ULAZIMA WA KUTOA ZAKATUL FITRY KWA WAISLAM

nyamwingi

JF-Expert Member
Mar 10, 2016
933
863
*KCWW RAM/29 1438*

Darasa ya Ramadhani, Jumatatu tarehe 24 Ramadhani 1438, sawa na 19 Juni 2017

WAJIBU WA ZAKA YA FITRI

Zakatul-Fitr ni zaka/sadaka ya lazima inayotolewa baada ya ‎kumalizika Ramadhani, na kuingia tarehe mosi, Shawwaal/Mfungo Mosi: ‎mara tu baada ya kuandama mfungo wa Shawwaal, na hivyo kumalizika ‎Mfungo wa Ramadhani.‎

Inaitwa Zaka ya Fitri, kwa sababu ni Zaka inayotolewa baada ya ‎kufuturu/kumaliza Wajibu wa kufunga Ramadhani. ‎

Kama ilivyokuwa Sijdatus-Sahw, inayo sujudiwa mwisho wa ‎Swala–ni mfano wa raba au fidia ya kusahau kufanya Sunna maalum ndani ‎ya Swala, basi na Zakatul-Fitri ni kitakaso cha vijimakosa vidogo vidogo ‎vya Saumu, vilivyochumwa kwa kujua au kutokujua wakati wa kufunga ‎Ramadhani. Yaani ni kirekibisho cha palipoharibika kidogo katika Swaumu.‎

Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas ‎رضى الله عنهما‎ akisema: ‎Amesema Mtume ‎ﷺ‎,
زكاة الفطر طهرة للصائم من اللغو والرفث وطعمة للمساكين. فمن أداها فبل الصلاة فهي ‏زكاة مفبولة ومن ‏أداهابعد الصلاة فهي صدقة من الصدقات (رواه أبو داؤد ,ابن ماجه والدار قطنى)‏

‎“Zaka ya Fitri ni kitakaso cha aliyefunga kutokana na mambo ya ‎upuuzi na maneno machafu, na ni lishe kwa masikini. Hivyo, atayeitoa ‎kabla ya Swala, itapokewa kama Zaka, na atayeitoa baada ya Swala basi ‎ni sadaka kama sadaka yoyote ile nyengine.”‎

Wanachuoni wa Fiqh, huielezea na Zaka ya Fitri kwamba:‎

‏ زكاة الفطر: ‏صدقة معلومة بمقدار معلوم، من شخص مخصوص، بشروط مخصوصة، ‏عن ‏طائفة مخصوصة، لطائفة ‏مخصوصة، تجب بالفطر من رمضان، طهرة للصائم: ‏من اللغو، ‏والرفث، وطعمة للمساكين، ‏

‎“ Zaka ya Fitri ni Sadaka ya wajibu maalumu, ya kiwango ‎maalumu, ‎‏kutoka kwa mtu maalumu, kwa masharti maalumu, kwa niaba ya ‎watu maalumu, kupewa watu maalumu, kwa lengo maalumu, nalo ni ‎Kikataso cha Swaumu na chakula kwa masikini.”‎

Zaka ya Fitri imefaradhishwa mwezi wa Shaabani, mwaka wa pili ‎Hijriyya, kama ‎kitakaso cha mwenye kufunga Ramadhani.‎

Zaka ya Fitri imethibiti kwa Qu’aani na Sunna ya kauli na vitendo. ‎

Mwenyezi Mungu ‎سبحانه وتعالى‎ amesema, kwa wenye kujitakasa nafsi ‎zao kwa kutoa sadaka:
‎قَدْ أَفْلَحَ مَنْ تَزَكَّى* وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّى * بل تؤثرن الحياة الدنيا * ‏واللآخرة خير وأبقى

‎“ _Hakika amekwishafaulu aliyejitakasa na akakumbuka kutaja Jina la Mola ‎wake na akaswali. Ila ‎nyinyi mna hiari maisha ya dunia! Na ya Akhera ni ‎bora na yenye kudumu zaidi._” (Al-A‘la 87:14-15).‎

Wamesema Imam At-Tabari, Ibn Kathir na wengine, kuwa Sa‘id bin Al-‎Musayyib na ‘Umar bin ‘Abdul-‘Aziz (khalifa) na maswahaba wengine ‎wamesema Aya hizo zinazungumzia Zakatul-Fitr. _Tafsir At-Tabari_ 24/374, pia _‎Muswannaf ‘Abdurrazaaq,_ Hadithi [HASHTAG]#5795[/HASHTAG].‎

Kwa upande wa Sunna:‎

Zimepokewa kutoka Mtume ‎ﷺ‎ Hadithi mbali mbali kuhusu wajibu ‎wa Zaka ya Fitri. Miongoni mwa Hadithi hizo ni:

‎1. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Umar ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr juu ya binaadamu, katika Mwezi wa ‎Ramadhani. Nayo ni pishi moja ya tende au shayiri kwa kila mja, awe huru ‎asiwe huru (mtumwa) mwanamume au mwanamke, miongoni mwa ‎Waislamu.” _Muttafaq ‘alayhi_.
‎2. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Umar ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr katika Mwezi wa Ramadhani, nayo ‎ni pishi moja ya tende, au pishi moja ya shayiri, juu ya mja aliye huru, ‎mwanamume au mwanamke, mkubwa au mdogo, miongoni mwa Waislamu. ‎Na akaamrisha itolewe kabla ya watu kwenda kuswali Swala ya Idi.” ‎Ameipokea Bukhari.‎

