Chato: Yaliyojiri katika Maadhimisho ya mwaka 1 wa kifo cha Hayati Magufuli. Kasala, tusimamie ukweli na haki. Samia kuendeleza Mema

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969
1647520739082.png

Leo ni Maadhimisho ya Mwaka mmoja tangu Rais wa awamu ya Tano Dkt John Pombe Joseph Magufuli atukote. Maadhimisho hayo yanafanyika mkoani Geita katika wilaya ya Chato.

Maadhimisho hayo yatahudhuriwa na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Samia suluhu, Makamu wa Rais Dkt. Isdori Mpango, Waziri Mkuu Mh. Majaliwa Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi na viongozi mbalimbali wa serikali ya Jamuhuri.

Pia soma
1). TANZIA - Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar


2). Historia ya Dkt John Pombe Magufuli

===

UPDATES;

====


“Mh.Rais nilikupigia simu lakini kwa bahati mbaya sikukupata lakini baadae ulinipigia na nikakuomba uhudhurie shughuli hii ukakubali na uliniahidi kuwa utakuja japokuwa sikuomba kwa maandishi lakini umekuja,ASANTE SANA Umeniheshimu Sana MAMA,”-Mama Janeth Magufuli

"Tunakuombea Mungu akupe nguvu ya kuendelea kuongoza Taifa vema na Mungu azidi kukulinda akupe maisha marefu,"- Mama Janeth Magufuli

“Ni imani yangu Dini zote tumefundishwa kushukuru kwa kila jambo naomba muungane nami katika kumshukuru Mungu, tunamshukuru Mungu kwa Neema zake kwani ilimpendeza kujifunza mema mengi kutoa kwa Hayati Magufuli hakika tutayaishi na kuyaenzi daima,"-Mama Janeth Magufuli


Askofu Kasala awataka Watanzania kusimamia ukweli, haki

1647520470699.png

Picha: Askofu Flavian Kasala
Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Askofu Flavian Kasala amewataka Watanzania kusimamia ukweli na haki katika kumuenzi Rais wa awamu ya tano, hayati John Magufuli.

Askofu Kasala ametoa rai hiyo leo Alhamisi Machi 17, 2022 kwenye ibada ya misa ya kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha hayati John Magufuli inayofanyika katika uwanja wa Magufuli Chato.

Amesema Hayati Magufuli alisimamia ukweli na kile anachokiamini hivyo kuwataka wananchi na viongozi kushuhudia ukweli huo katika maisha yao.

“Tukisimamia ukweli na haki, marehemu wetu wanazo dhawabu walizoondoka nazo, tuko tayari kuyachukua hayo kuwa kama dira ya maisha yetu? amesema

Askofu Kasala amesema kila mmoja kwa nafasi yake awe na kiu ya haki katika maisha na kujitoa kuietea.

“Njaa ya haki ni pale katika ubinadamu wako unaposema siwezi kushuhudia kuona mtu akiwa anaonewa, ananyanyaswa na kudhulumiwa,

Maudhi kwa ajili ya haki yanakuja pale tu mmoja anaposimamia haki bila kijibakiza na kusimamia haki ni kujitoa sadaka lakini bora niudhiwe lakini haki itendeke” amesema Askofu Kasala

Amewataka wananchi kuzidi kumombea toba kwa Mungu Hayati Magufuli

"Tunapokua kwenye ibada hii tunapaswa kukumbuka huyu alikua kiongozi wetu na kuna mema mengi alitenda akiwa na sisi na kama imani ya kanisa inavyo tuambia tuendelee kumuombea toba ili Mungu ampokee mbinguni" amesema Askofu Kasala.

Ibada hiyo imehudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hasani na viongozi mbalimbali wa Serikali, taasisi, wastaafu na wananchi.

Viongozi wengine waliohudhuria ibada hiyo ni pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hassein Mwinyi na mkewe pamoja na makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Philip Mpango.

Wengine ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson, Waziri wa Ardhi, Angelina Mabula, Waziri wa Tamisemi, Inocent Bashungwa, Mbunge wa Jimbo la Ismani, William Lukuvi pamoja na Balozi Tanzania nchini Malawi, Humphrey Polepole.

Pia wapo viongozi wastaafu wakiwamo Makamu wa Rais wa awamu ya nne, Ghalib Bilali, mawaziri wakuu wastaafu Joseph Warioba na Mizengo Pinda.

Wengine ni aliyekuwa Spika wa Bunge, Anna Makinda mke wa Rais wa awamu ya tatu hayati, Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa.

Wakati wa ibada hiyo ikiendelea mvua kubwa imenyesha huku mamia ya wananchi waliopo kwenye uwanja huo wakiendelea kushiriki kwenye ibada.

Baada ya ibada Rais, viongozi pamoja na familia wataambatana kwenda kwenye kaburi la Hayati Magufuli kwa ajili ya kuweka mashada ya maua.


