Ulinzi wa ajabu Central Police kwa ajili ya Mbowe; asafirishwa kwa ndege ya JWTZ kwenda Arusha!

Haijawahi tokea Central kukawa na ulinzi kama huu.

Kituo kikuu kimezingirwa na askari wa kutuliza ghasia wengi sana ambao wote wamejitanda vizuri sare za kivita na bunduki mikononi mwao. Hakuna ruhusa ya mtu yoyote kuingia ndani ya kituo.

Viongozi wa CHADEMA wamehoji kuhusu namna Mbowe atakavyosafirishwa kwenda Arusha wakajibiwa kuwa hilo ni juu ya jeshi. Watamsafirisha kwa usafiri wa jeshi kwa saa wanayotaka wao.

Inaonekana kuwa watamsafirisha usiku huu huu ama alfajiri sana kesho. Kuna wasiwasi kuwa watamchoma sindano ili apoteze fahamu hadi atakapofikishwa Arusha.

Lolote litakalotokea sisi tunaamini kuwa saa ya Mungu ya kuikomboa Tanzania imefika.

============

UPDATED:

Wakuu,

Dakika tano zilizopita (Juni 6, 2011) saa 1:35 ndege ya jeshi iliyombeba Freeman Mbowe imetua Uwanja wa Ndege wa Kilimanjaro International Airport. (KIA)

Sasa ndo wanapanga msafara kwa ajili ya kumsafirisha kwenda Arusha Mjini.

Hyperbole
 
Mbowe usilalamike eti serikali wametumia fedha nyingi za wananchi kumpeleka Arusha, mbona useme pesa za wananchi Ruzuku mnazotumutia kwenye maandamano yenu yasikuwa na tija kwa taifa, posho mnazolipana kila baada ya maandamano

Wewe ni mjinga, kwani kazi ya chama cha siasa ni ipi? Au ulifikiri ni kupeleka ruzuku yao kwenye shuhuli za maendeleo? Cdm wanafanya siasa na ndiyo kazi ya ruzuku wala si vinginevyo
 
Hawa Polisi ni semi-literate. Kivuyo na Kagonja wanatamka bila aibu au kusita kwamba hakuna mtu yeyote ambaye hawezi kukamatwa!!! Hawajasoma Ibara ya 100 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayotoa kinga kwa Wabunge?

Umbu mbu mbu wa viongozi wetu katika Jeshi la Polisi utatupeleka pabaya.

Na umbumbu wao utawagharimu maana siku si nyingi watapaswa kuwakamata wanaowatuma sasa sijui watasema nini kwa watanzania
 
Wewe ni mjinga, kwani kazi ya chama cha siasa ni ipi? Au ulifikiri ni kupeleka ruzuku yao kwenye shuhuli za maendeleo? Cdm wanafanya siasa na ndiyo kazi ya ruzuku wala si vinginevyo

Kwa hiyo kazi ya ruzuku ni maandamano na kugawana posho kila maandamano? wewe kweli pumba kabisa
 
Makadirio ya Gharama za Drama ya Polisi na Mbowe

Helicopter Expenses(Fuel) 4,650,000/=Go & Return
Pilot and Co-pilot@ 300,000 1,200,000/=
Helicopter staff(6pax) @100,000 1,200,000/=
Police escort Dar-Ars(10Police)@50,000 askari waliopanda chopper 1,000,000/=
Police escort Central to JNIA 8cars full tank @200,000 1,600,000/=
Police escort Central to JNIA 8CARS@10Police staff@50,000 allowance 4,000,000/=
Police escort Ars Airport to court 10cars full tank @200,000 2,000,000/=
Police escort Central to JNIA 10CARS@10Police staff@50,000 allowance 5,000,000/=
TISS allowances Dar 3,000,000/=
TISS allowances Ars 3,000,000/=
SUB TOTAL 26,650,000/=
Uchakachuaji = Sub total 26,650,000/=
Kimjini mjini for Riz1 and others= Uchakachuaji 26,650,000/=
Time wasted,Depreciation of Assets(Choper and cars etc) 26,650,000/=
GRAND TOTAL 106,600,000/=(Millioni Mia moja na sita Laki sita)

JAMANI PESA HIZI ZINGENUNUA VITANDA DOUBLE DECKER 1,776(Kila kitanda Tsh.60,000) KWA WANAFUNZI 3,550 KWA MABWENI YA SHULE ZETU ZA KATA.

