Ulikuwa wapi kabla haujaja duniani kama kiumbe hai? Umewahi kutaka kujua ulipotoka?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,556
46,095
Dini zote duniani zina nadharia na mafundisho tele kuhusu maisha baada ya kifo. Kila dini ninayoifahamu imelizingumzia suala la maisha ya baada ya safari ya uhai wa binadamu kufika mwisho kwa undani sana tofauti na suala la alipotoka binadamu.

Japo kuna mjadala mkali kwa mafundisho na nadharia hizo lakini hakuna ubishi kwamba zipo, hii ni tofauti sana na mafundisho kuhusu alipotoka binadamu

Sehemu kubwa ya dini ninazozijua hazizungumzii alipokuwepo binadamu fulani kabla hajazaliwa na kuanza kuishi duniani.

Je mtu huwa anakuwa wapi kabla ya kuzaliwa kwake hapa duniani?

Kwa nini binadamu wengi pia hawahangahishwi na kutaka kujua walipokuwa kabla ya kuzaliwa?
 
Hili swali kwangu naliona lina jibu jepesi sana. Kabla ya ku exist hauku exist, kutafuta sababu ya uwepo wako kabla ya uwepo wako ni contradiction

Kwasababu tunawexa tukasema foundation ya mtu ilianza kwa sperm baada ya wazazi kukutana kimwili

Swali ambalo linasumbua akili ni kuhusu huyu mungu ambaye tunahadithiwa kua alikuwepo tangu na tangu.

Alikua akiishi wapi kipindi chote hicho cha nyuma kabla hajaumba mbingu na ardhi ambayo ndio makao yake rasmi sasa hivi?

Huko alikokua anaishi kuliumbwa na nani maana genesis inaeleza kua uumbaji wa kwanza mungu kuufanya ni ule wa mbingu na ardhi?
 
Dunia ni gereza, kwa hiyo hapo wanadamu wote unaowaona ni wafungwa, na kila mtu ana adhabu yake kutegemeana na makosa aliyofanya huku nyumbani(mojawapo ya sayari kubwa) kuna maisha mnaita ya raha, mengine ya karaha zote ni adhabu tu, na kuna wafungwa wanaongoza wenzao, wengine werevu, wababe n.k.'
 
Dunia ni gereza, kwa hiyo hapo wanadamu wote unaowaona ni wafungwa, na kila mtu ana adhabu yake kutegemeana na makosa aliyofanya huku nyumbani(mojawapo ya sayari kubwa) kuna maisha mnaita ya raha, mengine ya karaha zote ni adhabu tu, na kuna wafungwa wanaongoza wenzao, wengine werevu, wababe n.k.'

Majibu yako mbona kama makubwa sanaa..........yaani kama kunakitu unajaribu kueleza ila bado hujakieleza. Any way nimependa hii kitu
 
Kwa kuwa inasemekana roho haifi, basi kabla kurutubishwa yai la mwanamke na mbegu ya kiume, roho iliunganishwa ambayo ilikuwepo japo hatujui ilikuwa inakaa wapi. Ila baada ya kifo roho inasepa tena na kutokomea sehemu isiyojulikana. Haya mambo ya mbinguni na motoni ni siasa tu za kimisionari.
 
Habari zenu waungwana.
Muuliza swali kauliza swali zuri japo ni dhaifu.
Udhaifu wa swali hili lipo kwenye matumizi ya neno WAPI.Neno WAPI hutumika kuelezea uwepo wa viumbe au vitu vyenye miili tu( physical bodies) katika eneo fulani.Kuuliza mwanadamu alikuwa WAPI kabla ya kuzaliwa maana yake ni kusema kuwa kabla mwanadamu hajazaliwa alikuwa na mwili,kitu ambacho sio sahii kwa sababu mwanadamu hupata mwili pindi akiwa tumboni( baada ya manii na yai kuungana).Hivyo basi swali la muungwana huyu la "ulikuwa wapi kabla hujaja duniani" linakosa mashiko kwa sababu linalazimisha mwanadamu aonekane alikuwa na mwili hata kabla hajaja duniani,kitu ambacho sio sahihi.
 
Neno wapi haliwezi kutumika kuelezea roho?
Waamini wa Incarnation wanaamini viumbe vinabadilika kutoka kiumbe kimoja kwenda kingine.
Habari zenu waungwana.
Muuliza swali kauliza swali zuri japo ni dhaifu.
Udhaifu wa swali hili lipo kwenye matumizi ya neno WAPI.Neno WAPI hutumika kuelezea uwepo wa viumbe au vitu vyenye miili tu( physical bodies) katika eneo fulani.Kuuliza mwanadamu alikuwa WAPI kabla ya kuzaliwa maana yake ni kusema kuwa kabla mwanadamu hajazaliwa alikuwa na mwili,kitu ambacho sio sahii kwa sababu mwanadamu hupata mwili pindi akiwa tumboni( baada ya manii na yai kuungana).Hivyo basi swali la muungwana huyu la "ulikuwa wapi kabla hujaja duniani" linakosa mashiko kwa sababu linalazimisha mwanadamu aonekane alikuwa na mwili hata kabla hajaja duniani,kitu ambacho sio sahihi.
 
mara kadhaa nimekuwa najiuliza hili swali.
roho yangu kabla mimi sijazaliwa na kuwa binadamu, ilikuwa inaishi wapi. nakosa jibu. sikubaliani na hoja za wafuasi wa imani za kidini.

labda roho yangu ilikuwa sayari nyingine au pengine ilikuwa inarandaranda hapa duniani ikiwa imejihifadhi kwa wanyama kama kuku, ngo'mbe au mbwa.

kiukweli kuna siri nzito sana inayohusu uumbaji wa mwanadamu, sidhani kama yupo anayeweza kuielezea kwa usahihi akaeleweka.

labda huku tulipo(duniani), tupo gerezani kutumikia adhabu baada ya roho zetu kutenda makosa kwenye universe nyingine.

labda kifo ni portal(mlango) ya kurudisha roho zetu kwenye universe yake ya awali baada ya kumaliza kutumikia adhabu hapa duniani(gerezani).

najiuliza maswali haya kwasababu sayari tuliyopo haina usawa, ina watu wanyonge sana, watu makatili sana, watu matajiri, watu masikini, watu wenye madaraka, wasio na madaraka na kadhalika.

ni kama tupo kwenye uwanja wa vita vile.
 
Kabla ya kuzaliwa wewe hukuwa mwanadamu bali ulikuwa mbegu, nusu kwenye korodani za baba yako na nusu kwenye ovari za mama yako.

Baada ya tendo la ndoa kufanyika ndipo hizo mbegu mbili zikaungana na wewe ukatengenezwa tumboni mwa mama yako.

Hii maana yake ni kwamba kama baba yako angelala na mwanamke mwingine basi wewe usingekuwepo kabisa hapa duniani.
 
pengine ilikuwa sayari nyingine au pengine ilikuwa imejihifadhi kwa manyama kama kuku, ngo'ombe au mbwa.
Mkuu hapa unaizungumzia mwili sio roho.

Alafu angalia maajabu..

Miili yetu inatokana na seli moja tu inajigawagawa then baadae anakuja complex organism.

Wakati huo unaweza kumkuta complex organism katimia kila kiungo lakini hayupo hai.

Sasa hiko kinachomfanya awe hai ndo tukijadili.

Kwa ufupi tuseme roho,je hii roho kabla ya kutiwa mtu akawa anaishi ilikuwa wapi ?

Mimi naamini roho ilikuwa kwenye milki ya Mungu.

Kuna hadithi ya Mtume muhammad(sijui imani yako samahani) imeelezea hii concept ya kuwa mtu anaanza kuumbwa kisha akikamilika baadae ndo anatiwa roho ili aanze kujifahamu na kuanza kufanya harakati kama mtoto tumboni.
 
Kabla ya kuzaliwa wewe hukuwa mwanadamu bali ulikuwa mbegu, nusu kwenye korodani za baba yako na nusu kwenye ovari za mama yako.

Baada ya tendo la ndoa kufanyika ndipo hizo mbegu mbili zikaungana na wewe ukatengenezwa tumboni mwa mama yako.

Hii maana yake ni kwamba kama baba yako angelala na mwanamke mwingine basi wewe usingekuwepo kabisa hapa duniani.
Wewe unazungimzia mwili.

Mtu anakufa na mwili wake uko vile vile.

Tunataka kujafili hiki kinachomfanya mtu afe ni nini kinaondoka ?

Concept zinasema ni roho hiyo,roho ni nini hatujui.

Ukizungumzia seli zipo,tena mtu alianza kama seli moja tu baadae zikajigawa akawa mtu kamili,lakini ajabuu mtu huyu anakufa akiwa na trilion of cell lakini anakufa licha ya uwingi alokuwa nao wa seli zake.

Hivyos seli za mwili au mwili haumati katika mjadala huu,kinachomata ni roho
 
Habari zenu waungwana.
Muuliza swali kauliza swali zuri japo ni dhaifu.
Udhaifu wa swali hili lipo kwenye matumizi ya neno WAPI.Neno WAPI hutumika kuelezea uwepo wa viumbe au vitu vyenye miili tu( physical bodies) katika eneo fulani.Kuuliza mwanadamu alikuwa WAPI kabla ya kuzaliwa maana yake ni kusema kuwa kabla mwanadamu hajazaliwa alikuwa na mwili,kitu ambacho sio sahii kwa sababu mwanadamu hupata mwili pindi akiwa tumboni( baada ya manii na yai kuungana).Hivyo basi swali la muungwana huyu la "ulikuwa wapi kabla hujaja duniani" linakosa mashiko kwa sababu linalazimisha mwanadamu aonekane alikuwa na mwili hata kabla hajaja duniani,kitu ambacho sio sahihi.
Hakika umenena vyema.
 
Hivi ushawahi kuwaza siku moja kwamba haupo popote na wewe sio chochote?

Mimi sijawahi kuwaza kwamba sipo popote kwenye ulimwengu,kila nikiwaza najiona nipo tu.

Hili ni fumbo kubwa ambalo tunatakiwa tujiulize sana
Ni fumbo kweli, ila nadhani sasa hivi nipo, na itafika muda sitakuwepo
 
Back
Top Bottom