Hivyo, Zaka ya Fitri ni Zaka ya kiwiliwili SI zaka ya Mali. Inatolewa ‎kutakasa nafsi ya mja na kuisafisha, hata kama haina makosa au uchafu. ‎Na hiyo inamaanisha ni wajibu kutolewa kwa kila kiumbe Mwislamu, hata ‎aliyezaliwa leo, mwamume au mwanamke, mdogo au mkubwa, ‎muungwana au mtumwa.
3. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr kuwa ni kitakaso cha Swaumu ‎kutokana na makosa madogo madogo na mambo machafu, na kuwa ni ‎chakula kwa masikini. Hivyo basi, atayeitoa kabla ya Swala (ya Idi), Zaka ‎yake ya Fitr itakubaliwa, lakini atayeitoa baada ya Swala (ya Idi) basi hiyo ‎itakuwa ni sadaka tu kama sadaka yoyote nyengine.” Ameipokea Abu Daud.
‎4. Imepokewa kutoka kwa Abu Sa‘id Al-Khudriyy ‎رضي الله عنه‎ ‎akisema: Tulikuwa tukitoa sadaka ya Zakatul-Fitr (wakati wa Mtume ‎ﷺ‎) ‎pishi moja ya chakula, au shayiri, au pishi moja ya tende, au pishi moja ya ‎samli, au pishi moja ya zabibu.” _Muttafaq 'alayhi_. Na imepokewa vile vile na ‎Tirmidhi, Nasaa'i, Ibn Maajah, Abu Daud na Ahmad. ‎

*UFAFANUZI*

Zaka ya Fitri ni wajibu kwa kila nafsi ya Mwislamu anayetweta–yaani anaepumua. Ni Zaka ya kiwiliwili, si Zaka ya mali. Hivyo, midhali kiwiliwili ‎kipo basi lazima kitolewe Zaka ya Fitri. Ni wajibu. Ni Faradhi. Haiepukiki, ‎isipokuwa kwa yule ambaye hana uwezo kabisa. Hapo ‎لايكلف الله نفسا إلا وسعها‎.‎

Ama mwenye kipato, au mwenye wajibu wa kumtunza mtu mwengine, ‎kama mke, watoto, wazazi wake wawili wasiojiweza, watumishi wa ‎nyumbani na kadhalika, na kipato chake kikawa kinazidi wajibu wake wa ‎kuwatunza anaowatunza, basi ni wajibu KWAKE kujitolea yeye mwenyewe, ‎kwanza, na kisha kuwatolea wote wale anaowajibika kuwatunza, kwa hali na ‎mali. Yaani, lazima awe na chakula cha ziada ya kula yeye na familia yake, ‎siku ya Idi. Hicho kitachozidi ndicho kinachotolewa Zaka ya fitri. Kikiwa ‎hakitoshi kulisha familia yake hiyo siku ya Idi, basi hana jukumu la kutoa ‎Zaka ya Fitri.‎

Kwa maneno mengine, iwapo baba mwenye nyumba ni masikini, hana ‎cha kumtosha yeye na familia yake siku ya Idi, basi huyo hana wajibu wa ‎kutoa Zaka ya Fitri. Wala hana wajibu wa kumtolea mkewe, hata kama mke ‎huyo ni mwenye uwezo kutokana na kipato chake mwenyewe. ‎

Lakini mke mwenye kipato chake mwenyewe, anaweza kujitolea ‎kumtolea mumewe na watoto wake akipenda. Maana hana wajibu wa ‎kujitunza, wala kumtunza mumewe wala watoto wake. Ni hiari yake, na ni ‎fadhila kubwa, sana, kufanya hivyo. Ila SI wajibu juu yake. ‎

Zaka ya Fitri ni chakula, SI pesa. Na kiwango cha kutolewa ni ‎pishi moja ya chakula kinacholiwa sana katika jamii husika. Hivyo, vyakula ‎vinavyoingia hapa ni nafaka zote, kuanzia ngano, shayiri, mchele, unga wa ‎ngano, sembe, maharage, ulezi, nk. Ni chakula kinacholiwa sana ‎na watu wengi katika jamii ya mtoa Zaka hiyo.‎

Kiwango cha Zaka ya Fitri ni pishi moja, ambayo ni sawa na kilo mbili ‎na gram 400; kwa pishi ya Mtume ‎ﷺ‎ (ambayo ni sawa na vibaba ‎vine vya Mtume ‎ﷺ‎, na kibaba kimoja ni ujazo wa nafaka kwenye viganja ‎viwili–kwa pamoja–vya mtu wa kawaida). Hivyo, ni kama kilo mbili na ‎nusu za chakula kinachopendwa sana na jamii husika. Kiwango hicho ni kwa ‎kila kiumbe chenye uwezo wa kujitolea chenyewe. ‎