KARIBUNI TANZANIA KILA KITU KINAWEZEKANA ISIPOKUWA KUMSAIDIA MTANZANIA!!!!!!!!!!!!
Mkuu unaonekana unajua hesabu vizuri, ebu tunaomba utupigie hii hesabu, posho za maandamano viongozi wakuu wanapokea 500,000 kila maandamano wabunge wao wanapokea posho 300,000 kila baada ya maandamano, halafu mkuu piga na ile hesabu ya Helicopta kipindi cha kampeni chote, tunasubiri mkuu hesabu
 
Gharama za kufanya yote waliyoyafanya kumweka hapo police central kumsafirisha hadi airport kumpakia kwenye ndege tena ya jeshi hadi kia escort toka kia hadi mahakamani halafu eti anatakiwa abadilishe mdhamini ni wake hii ni aibu kubwa sana...

Kwa wale ambao hawajui gharama hiyo siyo chini ya ten million..

Serekali inapashwa kutoa msimamo wao haraka sana....
 



• Ni mtuhumiwa wa kwanza kupelekwa mahakamani kwa ndege
• Ulinzi, usafiri wake Arusha watumia mamilioni ya walipakodi
• Makamanda CHADEMA waungana naye kuonyesha umoja

Eliya Mbonea na Abraham Gwandu, Arusha



KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Hai kwa tiketi ya CHADEMA, Freeman Mbowe ameachiwa huru kwa kufutiwa hati ya kukamatwa, huku akiweka rekodi ya kuwa mmoja wa watuhumiwa wachache waliowahi kupelekwa mahakamani kwa ndege.

Mbowe alikamatwa jijini Dar es Salaam juzi na polisi waliokuwa wakitekeleza amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, iliyotaka akamatwe, akidaiwa kudharau amri ya kumtaka ahudhurie kesi inayomkabili.

Mshitakiwa huyo wa kwanza katika kesi ya kufanya kusanyiko lisilo halali inayomkabili yeye na viongozi wengine wa CHADEMA, akiwamo Katibu Mkuu, Dk. Willbroad Slaa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, mchumba wa Dk. Slaa, Josephine Mushumbusi, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndensamburo, viongozi na wanachama wengine wa chama hicho ambao walitakiwa kufika mahakamani hapo Mei 27 mwaka huu.

Vurugu za Dar es Salaam
Baada ya kukamatwa jijini Dar es Salaam juzi, wafuasi kadhaa wa CHADEMA waliandamana hadi katika Kituo Kikuu cha Polisi kilichopo barabara ya samora, wakishinikiza aachiwe kwa dhamana, ombi ambalo lilikataliwa na polisi ambao walisema walimkamata kutokana na amri ya Mahakama.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, aliwaambia waandishi wa habari kwamba kukamatwa kwa kiongozi huyo kunatokana na amri ya Mahakama ya Arusha na kwamba kulikuwa hakuna uwezekano wa kumwachia kwa dhamana, bali kumpelaka Arusha Ambato ndiko mahakama iliyoamuru akamatwe ilikuwa na mamlaka ya kumwachia kwa dhamana au la.


Kutokana na wingi wa wafuasi wa CHADEMA waliojitokeza katika kituo hicho cha polisi, ulinzi mkali uliimarishwa, huku waakiitwa askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) pamoja na Magari ya deraya yanayotumika kutawanya makundi ya watu wanaoandamana kinyume cha sheria kwa kumwaga maji yanayowasha.

Saa mbili asubuhi yupo kortini
Habari zilizopatikana kutoka katika viwanja vya mahakama jijini Arusha zilisema kwamba polisi walilazimika kukodi ndege mapema jana asubuhi iliyombeba kiongozi huyo wa CHADEMA hadi Arusha ambako aliwasili mahakamani saa 2:13 asubuhi, akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliokuwa na silaha.


