Uliza chochote kuhusu Karagwe na Wanyambo wanaopatikana mkoa wa Kagera

je wanyambo ni wakimbiz

Mkuu,ndio maana kuna kila sababu ya watu kuachana na ubaguzi wa kijinga kijinga.
Nasema hivyo kwa sababu moja: watu walio wengi wanajua ukanda huo wa wanyarwanda.Lakini hayo makabila mnayoyaongelea,ukienda Rwanda utaambiwa enzi za utawala wa kifalme maeneo hayo yalikuwa ya Rwanda,ndo maana wanafanana.Lakini swali la kujiuliza,wanyarwanda wana sura za kipekee? Ukienda Uganda,hao hao wataitwa wanyankole.Na huko utaambiwa hivo hivo. Sasa najiuliza,kwa nini badhi watambuliwe kama watanzania,wengine wafukuzwe? Na kama ungefika kambini ukaona wanavyohangaika,hawana ndugu hata mmoja,ndo ungegundua kwamba kuhukumu mtu kwa sura ni kosa kubwa.Kuna haja watu wakaweka utu mbele kwanza kuliko chuki binafsi.Mfano ukiulizwa wajaluo na wamasai kabila gani siyo watanzania utajibu lipi?
Kwa hiyo siamini kama ni wakimbizi kweli kwa sababu wamekuwepo toka enzi.Af kumbuka wanavozaliana na kuoana na wale mnaowaita watanzania halisi,kitatokea kitu gani?
 
Je kati ya Wanyambo na Wahaya nani anajua kupika rubisi? Na nani mtaalam wa senene?

Na kwenye lugha je Kinyambo na Kihaya vinafanana?
 
Jodoki Kalimilo, Maisha siku zote ndivyo yalivyo,unaenda sehemu ambazo hata hukutarajia kufika,BTW najua ulipata kuona ukarimu wa watu wa Karagwe na kwa namna moja au nyingine kuna jambo ulijifunza.
Nilishtuka Sana kukuta magodoro yanga nailoni kwenye lodge nyingi,je hutengenezwa huko au ni spesho order kutoka kiwandani?
 
Labda kama utakuwa unaongea bila kujua historia ya kabila la Wanyambo. Lakini ungekuwa unawajua usingedhubutu kusema wamemezwa na wahaya. Kawaida Wahaya uwa wanapenda kuwaita Wanyambo Wahaya bila kujua au historia yao au katika kujikuza kwa wahaya na kufikiri mkoa wa Kagera ni wao peke yao.
Pia wengine uwa wanawaita wahaya labda kwa sababu ya kushabihiana kwa lugha japo ni tofauti ni tofauti kimatashi na rafudhi na baadhi ya maneno ambayo ya kinyambo huwezi kuyakuta kwenye kihaya na ya kihaya huwezi kuyakuta kwenye kinyambo:
Kwa ufupi huu ndio utawala wa wa Karagwe (Karagwe Kingdom):
1675 - 1700 Ruhinda V
1700 - 1725 Rusatira
1725 - 1750 Mehinga
1750 - 1775 Kalemera I Ntagara Bwiragenda (alifariki 1775)
1775 - 1795 Ntare V "Kiitabanyoro"
1795 - 1820 Ruhinda VI Orushongo "Lwanyabugondo" (b. 1777 - d. 1820)
1820 - 1853 Ndagara I "Luzingamcucu lwa nkwanzi"
1853 - 1881 Rumanyika I Rugundu
1882 - 1886 Ndagara II Nyamkuba
1886 - 1893 Kalemera II Kanyenje
1886 - 1893 Kakoko -Regent
1893 - 1914 Ntare VI
1914 - 1916 Kahigi -Regent
1916 - 1939 Daudi Rumanyika II
1939 - 1962 - 9.12. B. Itogo Ruhinda VII
Kwa hiyo unaweza kuona si utawala wa jana na si utawala wa kumezwa na wahaya kama unavyodhani.
Jina Karagwe inasemekana lilitokana na simulizi za wazee mbalimbali na watafiti wa historia ya Karagwe, eti jina linatokana na Kilima (ziwa kitete) kinachopatikana kusini magharibi mwa makao makuu ya wilaya hii, kijiji cha kandegesho katika tarafa ya Nyabiyonza. Kwa Omukama (nono ya malija yaani ukoo wa abhasita)

Kuhusu Wanyambo wanasema walitokana na kizazi cha Kanyambo mtoto wa Ruhanga (Mungu) ambaye alitumwa kuanzisha nchi ya Karagwe toka Bunyoro, lakini watu husema kuwa nchini Uganda kuna mababu zao waliozaliwa kutoka Karagwe na zipo aina za ndizi asilia inaitwa enyambo na ng'ombe asilia wenye pembe fupi aitwaye Ente ye Nyambo, lakini ukitazama kwa umakini sana Kinyambo kinashabihana na Kinyakole na wala siyo Kihaya.
Mvumbuzi Speke, hakuwa na lengo la kwenda Karagwe, lakini alipokuwa njiani kwenda Maziwa Makuu, alipata habari za “Umugabe” wa Karagwe, aliyejulikana kama Rumanyika, aliyekuwa akiwatawala watu wake vizuri na alikuwa mstaarabu. Alivutiwa na maelezo hayo na kuamua kwenda kumtembelea.