Iwapo hakina uwezo basi ni juu ya mwenye jukumu la kumtunza ‎kiumbe huyo, ilimradi ana uwezo wa shibe yake na shibe za watoto wake ‎wote, siku ya Idi. Kitachozidi ndicho kitachotolewa Zaka. Kama hakitoshi, ‎basi akigawe kwa utaratibu aliouweka Mtume ‎ﷺ‎ kama ifuatavyo: ‎

عن جابر رضي الله عنه قال قال رسل الله صلى الله عليه وسلم: ((ابدأ بنفسك فتصدق عليها، فإن ‏فضل شيء فلأهلك، فإن فضل عن أهلك شيء فلذي قرابتك، فإن فضل عن ذي قرابتك شيء فهكذا ‏وهكذا)) يقول: فبين يديك، وعن يمينك، وعن شمالك.(رواه مسلم) ‏

‎“Anza kujitolea mwenyewe. Kikizidi kitu watolee watu wako wa nyumbani ‎‎(anza na mke, kwanza, kisha watoto). Kikizidi kitu, watolee ndugu na jamaa ‎zako (anza na ndugu na jamaa wa karibu, kisha wa mbali). Kikizidi basi ‎watolee wa huku na huko, na kule na hapa (walio karibu zaidi nawe na ‎ambao si watu wa ukoo wako, kama majirani wa karibu).” Ameipokea ‎Muslim. ‎

*SUNNA ZA KUTOA ZAKA YA FITRI*

a) Kuitoa mara baada ya kuandama mwezi wa Shawwaal–yaani usiku wa ‎kuamkia Sikukuu, au kabla ya kwenda kuswali Swala ya Idi, au siku moja au mbili kabla ya kumalizika Ramadhani.
b) Kumtolea hata mtoto aliye tumboni, kama alivyokuwa akifanya ‎Sayyidina ‘Uthman bin ‘Affaan ‎رضي الله عنه‎. Ameipokea Ahmad na Ibn Abi ‎Shayba.
c) Kuigawa kwa mikono yako mwenyewe, badala ya kuwapa watu ‎wengine waitoe kwa niaba yako. Mtume ‎ﷺ‎ alikuwa akifanya hivyo, na ‎kuwausia Maswahaba nao wafanye hivyo.
d) Ukiwapa watoto wako nyumbani kuitoa, ni sawa na kuigawa ‎mwenyewe.
e) Kuwapa masikini jamaa zako, wenye kustahiki na ambao huna wajibu ‎wa kuwatunza.
f) Kuigawa kwa masikini wa mahali ulipo, ila ikiwa kuna wanaohitaji ‎zaidi, na ni jamaa zako, nchi nyengine.
‎g) Iwapo chakula unachotoa kina viwango mbali mbali, basi chagua ‎kiwango cha juu: Mwenyezi Mungu amesema: _“Hamtaipata Pepo ‎mpaka mtoe mnavyovipenda.”_
h) Kutoa nafaka kavu, inayoweza kuhifadhika kwa siku kadhaa bila ya ‎kuharibika, ni bora kuliko chakula kisichoweza kuhifadhika kwa ‎muda mrefu.
i) Kwa upande wa Wazazi wako wawili, ni Sunna kumtolea Mama ‎mzazi kwanza, kisha ndiyo Baba mzazi–iwapo wanakutegemea ‎kuwatunza.
j) Kuwapa majirani zako masikini, ni bora kuliko masikini wa mbali.‎

*YALIYOMO NA YATOKANAYO*

Kutokana na Aya za Qur’aani na Hadithi za hapo juu, maulamaa wema ‎waliotutangulia wamefafanua YALIYOMO NA YATOKANAYO kama ‎ifuatavyo:

‎1. Zakatul-Fitr ni wajibu, kwa kila mwenye kuweza, na ambaye ana ‎chakula cha ziada ya chakula chake cha Sikukuu ya mwanzo.
‎2. Asiye na uwezo, na ambaye yumo chini ya kukimiwa na mtu ‎mwengine, kama vile Baba mzazi, au hata mlezi wake tu, basi wajibu ‎wa kutolewa upo juu ya mabega ya mwenye kumkimu. Kwa maana ‎hiyo, Mume anamtolea mkewe, watoto wake, wazee wake–iwapo ‎wamo chini ya himaya yake–mtumishi au watumishi wake, bila ya ‎kujali umri au jinsia. Hata mtoto aliyezaliwa saa moja kabla ya ‎kuandama mwezi wa Shawwaal, anapaswa kutolewa sadaka ya Zakatul-Fitr.
‎3.‎ Zakatul-Fitr ni Zaka ya kutakasa mwili wa aliyefunga, kwa upande ‎mmoja, na hata asiyekuwa na wajibu wa kufunga, kwa upande wa pili, ‎ilimradi umeingia Mwezi wa Rehema na yeye yupo hai. Kwa maana ‎hiyo, Zakatul-Fitri ni Zaka ya NAFSI, SI ZAKA ya mali. Ndiyo maana inampasa kila mtu, mwanamume kwa mwanamke, ‎mdogo kwa mkubwa, muungwana na asiye muungwana.
‎4. Zakatul-Fitr inapaswa kutolewa kwa aliyoko karibu na aliyoko mbali, ‎ilimradi matunzo yake yapo juu ya mabega ya mzee wake. Hivyo, ‎mwanafunzi anayesoma ugenini–na anayetunzwa na wazee wake–‎anapaswa kutolewa Zaka yake ya Fitri.
‎5. Zakatul-Fitr ni mfano wa Sijdatus-Sahw kwenye Swala. ‎Imefaradhishwa ili kuziba mapengo yatayotokea, bila ya kujua, wakati ‎wa kufunga mwezi wa Ramadhani, kwa aliyefunga, au makosa ‎madogo madogo mengine, kwa aliyeruhusiwa kutokufunga–yaani ‎makosa madogo madogo yanayoweza kuchumwa katika mwezi wa ‎Ramadhani. Kwa lugha nyengine ya kisasa: Zakatul-Fitr ni RABA ya ‎kufuta makosa madogo madogo.
‎6. Kwa maana hiyo, Zakatul-Fitr anatolewa vile vile mtumishi Mwislamu, ‎kwa vile wajibu wa Swaumu upo juu yake kama Mwislamu yeyote ‎mwengine. Ama asiyekuwa mwislamu hatolewi Zakatul-Fitr, maana ‎wajibu wake kwanza, ni kuwa Mwislamu kabla ya kuanza kufunga.
‎7. Inaitwa Zakatul-Fitr kwa sababu ni Sadaka iliyokusudiwa kumlisha ‎masikini katika siku ya Idi. Yaani ni Zaka ya kumsaidia masikini ‎aweze kufungua kinywa Sikukuu ya Idi, na afurahike kama wanavyofurahika Waislamu wenziwe wenye kujiweza.
‎8. Kutokana na sababu hiyo kuu, ndiyo maana inatakiwa itolewe ‎KABLA ya Swala ya Idi. Na kama itatolewa mwishoni mwa ‎Ramadhani ni bora zaidi. Hivyo, mwezi mzima wa Ramadhani, hadi ‎kabla ya kuswaliwa Swala ya Idi, ni muda halali wa kutoa Zakatul-‎Fitr.
‎9. Kwa vile lengo la Zakatul-Fitr ni kumlisha masikini, basi ‎kinachotolewa ni chakula kinacholiwa sana katika jamii. Hivyo basi, ‎ama ni ngano, shayiri, tende, kitoweo kikuu (samli) na kadhalika. Kwa ‎jamii zetu, ni mchele, sembe, maharage, ulezi nk.
‎10. Kwa sababu kumetajwaa “Kumlisha” au “Chakula” kwa masikini, ‎basi maulamaa wengi, wanashurutisha kutolewa chakula chenyewe na ‎si mbadala wa chakula. Huu ndio msimamo rasmi, wa Imam Shafi, ‎Malik na Ahmad.
‎11. Hata hivyo, Imam Abu Hanifa–na anaungwa mkono na maulamaa ‎wengi kutoka madhehebu zote nyengine–inajuzu kutoa mbadala, yaani ‎thamani ya chakula kikuu cha jamii–maana lengo ni kumwezesha ‎masikini kujipatia chakula siku ya Idi, na siyo kumlazimisha kula ‎chakula kinacholiwa na watu wengi kwenye jamii. Amejenga hoja ‎yake kwamba siku ya Idi, mtu hupenda kula kile ambacho ni nadra ‎kukipata. Hula chakula tunu. Kwa hivyo, anaweza kupewa thamani ya ‎kiwango kinachotakiwa kutolewa.
‎12. Kiwango cha wastani ni pishi moja ya chakula cha kawaida–sawasawa ‎na kilo mbili na nusu.
13. Kwa nchi kama zetu za Afrika ya Mashariki, mchele wa kawaida ‎huuzwa mfuko wa Kilo TANO kwa bei ya baina ya shilingi 10,000 hadi 12,000. Hivyo, kilo mbili na nusu ni sawa na 5000 hadi 6000 ‎kwa kila mtu mmoja (sijui bei za sasa ni kiasi gani. Ila kigezo ni hicho ‎cha mfuko wa kilo tano). Bila ya shaka, bei ya sembe itakuwa ‎tofauti na bei ya mchele, ila kwa vile sembe ni kitu kinacholiwa sana ‎na watu wengi wasiojiweza, na hula wali nyakati za furaha na nadra, ‎basi ni bora kutoa mchele kuliko sembe. ‎

*INAENDELEA …* ‎

والله أعلم وبالله التوفيق‎
الحقير إلى الله تعلى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم

Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef

Kutoka “Kitalu cha Waja Wema: Maneno ya Muokozi ‎wa ‎Umma”, kitabu ‎ambacho ni tafsiri kamili ya ‎رياض الصالحين من كلام سيد المرسلين للإمام ‏النووي ‏‎ ‎kilichotungwa na Imam An-Nawawi na kufasiriwa kwa ‎Kiswahili na ‎Sayyid ‎Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim.‎

NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.‎

kcwajawema@gmail.com
 
KCWW RAM/29 1438

Darasa ya Ramadhani, Jumatatu tarehe 24 Ramadhani 1438, sawa na 19 Juni 2017

WAJIBU WA ZAKA YA FITRI

Zakatul-Fitr ni zaka/sadaka ya lazima inayotolewa baada ya ‎kumalizika Ramadhani, na kuingia tarehe mosi, Shawwaal/Mfungo Mosi: ‎mara tu baada ya kuandama mfungo wa Shawwaal, na hivyo kumalizika ‎Mfungo wa Ramadhani.‎