Baada ya kufikishwa mahakamani, Mbowe, ambaye aliwasili katika viwanja vya Mahakama akiwa kwenye gari ya Toyota Landcruiser nyeupe, aliingizwa moja kwa moja hadi chumba cha wazi cha mahakama hiyo.

Akizungumza ndani ya Mahakama, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Moka wa Arusha, Charles Magesa, alimuonya mshitakiwa kwa kitendo chake cha kukaidi amri ya Mahakama iliyomtaka kufika mahakamani kama ilivyokuwa imeamriwa bila ya kutoa udhuru wowote.

Mdhamini abadilishwa
Hakimu Mkazi Magesa pia aliutaka upande wa washitakiwa kumbadilisha mdhamini wa Mbowe, Isaya Magwa, kutokana na kukabiliwa na kesi nyingine katika Mahakama ya Mwanzo ya Maromboso ya mjini hapa.


Awali, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Juma Ramadhani, aliiomba Mahakama kutoa onyo kwa mshitakiwa ili iwe fundisho kwa watuhumiwa wengine wanaokaidi amri halali zinazotolewa na Mahakama.

Akihitimisha hoja zake, Mwendesha Mashitaka huyo alisema kwa vile hapakuwa na ugumu wowote wa kupatikana kwa mshtakiwa huyo na kwamba upande wa Serikali hauoni haja ya kwa nini amri hiyo ya kukamatwa kwake pamoja na kunyimwa dhamana yake visifutwe.

Naye Wakili wa Upande wa Utetezi, Method Kimomogolo, akisaidiana na Wakili Albert Msando, ambao ndiyo wanaowatetea watuhumiwa 19 katika kesi hiyo, alidai kuwa mteja wake hakukaidi amri halali ya Mahakama iliyomtaka kufika mahakamani Mei 27, bali alishindwa kufika kutokana na majukumu yaliyokuwa yakimkabili ya maandalizi ya vikao vya Bunge la bajeti linaloanza leo mjini Dodoma. Alidai mdhamini wa mshtakiwa alifika mahakamani hapo kutoa udhuru.

Baada ya kuhitimisha kutoa hoja za utetezi, Hakimu Magesa alimtaka mdhamini wa mshtakiwa kwanza, Magwa, kueleza ni kwa nini Mahakama hiyo haikupata taarifa za udhuru wake.

Hata hivyo, katika maelezo yake yaliyoonyesha kujichanganya kwa kutaja tarehe na siku tofauti, mdhamini Magwa alidai alikuwapo siku hiyo isipokuwa Mahakama haikumpa fursa ya kutoa taarifa za udhuru wa Mbowe.

Maelezo hayo yalimfanya Hakimu Magesa kumuuliza tena mdhamini huyo siku na tarehe aliyodai kuwa alifika mahakamani hapo na mahakama kushindwa kupokea taarifa ya udhuru wa mshtakiwa Mbowe wakati washtakiwa wengine katika kesi inayowakabili kwa pamoja, wadhamini wao walitoa taarifa, Edipo mshitakiwa huyo alipoanza kujikanganya.

Kutokana na mdhamini huyo kujikanganya katika maelezo yake, Wakili wa Serikali alitaka maelezo ya mdhamini huyo aliyemwita muongo, yasizingatiwe na mahakama hiyo na kwamba upande wa washitakiwa utafute mdhamini mwingine atakayeaminiwa na pande zote, jambo lililokubaliwa na pande zote.

Baada ya pande zote kuridhika na hatua hiyo, ndipo Diwani wa Kata ya Elerai, John Bayyo (Chadema) alipojitokeza kumdhamini Mbowe.

Wabunge waombewa ruhusa
Mahakama pia ilikubali ombi la upande wa utetezi la kuwaombea tena ruhusa kwa pamoja, washitakiwa ambao ni wabunge ili waweze kuhudhuria vikao vya Bunge la bajeti.


Mshitakiwa mwingine aliyeombewa udhuru wa kutokuwapo mahakamani hapo kutokana na kukaribia kujifungua ni mchumba wa Dk. Slaa, Mushumbusi, ambaye anatarajiwa kujifungua wakati wowote. Kesi hiyo imepangwa kuendelea tena Juni 24 mwaka huu.