Alishangazwa na maendeleo yaliyokuwa Karagwe enzi hizo; kijiji kinachojulikana kwa jina la Kafuro kule Bushangaro Karagwe, kilikuwa ni mji wa kisasa, ambao Speke aliulinganisha na Tabora na Ujiji. Wanyambo walitengeneza pombe tamu na kali ambayo Wazaramo waliokuwa wanabeba mizigo ya Speke walikunywa hadi wakashindwa kutembea.

Ingaasnte kwa kuwa nyumba za Rumanyika zilikuwa ni za nyasi, lakini Speke, anaelezea usafi wa hali ya juu uliokuwa kwenye nyumba hizo. Pia Rumanyika, alikuwa na jumba la makumbusho, ambalo lilitunza vitu vya zamani vilivyokuwa vimetengenezwa na watawala waliokuwa wamemtangulia.
Wanyambo ni wakarimu, hawana unafiki – hawazungumzi kwa mafumbo kama ndugu zao Wahaya; wakichukia wanaonyesha wazi na wakifurahi wanaonyesha wazi.

Kwa machache haya nadhani utakuwa umeondokana na dhana uliyokuwa nayo ya kuambiwa
Nimeshukuru kwa hii taarifa yako, ila ningekuomba sana tuwasiliane maana mm asili yangu imekuwa na utata kidogo! Mimi ni omuganga na Babu yetu alitokeya Karagwe akiwa ni askari wa wajerumani na huko Rwanda amewaza mababa zetu kutokana na mama wa kinyarwanda. Na hii imepelekeya sisi wajukuu kuyipoteza asili yetu na lugha ya asili. Basi namba yangu ni (+49)15215156891 (WhatsApp)
 
Sirika na hulka ya wakazi wa mkoa wa Kagera hasa wenyeji wa Mureba na Kiziba hawana utamaduni wa kuendekeza kabila wao utambuana kwa koo zao
Hivyo ukiwaangalia hao watemi wa karagwe wengi walitokea ktk ukoo wa Bashambo bamporolo
Hii jamii ipo maeneo yote ya Uganda, Rwanda, Congo. Na baadhi ya maeneo ya mkoa wa Tabora

Kujinasbisha na Unyambo hakuwatoi wanyambo katika Jamii ya Washambo ambao ni Watutsi

Hawezi kuwagawa wanyambo kwa histori tu
Mimi ni omuganga (omushambo). Je kunayeyote ambaye anataarifa kuwahusu clan hii niliyoitaja hapo juu? Basi ninawaombeni maelezo zaidi kuhusiyana nao na iwapo kuna ndugu zangu waganga ninahitaji ufafanuzi zaidi jamani. Asanteni
 
Hii ni nzuri, angalau imefanya uchambuzi wa kina kuhusu Karagwe. SISI Abakaraza ba Kasheshe tulikuwa karibu sana na Omukama Rumanyika hasa kwenye kutoa miongozo ya utawala. Babu zetu walikuwa watumishi wao wa karibu. Binafsi nimemwona na kumshuhudia omukama wa mwisho bwana Cosmas Rumanyika (Marehemu) alifika nyumbani miaka ya mwisho ya 80 kuonana na babu yetu Mzee Zakariah Kajungu, babake Balozi Andrew Tibandebage Kajungu, ili kupewa abcs za kuendesha uchifu. Nakumbuka tulim-host pale nyumbani kwa usikummoja na wakati akiondoka tulimbebea handbag yake nzuri ya ngozi lainii ambayo alitulezea kuwa imekuwa ikirithishwa toka kizazi kinoja hadi kingine ikiwa ni moja ya zawadi zilizotolewa na kina Morton Henry Stanley walipomtembelea Omukama Rumanyika miaka hiyooo...
very interesting. Nimeandika kuhusu abakaraza clan pia ambao ndio ukoo wetu...
 
Kwanza kabla sijakuuliza swali langu, nikuombe radhi mkuu Chachu Ombara maana siulizi kwa nia mbaya pia nakuheshimu.
Swali langu: HIVI KWANINI WANYAMBO WENGI NI WACHOYO, WABINAFSI, ROHO MBAYA, WAROHO yaani wamezidi wazaliwa wengine wa mkoa wa Kagera.
Hiki kitu huwa najiuliza sana. Kuna dada tulisoma naye undergraduate yaani alikuwa mchoyo balaa yaani nihivi hata kwenye group discussion akiona mnaingia chaka anaona uchoyo kuwashirikisha ukweli anaojua yeye.
Sehemu mbalimbali nilizopita wanyambo wote niliowaona nakuwa nao karibu ni wachoyo, wabinafsi, waroho. Akiona wewe unakitu ambacho anakihitaji atakushupalia hadi apate lakini vya kwake Mungu wangu! uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Back
Top Bottom