Inaitwa Zaka ya Fitri, kwa sababu ni Zaka inayotolewa baada ya ‎kufuturu/kumaliza Wajibu wa kufunga Ramadhani. ‎

Kama ilivyokuwa Sijdatus-Sahw, inayo sujudiwa mwisho wa ‎Swala–ni mfano wa raba au fidia ya kusahau kufanya Sunna maalum ndani ‎ya Swala, basi na Zakatul-Fitri ni kitakaso cha vijimakosa vidogo vidogo ‎vya Saumu, vilivyochumwa kwa kujua au kutokujua wakati wa kufunga ‎Ramadhani. Yaani ni kirekibisho cha palipoharibika kidogo katika Swaumu.‎

Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas ‎رضى الله عنهما‎ akisema: ‎Amesema Mtume ‎ﷺ‎,
زكاة الفطر طهرة للصائم من اللغو والرفث وطعمة للمساكين. فمن أداها فبل الصلاة فهي ‏زكاة مفبولة ومن ‏أداهابعد الصلاة فهي صدقة من الصدقات (رواه أبو داؤد ,ابن ماجه والدار قطنى)‏

‎“Zaka ya Fitri ni kitakaso cha aliyefunga kutokana na mambo ya ‎upuuzi na maneno machafu, na ni lishe kwa masikini. Hivyo, atayeitoa ‎kabla ya Swala, itapokewa kama Zaka, na atayeitoa baada ya Swala basi ‎ni sadaka kama sadaka yoyote ile nyengine.”‎

Wanachuoni wa Fiqh, huielezea na Zaka ya Fitri kwamba:‎

‏ زكاة الفطر: ‏صدقة معلومة بمقدار معلوم، من شخص مخصوص، بشروط مخصوصة، ‏عن ‏طائفة مخصوصة، لطائفة ‏مخصوصة، تجب بالفطر من رمضان، طهرة للصائم: ‏من اللغو، ‏والرفث، وطعمة للمساكين، ‏

‎“ Zaka ya Fitri ni Sadaka ya wajibu maalumu, ya kiwango ‎maalumu, ‎‏kutoka kwa mtu maalumu, kwa masharti maalumu, kwa niaba ya ‎watu maalumu, kupewa watu maalumu, kwa lengo maalumu, nalo ni ‎Kikataso cha Swaumu na chakula kwa masikini.”‎

Zaka ya Fitri imefaradhishwa mwezi wa Shaabani, mwaka wa pili ‎Hijriyya, kama ‎kitakaso cha mwenye kufunga Ramadhani.‎

Zaka ya Fitri imethibiti kwa Qu’aani na Sunna ya kauli na vitendo. ‎

Mwenyezi Mungu ‎سبحانه وتعالى‎ amesema, kwa wenye kujitakasa nafsi ‎zao kwa kutoa sadaka:
‎قَدْ أَفْلَحَ مَنْ تَزَكَّى* وَذَكَرَ اسْمَ رَبِّهِ فَصَلَّى * بل تؤثرن الحياة الدنيا * ‏واللآخرة خير وأبقى

‎“ Hakika amekwishafaulu aliyejitakasa na akakumbuka kutaja Jina la Mola ‎wake na akaswali. Ila ‎nyinyi mna hiari maisha ya dunia! Na ya Akhera ni ‎bora na yenye kudumu zaidi.” (Al-A‘la 87:14-15).‎

Wamesema Imam At-Tabari, Ibn Kathir na wengine, kuwa Sa‘id bin Al-‎Musayyib na ‘Umar bin ‘Abdul-‘Aziz (khalifa) na maswahaba wengine ‎wamesema Aya hizo zinazungumzia Zakatul-Fitr. Tafsir At-Tabari 24/374, pia ‎Muswannaf ‘Abdurrazaaq, Hadithi [HASHTAG]#5795[/HASHTAG].‎

Kwa upande wa Sunna:‎

Zimepokewa kutoka Mtume ‎ﷺ‎ Hadithi mbali mbali kuhusu wajibu ‎wa Zaka ya Fitri. Miongoni mwa Hadithi hizo ni:

‎1. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Umar ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr juu ya binaadamu, katika Mwezi wa ‎Ramadhani. Nayo ni pishi moja ya tende au shayiri kwa kila mja, awe huru ‎asiwe huru (mtumwa) mwanamume au mwanamke, miongoni mwa ‎Waislamu.” Muttafaq ‘alayhi.
‎2. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Umar ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr katika Mwezi wa Ramadhani, nayo ‎ni pishi moja ya tende, au pishi moja ya shayiri, juu ya mja aliye huru, ‎mwanamume au mwanamke, mkubwa au mdogo, miongoni mwa Waislamu. ‎Na akaamrisha itolewe kabla ya watu kwenda kuswali Swala ya Idi.” ‎Ameipokea Bukhari.‎