Katika kusisitiza ruhusa ya washitakiwa ambao ni wabunge imekubaliwa, Wakili wa Serikali Ramadhani, alikubaliana na maombi ya upande wa utetezi juu ya washitakiwa hao kutohudhuria mahakamani Juni 24 mwaka huu, lakini aliomba muda kwa mshitakiwa Mushumbusi kutokana na suala lake kugusa masuala ya utabibu.

Polisi wawa wapole mahakamani
Baada ya Mahakama kufuta amri ya awali iliyokuwa ikitaka Mbowe akamatwe na kisha afutiwe dhamana, mamia ya wafuasi wa CHADEMA waliokuwa wamefurika katika viwanja vya jengo la Mahakama, walipiga kelele za kumshangilia kiongozi huyo.


Huku wakiwa na bendela za chama chao na wakiimba nyimbo mbalimbali, wafuasi hao walionekana kutaka kujua kila jambo lililokuwa likiendelea katika ukumbi wa Mahakama, huku polisi, ambao situ zote huonyesha kuwa wakali, wakiwaacha wafanye watakavyo.

Hata baada ya suala hili kumalizwa kistaraabu na bila ya mvutano wowote wa kisheria, wafuasi hao wa Chadema waliondoka huku wakiimba nyimbo mbalimbali na wengine wakipiga kelele kuonyesha ishara ya ushindi kwa kiongozi wao kuendelea kubaki nje.

Makamanda waonyesha mshikamano
Wabunge kadhaa wa CHADEMA, wakiwamo Kabwe Zitto, Lema, Halima Mdee, Israel Natse, Joseph Mbilinyi, Susan Kiwanga, Paulina Gekul, Raya Ibrahimu, Christna Mughway na Susan Lyimo, wakiongozwa na Katibu Mkuu, Dk. Slaa, pia walifika mahakamani hapo kuonyesha mshikamano na mwenyekiti wao.


Wabunge wengine waliohudhuria mahakamani hapo baadaye kuonyesha mshikamano wao kwa mwenyekiti wao ni Joseph Selasini, Ezekiah Wenje, Tundu Lisu pamoja na na Wakili Mabere Marando.

Hivi karibuni, Mahakama hiyo iliwafutia pia amri ya kuwataka wakamatwe baadhi ya viongozi wa chama hicho kwa kosa kama la Mbowe la kushindwa kufika mahakamani katika situ iliyopangwa bila ya kutoa taarifa yeyote. Viongozi walioanza kufutiwa amri ya kutakiwa kukamatwa ni Dk. Slaa, Lema, Aquileni, Joseph Mtui.
 
Du, kumbe serikali ina pesa za kutosha kwa ajili ya kuwashughlikia wapinzani. Niseme tu ukweli, tangu nizaliwe sijawahi panda ndege ya kukodi, lakini tumeshuhudia juzi Mheshimiwa Mbowe amechukuliwa kwa ndege ya Jeshi kutoka Dar to Kia. Na Dar alisindikizwa na Magari 8 full armed.

Kufika KIA nako kapokelewa na kundi la Polisi full armed. Mimi kwakweli sijaona mantiki ya kufanya hayo yote wakati mtu alijipeleka mwenyewe kituoni.

Je, Pesa iliyotumika kwa ajili ya kuhangaika na Mbowe itarudi vipi? Je, huu si ufisadi mwingine?
 
Kukosa elimu ni mama ya ujinga.
Hivi jeshi letu lina ndege ya kubeba watu 100?
Na je hao watatu waliokuwemo mmoja ni Mbowe mwingine askari na wa tatu ndo rubani au siyo?
Tha only explains the level of knowledge of some JF members
 
Kukosa elimu ni mama ya ujinga.
Hivi jeshi letu lina ndege ya kubeba watu 100?
Na je hao watatu waliokuwemo mmoja ni Mbowe mwingine askari na wa tatu ndo rubani au siyo?
Tha only explains the level of knowledge of some JF members

Mkuu Acha dharau, we ni gamba nini? Mbona hutaki kusoma unakimbilia kutukana? Ok, soma hapa na si kukurupuka kama magamba menzio.

"Wamenisafirisha kuja Arusha kwa ndege ya JWTZ kama mtuhumiwa wa ujambazi. Haya ni matumizi makubwa ya fedha na rasilimali za umma. Ile ndege ina uwezo wa kubeba zaidi ya watu 100, wametuleta watu watatu, mimi kama mtuhumiwa, Kamishna mmoja wa polisi Wilaya ya Ilala na Kamishna wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)," alidai Mbowe.

Source: Mbowe huru, polisi watumia ndege ya JWTZ
 
hao maofisa walikuwa na hamu ya kupanda ndege hao, hakuna lolote hapao, walishindwaje kumwambia Mbowe aende mwenyewe Arusha?
 
Mkuu Acha dharau, we ni gamba nini? Mbona hutaki kusoma unakimbilia kutukana? Ok, soma hapa na si kukurupuka kama magamba menzio.

"Wamenisafirisha kuja Arusha kwa ndege ya JWTZ kama mtuhumiwa wa ujambazi. Haya ni matumizi makubwa ya fedha na rasilimali za umma. Ile ndege ina uwezo wa kubeba zaidi ya watu 100, wametuleta watu watatu, mimi kama mtuhumiwa, Kamishna mmoja wa polisi Wilaya ya Ilala na Kamishna wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)," alidai Mbowe.

Source: Mbowe huru, polisi watumia ndege ya JWTZ

Asante mkuu, it takes just a little intelligence kuamini au kutoamini kile mtu unachoambiwa-kwa kifupi akili mukichwa.
Ukiambiwa huko selo nilienda choo size ya tembo basi we ni mguu na njia kuandamana, ndo tuawaita wasukuma mikokoteni.
 
Kukosa elimu ni mama ya ujinga.
Hivi jeshi letu lina ndege ya kubeba watu 100?
Na je hao watatu waliokuwemo mmoja ni Mbowe mwingine askari na wa tatu ndo rubani au siyo?
Tha only explains the level of knowledge of some JF members

...Mwaka 2004 ...jeshi letu la anga lilinunuliwa ndege 2 kubwa zenye uwezo wa kubeba abiria[askari] 100 na vifaa vyao...pamoja na mizigo tani 30-40........inafunguka kwa pembeni na nyuma ....kuna mlango mkubwa wa kushushia magari/vifaru au askari pia hutumia njia hii kushuka kwenye hali ya medani......kipindi hicho hicho walinunuliwa Mig 8 toka china....,helicopter 6[hizi walitapeliwa kwani zilikuja 4 tu .....aina ya Augusta Bell..na wala hazikuwa na feutures za mapigano ya kisasa....na mbili zimeshaanguka...tapeli aliyeuza hizi anaitwa Vithlani....]......pia mwaka huo huo walinunuliwa malori ya aina mbali mbali[troop carrier,heavy duty carriers,water bousers,fuel tankers...caterpillar,winches,etc] yapatayo 1,000 toka Italia....

Itakuwa missuse of resource kama jeshi wameamua kutumia ndege yake kubwa ya medani kusafirisha watu watatu....kwani inajulikana wanazo ndege nyingine kama mbili ..light za abiria 15-28.....kwa usafiri wa kawaida.....hata hivyo HUWEZI JUWA KWANINI WALITUMIA NDEGE YENYE UWEZO MKUBWA ....LABDA WALIKUWA NA TAARIFA ZA KIINTELIGESIA ZA MSAFARA KUHUJUMIWA ANGANI.....WAKAONA WATUMIE NDEGE YENYE MFUMO WA KIULINZI NA UWEZO WA KUJIBU MAPIGO PALE INAPOSHAMBULIWA.....NASISITIZA NI TAARIFA ZA KIINTELIGESIA........NA NI WAZI ITAKUWA ILIPEWA ESCORT YA MiG 2 za ngerengere hadi inafika KIA.........Huwezi juwa bwana maadui wa nchi wangemtungua wangesababisha sintofahamu na kutuletea vita ya wenyewe kwa wenyewe.......kama Rwanda na Burundi walivyouwana baada ya viongozi wao kudunguliwa....
 
...Mwaka 2004 ...jeshi letu la anga lilinunuliwa ndege 2 kubwa zenye uwezo wa kubeba abiria[askari] 100 na vifaa vyao...pamoja na mizigo tani 30-40........inafunguka kwa pembeni na nyuma ....kuna mlango mkubwa wa kushushia magari/vifaru au askari pia hutumia njia hii kushuka kwenye hali ya medani......kipindi hicho hicho walinunuliwa Mig 8 toka china....,helicopter 6[hizi walitapeliwa kwani zilikuja 4 tu .....aina ya Augusta Bell..na wala hazikuwa na feutures za mapigano ya kisasa....na mbili zimeshaanguka...tapeli aliyeuza hizi anaitwa Vithlani....]......pia mwaka huo huo walinunuliwa malori ya aina mbali mbali[troop carrier,heavy duty carriers,water bousers,fuel tankers...caterpillar,winches,etc] yapatayo 1,000 toka Italia....

Itakuwa missuse of resource kama jeshi wameamua kutumia ndege yake kubwa ya medani kusafirisha watu watatu....kwani inajulikana wanazo ndege nyingine kama mbili ..light za abiria 15-28.....kwa usafiri wa kawaida.....hata hivyo HUWEZI JUWA KWANINI WALITUMIA NDEGE YENYE UWEZO MKUBWA ....LABDA WALIKUWA NA TAARIFA ZA KIINTELIGESIA ZA MSAFARA KUHUJUMIWA ANGANI.....WAKAONA WATUMIE NDEGE YENYE MFUMO WA KIULINZI NA UWEZO WA KUJIBU MAPIGO PALE INAPOSHAMBULIWA.....NASISITIZA NI TAARIFA ZA KIINTELIGESIA........NA NI WAZI ITAKUWA ILIPEWA ESCORT YA MiG 2 za ngerengere hadi inafika KIA.........Huwezi juwa bwana maadui wa nchi wangemtungua wangesababisha sintofahamu na kutuletea vita ya wenyewe kwa wenyewe.......kama Rwanda na Burundi walivyouwana baada ya viongozi wao kudunguliwa....

hahhahhaahahahaah,,, mkuu unanifurahisha sana, kweli data unazo, mpaka majina ya matapeli waliotuuzia ndege?? I thot hii inakuaga siri ya jeshi... I lyk watu wenye data kama wewe hapa jf,, u kip jf active
 
hivi huyo Vithlan si ndo huyo huyo alituuzia na Ndege ya Mkapa wakati ule wa Mramba kutulisha majani?
 
Du, kumbe serikali ina pesa za kutosha kwa ajili ya kuwashughlikia wapinzani. Niseme tu ukweli, tangu nizaliwe sijawahi panda ndege ya kukodi, lakini tumeshuhudia juzi Mheshimiwa Mbowe amechukuliwa kwa ndege ya Jeshi kutoka Dar to Kia. Na Dar alisindikizwa na Magari 8 full armed.

Kufika KIA nako kapokelewa na kundi la Polisi full armed. Mimi kwakweli sijaona mantiki ya kufanya hayo yote wakati mtu alijipeleka mwenyewe kituoni.

Je, Pesa iliyotumika kwa ajili ya kuhangaika na Mbowe itarudi vipi? Je, huu si ufisadi mwingine?


Ninajizuia kufikiria nini kingetokea iwapo jeshi la Polisi lingeamua kumsafirisha Mbowe kwa gari mpaka Arusha na pengine ikatokea ajali njiani akadhurika au kutodhurika kabisa! Kwa mwenendo wa wafuasi wake .............. nini kingetokea? Inahitaji busara ya kuzaliwa sio ya .com
 
UKITAKA KUONA MTU ALIVYO MJINGA ANGALIA VIPAUMBELE VYAKE. Kweli hii serikali inaongozwa na majuha. HIYO FEDHA SI INGENUNULIA HATA VITANDA VYA HOSPITALI YA MOMBO WARD YA WAJAWAZITO?
KWANI MBOWE ANA HATARI GANI HIYO? NADHANI WALITAKA WAFANYE JAMBO BAYA LAKINI WAMEOGOPA NGUVU YA UMA. HII MAHAKAMA INATISHA
UNIQUE
 
Back
Top Bottom