CarloJesus
JF-Expert Member
- Nov 5, 2019
- 431
- 833
Ushawahi kukutana na swali hili: "Hivi unanionaje; jamani muoneni huyu!! Hivi nina mkosi gani mimi?!" Baada ya kumwambia au kumuonesha mtu unampenda? Au ushawahi kuambiwa "we siyo type yangu?"
Wakati kupenda linaaminika ni zawadi ya Mungu kwa wanadamu, kukamilisha furaha ya juu kabisa ya baraka zote ambazo Mungu kaziweka kumzunguka binadamu kama mali nk, upendo ndio utimilifu wa yote, wengine imekua ni fimbo ya kuvunja mioyo ya watu kiasi wamejiona siyo kitu tena.
Ndio, ndio maana mtu anakwambia nahangaika ili familia yangu ifanikiwe katika hili, katika hili na lile. Familia ni matokeo ya Upendo.
Dada mmoja na kaka mmoja walivutwa na upendo, kwahiyo inakuja kuleta maana kubwa sana baadaye, watoto, wajukuu nk. hadi kutengeneza amii ya kuchukuliana na kuvumiliana katika kubebeana madhaifu katika shida na raha, yaani FAMILIA.
Jambo hili jema mara nyingi mwanzo wake umekua wa vituko vingi na wakati mwingine maumivu kama siyo kabisa kumkosea alieliumba, yaani Mwenyezi Mungu.
Wako ambao leo ni mume na mke kwa sababu tu walipigana vikumbo katika daladala au walikutana masomoni, au ya uadui wao. Ni vema Basi tujifunze kuuheshimu mwanzo mzuri unaweza kuleta kitu kikibwa kizuri zaidi. Kila mtu hupenda kupendwa hata wale ambao wana kasoro kiakili; hata walio katika comma hupenda kupendwa; watoto wachanga pia, hutabasamu wakiambiwa wanapendwa.
Dada inawezekana una "mshape" wa haja, una chura, una sura nzuri kama malaika, wewe ni mzuri saana kiasi watu wanajikwaa barabarani, ukiambiwa unapendwa, bila kujali na nani au mtu gani ameonesha hisia kweli za kukupenda, hiyo ni zawadi kubwa sana amekupatia. Usimdharau, usimshushe mtu kwa maneno ya kumnyong'onesha kama wewe siyo type yangu, unanionaje nk. Hata kama hujavutika naye, ogopa dhambi ya kujiona kuwa wewe ni daraja nyingine ya binadamu na kuanza kudharau wengine.
Hiyo ni housing tu na ina undergo deterioration as well. Kumbuka hiyo shape, hilo tako, hiyo sura ni namna inayofaa tu, labda Mungu ameiweka kukukutanisha na Mr Right wako.
Nadhani unajifunza ma first lady jinsi wako wa kawaida na wanaume wao wanaonekana kutulia kabisa; labda wako wanawake kibao leo wakimuona Magufuli, Kikwete, Kenyatta n.k walifanya kosa kama hilo. Tafuta namna nzuri ya kumshukuru Mungu wako kwa zawadi ya uzuri kuung'arisha na usafi, unyenyekevu, utu wema, saburi na uvumilivu.
Kaka kweli inawezekana una umbo, sura nzuri, lakini financially uko vizuri pia na yoote yanayofanya wanawake/dada zetu wengi wakose amani kwa kuhamanika kukukosa hata kama hawajakupata kwa mvuto wako.
Ni kweli labda tayari roho ya kiburi imekuingia na una standards zako unataka mwanamume wako awe nazo lakini Mungu amekuweka katika Jamii. Hizo standards ni za nje tu, ndani ya moyo hao wanawake wanatumia sawa, wanapendana sawa. Ikitokea, ametokea mmoja akaonesha kukupenda au anakwambia anakupenda, tafadhali usimvunje moyo; ng'arisha mvuto wako na busara asiondoke ameumia hata kama umeshaamua huwezi kuwa naye.
Mwisho nisiwachoshe. Ni ngumu kukutana na mtu umevutika naye sana, naye amevutika nawe sana. Tunachofanya kufanikisha hili, ikitokea fulani ameonesha kukupenda sana usipuuze hata kama unaona haja-meet 100% ya matarajio yako, wala usimvunje moyo.
Kama hisia zako lau kwa mbali unaona unamkubali kubali, basi just huyo ni "Mr Right au Mrs Right"
We learn to love. Niliwahi kuvutika na binti siku ya kwanza nkachukuwa na no ya simu, lakini kesho nikamuona tofauti, kesho yake zaidi, kila siku nikianza kumuona mtu mwingine.
