Ulaya huwezi kumuita Mtoto wako jina la Kiafrika!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,786
Nimesoma mahali kwamba mpaka hivi majuzi nchi za Ulaya ulikuwa hauruhusiwi kumpa mtoto wako jina la Kiafrika, yaani kama wewe ni Raia wa nchi ya Ulaya halafu ukapata mtoto wa Kiafrika ambaye atakuwa raia moja kwa moja sasa labda ukataka kumpa jina la KitanZania sheria za Ulaya haziruhusu, yaani lazima umuite mtoto jina la hiyo nchi!

Na ndiyo maana Mario Baloteli ambaye wazazi wake asilia walikuwa ni wahamiaji haramu ktk Ghana kutokana na ugumu wa maisha ikabidi wamkabidhi mtoto wao kwa familia ya Kiitaliano, sasa ikawa ili aweze kuwa Muitalino ni lazima awe na jina la Kiitaliano na ndiyo hapo alipopoteza jina lake la Kiafrika na kupewa Mario Baloteli!

Na ndiyo maana hata Marekani, Wamarekani weusi wote hakuna mwenye jina la Kiafrika ingawaje walipoondoka Afrika walikuwa na majina yao ya kiafrika, sasa yalienda wapi?

Wazungu wote Wamarekani mpaka leo hii jina lake linaashiria nchi yake asilia ambako wazazi wake walitoka huko Ulaya, na hawajabadilisha!

Je kuna cha kujifunza hapa? Kama Wazungu hawaruhusu kumuita mtoto wako jina la Kiafrika ni kwa nini sisi tunaita watoto wetu majina ya Kizungu? Unakuta mtoto kazaliwa Tanzania anaitwa Michelle, John, Michael, George, Christoph, Ahmad, Mohamad, kwa nini tusitumie majina yetu?

Tena tunakwenda mbali kabisa ukiwa na jina la Kiafrika unachekwa kwamba ni baya, ukimuuliza Mtanzania akwambie jina zuri utasikia Sidney, Florenz, Irene n.k sasa ni kwa nini?
 
Wenyewe wanasema to be civilized lazima tuachane na all primitives norms including our good names.

Majina yetu pia yanaonekana hayaendani na wakati. Nadhani haitowezekana tena maana sisi wenyewe hata tusipokuwa ulaya watoto wetu hatuwapi majina yetu ya asili kama vile Mrisho,Komba,Mbuna ,Kinjeketile nk. naamini hata wewe mtoa mada wazazi wako wangekuita Mwajuma ungetafuta jina mbadala la kujitambulisha.
 
Wenyewe wanasema to be civilized lazima tuachane na all primitives norms including our good names.Majina yetu pia yanaonekana hayaendani na wakati. Nadhani haitowezekana tena maana sisi wenyewe hata tusipokuwa ulaya watoto wetu hatuwapi majina yetu ya asili kama vile Mrisho,Komba,Mbuna ,Kinjeketile nk. naamini hata wewe mtoa mada wazazi wako wangekuita Mwajuma ungetafuta jina mbadala la kujitambulisha.


Lakini swali langu ni kwamba ni kwa nini sisi tu Dunia nzima ndiyo tuko hivi? Yaani Waafrika weusi?
 
Wenyewe wanasema to be civilized lazima tuachane na all primitives norms including our good names.Majina yetu pia yanaonekana hayaendani na wakati. Nadhani haitowezekana tena maana sisi wenyewe hata tusipokuwa ulaya watoto wetu hatuwapi majina yetu ya asili kama vile Mrisho,Komba,Mbuna ,Kinjeketile nk. naamini hata wewe mtoa mada wazazi wako wangekuita Mwajuma ungetafuta jina mbadala la kujitambulisha.

Samahani kwa kumtaja mtu, lakini Mtangazaji mmoja alikuwa ananipa raha sana kwa jina lake, Izengo Bujago Kadago, sijui yuko wapi huyu. Sasa siku hizi vijana hata majina ya ukoo hawataki kutumia, utasikia naitwa John Peter, Neema Peter, ukimuuliza la tatu, anakwambia natumia mawili tu, swine kabisa.
 
asili ya mwafrika inapotea. mamlaka husika zipo kimyaaaaa kama hawapo vile
 
Nimesoma mahali kwamba mpaka hivi majuzi nchi za Ulaya ulikuwa hauruhusiwi kumpa mtoto wako jina la Kiafrika, yaani kama wewe ni Raia wa nchi ya Ulaya halafu ukapata mtoto wa Kiafrika ambaye atakuwa raia moja kwa moja sasa labda ukataka kumpa jina la KitanZania sheria za Ulaya haziruhusu, yaani lazima umuite mtoto jina la hiyo nchi!

