Uliyempigia Kura Magufuli mwaka 2015, ulipenda kipi kwake baadae ukagundua siyo? Na ulomnyima ulichukia nini kwake baadae ukagundua siyo?

Ukweli ni kwamba uchaguzi wa 2015 haukuwa na mgombea urais mzuri; si Lowassa wala Magufuli. Kama ali yosema Mzee Ruksa kwamba wagombea wote ni wa CCM bali wao (UKAWA) wana CCM B na sisi CCM tuna CCM A.

Binafsi ilinilazimu kumpigia kura Magufuli sio kwasababu nilikuwa na matumaini angekuwa rais bora, bali kutokana na kukosa mgombea sahihi kwa upande wa UKAWA. Bali nilimchagua Magufuli kutokana na hasira za maamuzi ya msaliti Mbowe ya kubadili gia angani.

Tofauti na watu wengine, mimi nilimkataa Lowassa si kwasababu ya tuhuma ya ufisadi wa Richmond juu yake. Sikumkubali Lowassa kutokana na mambo yafuatayo.

1. Aliutamani na kuupania urais kiasi cha kuogofya.
2. Lowassa aliamini urais baada ya JK ni haki yake yeye peke yake.
3. Alianza kufanya harakati za "nguvu" (safari ya matumaini) za "kuufukuzia" urais mara tu baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu kana kwamba alitaka kuutumia urais kulipiza kisasi kwa wale waliopelekea ajiuzulu.
4. Aligeuza kashfa ya Richmond kuwa mtaji wa kujipatia huruma ya wananchi katika kuendeleza harakati za Safari ya Matumaini.
5.Aliuaminisha umma kuwa kujiuzulu kwake ni matokeo ya fitna dhidi yeke kutokana na uwaziri mkuu wake na si kutokana na kuhusika kwake na upendeleo wake kwa kampuni ya kitapeli ya Richmond katika zabuni za TANESCO.
6. Alifanya "mchezo" aonekane anapendwa na wananchi kwa kuandaa makundi mbali mbali ya watu wa "kumshawishi" ajaze fomu wakati mwenyewe alishapania awe rais.
7. Alifanya hira kuwakwamisha wagombea wenzie ndani ya chama wakose wazamini kwa "kuwatekaka" viongozi wa chama wa wilaya na mikoa na "kukomba" wazimini wengi zaidi ya idadi iliyotakiwa.
8. Alizunguka nchi nzima kuandikisha na kufanya mikutano mikubwa ya hadhara kwa ajili ya kuandikisha wazamini. Badala ya wazamini 30, aliandikisha zaidi ya makumi elfu katika mkoa mmoja.
9. Ziara zake za kutafuta wazamini ilikuwa ni zaidi ya kampeni na zilitumia magari mengi ya msafara kana kwamba tayari alishakuwa rais. Alitumia rasilimali nyingi kwa ajili na kufanya mkutano mkubwa wa hadhara kwa ajili ya kutangaza nia
10. Yote tisa, kumi alitumia walinzi wa chama kumpiga na kumdhalilisha mgombea mwenzie ndani ya chama Dr. Kalokola katika mkutano wake wa kutafuta wazamini Tanga mjini.
11. Alipohamia CHADEMA ni wazi ilionekana hakuwa na mapenzi ya dhati na chama hicho na UKAWA, bali alifanya uwamuzi huo ili apate jukwaa la kupata urais alioupania.
12. Hakuwa tayari kushindanishwa na wenzie kwa utaratibu uliokuwa umepangwa wa kumpata mgombea wa kuwakilisha UKAWA, bali aliendeleza matakwa yake kuwa urais baada ya JK ni haki yake yeye tu.

Mbinu, hira na njama zilizotumiwa na Lowassa kuuendea urais zilinifanya nimchukie Lowassa. Bali zilinifanya niwe na mashaka naye nikijiuliza kwanini alipania kwa gharama yoyote awe rais.
Tumefanana
 
Tumefanana
Hapana! Hatufanani! Wewe ulimchagua Magufuli kwa dhana kuwa angefaa na matokeo yake ikawa sivyo, wakati mimi nilimchagua nikijua kuwa hawezi kuwa rais bora.

Nilimpa kura yangu kwavile tu hakufanya hira na kukiuka mipaka dhidi ya wagombea wenzie bali yeye alikuwa mnyonge na miongoni mwa wahanga wa hira za Lowassa.

