Ulinzi wa Rais Samia Marekani upoje?

Naona wengi wanatetea ulinzi na mama kuwa salama
Hata kama ana maadui wanaomsema humu kila siku na hakuna mtu anaependwa na wote

Rajiv Gandhi aliuwawa akiwa ameshuka kwenye gari wakati wa kampeni tena kapelekewa shada la maua na ndani kukiwa na Bomb

Hata aliempiga risasi Pope hakuna na uadui nae ila alitaka umaarufu tu

Kiongozi ni kiongozi tu na ulinzi amepewa wamlinde ila likitokea la kutokea basi ila wamemlinda
Hapo na simu kabisa mlinzi anaipokea

Wengi watapinga ila najua mengi
 
MANGE NA SAMIA WANAJUANA HAO...../
nawasiwasi na zile taarifa nyeti zilizokuwa zikivuja toka ikulu na kumfikia Mange , enzi ya utawala wa awam ya five.
!!!!!!!
 
Huyo Mange na Yule Iron Lady ni zuga za Usalama,Usishangae kabisa kwa Mlinzi kupokea simu ya Mange na kupiga picha,
Mange ni mulemule.Wapo huko walipo kwa kazi maalum
 
Sasa Tz nayo Rais nae ana ulinzi? Tz Rais hana ulinzi ila ana watu wa kuzuia Raia wasimsogelee Rais basi.
ile tabia ya Rais kuongea kwenye roof ya gari ni moja ya ishara inayo tambulisha Rais hana ulinzi ila ana watu wa kuzuia Raia wasimsogelee tu maana ni hatari sana hata Sniper aliekaa mita 1500 anaweza kumtungua

Acha NewYork wawafundishe jinsi ya kulinda viongozi maana ulinzi wa Tz ni bure kabisa
 
Yaani yule mpambe Kanali, kakubali hadi kumbebea Mange handbag ili ampe nafasi nzuri ya kupiga picha

Yule PSU wa Tiss nae akakubali kushika simu ya Mange ampige picha akiwa na Namba moja!!

Wakuu wa Makumbusho na Mbweni hakika leo vijana wenu wamewavua nguo mchana kweupeeee


Inashangaza Kwa kweli lazima Safari ikimalizika watu wawajinishwe vijana tupo tuu hatuna ajira watu Wana piga watu picture
 
NADHANI WALINZI WOTE HAO NDO MARA YA KWANZA KUPATA HIYO EXPERIENCE WAZEEWW

ILA INAUMIZA MOYO WADAU
 
Wale wanaitwa special weapon and tactics unit (Combat bakabaka) ni kikosi maalamu ndani ya kikosi cha ulinzi wa raisi kwa ajili ya kuboresha ulizi wa rais.

Na kwa ufupi ni kwamba kila nchi zina utaratibu wake wa ulinzi, hata kwa mama pia alipotua US kuna special security anakuwa amepangiwa na UN tena wale ndio wanaume kwelikweli achana na hawa wavulana wetu.

Ila nikirudi kwenye ile clip ya jana nimeumia mno kumuona mmoja wa walinzi wa Rais anaacha jukumu lake la ulinzi na kushika simu ya Mange kimambi (malaya wa kisiasa) na kuruhusu kupiga nae picha.

Tukifuata protokali za ulinzi hakupaswa kufanya vile kabisa, amevunja miiko ya ulinzi.
Ukiachana na huyo aliyepiga picha kuna wale wadada wawili wanaokuwa pembeni na Rais mmoja alikuwa anavuta mabegi hadi nikajiuliza ulinzi anafanya saa ngapi sasa alikosekana mwingine wa kubeba.!
 
Sio kweli! Obama au Bush walipokuja Tanzania,walikua wanalindwa na walinzi wa Tanzania walipokua nje ya Hoteli??
Mkuu kwanza usibishe Kama hujui soma viena convention.

Pili Kuna exceptions za Marais watano ambao, ulinzi wa viongozi wao ni jukumu lao muda wote.

Somma Kisha utuambie Nani mkweli
 
Nawasalimu katika jina la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania!

Wapendwa tumekua tukiona kwa macho yetu,kwamba Mh Rais Samia ana walinzi wenye mabunduki mazito mazito pindi anapokua kwenye tukio au sehemu yoyote hapa Nyumbani Tanzania!

Wale wana usalama ni wenye miili mikubwa,warefu na wamekula gwanda la kijeshi na pia zile bunduki sijui ni aina gani,maana hua ni heavy machines!

Sasa Jana Mh Rais Samia kaingia Marekani,Nchi ya watu watukutu,wanatembea na bunduki zao mifukoni na wananunua bunduki madukani kama sisi tunavyonunua unga wa ugali kwa Mpemba au kwa Mangi!

Sasa Jana sijawaona kabisa wale wanausalama wetu,Jana kina Mange Kimambi walikua wanamsogelea Mh Rais wetu,hadi yule mpambe wa Mh Rais,akawa na kazi yakumzuia Mange Kimambi,sijui alikua anataka kumpa zawadi gani Mh Rais!

Sasa nauliza,huu Ulinzi mzito wa Mh Rais wetu,hua ni wa hapa kwetu, Tanzania pekee?? Mbona wao wakija hapa kwetu hua wanaweka Ulinzi mzito hadi kupanda kwenye paa letu la Ikulu? Airport yetu wanaichukua kwa mda wote ambao Rais wao yupo?? Je tunawaamini sana kwa ulinzi wa kiongozi wetu,ila wao hawatuamini kwa ulinzi wa kiongozi wao??
Walinzi wa connection hawajui wajibu wao
 
Mange Kimambi ni mtanzania anayeishi Marekani.

Alijizolewa umaarafu kwa kupinga wazi wazi sera za Hayati JPM. Alishangalia kifo cha JPM na kuweka mitandaoni.

Bila kujadili kama alikua sahihi kumpinga JPM kulikua na ulazima kwa wanausalama kumruhusu kupiga picha na Raisi Samia.

Kulikua na ulazima taasisi ya uraisi kujishugulisha na Mange Kimambi?

Kwa upande wangu haikua sahihi na one of the security protocols blunder.
 
Chief Hangaya sio adui wa Mange.

Adui wa Mange walikuwa
-Magufuli
-Makonda
-Na yule Sheikh
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom