Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,901
- 453,461
Mtunzi
*NYEMO CHILONGANI*
*ULINIUA GLORIA*
*Sehemu ya 01*
Kelele za shangwe zilikuwa zikisikika kutoka katika nyumba ya mzee Steven. Vigelegele kutoka kwa wakinamama vilikuwa miongoni mwa sauti za shangwe zilizoendelea kusikika kutoka ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa imejengwa kisasa katika Mtaa wa Magomeni Kondoa.
Magari kadhaa yalikuwa yamekusanyika ndani ya eneo la nyumba hiyo, idadi kubwa ya magari hayo yalikuwa ya kifahari ambayo wala hakukuwa na mtu ambaye alishangaa kuyaona yakiwa yamepakiwa ndani ya eneo la nyumba hiyo.
Sauti ya muziki ilikuwa juu ingawa wakati mwingine ilikuwa ikipunguzwa kutokana na mtu yeyote ambaye alikuwa akitaka kuongea lake katika hafla hiyo fupi ya kuwapongeza Peter na Gloria ambao walikuwa wakitarajia kufunga ndoa mwezi mmoja baadae ndani ya Kanisa la Praise and Worship lililokuwa Mwenge.
Wote ndani ya nyumba hiyo walionekana katika nyuso zilizokuwa na furaha, walipenda kuwaona watoto wao wakiingia katika maisha ya ndoa, maisha yaliyoonekana kutamaniwa na watu ambao walikuwa nje nayo lakini kuchukiwa na watu ambao tayari walikuwa ndani ya maisha hayo.
Gloria hakuwa mbali na Peter, muda wote alikuwa pembeni yake huku akipigapiga picha kwa kutumia simu yake katika kila tukio lililokuwa likiendelea mahali hapo. Kazi kubwa ya Peter ilikuwa ni kukishika kiuno cha Gloria, kumbusu mara kwa mara huku akimuachia tabasamu pana.
Baba yake Peter, mzee Steven alionekana kuwa mwenye furaha kubwa, muda wote alipokuwa akiongea, alikuwa akitabasamu tu huku akionekana kuzidiwa na furaha ambayo alikuwa nayo kwa kile kitu ambacho kilikuwa kinaendelea.
Katika maisha yake alibahatika kupata watoto wawili tu, wa kwanza alikuwa Rachel ambaye alikuwa amekwishaolewa na wa pili alikuwa Peter ambaye baada ya siku kadhaa nae angeanza maisha ya ndoa na msichana Gloria Michael.
Katika sherehe hiyo, wazazi wake Gloria, mzee Michael Mshama na Bi Justina walikuwa miongoni mwa watu ambao walikuwa wamekusanyika katika hafla hiyo fupi ya kuwapongeza kwa hatua ile waliyokuwa wameifikia.
Mpaka kufikia katika kipindi hicho, wao pia walionekana kuwa na furaha kubwa, hawakuamini kama binti yao, Gloria alikuwa akitarajiwa kufunga ndoa na baada ya hapo kuitwa mke wa mtu huku ukichukua muda mchache kabla ya kuitwa mama.
Gloria ndiye alikuwa binti yao ambaye walikuwa wakimpenda kupita kawaida, walimthamini na kumpa kila kitu ambacho kama wazazi walitakiwa kumpa binti yao mpendwa. Kwao, Gloria ndiye alikuwa kila kitu, yeye ndiye alikuwa tabasamu nyusoni mwao.
Ukaribu wa Peter na Gloria ulianza tangu walipokuwa darasa la pili katika Shule ya Msingi ya Mwalimu Nyerere huku baada ya kufika kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Benjamini wakaanza kuingia katika uhusiano wa kimapenzi. Ingawa walikuwa na furaha lakini uhusiano wao ulionekana kuwa na vizuizi vingi huku kizuizi kimoja na kikubwa kikiwa ni masomo.
Walitamani kufanya mambo mengi katika maisha yao kwa wakati huo lakini masomo ndio kilikuwa kizuizi kikubwa. Muda mwingi walikuwa wakitamani kusoma pamoja lakini kila walipojaribu kufanya hivyo, walijikuta wakianza kushikanashikana na hatimae kulaliana na kufanya mapenzi.
Kila mmoja kichwani alikuwa na ndoto yake ambayo alikuwa amejiwekea. Peter alikuwa na hamu kubwa ya kuwa Mchumi mkubwa hapo baadae huku Gloria akiwa na hamu ya kuwa Mwanasheria mkubwa hapo baadae. Kila mmoja alikuwa akiishi katika ndoto yake ambayo ilikuwa ikiendelea kukua kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Wakamaliza kidato cha nne na kukaa nyumbani kusubiri matokeo, yalipotoka, kila mmoja alikuwa amefaulu vizuri ila kwa wakati huu kila mmoja alikuwa akielekea kusoma tofauti na mwenzake. Peter alichaguliwa kujiunga na shule ya Tambaza huku Gloria akichaguliwa kujiunga na shule ya Zanaki zote zikiwa jijini Dar es Salaam.
Kidogo sana ukaribu wao ukaanza kupungua, mambo yakaanza kubadilika, kila mtu akaanza kuukumbuka ukaribu ambao alikuwa nao kwa mwenzake katika kipindi kile ambacho walikuwa shule moja, tena darasa moja.
Simu ndicho kilikuwa chombo cha mawasiliano ambacho walikuwa wakipenda kukitumia kuwasiliana, ingawa walikuwa mbalimbali lakini simu zikaonekana kuwafanya kuwa karibu sana. Kila siku walikuwa wakiwasiliana usiku, walikuwa wakichukua muda mwingi kuongea simuni, mchana wakiandikiana meseji mbalimbali na wakati mwingine kuonana faragha.
Ingawa walikuwa wakifanya mambo mengi kama wapenzi lakini kamwe hawakusahau kuhusu Elimu, walikuwa wakiendelea kusoma zaidi na zaidi huku upendo wao ukiendelea kukua kadri siku zilivyokuwa zikizidi kusonga mbele.
Wakafanikiwa kumaliza kidato cha sita na wote kuchaguliwa chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Walionekana kuwa na furaha kupita kawaida, wakaanza kusoma huku ukaribu wao ukiwa wazi kabisa na kutambulishana kwa wazazi wao.
Hiyo ilikuwa ni furaha kwao na kwa wazazi wao pia, wakaamua kuanza kufanya vitu kwa wazi kabisa kwani hawakuwa wakihofia kitu chochote kwa wakati huo. Mwaka wa kwanza ukakatika, mwaka wa pili ukaingia na ndipo walipoamua kuwaeleza wazazi juu ya lengo lao la kutaka kufunga ndoa na kuwa pamoja.
Taarifa hiyo ikaonekana kuwa ya furaha kwa wazazi wao, wakatoa baraka zote na kuwaruhusu kwa moyo mmoja vijana wao kuoana na kuishi pamoja. Siku zilikuwa zimekatika sana, maandalizi ya harusi yalikuwa yamefanyika vya kutosha na katika kipindi hiki zilikuwa zimebakia siku thelathini kabla ya kufungwa kwa harusi hiyo kanisani.
Wazazi waliongea sana katika hafla hiyo fupi isiyokuwa na watu wengi huku kila mmoja akijaribu kuionyesha furaha yake ya waziwazi mahali pale walipokuwa. Kila mmoja alipomaliza kuongea, Peter akatakiwa kuongea kitu chochote alichokuwa nacho moyoni hata kabla ya Gloria nae kuitwa na kuongea.
“Sijui niseme nini. Yaani najiona nimezidiwa na furaha kabisa. Kila ninapomuangalia Gloria nakumbuka kipindi kile alipokuwa mdogo na kuanza kuelekea nae shuleni. Unakumbuka Gloria?” Peter alisema na kumuuliza Gloria.
“Nakumbuka. Ila sikuwa mdogo peke yangu. Sema tulikuwa wadogo,” Gloria alimwambia Peter na kuwafanya watu wote mahali pale kuanza kucheka.
“Nafahamu. Ila si unakumbuka kwamba nilikuwa mtu wa kwanza kukuvusha barabara? Nisingekuwa makini na wewe ungekuwa umekwishagongwa na gari.
Nilianza kukulinda toka zamani sana, japokuwa tulikuwa wadogo lakini bado nilikuwa nikikuonyeshea jinsi gani ninakuthamini na kukulinda, sikutaka uvuke barabara peke yako, nilikuwa nikikushika mkono na kukuvusha barabara. Ulinzi ule ule ambao nilikuwa nikikupa toka utotoni ndiyo ulinzi ule ule ambao nitaendelea kukupa hadi uzeeni,” Peter alisema huku akimwangalia Gloria.
Watu wote waliokuwa wamekaa sebuleni pale wakabaki kimya, maneno ambayo alikuwa akiyaongea Peter yalionekana kuwa maneno mazito ambayo kwa msichana yeyote angeyasikia ni lazima angejiona ni kwa namna gani alikuwa akipendwa na kuthamaniwa.
“Naona siku ya harusi ni mbali sana, acha nianze kukuahidi leo hii hii hata kabla ya harusi yenyewe,” Peter alisema huku akimnyanyua Gloria na kuupitisha mkono katika kiuno cha Gloria na kisha kuendelea.
“Nakuahidi kuwa nawe katika maisha yangu yote, nakuahidi kukupenda katika shida na raha, magonjwa na afya, furaha na maumivu. Naahidi kukupenda katika kila hatua ya maisha ambayo tutayapitia baada ya kuingia katika ndoa,” Peter aliwambia Goria ambaye alibaki kimya huku kwa mbali macho yake yakianza kulengwa na machozi.
Peter akabaki kimya kwa muda, alikuwa akimwangalia Gloria usoni, kwake, Gloria akaonekana kuwa mtu mpya, msichana mpya ambaye alikuwa ameongezewa uzuri zaidi ya ule ambao alikuwa nao kabla.
Lipsi za midomo yake zilikuwa zikichezacheza tu huku akizitamani lipsi za Gloria. Alipoona ameridhika kumwangalia Gloria, akayarudisha macho yake kwa wazazi wa Gloria, mzee Michael na Bi Justina.
“Nimeahidi mengi, nimeahidi kumtunza binti yenu katika njia iliyo njema. Ninawaomba ninyi pia mniruhusu kumchukua binti yenu, muda wenu wa kumlea naona unafikia tamati, sasa hivi nadhani ni muda wangu kumlea binti huyu mrembo, binti huyu aliyeuteka moyo wangu,” Peter aliwaambia mzee Michael na Bi Justina.
Ilipofika zamu ya Gloria kuongea, akashindwa kabisa kuongea kitu chochote kile, akaamua kumkumbatia Peter na kuanza kulia. Maneno ambayo aliyaongea Peter yalikuwa yamemgusa, aliyaona maneno mazito ambayo yalikuwa yakijirudia rudia moyoni mwake.
“Nakupenda Peter. Nakupenda mpenzi,” Gloria alimwambia Peter huku wakiwa wamekumbatiana.
“Nakupenda pia Gloria,” Peter alimwambia Gloria.
Baada ya hapo, wote wakatawanyika na kuyafuata magari yao. Peter hakutaka kumuacha Gloria mikononi mwake, alikuwa amemshikilia vilivyo japokuwa mzee Michael alikuwa akimuita.
Wote wakabaki wakiangaliana tu, mapenzi ambayo waliyokuwa nayo mioyoni mwao yalikuwa yakiendelea kuchipuka.
“Ninakupenda sana Gloria,” Peter alimwambia Gloria.
“Ninakupenda pia.”
Baada ya hapo, Gloria akaingia garini na kuondoka mahali hapo. Muda wote huo Peter alikuwa amesimama tu mpaka pale gari lilipotoka machoni mwake. Akaanza kupiga hatua na kuelekea ndani ambapo akapitiliza hadi chumbani.
Alipofika chumbani, akaanza kuchati na Gloria huku akionekana kuwa na furaha tele. Waliendelea kuchati mpaka saa tisa usiku, muda ambao akapitiwa na usingizi kitandani pale. Ingawa meseji zilikuwa zikiendelea kuingia, Peter alikuwa amekwishalala kitambo kutokana na uchovu mkubwa ambao alikuwa nao siku hiyo.
“Nakupenda mpenzi. Najua umeshalala, ila utakapoamka naomba ujue kwamba ninakupenda sana. Mwaaaaaaaa! Hiyo ni kwa ajili yako peke yako” Hiyo ilikuwa ni meseji ya mwisho ambayo Gloria alikuwa amemuandikia Peter ambaye alikuwa amekwishalala.
*Je, nini kiliendelea?*
*NYEMO CHILONGANI*
*ULINIUA GLORIA*
*Sehemu ya 01*
Kelele za shangwe zilikuwa zikisikika kutoka katika nyumba ya mzee Steven. Vigelegele kutoka kwa wakinamama vilikuwa miongoni mwa sauti za shangwe zilizoendelea kusikika kutoka ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa imejengwa kisasa katika Mtaa wa Magomeni Kondoa.
Magari kadhaa yalikuwa yamekusanyika ndani ya eneo la nyumba hiyo, idadi kubwa ya magari hayo yalikuwa ya kifahari ambayo wala hakukuwa na mtu ambaye alishangaa kuyaona yakiwa yamepakiwa ndani ya eneo la nyumba hiyo.
Sauti ya muziki ilikuwa juu ingawa wakati mwingine ilikuwa ikipunguzwa kutokana na mtu yeyote ambaye alikuwa akitaka kuongea lake katika hafla hiyo fupi ya kuwapongeza Peter na Gloria ambao walikuwa wakitarajia kufunga ndoa mwezi mmoja baadae ndani ya Kanisa la Praise and Worship lililokuwa Mwenge.
Wote ndani ya nyumba hiyo walionekana katika nyuso zilizokuwa na furaha, walipenda kuwaona watoto wao wakiingia katika maisha ya ndoa, maisha yaliyoonekana kutamaniwa na watu ambao walikuwa nje nayo lakini kuchukiwa na watu ambao tayari walikuwa ndani ya maisha hayo.
Gloria hakuwa mbali na Peter, muda wote alikuwa pembeni yake huku akipigapiga picha kwa kutumia simu yake katika kila tukio lililokuwa likiendelea mahali hapo. Kazi kubwa ya Peter ilikuwa ni kukishika kiuno cha Gloria, kumbusu mara kwa mara huku akimuachia tabasamu pana.
Baba yake Peter, mzee Steven alionekana kuwa mwenye furaha kubwa, muda wote alipokuwa akiongea, alikuwa akitabasamu tu huku akionekana kuzidiwa na furaha ambayo alikuwa nayo kwa kile kitu ambacho kilikuwa kinaendelea.
Katika maisha yake alibahatika kupata watoto wawili tu, wa kwanza alikuwa Rachel ambaye alikuwa amekwishaolewa na wa pili alikuwa Peter ambaye baada ya siku kadhaa nae angeanza maisha ya ndoa na msichana Gloria Michael.
Katika sherehe hiyo, wazazi wake Gloria, mzee Michael Mshama na Bi Justina walikuwa miongoni mwa watu ambao walikuwa wamekusanyika katika hafla hiyo fupi ya kuwapongeza kwa hatua ile waliyokuwa wameifikia.
Mpaka kufikia katika kipindi hicho, wao pia walionekana kuwa na furaha kubwa, hawakuamini kama binti yao, Gloria alikuwa akitarajiwa kufunga ndoa na baada ya hapo kuitwa mke wa mtu huku ukichukua muda mchache kabla ya kuitwa mama.
Gloria ndiye alikuwa binti yao ambaye walikuwa wakimpenda kupita kawaida, walimthamini na kumpa kila kitu ambacho kama wazazi walitakiwa kumpa binti yao mpendwa. Kwao, Gloria ndiye alikuwa kila kitu, yeye ndiye alikuwa tabasamu nyusoni mwao.
Ukaribu wa Peter na Gloria ulianza tangu walipokuwa darasa la pili katika Shule ya Msingi ya Mwalimu Nyerere huku baada ya kufika kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Benjamini wakaanza kuingia katika uhusiano wa kimapenzi. Ingawa walikuwa na furaha lakini uhusiano wao ulionekana kuwa na vizuizi vingi huku kizuizi kimoja na kikubwa kikiwa ni masomo.
Walitamani kufanya mambo mengi katika maisha yao kwa wakati huo lakini masomo ndio kilikuwa kizuizi kikubwa. Muda mwingi walikuwa wakitamani kusoma pamoja lakini kila walipojaribu kufanya hivyo, walijikuta wakianza kushikanashikana na hatimae kulaliana na kufanya mapenzi.
Kila mmoja kichwani alikuwa na ndoto yake ambayo alikuwa amejiwekea. Peter alikuwa na hamu kubwa ya kuwa Mchumi mkubwa hapo baadae huku Gloria akiwa na hamu ya kuwa Mwanasheria mkubwa hapo baadae. Kila mmoja alikuwa akiishi katika ndoto yake ambayo ilikuwa ikiendelea kukua kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Wakamaliza kidato cha nne na kukaa nyumbani kusubiri matokeo, yalipotoka, kila mmoja alikuwa amefaulu vizuri ila kwa wakati huu kila mmoja alikuwa akielekea kusoma tofauti na mwenzake. Peter alichaguliwa kujiunga na shule ya Tambaza huku Gloria akichaguliwa kujiunga na shule ya Zanaki zote zikiwa jijini Dar es Salaam.
Kidogo sana ukaribu wao ukaanza kupungua, mambo yakaanza kubadilika, kila mtu akaanza kuukumbuka ukaribu ambao alikuwa nao kwa mwenzake katika kipindi kile ambacho walikuwa shule moja, tena darasa moja.
Simu ndicho kilikuwa chombo cha mawasiliano ambacho walikuwa wakipenda kukitumia kuwasiliana, ingawa walikuwa mbalimbali lakini simu zikaonekana kuwafanya kuwa karibu sana. Kila siku walikuwa wakiwasiliana usiku, walikuwa wakichukua muda mwingi kuongea simuni, mchana wakiandikiana meseji mbalimbali na wakati mwingine kuonana faragha.
Ingawa walikuwa wakifanya mambo mengi kama wapenzi lakini kamwe hawakusahau kuhusu Elimu, walikuwa wakiendelea kusoma zaidi na zaidi huku upendo wao ukiendelea kukua kadri siku zilivyokuwa zikizidi kusonga mbele.
Wakafanikiwa kumaliza kidato cha sita na wote kuchaguliwa chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Walionekana kuwa na furaha kupita kawaida, wakaanza kusoma huku ukaribu wao ukiwa wazi kabisa na kutambulishana kwa wazazi wao.
Hiyo ilikuwa ni furaha kwao na kwa wazazi wao pia, wakaamua kuanza kufanya vitu kwa wazi kabisa kwani hawakuwa wakihofia kitu chochote kwa wakati huo. Mwaka wa kwanza ukakatika, mwaka wa pili ukaingia na ndipo walipoamua kuwaeleza wazazi juu ya lengo lao la kutaka kufunga ndoa na kuwa pamoja.
Taarifa hiyo ikaonekana kuwa ya furaha kwa wazazi wao, wakatoa baraka zote na kuwaruhusu kwa moyo mmoja vijana wao kuoana na kuishi pamoja. Siku zilikuwa zimekatika sana, maandalizi ya harusi yalikuwa yamefanyika vya kutosha na katika kipindi hiki zilikuwa zimebakia siku thelathini kabla ya kufungwa kwa harusi hiyo kanisani.
Wazazi waliongea sana katika hafla hiyo fupi isiyokuwa na watu wengi huku kila mmoja akijaribu kuionyesha furaha yake ya waziwazi mahali pale walipokuwa. Kila mmoja alipomaliza kuongea, Peter akatakiwa kuongea kitu chochote alichokuwa nacho moyoni hata kabla ya Gloria nae kuitwa na kuongea.
“Sijui niseme nini. Yaani najiona nimezidiwa na furaha kabisa. Kila ninapomuangalia Gloria nakumbuka kipindi kile alipokuwa mdogo na kuanza kuelekea nae shuleni. Unakumbuka Gloria?” Peter alisema na kumuuliza Gloria.
“Nakumbuka. Ila sikuwa mdogo peke yangu. Sema tulikuwa wadogo,” Gloria alimwambia Peter na kuwafanya watu wote mahali pale kuanza kucheka.
“Nafahamu. Ila si unakumbuka kwamba nilikuwa mtu wa kwanza kukuvusha barabara? Nisingekuwa makini na wewe ungekuwa umekwishagongwa na gari.
Nilianza kukulinda toka zamani sana, japokuwa tulikuwa wadogo lakini bado nilikuwa nikikuonyeshea jinsi gani ninakuthamini na kukulinda, sikutaka uvuke barabara peke yako, nilikuwa nikikushika mkono na kukuvusha barabara. Ulinzi ule ule ambao nilikuwa nikikupa toka utotoni ndiyo ulinzi ule ule ambao nitaendelea kukupa hadi uzeeni,” Peter alisema huku akimwangalia Gloria.
Watu wote waliokuwa wamekaa sebuleni pale wakabaki kimya, maneno ambayo alikuwa akiyaongea Peter yalionekana kuwa maneno mazito ambayo kwa msichana yeyote angeyasikia ni lazima angejiona ni kwa namna gani alikuwa akipendwa na kuthamaniwa.
“Naona siku ya harusi ni mbali sana, acha nianze kukuahidi leo hii hii hata kabla ya harusi yenyewe,” Peter alisema huku akimnyanyua Gloria na kuupitisha mkono katika kiuno cha Gloria na kisha kuendelea.
“Nakuahidi kuwa nawe katika maisha yangu yote, nakuahidi kukupenda katika shida na raha, magonjwa na afya, furaha na maumivu. Naahidi kukupenda katika kila hatua ya maisha ambayo tutayapitia baada ya kuingia katika ndoa,” Peter aliwambia Goria ambaye alibaki kimya huku kwa mbali macho yake yakianza kulengwa na machozi.
Peter akabaki kimya kwa muda, alikuwa akimwangalia Gloria usoni, kwake, Gloria akaonekana kuwa mtu mpya, msichana mpya ambaye alikuwa ameongezewa uzuri zaidi ya ule ambao alikuwa nao kabla.
Lipsi za midomo yake zilikuwa zikichezacheza tu huku akizitamani lipsi za Gloria. Alipoona ameridhika kumwangalia Gloria, akayarudisha macho yake kwa wazazi wa Gloria, mzee Michael na Bi Justina.
“Nimeahidi mengi, nimeahidi kumtunza binti yenu katika njia iliyo njema. Ninawaomba ninyi pia mniruhusu kumchukua binti yenu, muda wenu wa kumlea naona unafikia tamati, sasa hivi nadhani ni muda wangu kumlea binti huyu mrembo, binti huyu aliyeuteka moyo wangu,” Peter aliwaambia mzee Michael na Bi Justina.
Ilipofika zamu ya Gloria kuongea, akashindwa kabisa kuongea kitu chochote kile, akaamua kumkumbatia Peter na kuanza kulia. Maneno ambayo aliyaongea Peter yalikuwa yamemgusa, aliyaona maneno mazito ambayo yalikuwa yakijirudia rudia moyoni mwake.
“Nakupenda Peter. Nakupenda mpenzi,” Gloria alimwambia Peter huku wakiwa wamekumbatiana.
“Nakupenda pia Gloria,” Peter alimwambia Gloria.
Baada ya hapo, wote wakatawanyika na kuyafuata magari yao. Peter hakutaka kumuacha Gloria mikononi mwake, alikuwa amemshikilia vilivyo japokuwa mzee Michael alikuwa akimuita.
Wote wakabaki wakiangaliana tu, mapenzi ambayo waliyokuwa nayo mioyoni mwao yalikuwa yakiendelea kuchipuka.
“Ninakupenda sana Gloria,” Peter alimwambia Gloria.
“Ninakupenda pia.”
Baada ya hapo, Gloria akaingia garini na kuondoka mahali hapo. Muda wote huo Peter alikuwa amesimama tu mpaka pale gari lilipotoka machoni mwake. Akaanza kupiga hatua na kuelekea ndani ambapo akapitiliza hadi chumbani.
Alipofika chumbani, akaanza kuchati na Gloria huku akionekana kuwa na furaha tele. Waliendelea kuchati mpaka saa tisa usiku, muda ambao akapitiwa na usingizi kitandani pale. Ingawa meseji zilikuwa zikiendelea kuingia, Peter alikuwa amekwishalala kitambo kutokana na uchovu mkubwa ambao alikuwa nao siku hiyo.
“Nakupenda mpenzi. Najua umeshalala, ila utakapoamka naomba ujue kwamba ninakupenda sana. Mwaaaaaaaa! Hiyo ni kwa ajili yako peke yako” Hiyo ilikuwa ni meseji ya mwisho ambayo Gloria alikuwa amemuandikia Peter ambaye alikuwa amekwishalala.
*Je, nini kiliendelea?*