Ulikuwa utawala wa Chuma, tusiwabeze wapiga kelele sasa, tusiwakasirikie, badala yake tuwasikilize na tuwaelewe

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,298
45,585
Tukubali miaka mitano iliyopita kulikiwa na mwanaume mmoja aliyeweza kuwaweka wanaume na wanawake wote chini ya himaya yake bila kufurukuta. Wengine walikaa wakatulia kimya, wengine walibaki mashuja wa mitandaoni, wengi walimsifia na wote kwa pamoja tulimuogopa.

Wote walifanya hivyo kwa sababu nyingi. Wapo waliompenda kweli, wapo waliopenda maslahi yao tu na yeye aliwahakikishia hilo, wapo waliokipenda chama chao, wapo waliosema wana familia za kutunza, wapo walioogopa mkono wa chuma kupitia dola n.k

Wakati huu ambapo chuma hayupo na watu wanapokosa utendaji wa Serikali, Bunge, wanapodai Katiba Mpya, wanapohoji kuhusu muungano, wanapouliza kutenganisha kofia mbili n.k tusiwasakame sana na kuwabeza sana mbona hawakusema wakati wote.

Tuwaelewe na tujifunze kutokana na historia kwa sababu ambao hawajifunzi kutoka katika historia wana hatari ya kuirudia.
 
Hao wapiga kelele, wengi wao hawana huruma na Watanzania wenzao masikini. Wanaangalia matumbo yao tu. JPM aliona mbali hata wale ambao wanampinga wanafahamu kwa nini alikuwa anafanya vile. Tanzania ni tajiri na mahali ambapo tumefika hatuhitaji sana wazungu waje watuamulie mambo yetu.

Wazungu wengi werevu walikuwa wanamkubali sana, ni aibu Watanzania wengi makuwadi hata hawafahamu kwa nini waliumbwa na mwenyezi mungu.
 
Ulikuwa utawala dhalimu, utawala wa kishenzi, uliojaa ufedhuli, ukatili na u-imla. Kamwa asitokee kiongozi kama huyu tena hapa nchini!
 
Ukiondoa mwanaume Antipas Mughwai Lisu ambaye alimpa za uso dikteta bila kupepesa macho.
umesahau wewe Zitto alimuita mpaka mshamba? Balozi Kagasheki Je? Jenerali Ulimwengu je? vipi kuhusu Prof Mwandosya? B. Membe? Just to mention few, they are so many out there.... akina Nyangali Mdude & Co!
 
Back
Top Bottom