Ingawa kabla ya urais nilikuwa na mtazamo "neutral" juu yake, sasa hivi namchukia kwavile si mnyonge tena bali yeye ndo anafanya hira na kuwakamia wapinzani wake na wananchi kwa ujumla. Anajiita yeye ni Jiwe na Kichaa ambaye hapangiwi cha kufanya.
 
Hapana! Hatufanani! Wewe ulimchagua Magufuli kwa dhana kuwa angefaa na matokeo yake ikawa sivyo, wakati mimi nilimchagua nikijua kuwa hawezi kuwa rais bora.

Nilimpa kura yangu kwavile tu hakufanya hira na kukuika mipaka dhidi ya wagombea wenzie bali yeye alikuwa mnyonge na miongoni mwa wahanga wa hira za Lowassa.
Waziri zaidi ya miaka ishirini eti unamuita mnyonge,unafiki na kujipendekeza kutakumaliza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waziri zaidi ya miaka ishirini eti unamuita mnyonge,unafiki na kujipendekeza kutakumaliza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Rudia kusoma nilichoandika na utaelewa kuwa nimemuita mnyonge kwa kulinganisha nguvu yake na ile ya Lowassa ndani ya chama.

Lakini zaidi ya ubunge/uwaziri Magufuli alikuwa na nguvu/nafasi gani ndani ya ccm? Hivi hujui kuwa aliukwaa urais si kwa mbinu/nguvu zake mwenyewe bali ni kutokana na kubebwa na nguvu za viongozi wa juu wa chama? Hivi hujawahi kumsikia mwenyewe anakiri kama si JK asingetoboa?

Kwa taarifa yako Magufuli angeshindanishwa na January Makamba katika "tatu bora" asingepenya. Tumuiteje kama sio mnyonge? Acha kufanyana wanafiki wakati watu wazima tunaojitambua
 
Kwa hio kwenye hio nafasi ya urais alisukumizwa na wakina JK (hakua amejipanga kama anavyosema mwenyewe) sio?
Rudia kusoma nilichoandika na utaelewa kuwa nimemuita mnyonge kwa kulinganisha nguvu yake na ile ya Lowassa ndani ya chama.

Lakini zaidi ya ubunge/uwaziri Magufuli alikuwa na nguvu/nafasi gani ndani ya ccm? Hivi hujui kuwa aliukwaa urais si kwa mbinu/nguvu zake mwenyewe bali ni kutokana na kubebwa na nguvu za viongozi wa juu wa chama? Hivi hujawahi kumsikia mwenyewe anakiri kama si JK asingetoboa?

Kwa taarifa yako Magufuli angeshindanishwa na January Makamba katika "tatu bora" asingepenya. Tumuiteje kama sio mnyonge? Acha kufanyana wanafiki wakati watu wazima tunaojitambua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuna Mategemeo Kibao kila ziliapo kengele za Kuanza mchakato wa kampeni za Uchaguzi mkuu kitaifa!

Kilichonivutia kwa Magufuli
1.Jinsi ya Kusimamia anayoyaamini hasa kwa wale wanaokwamisha maendeleo

Nikasahau kwamba kumbe kuna ambayo naye anakuwa kinyuma hivyo inabidi asikilize washauri duh kumbe yakaanza ya sipangiwi na mtu , ikaleta SIMPLE DICTATORSHIP IN TANZANIA

2.Nilikutana na Magufuli mara kadhaa alionekana ni MTU anayeumizwa mno na kunyanyasika kwa watanzania hasa wasio na vyeo,

Lakin baada ya Urais nikajua sikufikilia vyema maana angekuwa hivyo mama yake Eriki asingekuwa Amalia vile

3.Mimi kusema Ukweli nilimpenda kwa kuchukia Rushwa sana, hasa akipita kwenye Mizani ya mabarabara

Baada ya Kuwa rais nikagundua kuwa yawezekana sikufikiria vema, maana Masuala ya Lugumi, Mizengwe ya Lukuvi kwenye ardh,
Tuhuma kwa Makonda dhidi ya mambo Mbali mbali na akakausha kama asikiii, mbaya zaidi akajionea mpaka makontena Bandarini lakin ameendelea kumkumbatia

4.Alivyokuwa anasoma UDSm watu wakiandamana kudai mikopo anasikitika sana na kusema utaratibu si mzuri tukadhani tukimpata huyu itakuwa powa

Baada ya Urais yamekuwa mengine na wengine wamefukuzwa juzi

5.Alivyokuwa waziri alitoa hotuba bila kusoma popote pale zilisisimua Sana hasa alivyokuwa akitaja Vipengele vya sheria na Km za Barabara ambazo hakukosa kutaja 7,7,7,7

Nikaja kugundua mambo mengi anayoongea kuna mambo si kweli kwa kufuatilia matamko na reference,


Je we Ulidhania nini kwake na ukakuta tofauti?

