Ulipata milioni yako ya kwanza ukiwa na umri gani? Ulipataje?

Binafsi miaka 30 sasa ni mtu wa Kujaribu Jaribu vitu vingi ( ideas ) hivyo nikipata laki 2, 3 au 4 najaribu kitu kipya.

Kukusanya Milioni NET nikawa nayo mkononi SIJAWAHI kwasababu siyo muumini wa Saving na sijawahi kupata Deal la kulipwa pesa hiyo.
jifunze kusave mkuu kama huna dili za pesa ndefu, ukipata hizo lakilaki kabla hujapanga chochote toa hata 50 peleka mahali huwezi ichukua kabisa.

Mimi nilikua na lain ya airtel money nilimpa maza aitunze na asinipe under no circumstance, wala nilikua sijui anaitunza wapi. Nikawa nikipata tu hela, kabla sijaitamani na kunua kitu natoa kiasi kadhaa naideposit kwenye lain inayobaki nachafua ninavyojua. Baada ya kila miezi 3 maza alikua ananipa najikuta nna laki nne hadi 8, ndo nakaa nawaza sasa hii hela itanizalishiaje zingine, huku nikihakikisha cashflow inaendelea kuwepo. Mana adui wa akiba ni ukate mrija wa cashflow, utaitumia tu
 
tunafanyaje mzee tushike maana naona tunalingana kwa kila namna
nadhani mtakua nyumbani, step ya kwanza toka nyumbani ujue bills, ujenge discipline ya hela, yani ujue kutafuta na kutumia vizuri pesa,jiweke karibu na watu waliotoka ama wenye michongo weka aibu pembeni. Jitume mtoto wa kiume mana kuna watu watakutegemea siku moja.
 
Nilipata mwaka jana mwezi wa 9 mwishoni. Hiyo ni baada ya form six watu kwenda jeshini nami najijua nilivyo kapuku jeshi nikapiga chini.
Nilipiga kazi mpaka nikakonda, mwendo wa kuamka saa kumi na kurudi nyumbani saa mbili usiku. Kazi zenyewe unasimama tu kasoro kupumzika saa moja tu.
Hiyo hela nilinunua vitu kadhaa maana sikuwa natafuta mtaji wala nini.
Kati ya hiyo milioni nilitoa kitu kama 80k pekee kwa ajili ya bata. Inaniuma sana sikuiwekeza sahivi naishi kwa mawazo.
Umenifanya nicheke sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli mimi nimeshashika pesa nyingi sana, ila less than 40 million. Nilichojifunza ni kuwa sina nidhamu na pesa, nilishazoea kupata pesa kirahisi hivyo huwa sina akiba au ni kidogo sana. Sasa huyu baba lao Corona umeniumbua sana, dili hakuna tena na mfukoni sina kitu, mshahara bado sana. Sijui mwisho wa mwezi ntafikaje, ndugu zangu jifunzeni nidhamu ya pesa. Sasa hivi namiliki shilling 300 yani mia mbili plus mia mbovu niliyoiyokota chumbani. Hahaahahaha hahahahaha unaweza dhani masihara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwakweli mimi nimeshashika pesa nyingi sana, ila less than 40 million. Nilichojifunza ni kuwa sina nidhamu na pesa, nilishazoea kupata pesa kirahisi hivyo huwa sina akiba au ni kidogo sana. Sasa huyu baba lao Corona umeniumbua sana, dili hakuna tena na mfukoni sina kitu, mshahara bado sana. Sijui mwisho wa mwezi ntafikaje, ndugu zangu jifunzeni nidhamu ya pesa. Sasa hivi namiliki shilling 300 yani mia mbili plus mia mbovu niliyoiyokota chumbani. Hahaahahaha hahahahaha unaweza dhani masihara.

Sent using Jamii Forums mobile app
dah kweli nidhamu ya pesa ni muhimu sana, unapata pesa unalipa watu wengine tu hadi inaisha-unamlipa mangi, unalipa bar, unamlipa mwenye nyumba, unalipa maduka ya nguo,s/market, na sehemu zote za bata unalipa. Kasoro unasahau kujilipa wewe kwa kuweka akiba.
Mtu mmoja nilimsikia akisema, you are not rich because of how much you earn, but how much you keep for yourself. Apo ukute mtu hajawai kuearn hata laki tano cash ila ana savings ya laki nane, wakati wewe mwenye uwezo wa kupiga deals za mamilioni kuna siku unaamka huna kitu kabisa
 
Nilipata nikiwa na miaka 22 biashara ikiwa dagaa nyasa..na vijiwe vya hapa na pale hiyo siku iliyotimia ilikua 27/1/2018 niliztandaza juu ya kitanda nikazilalia kwa furaha nikapiga picha nyingi sana baada ya miezi 3 ikafika 1.6M nikanunua boksa baada ya hapo kilichotokea sitaki kukumbuka kamwe.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kilitokea nini mkuu, tupe hiyo story tujifunze

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuelezee ilikuaje miaka 19 wengine hata hela ya boom hawajashika wewe 17 ushashika kiasi hicho
Maana koments zako zinanipa controversy flni, mara milio 40, mara 6, mara 4, hebu tueleze kinagaubaga

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikiwa na miaka 17 nilipewa 4 M kama urithi baada ya baba kufariki. Nilipofikisha miaka 19 nilianza biashara ya kukopesha pesa wakulima wa tumbaku amapo nilipata faida mpaka ya 1.3 M. Pamoja na kuja kishika pesa nyingi baadae lakini sijawahi kuzidi 40 M. Vp hapo umenielewa au niongeze sauti?
 
