CharmingLady
JF-Expert Member
- Apr 16, 2012
- 18,250
- 12,868
OOOOHHHHHHHH me sijampata ngoja nnikimpata ntakuja kusema nimempataje Rutashubanyuma
Last edited by a moderator:
Mtihani na fimbo gumu kulifumbua Ruta. Tunajiingiza hivyohivyo na feki zetu, yote yatajulikana mbele kwa mbele.
How would I know? Ila najua with time I will know ukweli na feki.
Hahaha...umejuaje Rutashubanyuma..namtafuta huyu tangu kipindi JF iko exile kwa ajili ya matengenezo...
OOOOHHHHHHHH me sijampata ngoja nnikimpata ntakuja kusema nimempataje Rutashubanyuma
Rutashubanyuma ngoja nim-PM.Rogi atathamini zaidi kama maombi hayo yatatoka kwako na wala siyo kwangu..............ataona huyu mshenga naye katokea wapi?
Rogi ni kitu gani kilikufanya uvutiwe na Elizabeth Dominic? Haya matengenzo ya JF yaelekea yameibua mambo......................wengi hata FB walikuwa hawaijui sikuhizi naona ninajipatia marafiki kibao wa JF....something ought to yield now..................
Rogi ni kitu gani kilikufanya uvutiwe na Elizabeth Dominic? Haya matengenzo ya JF yaelekea yameibua mambo......................wengi hata FB walikuwa hawaijui sikuhizi naona ninajipatia marafiki kibao wa JF....something ought to yield now..................
Yaani Rutashubanyuma ndio maana nikamwambia Rogi asubiri kwanza nitafakari maana naona naenda juu chini lakini sipati maana
ULIMTAMBUA VIPI KUWA HUYU NDIYE MWENYEWE…..
(Getting to know her/him)
Hivi mwandani wako ulimtambuaje kuwa ndiye yeye?
Hivi ni maujanja yepi wewe uliyatumia kumpima yeye?
Ni vigezo vipi vilikutongoza hadi kujua umelamba dume?
Hivi ni vichocheo vipi vilikufanya uone ya kuwa umewasili?
Nifahamuvyo kauli na taswira zimejaa hadaa tupu
Kauli yake mwenyewe huitia kitanzini na kuishibisha azma zake!
Aongeacho mara nyingi sicho kilichopo moyoni kwake wala!
Tabasamu lake lalenga kuijenga kauli ambayo si lazima iwe na kweli!
Kamwe kauli au hata tabasamu lake kuwa kioo cha moyo wake!
Nifahamuvyo kauli na taswira zimejaa hadaa tupu
Kauli na taswira yake huoana na moyo wake masijala ya kukataa…
Pindi moyo wake umekuasi kata katu basi shabaha wewe hulengwa…
Bila haya au huruma jipu kukupasulia kuwa hakuhitaji nawe kulia..
Na kwa kufanya hivyo huwa kajitendea mwenyewe ubinadamu..
Nifahamuvyo kauli na taswira zimejaa hadaa tupu
Ni mitihani ipi uliitumia kuupima moyo wake?
Hata kuridhia yeye ndiye na hakuna mwingineo?
Kama ulienda mkichamkichwa basi ilikula kwako!
Kama uliserereka na kauli au taswira basi wewe teja!
Nifahamuvyo kauli na taswira zimejaa hadaa tupu
Remmy mbona migongano ya kauli hapo...........huku unasema waenda mkichwamkichwa lakini bado unaamini maujanja unayo .......which is which............kama unayo hebu nifafanulie.....................nipo darasani nimetulizana vilivyo.............
Swali gumu afu rahisi hapo hapo
Alishafika kitambo hukumuona tu..Hivi Kongosho hajajitokeza kwenye uzi huu kweli!! Au nimesahanu kusoma?