unacheka unamana gani
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 483
- 470
Wakati nikiwa chuoni pale Mlimani, nilipitia kitu cha ajabu sana. Nilikuwa nasoma SANA, kwa maarifa na juhudi, ila matokeo yakija najikuta nina nne kati ya kumi, assignments kupata 2/5 ilikuwa ni kawaida mno kwangu. Kuna wale ambao walikuwa wanakesha club unakuta wanapata marks za juu, wasichana ambao walikuwa wanakesha kwa madanga weekends, wanapata higher marks than I got! Nilikuwa naumia sana.
Ni miaka mitano baadaye ndio nikaigundua SIRI, kwa nini hii nilikuwa naipata mimi tu? Mbona nilikuwa nina juhudi? Mbona nilikuwa nasali sana? Ilifika wakati mpaka nilitaka kwenda kwa manabii kuwekewa mikono na kuombewa ila nilikuwa ninaghairi tu nikiona ni kawaida, wakati huo nikizidi kudidimia katika giza nene.
Nilianza mpaka kuhisi nina MAPEPO, why me? Nilijiuliza sana swali hili. Kwa nini mimi? Kumbe nilikuwa nachezewa, na ukizingatia sikuwa naamini haya mambo, kumbe watu walinichukulia point hapo, nikawa nachezewa ila niliona ni hali tu ya kawaida, hakuna uchawi, japo nafsi ilinishuhudia sipo salama.
Mpaka hapo nilipochukua hatua, niliona mabadiliko makubwa, fikiria ningemaliza chuo na 1.7GPA? HII NILIIGUNDUA MWISHONI MWAKA WA PILI. JAMANI KUCHEZEWA KUPO, KUNA VIMICHEZO VYA KIJINGA SANA VYUONI, JAPO VIJANA HATUAMINIGI HIVI VITU.
Yaani jitu limekaa huko halisomi halafu linatumia kichwa changu kufaulu, haya mambo yapo aisee, sijui wanatumia mechanism gani mpaka MTU anafaulu kwa akili yako.
Nimejifunza somo kubwa mno nikiwa chuo. Namshukuru Mungu. Siku nikiamka vizuri nitaleta kisa kizito cha yote yaliyonipata wakati huo.
Uliwahi kupitia hali hii ukiwa chuo au kazini? Tupe uzoefu wako watu wapone, hali inatisha.
Ni miaka mitano baadaye ndio nikaigundua SIRI, kwa nini hii nilikuwa naipata mimi tu? Mbona nilikuwa nina juhudi? Mbona nilikuwa nasali sana? Ilifika wakati mpaka nilitaka kwenda kwa manabii kuwekewa mikono na kuombewa ila nilikuwa ninaghairi tu nikiona ni kawaida, wakati huo nikizidi kudidimia katika giza nene.
Nilianza mpaka kuhisi nina MAPEPO, why me? Nilijiuliza sana swali hili. Kwa nini mimi? Kumbe nilikuwa nachezewa, na ukizingatia sikuwa naamini haya mambo, kumbe watu walinichukulia point hapo, nikawa nachezewa ila niliona ni hali tu ya kawaida, hakuna uchawi, japo nafsi ilinishuhudia sipo salama.
Mpaka hapo nilipochukua hatua, niliona mabadiliko makubwa, fikiria ningemaliza chuo na 1.7GPA? HII NILIIGUNDUA MWISHONI MWAKA WA PILI. JAMANI KUCHEZEWA KUPO, KUNA VIMICHEZO VYA KIJINGA SANA VYUONI, JAPO VIJANA HATUAMINIGI HIVI VITU.
Yaani jitu limekaa huko halisomi halafu linatumia kichwa changu kufaulu, haya mambo yapo aisee, sijui wanatumia mechanism gani mpaka MTU anafaulu kwa akili yako.
Nimejifunza somo kubwa mno nikiwa chuo. Namshukuru Mungu. Siku nikiamka vizuri nitaleta kisa kizito cha yote yaliyonipata wakati huo.
Uliwahi kupitia hali hii ukiwa chuo au kazini? Tupe uzoefu wako watu wapone, hali inatisha.