Rais Samia mema yote yaliyoachwa na Hayati John Magufuli yataendelezwa

1647520554082.png

Picha: Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan amesema mema yote yaliyoachwa na aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli yataendelezwa.

Ameyasema hayo leo Alhamisi Machi 17, 2022 alipokuwa akitoa salamu za taifa katika maadhimisho ya mwaka mmoja wa kumbukizi ya kifo cha hayati Magufuli.

Rais Samia ameyataja mambo hayo kuwa ni pamoja na nidhamu, uadilifu na kupiga vita ubadhilifu.

"Hivi karibuni tutafungua daraja la Tanzanite lililoko jijini Dar es salaam hii ilikua ndoto ya Magufuli na nitaiendeleza kwa kuboresha huduma za maji, umeme na miundombinu"amesema Samia

Akizungumzia miradi iliyopo Geita, Rais Samia amesema mradi wa kivuko cha Chato-Nkome kilichogharimu Sh3.1 bilioni umekamilika.

Aidha mradi wa kituo kikuu cha mabasi unaojengwa kwa Sh13.2 bilioni umekamilika kwa asilimia 92 na kuahidi kuendelea kutoa fedha ili ukamilike kwa asilimia 100

Samia amesema mambo yote hayo yatawezekana kama watanzania wataendelea kuimarisha mshikamano.

"Sisi wanadamu hatuwezi lolote bila msaada wa mwenyezi Mungu".

Awali Makamu wa Rais wa Tanzania, Philip Mpango amesema Magufuli alikua mwalimu wake aliyemfundisha kumtegemea Mungu nyakati za shida.
 
Hii tarehe Nina mashaka nayo.

Kabla ya tarehe 17 mwezi wa 3 kufika siku tatu nyuma niliona mizinga na wanajeshi wakitokea bagamoyo na kuelekea DAR.

Na mizinga hyo hyo ndo ilitumika kwenye kumuaga magufuli pale uwanjani.

Swali walikuwa keshakufa au walijua kuwa atakufa?wakajiandaa mapema
 
Hii tarehe Nina mashaka nayo.
Kabla ya tarehe 17 mwezi wa 3 kufika siku tatu nyuma niliona mizinga na wanajeshi wakitokea bagamoyo na kuelekea DAR.
Na mizinga hyo hyo ndo ilitumika kwenye kumuaga magufuli pale uwanjani.
Swali walikuwa keshakufa au walijua kuwa atakufa?wakajiandaa mapema
Hayo yalizingumzwa na wengi sana huenda kuna ukweli nyuma yake lakini ibaki kusema tarehe ya leo ndio tuliambiwa tarehe rasmi ya kututoka.
 
Hii tarehe Nina mashaka nayo.
Kabla ya tarehe 17 mwezi wa 3 kufika siku tatu nyuma niliona mizinga na wanajeshi wakitokea bagamoyo na kuelekea DAR.
Na mizinga hyo hyo ndo ilitumika kwenye kumuaga magufuli pale uwanjani.
Swali walikuwa keshakufa au walijua kuwa atakufa?wakajiandaa mapema
Yule alikuwa kitambo sn hata wiki 2 kabla
 
Nipe tathimini ya kiuchumi ya ilo daraja refu la busisi , au huko linako elekea Kuna resources gani ambayo itainua uchumi wetu, otherwise ni zawadi kwa mkwe wake kama wanavyosema wengi
 
Mungu ni mwema kwa wote waliompenda na wasiompenda .ila Mungu alimpenda zaidi na alisikia maombi ya wengi ndio maana hayupo.Nchi imekuwa shwari,tuna amani mioyoni mwetu ,watu waliishi kama wako Ukraine why,watanzani walio wengi hawakujua wafanyeje wale waliokua na roho ya "nacist "walishangilia wenzao kufungiwa account, kunyanganywa hela kwa nguvu ,kupotea kwenye mazingira ya kutatanusha na pia kubambikiwa kesi za uhujumu uchumi.Tuanatoa pole kwa familia Mama Janet na Watoto Mungu awape nguvu ila mmepumua sasa hata umenenepa mama yetu ingawa kuondokewa na Mume sio jambo jepesi
 
Daima tutakukumbuka uliwatetea wanyonge mbele ya wanyonyaji na vibaka wa Mali za uma.

Ukaitetea nchi mbele ya ulimwengu wa dhulumu, kazi uliifanya na Mungu akujalie huruma yake isiyo na ukome.

Pumzika kwa amani shujaa wa taifa letu.

Nipo hapa CHATO kuhadhimisha mwaka mmoja wa Jemedari wetu JOHN POMBE MAGUFULI.
 
1. Daraja la Tanzanite Dar
2. Mikataba ya madini
3. Ukuta wa mererani
4. Utumbuaji
5. Uzinduzi wa malipo ya serikali kupitia control number
5. Umeme wa Tsh 27,000/=
6. Elimu bure darasa la kwanza hadi form four
7. Ukarabati wa. Viwanja vya ndege na meli
8. Bomba la mafuta Hoima kwenda Tanga
9. Kuanzisha Tarura, Latra,
10. Kununua radar kwenye viwanja vya ndege vyote.
11. Kuivunja bodi ya ununuzibwa madini
12. Kuanzisha tume ya madini na madoko ya kuuzia madini
13. Kuvunja Jiji la Dar es salaam
14. Kumfukuza kazi Nape mnauye, mchechu wa NHC,
15. Kwa miaka mitano kutokwenda ulaya
16. Kuzirudisha halmashauri zote ofisi ya Rais.
17. Kuondoa watu wenye vyeti feki kwenye mfumo wa mishahara ya serikali.
18. Kukarabati shule za serikali za zamani
19. Kununua ndege mpya 11
20. Kufufua reli ya Dar to arushaTanzania
21. Kukarabati bandari ya mtwara, tanga na Dar
22. Kukusanya na kuzitambua mali za CCM
23. Kuanzishwa wizara mpya ya Madini
24. Miaka mitano umeme haujawahi kukatika
25.ujenzi wa hospitali za kanda, mikoa na wilaya
26. Ujenzi wa mshakama za wilaya
27. Kuongeza idadi ya hifadhi za tsifa na jeshi usu.
28. Kufuta mishahara ya 45,000,000
29. Kuongeza viwanda nchini
30. Kuwaeleza ukweli watanzania kuhusu covid 19
31. Kupunguza urasimu kwa watumishi wa umma
32. Kuanxisha ofisi za msajili wa hati za ardhi kila mkoa na kufuta ofisi za kanda
33. Kukamata wakwepa ushuru
34. Kampuni ya Halotel ya JK , wabia wake kwenda segerea kwa kutokulipa kodi
35. Serikali kununua magari yake kwa mfumo maalumu kupunguza madalali
36. Kiswahili kuanza kutumika mahakamani kutolea hukumu
37. …..,, Samia haya niliyoyataja anayaweza kuyasimamia?kuyaendeleza?kubuni vingine ? CCM tujiuliza maswali kabla hatujamwambia Samia achukue fomu 2025
Miaka 5 umeme haujawahi kukatika?
 
1. Daraja la Tanzanite Dar
2. Mikataba ya madini
3. Ukuta wa mererani
4. Utumbuaji
5. Uzinduzi wa malipo ya serikali kupitia control number
5. Umeme wa Tsh 27,000/=
6. Elimu bure darasa la kwanza hadi form four
7. Ukarabati wa. Viwanja vya ndege na meli
8. Bomba la mafuta Hoima kwenda Tanga
9. Kuanzisha Tarura, Latra,
10. Kununua radar kwenye viwanja vya ndege vyote.
11. Kuivunja bodi ya ununuzibwa madini
12. Kuanzisha tume ya madini na madoko ya kuuzia madini
13. Kuvunja Jiji la Dar es salaam
14. Kumfukuza kazi Nape mnauye, mchechu wa NHC,
15. Kwa miaka mitano kutokwenda ulaya
16. Kuzirudisha halmashauri zote ofisi ya Rais.
17. Kuondoa watu wenye vyeti feki kwenye mfumo wa mishahara ya serikali.
18. Kukarabati shule za serikali za zamani
19. Kununua ndege mpya 11
20. Kufufua reli ya Dar to arushaTanzania
21. Kukarabati bandari ya mtwara, tanga na Dar
22. Kukusanya na kuzitambua mali za CCM
23. Kuanzishwa wizara mpya ya Madini
24. Miaka mitano umeme haujawahi kukatika
25.ujenzi wa hospitali za kanda, mikoa na wilaya
26. Ujenzi wa mshakama za wilaya
27. Kuongeza idadi ya hifadhi za tsifa na jeshi usu.
28. Kufuta mishahara ya 45,000,000
29. Kuongeza viwanda nchini
30. Kuwaeleza ukweli watanzania kuhusu covid 19
31. Kupunguza urasimu kwa watumishi wa umma
32. Kuanxisha ofisi za msajili wa hati za ardhi kila mkoa na kufuta ofisi za kanda
33. Kukamata wakwepa ushuru
34. Kampuni ya Halotel ya JK , wabia wake kwenda segerea kwa kutokulipa kodi
35. Serikali kununua magari yake kwa mfumo maalumu kupunguza madalali
36. Kiswahili kuanza kutumika mahakamani kutolea hukumu
37. …..,, Samia haya niliyoyataja anayaweza kuyasimamia?kuyaendeleza?kubuni vingine ? CCM tujiuliza maswali kabla hatujamwambia Samia achukue fomu 2025
Endelea kupumzika kwa amani JPM! Kwa hakika maisha yako mafupi ktk kiti cha Uraisi yalikuwa ni TUNU kwa nchi yetu na Afrika kwa ujumla. Ni Mungu mwenyewe aliyemwinua, na ni Mungu mwenyewe alimtwaa Raisi wetu, Basi jina la Mungu wetu LIHIMIDIWE MILELE
 
Back
Top Bottom