Hivyo, Zaka ya Fitri ni Zaka ya kiwiliwili SI zaka ya Mali. Inatolewa ‎kutakasa nafsi ya mja na kuisafisha, hata kama haina makosa au uchafu. ‎Na hiyo inamaanisha ni wajibu kutolewa kwa kila kiumbe Mwislamu, hata ‎aliyezaliwa leo, mwamume au mwanamke, mdogo au mkubwa, ‎muungwana au mtumwa.
3. Imepokewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas ‎رضي الله عنهما‎ akisema: ‎Amefaradhisha Mtume ‎ﷺ‎ Zakatul-Fitr kuwa ni kitakaso cha Swaumu ‎kutokana na makosa madogo madogo na mambo machafu, na kuwa ni ‎chakula kwa masikini. Hivyo basi, atayeitoa kabla ya Swala (ya Idi), Zaka ‎yake ya Fitr itakubaliwa, lakini atayeitoa baada ya Swala (ya Idi) basi hiyo ‎itakuwa ni sadaka tu kama sadaka yoyote nyengine.” Ameipokea Abu Daud.
‎4. Imepokewa kutoka kwa Abu Sa‘id Al-Khudriyy ‎رضي الله عنه‎ ‎akisema: Tulikuwa tukitoa sadaka ya Zakatul-Fitr (wakati wa Mtume ‎ﷺ‎) ‎pishi moja ya chakula, au shayiri, au pishi moja ya tende, au pishi moja ya ‎samli, au pishi moja ya zabibu.” Muttafaq 'alayhi. Na imepokewa vile vile na ‎Tirmidhi, Nasaa'i, Ibn Maajah, Abu Daud na Ahmad. ‎

UFAFANUZI

Zaka ya Fitri ni wajibu kwa kila nafsi ya Mwislamu anayetweta–yaani anaepumua. Ni Zaka ya kiwiliwili, si Zaka ya mali. Hivyo, midhali kiwiliwili ‎kipo basi lazima kitolewe Zaka ya Fitri. Ni wajibu. Ni Faradhi. Haiepukiki, ‎isipokuwa kwa yule ambaye hana uwezo kabisa. Hapo ‎لايكلف الله نفسا إلا وسعها‎.‎

Ama mwenye kipato, au mwenye wajibu wa kumtunza mtu mwengine, ‎kama mke, watoto, wazazi wake wawili wasiojiweza, watumishi wa ‎nyumbani na kadhalika, na kipato chake kikawa kinazidi wajibu wake wa ‎kuwatunza anaowatunza, basi ni wajibu KWAKE kujitolea yeye mwenyewe, ‎kwanza, na kisha kuwatolea wote wale anaowajibika kuwatunza, kwa hali na ‎mali. Yaani, lazima awe na chakula cha ziada ya kula yeye na familia yake, ‎siku ya Idi. Hicho kitachozidi ndicho kinachotolewa Zaka ya fitri. Kikiwa ‎hakitoshi kulisha familia yake hiyo siku ya Idi, basi hana jukumu la kutoa ‎Zaka ya Fitri.‎

Kwa maneno mengine, iwapo baba mwenye nyumba ni masikini, hana ‎cha kumtosha yeye na familia yake siku ya Idi, basi huyo hana wajibu wa ‎kutoa Zaka ya Fitri. Wala hana wajibu wa kumtolea mkewe, hata kama mke ‎huyo ni mwenye uwezo kutokana na kipato chake mwenyewe. ‎

Lakini mke mwenye kipato chake mwenyewe, anaweza kujitolea ‎kumtolea mumewe na watoto wake akipenda. Maana hana wajibu wa ‎kujitunza, wala kumtunza mumewe wala watoto wake. Ni hiari yake, na ni ‎fadhila kubwa, sana, kufanya hivyo. Ila SI wajibu juu yake. ‎

Zaka ya Fitri ni chakula, SI pesa. Na kiwango cha kutolewa ni ‎pishi moja ya chakula kinacholiwa sana katika jamii husika. Hivyo, vyakula ‎vinavyoingia hapa ni nafaka zote, kuanzia ngano, shayiri, mchele, unga wa ‎ngano, sembe, maharage, ulezi, nk. Ni chakula kinacholiwa sana ‎na watu wengi katika jamii ya mtoa Zaka hiyo.‎

Kiwango cha Zaka ya Fitri ni pishi moja, ambayo ni sawa na kilo mbili ‎na gram 400; kwa pishi ya Mtume ‎ﷺ‎ (ambayo ni sawa na vibaba ‎vine vya Mtume ‎ﷺ‎, na kibaba kimoja ni ujazo wa nafaka kwenye viganja ‎viwili–kwa pamoja–vya mtu wa kawaida). Hivyo, ni kama kilo mbili na ‎nusu za chakula kinachopendwa sana na jamii husika. Kiwango hicho ni kwa ‎kila kiumbe chenye uwezo wa kujitolea chenyewe. ‎

Iwapo hakina uwezo basi ni juu ya mwenye jukumu la kumtunza ‎kiumbe huyo, ilimradi ana uwezo wa shibe yake na shibe za watoto wake ‎wote, siku ya Idi. Kitachozidi ndicho kitachotolewa Zaka. Kama hakitoshi, ‎basi akigawe kwa utaratibu aliouweka Mtume ‎ﷺ‎ kama ifuatavyo: ‎