Tuelezee ilikuaje miaka 19 wengine hata hela ya boom hawajashika wewe 17 ushashika kiasi hicho
Maana koments zako zinanipa controversy flni, mara milio 40, mara 6, mara 4, hebu tueleze kinagaubaga

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikiwa na miaka 17 nilipewa 4 M kama urithi baada ya baba kufariki. Nilipofikisha miaka 19 nilianza biashara ya kukopesha pesa wakulima wa tumbaku amapo nilipata faida mpaka ya 1.3 M. Pamoja na kuja kishika pesa nyingi baadae lakini sijawahi kuzidi 40 M. Vp hapo umenielewa au niongeze sauti?
 
dah kweli nidhamu ya pesa ni muhimu sana, unapata pesa unalipa watu wengine tu hadi inaisha-unamlipa mangi, unalipa bar, unamlipa mwenye nyumba, unalipa maduka ya nguo,s/market, na sehemu zote za bata unalipa. Kasoro unasahau kujilipa wewe kwa kuweka akiba.
Mtu mmoja nilimsikia akisema, you are not rich because of how much you earn, but how much you keep for yourself. Apo ukute mtu hajawai kuearn hata laki tano cash ila ana savings ya laki nane, wakati wewe mwenye uwezo wa kupiga deals za mamilioni kuna siku unaamka huna kitu kabisa
Huu ni ukweli mchungu. Tubadili tabia
 
Habari zenu jamani,

Bila kupoteza muda nijikite kwenye mada.

Mada hii nimeiweka hapa ili tujadili kwa ajili ya kuhamasishana na kujifunza pia. Sio kwa ajili ya kusema mambo ya kufikirika yasiyo na tija ambayo hayatamsaidia mwanajamvi yoyote kuokota kitu.

Niwaombe unapocomment, tuelezee kidogo ili uzi uchangamke na watu wajifunze hasa vijana ambao bado wapo kwenye hustle pamoja na kuwatia moyo wale waliokata tamaa

Mimi binafsi ni moja kati ya watu ambao hawakuwa na bahati ya kuishi maisha ya ushuani, nilizaliwa na kukulia naweza kusema uswahilini tu japo sio kwenye uswahili ule tunaoujua wa sasa.

Sikubahatika kusomeshwa na wazazi hadi Chuo Kikuu, walinisomesha hadi form 4, nikaingia mtaani kupambana nikajiendeleza mwenyewe nina BA ya fani fulani kwa sasa

Baada ya kumaliza Form four niliingia mtaani na kujichanganya na mafundi wa ujenzi nikiwa bado naishi nyumbani kwahiyo niliweza kujinunulia mahitaji yangu tangu hapo, nikashika kila kibarua kilichoingiza pesa ikiwa ni pamoja na kufanya kazi viwandani kwa posho ya kuanzia 2900 kwa siku, nilipoacha kazi za viwandani nilikua nimefikia kwenye posho ya 7000 kwa siku. Hizi zilikuwa kazi ngumu sana. Ila zilinijenga na nikajua kwamba hakuna kinachotokea bila sababu.

Kwa nini nimesema hivyo, kwa sababu kila kiwanda nilichopitia niliondoka na ujuzi fulani ambao ulinifanya baadae nije kuanzisha miradi mbalimbali.

Baada ya kuchuma kwenye jua la saa sita kwa muda mrefu nikapata kibarua kwenye kampuni ya wahindi ambao walinipenda sana, (tofauti na msemo wa kusema wahindi watu wabaya, mimi nilikutana na wazuri)

Nikapanda chati kidogo nikawa napokea 200,000 kwa mwezi na kutokana na uchapa kazi nikaongezewa ikawa 250,000 pamoja na nauli na chakula pembeni. Ni wakati huu ndipo nilipojichanga nikajilipia VETA kusoma kozi fulani ya viwandani.

Alipoona nia yangu ya kusoma Mr. *** Bosi wangu alinipa mkopo isio na riba ili nijiendeleze hivyo nikaenda DP.

