Maujohnsimba
JF-Expert Member
- May 20, 2018
- 243
- 222
Ije mkuu..Kiufupi yule maza hausi alikuwa Kama katufumania hivi maana niliamua kutoka nje kumsikiliza,nikamsalimia kwa heshima akadai alisikia mtoto analia Sana akagonga sana mlango hakujibiwa ndo akaingia kujua kulikoni
Kiukweli nilitahayari na aligundua hilo,akamuulizia yule demu Yuko wapi,nikamwambia yupo room anapanga nguo za mtoto (hapa nilijikanyaga maneno live,basi yule mama aliishia kuguna tu)
Alivyotoka nje nikarudi room kumtoa yule demu huku tukibishana kujua ipi ni busara Kati ya kubaki kumngoja mama mtoto wangu au yeye kuondoka kabisa kwao ili kuua soo.
Baada ya muda nikapata jibu kuwa mie ndo nitoke kwa muda pale home nirudi baadae,lakini kabla sijaondoka pale nikawa najipitisha sana kwenye korido ya ile nyumba ili nimuone maza hausi nimfinyie elf 20 afunge mdomo wake (rushwa haiwezi kuisha abadani) baada ya raundi kadhaa za korido sikumuona kupita ikabidi nimuite atoke nimuage,akiwa ananishangaa nikanyoosha mkono kumpa ile hela. Akaipokea huku anababaika (ilikuwa kubwa kwake maana hata kodi huwa hagusi,anapokea mumewe) basi alifurahia na kuniaga mara nyingi huku akiniita baba.
Nikaondoka zangu huku nikiwa nawaza jinsi ya kujitetea kwa mzazi mwenzangu km maza hausi ataamua kunichomea japo nimemuhonga.
Huo ukawa mwanzo wa yule mama kunizoea na akawa anakula sana noti zangu. Kule kumpa hela mara nyingi ili kutunza siri yangu ya kumla yule demu wa kitaa anayeshinda kwa mzazi mwenzangu ambaye bado tulikuwa tunaendelea kupeana raha kila tukitaka kukazua jambo jipya kabisa ambalo haikuwa kula kwa masihara so sitoihadithia hapa ila kwa ufupi alinipigia chapuo nimle mwanae ili aendelee kula noti zangu za ngama.
Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app