عن جابر رضي الله عنه قال قال رسل الله صلى الله عليه وسلم: ((ابدأ بنفسك فتصدق عليها، فإن ‏فضل شيء فلأهلك، فإن فضل عن أهلك شيء فلذي قرابتك، فإن فضل عن ذي قرابتك شيء فهكذا ‏وهكذا)) يقول: فبين يديك، وعن يمينك، وعن شمالك.(رواه مسلم) ‏

‎“Anza kujitolea mwenyewe. Kikizidi kitu watolee watu wako wa nyumbani ‎‎(anza na mke, kwanza, kisha watoto). Kikizidi kitu, watolee ndugu na jamaa ‎zako (anza na ndugu na jamaa wa karibu, kisha wa mbali). Kikizidi basi ‎watolee wa huku na huko, na kule na hapa (walio karibu zaidi nawe na ‎ambao si watu wa ukoo wako, kama majirani wa karibu).” Ameipokea ‎Muslim. ‎

SUNNA ZA KUTOA ZAKA YA FITRI

a) Kuitoa mara baada ya kuandama mwezi wa Shawwaal–yaani usiku wa ‎kuamkia Sikukuu, au kabla ya kwenda kuswali Swala ya Idi, au siku moja au mbili kabla ya kumalizika Ramadhani.
b) Kumtolea hata mtoto aliye tumboni, kama alivyokuwa akifanya ‎Sayyidina ‘Uthman bin ‘Affaan ‎رضي الله عنه‎. Ameipokea Ahmad na Ibn Abi ‎Shayba.
c) Kuigawa kwa mikono yako mwenyewe, badala ya kuwapa watu ‎wengine waitoe kwa niaba yako. Mtume ‎ﷺ‎ alikuwa akifanya hivyo, na ‎kuwausia Maswahaba nao wafanye hivyo.
d) Ukiwapa watoto wako nyumbani kuitoa, ni sawa na kuigawa ‎mwenyewe.
e) Kuwapa masikini jamaa zako, wenye kustahiki na ambao huna wajibu ‎wa kuwatunza.
f) Kuigawa kwa masikini wa mahali ulipo, ila ikiwa kuna wanaohitaji ‎zaidi, na ni jamaa zako, nchi nyengine.
‎g) Iwapo chakula unachotoa kina viwango mbali mbali, basi chagua ‎kiwango cha juu: Mwenyezi Mungu amesema: “Hamtaipata Pepo ‎mpaka mtoe mnavyovipenda.”
h) Kutoa nafaka kavu, inayoweza kuhifadhika kwa siku kadhaa bila ya ‎kuharibika, ni bora kuliko chakula kisichoweza kuhifadhika kwa ‎muda mrefu.
i) Kwa upande wa Wazazi wako wawili, ni Sunna kumtolea Mama ‎mzazi kwanza, kisha ndiyo Baba mzazi–iwapo wanakutegemea ‎kuwatunza.
j) Kuwapa majirani zako masikini, ni bora kuliko masikini wa mbali.‎

YALIYOMO NA YATOKANAYO

Kutokana na Aya za Qur’aani na Hadithi za hapo juu, maulamaa wema ‎waliotutangulia wamefafanua YALIYOMO NA YATOKANAYO kama ‎ifuatavyo:

‎1. Zakatul-Fitr ni wajibu, kwa kila mwenye kuweza, na ambaye ana ‎chakula cha ziada ya chakula chake cha Sikukuu ya mwanzo.
‎2. Asiye na uwezo, na ambaye yumo chini ya kukimiwa na mtu ‎mwengine, kama vile Baba mzazi, au hata mlezi wake tu, basi wajibu ‎wa kutolewa upo juu ya mabega ya mwenye kumkimu. Kwa maana ‎hiyo, Mume anamtolea mkewe, watoto wake, wazee wake–iwapo ‎wamo chini ya himaya yake–mtumishi au watumishi wake, bila ya ‎kujali umri au jinsia. Hata mtoto aliyezaliwa saa moja kabla ya ‎kuandama mwezi wa Shawwaal, anapaswa kutolewa sadaka ya Zakatul-Fitr.
‎3.‎ Zakatul-Fitr ni Zaka ya kutakasa mwili wa aliyefunga, kwa upande ‎mmoja, na hata asiyekuwa na wajibu wa kufunga, kwa upande wa pili, ‎ilimradi umeingia Mwezi wa Rehema na yeye yupo hai. Kwa maana ‎hiyo, Zakatul-Fitri ni Zaka ya NAFSI, SI ZAKA ya mali. Ndiyo maana inampasa kila mtu, mwanamume kwa mwanamke, ‎mdogo kwa mkubwa, muungwana na asiye muungwana.
‎4. Zakatul-Fitr inapaswa kutolewa kwa aliyoko karibu na aliyoko mbali, ‎ilimradi matunzo yake yapo juu ya mabega ya mzee wake. Hivyo, ‎mwanafunzi anayesoma ugenini–na anayetunzwa na wazee wake–‎anapaswa kutolewa Zaka yake ya Fitri.
‎5. Zakatul-Fitr ni mfano wa Sijdatus-Sahw kwenye Swala. ‎Imefaradhishwa ili kuziba mapengo yatayotokea, bila ya kujua, wakati ‎wa kufunga mwezi wa Ramadhani, kwa aliyefunga, au makosa ‎madogo madogo mengine, kwa aliyeruhusiwa kutokufunga–yaani ‎makosa madogo madogo yanayoweza kuchumwa katika mwezi wa ‎Ramadhani. Kwa lugha nyengine ya kisasa: Zakatul-Fitr ni RABA ya ‎kufuta makosa madogo madogo.
‎6. Kwa maana hiyo, Zakatul-Fitr anatolewa vile vile mtumishi Mwislamu, ‎kwa vile wajibu wa Swaumu upo juu yake kama Mwislamu yeyote ‎mwengine. Ama asiyekuwa mwislamu hatolewi Zakatul-Fitr, maana ‎wajibu wake kwanza, ni kuwa Mwislamu kabla ya kuanza kufunga.
‎7. Inaitwa Zakatul-Fitr kwa sababu ni Sadaka iliyokusudiwa kumlisha ‎masikini katika siku ya Idi. Yaani ni Zaka ya kumsaidia masikini ‎aweze kufungua kinywa Sikukuu ya Idi, na afurahike kama wanavyofurahika Waislamu wenziwe wenye kujiweza.
‎8. Kutokana na sababu hiyo kuu, ndiyo maana inatakiwa itolewe ‎KABLA ya Swala ya Idi. Na kama itatolewa mwishoni mwa ‎Ramadhani ni bora zaidi. Hivyo, mwezi mzima wa Ramadhani, hadi ‎kabla ya kuswaliwa Swala ya Idi, ni muda halali wa kutoa Zakatul-‎Fitr.
‎9. Kwa vile lengo la Zakatul-Fitr ni kumlisha masikini, basi ‎kinachotolewa ni chakula kinacholiwa sana katika jamii. Hivyo basi, ‎ama ni ngano, shayiri, tende, kitoweo kikuu (samli) na kadhalika. Kwa ‎jamii zetu, ni mchele, sembe, maharage, ulezi nk.
‎10. Kwa sababu kumetajwaa “Kumlisha” au “Chakula” kwa masikini, ‎basi maulamaa wengi, wanashurutisha kutolewa chakula chenyewe na ‎si mbadala wa chakula. Huu ndio msimamo rasmi, wa Imam Shafi, ‎Malik na Ahmad.
‎11. Hata hivyo, Imam Abu Hanifa–na anaungwa mkono na maulamaa ‎wengi kutoka madhehebu zote nyengine–inajuzu kutoa mbadala, yaani ‎thamani ya chakula kikuu cha jamii–maana lengo ni kumwezesha ‎masikini kujipatia chakula siku ya Idi, na siyo kumlazimisha kula ‎chakula kinacholiwa na watu wengi kwenye jamii. Amejenga hoja ‎yake kwamba siku ya Idi, mtu hupenda kula kile ambacho ni nadra ‎kukipata. Hula chakula tunu. Kwa hivyo, anaweza kupewa thamani ya ‎kiwango kinachotakiwa kutolewa.
‎12. Kiwango cha wastani ni pishi moja ya chakula cha kawaida–sawasawa ‎na kilo mbili na nusu.
13. Kwa nchi kama zetu za Afrika ya Mashariki, mchele wa kawaida ‎huuzwa mfuko wa Kilo TANO kwa bei ya baina ya shilingi 10,000 hadi 12,000. Hivyo, kilo mbili na nusu ni sawa na 5000 hadi 6000 ‎kwa kila mtu mmoja (sijui bei za sasa ni kiasi gani. Ila kigezo ni hicho ‎cha mfuko wa kilo tano). Bila ya shaka, bei ya sembe itakuwa ‎tofauti na bei ya mchele, ila kwa vile sembe ni kitu kinacholiwa sana ‎na watu wengi wasiojiweza, na hula wali nyakati za furaha na nadra, ‎basi ni bora kutoa mchele kuliko sembe. ‎

INAENDELEA …

والله أعلم وبالله التوفيق‎
الحقير إلى الله تعلى الدكتور السيد عبدالقادر شريف آل الشيخ أبى بكر بن سالم

Imetayarishwa na Sayyid Abdulqadir Shareef

Kutoka “Kitalu cha Waja Wema: Maneno ya Muokozi ‎wa ‎Umma”, kitabu ‎ambacho ni tafsiri kamili ya ‎رياض الصالحين من كلام سيد المرسلين للإمام ‏النووي ‏‎ ‎kilichotungwa na Imam An-Nawawi na kufasiriwa kwa ‎Kiswahili na ‎Sayyid ‎Abdulqadir Shareef Aal Shaykh Abi Bakr bin Salim.‎

NI RUHUSA KUNUKUU, kama ilivyo, pasi na kubadilisha au kuongeza chochote, ‎na ‎kuweka kwenye FB yako, ‎WhatsApp, na kwenye Makundi ‎ya ‎Mitandao ya Kijamii za Kiislamu, ‎kwa lengo la kusambaza na ‎kuelimisha ‎Dini. Changia kusambaza ‎Dini, ujipatie thawabu.‎

kcwajawema@gmail.com
باركا الله لك وكل مسلمين اجمعين.
 
Back
Top Bottom