Tukio hili ni kwamba siku moja nilisahau begi langu kazini, na kwa hisia za kibinadamu akalifungua kuangalia ndipo alipokuta vitabu pamoja na makaratasi mengine ndio akaniuliza nini hiki, nikamwambia ukweli bosi mimi nasoma na ndio maana nilikuomba ruhusa niwe nawahi kutoka mchana, mwqnzo alikua na hisia zingine ila baada ya tukio hili alikaa kama wiki ndio akaniambia atanikopesha na atanipa likizo. Japo hatanilipa.

Kipindi cha kusoma nilihangaika sana. Nasoma narudi nyumbani nakula mzee akiwa hayupo narudi geto, kodi ikiisha nilikuwa nahangaika sana ila hiyo ni story nyingine.

Bahati mbaya yule mhindi alikuja kufariki nikiwa nakaribia kumaliza na ndipo ndugu wa familia (watoto) wakanilazimisha nilipe mkopo ama nifanye kazi bila malipo kufidia.

Nashukuru Mungu nilivuka hicho kikwazo baada ya hapo nikahangaika sana kupata ajira sikupata pamoja na dp yangu. Nikatumia ujuzi niliopata kwenye moja ya kiwanda nikakopa kwa watu kama wanne nikapata laki 4 nikaanza kutengeneza bidhaa nazungusha madukani. Hii ilidumu kwa muda sana kama miaka miwili hivi nikawa na mtaji wa kama 800,000 hivi.

Nikaenda Manyara maeneo fulani yanaitwa Maole, ndanindani ya mbuyu wa mjerumani nikalima mahindi heka moja nikapata gunia 7, na soko halikua zuri soko. Ile hela ni kama nikaizika.

Nikarudi mjiji nikafanya kila kilichingiza hela halali (ni story ndefu) lakini siku navunja boksi nilipata kama 368,000 kisha nikaomba mkopo wa 400,000 kwa rafiki yngu ambaye alikuwa Vicoba (alikopa akanikatia kiasi hicho) kisha nikarudi shamba safari hii nilipata 1,500,000

Hiyo ikawa milioni yangu ya kwanza.

Siku nyingine tutaongelea maisha baada ya milioni ya kwanza (usidhani ilidumu)
Nawakaribisha kujadili
Ni mimi Mfalme (ni jina tu)

(Angalizo: unaposema kwa kifupi inapoteza maana ya uzi. Tuelezee kidogo. Ilikuwaje, ulikuwa na umri gani)
Niliipata nikiwa chuo ifm ,nilipewa ada na mama wakati mm nilikuwa nalipiwa na serikali (mama hakujua) ,nikanunua vyumba hostel ifm kipindi hicho hostel dili kinoma ,nilinunua vyumba vitatu kwa laki 6 kila chumba kina vitanda vi 4 ,kila kitanda wanalala watu wawili na kila kitanda unapangisha per person
300,00×2 =600,000
600,000×4=2,400,000
2,400,000×3=7,200,000 that was second year
Nikamchimbia kisima mama yangu ,she was able to earn 15,000 kwa siku minimum kwa kuuza kwakuwa alipokuwa anakaa palikuwa na shida ya maji

3rd year ilikuwa hatari ....nilipiga mpaka 10m no one knew niliifanya kwa displine kubwa nikarudi post graduate i did the same

Nikaja shtukiwa na warden nilivyomaliza post nikafanya kwa faida ndogo baadae soko la vyumba chuo likawa sio dili baaada ya wanafunzi wengi kuprefer kigambon na hostl za nje ...nami nikawa nafanya bznes huku naajaliwa ,nikaona upuuuzi nw naendelea na biashara maisha yangu si makubwa saaaana lakini nimaisha ambayo wengi wanayatamani ,napata changu ,napata cha kusomesha ndugu zangu sidaiwi kodi ,nabado nasave hela mara 5 ya mshahara niliokuwa napewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa na miaka 22 moshi Kilimanjaro nilikuwa nafanya kazi za kubeba mizigo milimani, tukawa tunabeba mizigo na kufanya biashara ya t-shirt na bracelet kwa wazungu, nikameki ad ikafika dollar 900.. Million mbili ivi. Nikampatia ujauzito girlfriend wangu akajifungua malezi yakawa makubwa mara dogo aumwe mara kodi mara kazi zikawa ngumu mliman na biashara ikazuiwa tena. Imebaki kama historia ata laki moja nimeimiss now. Inaniuma sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilikuwa na miaka 22 moshi Kilimanjaro nilikuwa nafanya kazi za kubeba mizigo milimani, tukawa tunabeba mizigo na kufanya biashara ya t-shirt na bracelet kwa wazungu, nikameki ad ikafika dollar 900.. Million mbili ivi. Nikampatia ujauzito girlfriend wangu akajifungua malezi yakawa makubwa mara dogo aumwe mara kodi mara kazi zikawa ngumu mliman na biashara ikazuiwa tena. Imebaki kama historia ata laki moja nimeimiss now. Inaniuma sana

Sent using Jamii Forums mobile app
ilo jina lako linafurahisha na maelezo yako, ila ya kwanza huwa haidumu mkuu, ila inakupa mwangaza kidogo
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom