakamtoa ili kunusuru uchumi,

mengi yanaongelewa ila ni mtu wa tofauti bado.
 
kuna ukweli uliyosema sababu ata mi numeshangaa waliokuwa wanamuita gaidi sasa hivi wanamuita shujaa. nimeweka nakala nzuri jukwaa la kimataifa kuhusiana na mandela kuitwa gaidi
aliwapa walichokitaka.
 
Kwa kusamehe watesi wake; Nelson Rolihlahla Mandela (Madiba) alijiwekea hazina Duniani na Mbinguni, Lakini Sifa zoote hizi hasa toka ulimwengu wa magharibi hazilengi nadharia hii. Bali sifa hizi zinalenga kukarimu ubepari wao ambao haukuathirika kwa kuachiwa kwake.
Ieleweke kuwa mataifa makubwa ya magharibi yaliwekeza kwa kiasi kikubwa Africa ya kusini hasa kwenye Migodi na mashamba kupitia ubia na makaburu hivyo mandela alipoachiwa na De Clack waliamini utakuwa ni mwisho wa uwekezaji wao na kwamba angetaifisha mali zao, badala yake hakufanya hivyo na hilo kwao ikawa ahueni na kwamba roho zao zikawa kwatu na hata kujuta kwa nini walimhofia wakatisio sio tishio kwa uchumi wao.
 
Mtu ukimfanyia makosa makubwa harafu akasamehe utampenda zaidi, lakn mapenzi hayo sio ya dhati ni majikombo kwa muhusika ili asije kumbushia madhira na madhara ulompatia hapo awali. Kwenye biblia imeandikwa mtu anayesahemewa deni kubwa huwa karibu zaidi na msamehe deni kuliko aliyesamehewa hela ya mboga.

Mandela ni mvumilivu kwel kweli, alisamehe deni kubwa na kusahau madhara yaliyosababishwa na watesi wa waafrika. Pengine ndo ilikuwa njia sahihi kwa wanyonge kutoweka ligi na wenye mabavu, atakumbukwa kwa hilo mchana ama usiku. Kweli mandela hakutaka kuwaoesha wazungu makosa yao, aliwafundisha kuwa wanaweza kupuuzwa kwa yale waliofanya. Alisamehe wazungu kirahisi kuliko hata weusi, alishindwa kumsamehe Winnie ambaye kama binadamu n baada ya Mzee kuwa jela miaka 27 alibanjuka na Dali Mpofu, ambaye alikuwa Mwanasheria wao.

Swali linalobaki kuwa nyeti sana na ambalo ningependa kuliongelea ni umaarufu ambao mandela alitunukiwa baada ya kushindwa kutoa hukumu ya haki kwa wazungu kwa makosa waliyoyafanya kwa makusudi, maana hawajafanya mara moja wala mbili, wala hakufanya mzungu mmoja wala wawili tuseme ilitokea bahati mbaya ktk maisha. Ghafla kama ilivyo ktk mikakati ya wazungu ktk kutoa kile kinaitwa elimu, walimbeba Mandela juu ya vongozi wote wa afrika juu ya kila mtu kama kwamba mandela alisaidia ukombozi wa Africa, kushinda aliyestahili tuzo hiyo Mwalimu Nyerere, Nyerere hakupendwa sana na wazungu maana aliwapinga waziwazi na kukemea vitendo vyao, aliyekosa nyerere kinyume na mandela amlipa adhabu yake. Mandela ukiacha S. Africa ambako kwa dhati kabisa anahitajika kuitwababa wa taifa, hakuna tena nchi ya afrika ambayo alitoa mchango wake.

Ukiwapinga wazungu unakuwa adui, kama ilivyo kwa Nyerere, Mugabe tunaona anapendwa sana ispokuwa ghafla anakuwa mbaya saaana baada tu ya kupinga wazungu kumiliki ardhi kubwa mno Zimbabwe. Gadafi alipotaka kuonesha nji kwa waafrika aliuawa na hawa hawa wazungu, tena juzi tu, kama kusamehe ni dili mbona hajaachwa, OSAMA mbona hakusamehewa? Kusamehe asamehewe mzungu sifa kibao.

Wasiwasi wangu Heshima anayopewa Mandela isije kuwa ni hongo kwa vile alivyosaliti weusi kwa kutotoa adhabu kwa makosa makubwa ya wazungu, sijui kama kutotoa adhabu ni sahihi, dunia inaangamia kwa watu wema kushindwa kuwakataza watu waovu, kushindwa kutoa adhabu stahiki kwa makosa kunawezajenga picha mbaya sana. kwa hili japo mandela ni baba afrika kusini sio baba afrika wala kwamaoni yangu hakaribii hata kwa nusu mchango wa Nyerere ambaye anasthili kuitwa baba wa afrika.

Mitego iko mingi huu nao ni mtego kwa mwafrika, lazima tuung'amue. Tumehongwa pesa, madaraka leo hata sifa tunahongwa tunafumbia macho ukweli. Kama ilivyo kwa elimu, pesa na wakati/muda hakuna mwafrika anayejua vyote hivyo zimetoka wapi, lakn tunatumia tu, madhara ya kuwa watumiaji tu ni kutambulika kama wajinga mbele ya mzungu (Biology, Chemistry Physics, Maths nani aliamua ziwe zilivyo), kutambulika kama masikini mbele ya mzungu maana ndo mwenyehela (kumbuka hoja za Muhongo jana Nkrumah Hall), kutambulika kama watu wasijali muda there is no hurry in Africa. Ukweli hatujui nani alileta vitu hivi kwa faida ya nani?

Japo sio vema sana kuwalinganisha marafiki hawa lakni ifahamike, Nyerere kakopwa sifa zake na kupewa Mandela kwa faida ya Wazungu.

Nawasilisha
 
Truly, well written and narrated , food for thought

nakubaliana na wewe,

wazungu waachaeni tu, Zuma leo anadharau nchi zingine za afrika, waafrika kusini weusi hawapendi wageni, South afika semeni yote msemayo.......hawako close na hawana undugu na nchi zingine za afrika
 
Back
Top Bottom