Pole The Sun-of-a Beach, kwa comment hii
My confession: Nasikitika kwamba nilimpigia kura, na nilikuwa nikigombana na wale waliokuwa 'wakimponda' na wengi wao niliwaona wajinga. MASKINI KUMBE MIMI NDO NILIKUWA MJINGA KWA KUMUUNGA MKONO MZEE WA CHATO. Will God forgive me? Oooh poor me!

1.Nilimpenda kwa kukemea rushwa, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka hadharani - my first encounter with him ilikuwa ni kwenye shule moja ya sekondari nikiwa mwanafunzi hapo. Jamaa akiwa NW wa Ujenzi alikuwa amealikwa kama mgeni rasmi kwenye graduation shuleni hapo. Basi, hotuba yake ilinifurahisha sana pale ' alipomchana live Headmaster' wa shule yangu hiyo kwa ubadhilifu/ kutumia pesa za shule kwa kuanzisha miradi ya shule bila idhini ya Bodi ya Shule. Sisi wanafunzi tulimshangilia mno mgeni rasmi JPM.

- Baada ya kura yangu, amekuja kufanya yale yale. Anaanzisha miradi bila idhini ya Bunge. Tena ambako CAG hawezi kukagua.

2.Akiwa Mbunge na Waziri, kuna wakati hata wabunge wa upinzani walikuwa wanamkubali. Ni Waziri ambaye alikutana na kashkashi kidogo sana kutoka kwa wabunge wa upinzani ukilinganisha na waliokuwa Mawaziri wenzake (kama Karamagi, Mustafa Mkulo, PM Pinda) na hata Rais Kikwete mwenyewe. Na hata kwenye kampeni za Urais 2015 wapinzani wala hawakumshambulia kiviiile ukilinganisha na mtangulizi wake.

- Aliponikera: Ni alipojenga bifu nzito dhidi ya upinzani baada ya kushinda Urais. Kuzuia mikutano halali ya vyama vya upinzani, kuwafungulia kesi za hovyo hovyo wapinzani, kuwateka, kuwatesa na hata 'kuwapoteza'. Mbona Mr.Smile (JK) ambaye alitukanwa na wapinzani kuliko Mr.Old Stone Man (JPM) yeye hakufanya hivyo? Why awamu ya 5 ifanye hivyo? Why?

3.Kwenye kampeni zake 2015 alisema atajali kilio cha muda mrefu cha watumishi wa umma; mishahara kiduchu, kutopandishwa madaraja kwa wakati, malimbikizo ya madai, kunyimwa ruhusa (likizo na masomo). Na kwamba kwakuwa yeye alikuwa Mwalimu na anazijua changamoto za Ualimu ataweka mambo sana.

- Kumbe alikuwa anaongea kinyume, kuongea kwake ni mithili ya mdudu aitwaye 'vingirisha mavi' huyu husafirisha mzigo wa mavi (hasa ya herbivores) huku akitembea kinyume nyume. Kuongea hivi halafu ukatenda vinginevyo huo ni unafiki. Jamaa ana roho mbaya kama mchawi. Hata hivyo, wachawi nao hutembea kinyumenyume wakiwa wanaingia kwenye nyumba ya mlengwa wao. Roho nyeusi!

He disappointed me, I'm going to disappoint him too. October 2020 is loading...hapati kura yangu.


Britanica
Hiyo dhambi ni mbaya sana kuliko dhambi ya kuua,jiwe ni fisadi kuliko awamu zote za chama cha majambazi,ndani ya miaka 4 kaiba kuliko ufisadi wa ben,jk.
Huko chato kajenga miradi mikubwa ambayo haina tija jana wamezindua soko la dhahabu wakti chato haina kitu.
Heri unyimwe pesa kuliko unyimwe akili kama jiwe


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hebu tuweke chuki na wivu pembeni! Hivi nisehem gani mh jpm alipokosea ktk miaka hii mitano kuacha mazuri! Badara ya kubaki kulaum bila ushahidi!
 
