Ulinzi wa ajabu Central Police kwa ajili ya Mbowe; asafirishwa kwa ndege ya JWTZ kwenda Arusha!

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Haijawahi tokea Central kukawa na ulinzi kama huu.

Kituo kikuu kimezingirwa na askari wa kutuliza ghasia wengi sana ambao wote wamejitanda vizuri sare za kivita na bunduki mikononi mwao. Hakuna ruhusa ya mtu yoyote kuingia ndani ya kituo.

Viongozi wa CHADEMA wamehoji kuhusu namna Mbowe atakavyosafirishwa kwenda Arusha wakajibiwa kuwa hilo ni juu ya jeshi. Watamsafirisha kwa usafiri wa jeshi kwa saa wanayotaka wao.

Inaonekana kuwa watamsafirisha usiku huu huu ama alfajiri sana kesho. Kuna wasiwasi kuwa watamchoma sindano ili apoteze fahamu hadi atakapofikishwa Arusha.

Lolote litakalotokea sisi tunaamini kuwa saa ya Mungu ya kuikomboa Tanzania imefika.

============

UPDATED:

Wakuu,

Dakika tano zilizopita (Juni 6, 2011) saa 1:35 ndege ya jeshi iliyombeba Freeman Mbowe imetua Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro International Airport. (KIA)

Sasa ndo wanapanga msafara kwa ajili ya kumsafirisha kwenda Arusha Mjini.
 
Tuwe makini asije chomwa sindando ya kuwa zuzu maana msimamo wa mbowe unawaumiza sana ccm. Vp kuna mtu atatoa eskot?
 
Mbona mmenitisha sana jamani,hivi hawa ccm wanataka nini jamani?
 
duh,comred tunamwombea awe jasiri. .his return wil be with huge impact kwa wapenda harakati,wanachadema na wenye kiu ya mabadiliko!. . ILA HAPO KWENYE SINDANO,duh u hv just spoiled my night.
 
Huku mtaani majambazi yanatumaliza, hatuna ulinzi, lakini polisi wanaokena kupiga kambi kwa Mbowe!
Kwa upande mwingine hiki ndicho kinaitwa 'STATE INTIMIDATION' and believe you me, magogoni hawatafurahia hata kidogo hayo maneno yakianza kutamkwa na wakina uncle Sam. It will be the begining of something unpleasant to the elite.
 
lazima atachomwa sindano ya sumu,watu wengi waliofariki kama sheikh kassim wa msikiti wa mtoro alifanywa hivyo hivyo
 
Naomba kuuliza wanajf na wanachadema kama mbowe atauwawa kwenye harakati hizi mtafanya nini?
 
Natoa rai kwa watanzania sasa tuingie barabarani

Ili-mtimize ajenda yenu yakuonyesha CDM ni chama cha fujo. Nyie tafuteni long-term soln hamuwezi kuwa-convince wananchi hali ya uchumi ni nzuri kwakumkamata Mbowe. Timizeni wajibu wenu wakuondoa matatizo ya mwananchi wa kawaidia; otherwise asipokuwapo Mbowe mwingine atakuwapo kuwakomboa wananchi. CCM kwanini hamuoni mbali lakini argh!
 
Jana tumevamiwa na vibaka tena uso kwa uso na kituo kdg cha polisi wameiba dukan na kupiga baadh ya watu vyumbani kisa polic hawakuwepo lindo. Kumbe wanachagua mahal na nan wa kumlinda?. Shame on dem
 
Jamaa mafia wanaweza mpa msosi wenye sumu ya kumuua taratibu humour maabusu....puuuuuuuuu Mungu apishie mbali. Washindwe na walegee CHAMA CHA MAJASUSI
 
Tunasubili kusikia viongozi wetu watatwambia tufanye nini. Tuko tayari kwa lolote. Ni heri kufa na mawazo yanayoishi kuliko kuishi na mawazo yaliyokufa. Dr. Slaa, tell us what to do.

Pamoja na kuwa kumkamata Mbowe ni kuipandisha chati CDM lakini nina uhakika viongozi wetu wanaonewa sana. Pasipo na kosa wanatengenezewa kosa!
 
Kwa kila hatua ya kulipiza inayofanywa na serikali hii ndivyo itakavyowaongezea Umaarufu watu hawa na chama... Yaani inaonyesha wazi kwamba serikali yetu imejikiza zaidi ktk siasa kuliko ujenzi wa Taifa..CCM wanazidi kujichimbia kaburi kwa sababu huwezi kutumia nguvu ktk siasa unazidisha chuki ya wananchi na mwisho wa yote utashindwa tu...
 
Jihadharini enyi watu wa mngu ili msitembee katika njia za wale ambao maneno yao hutofautiana na matendo yao jitahidini ili muwezeswe kudhihirisha kwa watu wa dunia ishara za mungu na kuonyesha nje na ndani amri zake acha matendo yenu yawe uongozi kwa binadamu wote kwa kuwa shughuli za watu wengi wadogo kwa wakubwa hutofautiana na mwenendo wao ni kwa njia ya matendo yenu mnaweza kujitofautisha na wengine kwakupitia hayo uangavu wa nuru yenu kutawanywa juu dunia nzima ni mwenye furaha mtu yule ambaye husikia ushauli wa mungu na hushika amuri zilizo agizwa na yeye ambaye ni mjuwa yote(mungu) mwenye hekima kabisa
 
Wanajf ahayo ndio mapinduz ya kwel na kila cku mimi namini mapinduz si lele mama lazima yaje kwa misukosuko kama hii cha muhimu tuendelee na mapambano refer to Egypty&TUNISIA.
 
Back
Top Bottom