Ulifanyaje mtoto wako akaacha kujikojolea na kunyonya kidole?

Nakukunda

JF-Expert Member
Jul 10, 2017
877
1,635
Wapendwa,

Naomba mnisaidie mbinu ya kumfanya mtoto wa miaka nane kuacha kukojoa na kunyonya kidole

Nimeshaomba na kufunga na bado namwamini Mungu atamfungua

Japo naamini mpo ambao watoto wenu wamepona na kuacha hizo tabia, naomba mnielekeze nimsaidie binti yangu.

Unaweza hata kumuamsha mara mbili na bado atakojoa, tunamzuia kunywa vitu vya maji maji kuanzia saa moja jioni ikiwa ni pamoja na kumsimamia akojoe kabla ya kulala na bado atakojoa.

Na kinachonishangaza anakuwa kama anatafuna na kujikaza misuli wakati wa kukojoa. Na anaweza lala hata ndani ya nusu saa na akakojoa.

Ameanza hii tabia akiwa na miaka mitatu chini ya hapo alikuwa hanyonyi kidole wala kukojoa Kuna nyumba niliwahi kupangisha miaka hiyo nahisi haikuwa nzuri sababu licha ya kuanza kukojoa mtoto alikuwa anaumwa kifua mno.

Nimeamua kujikita katika kumwombea japo ningeomba mnipe mbinu za malezi mlizowahi kutumia kusaidia watoto wenu waliopitia changamoto kama hii maana naona inamnyima mtoto wangu confidence maana hata yeye hapendi na namwona kabisa anaumia.

Naombeni mnipe mbinu ya malezi kwani ana wadogo wake wawili hawajikojolei hata wanywe maji vipi ila dada yao ndo ananipa wakati mgumu kwa kweli.

Ahsanteni
 
Vitu vingine ni masihara ila ni kipaji hicho dogo langu alikuwanacho yaani ilikuwa ata saa kumi na mbili kasoro asubuhi usipomwamsha atajikojolea. Solution hajawahi kugombezwa kwa kujikojolea we took it easy usiku anakunywa maji ya kutosha, mchana anacheza shuleni, nyumbani homework, ubongo kids. .. Saivi anaamka peke yake.

Kwanza akikojoa usimkaripie, kuna watu nawajua walikuwa wanajikojolea mpaka anamaliza darasa la saba?

Sema hawajikojolei kila siku inamuumiza but no way out! Ni rare cases inahusisha zaidi ubongo!

Pia achana kabisa na imani sijui namuombea! Hizo ni involuntary action, ubongo unajijengea taswrisa ya kuruhusu mkojo kutoka na stimulus za kwenye kibofu kufunguka!!

Mpe maji yaliooshewa mchele hii ni mbinu za kijijini sio lazima ikubali kwa kila mtumiaji ukimpatia unanuia " dawa hii ikamalize tatizo la kujikojolea kitandani kwa uweza wa mungu ikakusaidie amina" dawa za kienyeji zipo nyingi nyingine ni za makabila.

Mzoeze kufanya hesabu muda wa ziada pili afanye physical works kama zipo plus michezo ya kawaida ya watoto.

Mwisho anywe maji ya kutosha wala usimzuie
 
Mpake pilipili kidoleni ama aloevera mara kwa mara kitu kichungu.

Ama mwambie ukiacha ntakupa zawadi flani kitu anachopenda na uwe unampa-sio kumuadhibu

Kukojoa
Labda pia alale mchana kila siku au mara nyingi ili usiku asilale fofofo akibanwa astuke.

Ama asichoke sana na michezo ama kazi.

Mi hadi nna miaka 7 najikumbuka nlikua natandikwa mpira chumbani🙈.

Vinginevyo godoro litaanikwa.

Na ukubwani ilinikuta siku ambazo nimechoka kupitiliza.

So kupumzika muhimu

Wazazi jamani

Kweli ndo mana Mungu katoa amri kutii wazazi
 
Vitu vingine ni masihara ila ni kipaji hicho dogo langu alikuwanacho yaani ilikuwa ata saa kumi na mbili kasoro asubuhi usipomwamsha atajikojolea...
Maji ya mchele anapewa kwa muda wa siku ngapi au kila siku?
 
Apande juu ya mti akojoe akiwa huko huko juu hatarudia tena kukojoa kitandani.

Kuhusu kunyonya kidole paka pilipili tu hatarudia japokuwa kama ni mkubwa atakuwa anaosha kidole anaendelea tena.
Duh. Haya
 
Dah pole sana ndugu. Mbinu za zamani za kijijini kwetu zilikuwa 2;

1. Unamchukua mtoto unampeleka kwenye eneo linalotisha (ila asijue kama anapelekwa huko) mfano daraja kubwa lenye kimo kirefu kutoka usawa wa maji ya mto, halafu unamwambia avue chupi then akojoe hapo huku mkiwa kama mnataka kumsukumiza kwenye kuelekea mtoni. Mtoto ataanza kuresist huku tayri anakojoa. Hii mbinu inamsaidia kumfanya akiota anakojoa anakumbuka hilo tukio then anaacha.

2. Mbinu ya pili ni kumpeleka kwenye ngome ya siafu halafu unafanya kama ulivyofanya kwenye mbinu ya 1.
Mbinu zote hizo mbili ziliwezesha watoto wengi kuacha kukojoa huko kijijini kwetu.
Wapendwa,

Naomba mnisaidie mbinu ya kumfanya mtoto wa miaka nane kuacha kukojoa na kunyonya kidole

Nimeshaomba na kufunga na bado namwamini Mungu atamfungua

Japo naamini mpo ambao watoto wenu wamepona na kuacha hizo tabia, naomba mnielekeze nimsaidie binti yangu.

Unaweza hata kumuamsha mara mbili na bado atakojoa, tunamzuia kunywa vitu vya maji maji kuanzia saa moja jioni ikiwa ni pamoja na kumsimamia akojoe kabla ya kulala na bado atakojoa.

Na kinachonishangaza anakuwa kama anatafuna na kujikaza misuli wakati wa kukojoa. Na anaweza lala hata ndani ya nusu saa na akakojoa.

Ameanza hii tabia akiwa na miaka mitatu chini ya hapo alikuwa hanyonyi kidole wala kukojoa Kuna nyumba niliwahi kupangisha miaka hiyo nahisi haikuwa nzuri sababu licha ya kuanza kukojoa mtoto alikuwa anaumwa kifua mno.

Nimeamua kujikita katika kumwombea japo ningeomba mnipe mbinu za malezi mlizowahi kutumia kusaidia watoto wenu waliopitia changamoto kama hii maana naona inamnyima mtoto wangu confidence maana hata yeye hapendi na namwona kabisa anaumia.

Naombeni mnipe mbinu ya malezi kwani ana wadogo wake wawili hawajikojolei hata wanywe maji vipi ila dada yao ndo ananipa wakati mgumu kwa kweli.

Ahsanteni
 
Back
Top Bottom