Hiyo dhambi ni mbaya sana kuliko dhambi ya kuua,jiwe ni fisadi kuliko awamu zote za chama cha majambazi,ndani ya miaka 4 kaiba kuliko ufisadi wa ben,jk.
Huko chato kajenga miradi mikubwa ambayo haina tija jana wamezindua soko la dhahabu wakti chato haina kitu.
Heri unyimwe pesa kuliko unyimwe akili kama jiwe


Sent using Jamii Forums mobile app
Ungeanza kuuliza kwanza badara yakuja na hoja km unauhakika wahiki ukisemacho! Nyie ndo wale wa bu7 kushinda jf kupotosha watanzania kwa v2 msivyovijua. SOKO HILO LA DHAHABU HALIPO CHATO KULE KWAO ISIPOKUWA LIPO BUSELE SELE ambayo ipo ndani ya wilaya ya chato. Busele sele nimpakani mwa wilaya ya geita na chato mkoa wa geita.

HOJA YA KUWA HAKUNA DHAHABU hii nayo inaonyesha ni wivu na uongo ukiwemo uzandiki ulopindukia kwakuwa ukanda ule wa chato kuna migodi hii ifuatayo .Buseresere,matabe, nyakafuru, lwamgasa, iparamasa, igwamanoni,mwazimba, pale chato kwao ile milima yte nidhahabu hata pale ilipo harmashauri ya wilaya Pale pote nimachimbo ya dhahabu kumbuka mh spika ndugai sikuile alisema alikuwa akipita njiani anaona viroba vya mifuko anauliza anaambiwa ni mawe ya dhahabu! Kwahiyo muwe na tahadhari kabla ya kuongea MKIKAMATWA MKASHTAKIWA MNASEMA UHURU WA KUONGEA kweli bora kuongoza punda kuliko watu, Jpm anavyosema urais ni mzigo mzigo nipamoja nawatu kama nyinyi.
 
Tuna Mategemeo Kibao kila ziliapo kengele za Kuanza mchakato wa kampeni za Uchaguzi mkuu kitaifa!

Kilichonivutia kwa Magufuli
1.Jinsi ya Kusimamia anayoyaamini hasa kwa wale wanaokwamisha maendeleo

Nikasahau kwamba kumbe kuna ambayo naye anakuwa kinyuma hivyo inabidi asikilize washauri duh kumbe yakaanza ya sipangiwi na mtu , ikaleta SIMPLE DICTATORSHIP IN TANZANIA

2.Nilikutana na Magufuli mara kadhaa alionekana ni MTU anayeumizwa mno na kunyanyasika kwa watanzania hasa wasio na vyeo,

Lakin baada ya Urais nikajua sikufikilia vyema maana angekuwa hivyo mama yake Eriki asingekuwa Amalia vile

3.Mimi kusema Ukweli nilimpenda kwa kuchukia Rushwa sana, hasa akipita kwenye Mizani ya mabarabara

Baada ya Kuwa rais nikagundua kuwa yawezekana sikufikiria vema, maana Masuala ya Lugumi, Mizengwe ya Lukuvi kwenye ardh,
Tuhuma kwa Makonda dhidi ya mambo Mbali mbali na akakausha kama asikiii, mbaya zaidi akajionea mpaka makontena Bandarini lakin ameendelea kumkumbatia

4.Alivyokuwa anasoma UDSm watu wakiandamana kudai mikopo anasikitika sana na kusema utaratibu si mzuri tukadhani tukimpata huyu itakuwa powa

Baada ya Urais yamekuwa mengine na wengine wamefukuzwa juzi

5.Alivyokuwa waziri alitoa hotuba bila kusoma popote pale zilisisimua Sana hasa alivyokuwa akitaja Vipengele vya sheria na Km za Barabara ambazo hakukosa kutaja 7,7,7,7

Nikaja kugundua mambo mengi anayoongea kuna mambo si kweli kwa kufuatilia matamko na reference,


Je we Ulidhania nini kwake na ukakuta tofauti?

Pole The Sun-of-a Beach, kwa comment hii
My confession: Nasikitika kwamba nilimpigia kura, na nilikuwa nikigombana na wale waliokuwa 'wakimponda' na wengi wao niliwaona wajinga. MASKINI KUMBE MIMI NDO NILIKUWA MJINGA KWA KUMUUNGA MKONO MZEE WA CHATO. Will God forgive me? Oooh poor me!

1.Nilimpenda kwa kukemea rushwa, ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka hadharani - my first encounter with him ilikuwa ni kwenye shule moja ya sekondari nikiwa mwanafunzi hapo. Jamaa akiwa NW wa Ujenzi alikuwa amealikwa kama mgeni rasmi kwenye graduation shuleni hapo. Basi, hotuba yake ilinifurahisha sana pale ' alipomchana live Headmaster' wa shule yangu hiyo kwa ubadhilifu/ kutumia pesa za shule kwa kuanzisha miradi ya shule bila idhini ya Bodi ya Shule. Sisi wanafunzi tulimshangilia mno mgeni rasmi JPM.

- Baada ya kura yangu, amekuja kufanya yale yale. Anaanzisha miradi bila idhini ya Bunge. Tena ambako CAG hawezi kukagua.

2.Akiwa Mbunge na Waziri, kuna wakati hata wabunge wa upinzani walikuwa wanamkubali. Ni Waziri ambaye alikutana na kashkashi kidogo sana kutoka kwa wabunge wa upinzani ukilinganisha na waliokuwa Mawaziri wenzake (kama Karamagi, Mustafa Mkulo, PM Pinda) na hata Rais Kikwete mwenyewe. Na hata kwenye kampeni za Urais 2015 wapinzani wala hawakumshambulia kiviiile ukilinganisha na mtangulizi wake.

- Aliponikera: Ni alipojenga bifu nzito dhidi ya upinzani baada ya kushinda Urais. Kuzuia mikutano halali ya vyama vya upinzani, kuwafungulia kesi za hovyo hovyo wapinzani, kuwateka, kuwatesa na hata 'kuwapoteza'. Mbona Mr.Smile (JK) ambaye alitukanwa na wapinzani kuliko Mr.Old Stone Man (JPM) yeye hakufanya hivyo? Why awamu ya 5 ifanye hivyo? Why?

3.Kwenye kampeni zake 2015 alisema atajali kilio cha muda mrefu cha watumishi wa umma; mishahara kiduchu, kutopandishwa madaraja kwa wakati, malimbikizo ya madai, kunyimwa ruhusa (likizo na masomo). Na kwamba kwakuwa yeye alikuwa Mwalimu na anazijua changamoto za Ualimu ataweka mambo sana.

- Kumbe alikuwa anaongea kinyume, kuongea kwake ni mithili ya mdudu aitwaye 'vingirisha mavi' huyu husafirisha mzigo wa mavi (hasa ya herbivores) huku akitembea kinyume nyume. Kuongea hivi halafu ukatenda vinginevyo huo ni unafiki. Jamaa ana roho mbaya kama mchawi. Hata hivyo, wachawi nao hutembea kinyumenyume wakiwa wanaingia kwenye nyumba ya mlengwa wao. Roho nyeusi!

He disappointed me, I'm going to disappoint him too. October 2020 is loading...hapati kura yangu.


Britanica
Sikumpigia kwasababu ya CCM nikajua ni walewale mfumo hawezi kuubadili ila yeye atabadilishwa na mfumo. Magu kama Magu nilikuwa namkubali ila CCM nilishaichoka.

Nimegundua mfumo wa CCM haukumbadili ili yeye kaubadilisha.

2020 tupo wote nitampigia, Mungu jalia heri na uzima
 
ikizingatia umaskini wetu na wa kenya unafanana .
No kenya wako huu zaidi... hawategemei misaada kwenye budget yao wakati sisi tunategemea misaada..

Alisema sawa vya bure sio dunia hii
Aliwahi kutamka akiwa Waziri wa ujenzi kuhusu Abiria wa kivuko pale kigamboni ,mtu ambaye hana sh 500 apige mbizi,
Tangu hapo nilimuona hafai na kwa kauli yake ile nilimnyima Kura yangu.

Nenda pale Likoni Mombasa, watu wanavuka bure kwenye Feri,sijui kama watanzania walio wengi wanalifahamu hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
binafsi nilihitaji Raisi asiye mzuri maana wazuri wameifikisha Tz pabaya..
Magufuli kwa asili ni mchapakazi, lakini hafai kuwa rais na hatakaa afae. Kiongozi ambaye anadhani urais ni sehemu ya kutekeleza utashi wake na sio kutii sheria huyo hafai kuwa rais. Ni kweli amesimamia baadhi ya miradi, lakini bado sio rais mzuri na hafai kuendelea kuwa rais.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom