Dah umenikumbusha mbali sana mbali sana...miaka 12 iliyopita...nilikuwa kidato cha pili seminarini,tujiandaa kwa jiving na nyimbo za kuwaaga form four...mgeni rasmi mtarajiwa angekuwa Askofu TARCISIUS NGALALEKUMTWA(Jimbo katoliki Iringa),ghafla Gombera(Rector) wetu akaamuru kengele igongwe kitu ambacho ni adimu sana,ukiona ivo ujue mtu anafukuzwa seminar kwa utovu wa nidhamu...na mim nilikuwa na kesi ya kuiba maparachichi na mapera bustanin kwa Masista Kamadolesi,nkajua ndo safari ya home....HP wetu ambaye sasa ni Padri wa kanisa katoliki uko Parelmo Italy akampa Rector nafasi...akatangaza kwa Huzuni kuondokewa kwa baba wa Taifa...wote tukapoa...huzuni ikatanda...Tulikuwa na Tv room inashka DSTV tu!Tukafunguliwa chanel ya SABC-AFRICA,Wakawa wanatoa wasifu,hstoria ya mwalimu..24hrs...na siku ya mazishi Tulitazama kupitia SABC-AFRICA ya South Africa...nakmbuka mengi sana,lakn nimewakmbuka zaid marafik zangu waloamua kuendelea na Upadri..weng wako nje ya nchi wakihubiri Injili...Ni mda mrefu!!R.I.P J.K.NYERERE
Hii imenichekesha sana. Pole sana kwa yaliyokukuta, hasa mawazo ya kesi yako.