Mwisho nikajilaumu kwanini nilichukua no ya simu.
Ukipendwa pendeka, usivunje watu moyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wakati kupenda linaaminika ni zawadi ya Mungu kwa wanadamu, kukamilisha furaha ya juu kabisa ya baraka zote ambazo Mungu kaziweka kumzunguka binadamu kama mali nk, upendo ndio utimilifu wa yote, wengine imekua ni fimbo ya kuvunja mioyo ya watu kiasi wamejiona siyo kitu tena.
Ndio, ndio maana mtu anakwambia nahangaika ili familia yangu ifanikiwe katika hili, katika hili na lile. Familia ni matokeo ya Upendo.
Dada mmoja na kaka mmoja walivutwa na upendo, kwahiyo inakuja kuleta maana kubwa sana baadaye, watoto, wajukuu nk. hadi kutengeneza amii ya kuchukuliana na kuvumiliana katika kubebeana madhaifu katika shida na raha, yaani FAMILIA.
Jambo hili jema mara nyingi mwanzo wake umekua wa vituko vingi na wakati mwingine maumivu kama siyo kabisa kumkosea alieliumba, yaani Mwenyezi Mungu.
Wako ambao leo ni mume na mke kwa sababu tu walipigana vikumbo katika daladala au walikutana masomoni, au ya uadui wao. Ni vema Basi tujifunze kuuheshimu mwanzo mzuri unaweza kuleta kitu kikibwa kizuri zaidi. Kila mtu hupenda kupendwa hata wale ambao wana kasoro kiakili; hata walio katika comma hupenda kupendwa; watoto wachanga pia, hutabasamu wakiambiwa wanapendwa.
Dada inawezekana una "mshape" wa haja, una chura, una sura nzuri kama malaika, wewe ni mzuri saana kiasi watu wanajikwaa barabarani, ukiambiwa unapendwa, bila kujali na nani au mtu gani ameonesha hisia kweli za kukupenda, hiyo ni zawadi kubwa sana amekupatia. Usimdharau, usimshushe mtu kwa maneno ya kumnyong'onesha kama wewe siyo type yangu, unanionaje nk. Hata kama hujavutika naye, ogopa dhambi ya kujiona kuwa wewe ni daraja nyingine ya binadamu na kuanza kudharau wengine.
Hiyo ni housing tu na ina undergo deterioration as well. Kumbuka hiyo shape, hilo tako, hiyo sura ni namna inayofaa tu, labda Mungu ameiweka kukukutanisha na Mr Right wako.
Nadhani unajifunza ma first lady jinsi wako wa kawaida na wanaume wao wanaonekana kutulia kabisa; labda wako wanawake kibao leo wakimuona Magufuli, Kikwete, Kenyatta n.k walifanya kosa kama hilo. Tafuta namna nzuri ya kumshukuru Mungu wako kwa zawadi ya uzuri kuung'arisha na usafi, unyenyekevu, utu wema, saburi na uvumilivu.
Kaka kweli inawezekana una umbo, sura nzuri, lakini financially uko vizuri pia na yoote yanayofanya wanawake/dada zetu wengi wakose amani kwa kuhamanika kukukosa hata kama hawajakupata kwa mvuto wako.
Ni kweli labda tayari roho ya kiburi imekuingia na una standards zako unataka mwanamume wako awe nazo lakini Mungu amekuweka katika Jamii. Hizo standards ni za nje tu, ndani ya moyo hao wanawake wanatumia sawa, wanapendana sawa. Ikitokea, ametokea mmoja akaonesha kukupenda au anakwambia anakupenda, tafadhali usimvunje moyo; ng'arisha mvuto wako na busara asiondoke ameumia hata kama umeshaamua huwezi kuwa naye.
Mwisho nisiwachoshe. Ni ngumu kukutana na mtu umevutika naye sana, naye amevutika nawe sana. Tunachofanya kufanikisha hili, ikitokea fulani ameonesha kukupenda sana usipuuze hata kama unaona haja-meet 100% ya matarajio yako, wala usimvunje moyo.
Kama hisia zako lau kwa mbali unaona unamkubali kubali, basi just huyo ni "Mr Right au Mrs Right"
We learn to love. Niliwahi kuvutika na binti siku ya kwanza nkachukuwa na no ya simu, lakini kesho nikamuona tofauti, kesho yake zaidi, kila siku nikianza kumuona mtu mwingine.
Mwisho nikajilaumu kwanini nilichukua no ya simu.
Ukipendwa pendeka, usivunje watu moyo.
Sent using Jamii Forums mobile app