Na ndiyo maana Mario Baloteli ambaye wazazi wake asilia walikuwa ni wahamiaji haramu ktk Ghana kutokana na ugumu wa maisha ikabidi wamkabidhi mtoto wao kwa familia ya Kiitaliano, sasa ikawa ili aweze kuwa Muitalino ni lazima awe na jina la Kiitaliano na ndiyo hapo alipopoteza jina lake la Kiafrika na kupewa Mario Baloteli!

Na ndiyo maana hata Marekani, Wamarekani weusi wote hakuna mwenye jina la Kiafrika ingawaje walipoondoka Afrika walikuwa na majina yao ya kiafrika, sasa yalienda wapi??

Wazungu wote Wamarekani mpaka leo hii jina lake linaashiria nchi yake asilia ambako wazazi wake walitoka huko Ulaya, na hawajabadilisha!

Je kuna cha kujifunza hapa??? Kama Wazungu hawaruhusu kumuita mtoto wako jina la Kiafrika ni kwa nini sisi tunaita watoto wetu majina ya Kizungu? Unakuta mtoto kazaliwa Tanzania anaitwa Michelle, John, Michael, George, Christoph, Ahmad, Mohamad, kwa nini tusitumie majina yetu???
Tena tunakwenda mbali kabisa ukiwa na jina la Kiafrika unachekwa kwamba ni baya, ukimuuliza Mtanzania akwambie jina zuri utasikia Sidney, Florenz, Irene n.k sasa ni kwa nini?
Talib Kweli kwani jina lake kabisa ni nani?
 
Ndio maana namkubari sana mobutu na sera yake ya Africanization ikiwemo kutotumia majina ya kizungu badala yake tutumie ya kwetu kama vile ngosha, kibena, mkude, meku, masumbuko, shida, hawafu n.k.
Vipi kuhusu basketball player anaeitwa Rajon Rondo, Andre Iguodala, rapper anaeitwa Talib Kweli Greene na Aliaume Damala Badara yaani Akon? Ipe hoja yako nyama kaka
 
Talib Kweli kwani jina lake kabisa ni nani?


Huyo atakuwa amejipa tu, kama ni Mmarekani haswa yaani hawezi kuitwa Talib Kweli, hilo litakuwa baada ya kujitambua na kuuliza maswali kama ninayouliza hapa akauona ukweli na kuamua kubadilisha jina lake, lkn lazima jina lake alilopewa baada ya kuzaliwa litakuwa la Kizungu!
 
Lakini swali langu ni kwamba ni kwa nini sisi tu Dunia nzima ndiyo tuko hivi? Yaani Waafrika weusi?
Barbarosa sisi waafrica hatujikubali na hii yote kwa sababu tunajiona kama tumeumbwa kwa bahati mbaya hatuna haki yetu so kila tulichonacho akija mzungu au Mwarabu akisema hii ni laana basi tunaachana nacho hata kama ilikuwa ni mila yetu yenye kutufikisha kwenye mafanikio fulani.Ndio maana wazee wetu walikuwa wakibadilishwa dini na hao waleta dini baasi tena jina lake la asili amelitupa kapuni.
 
Vipi kuhusu basketball player anaeitwa Rajon Rondo, Andre Iguodala, rapper anaeitwa Talib Kweli Greene na Aliaume Damala Badara yaani Akon? Ipe hoja yako nyama kaka


Nimeshajibu kama ni Wamarekani haswa yaani kizazi cha utumwa hawezi kuitwa Talib Kweli, hao wote wamebadilisha ukubwani baada ya kujitambua!
 
Talib Kweli kwani jina lake kabisa ni nani?
Anaitwa Talib Kweli Greene
Nimeshajibu kama ni Wamarekani haswa yaani kizazi cha utumwa hawezi kuitwa Talib Kweli, hao wote wamebadilishi ukubwani baada ya kujitambua!
Ila mkuu uliongelea hata kwa kizazi cha sasa kama cjakosea. Ina maana kule kwa sasa wanaruhusiwa kujiita majina ya waafrika?
 
Nimesoma mahali kwamba mpaka hivi majuzi nchi za Ulaya ulikuwa hauruhusiwi kumpa mtoto wako jina la Kiafrika, yaani kama wewe ni Raia wa nchi ya Ulaya halafu ukapata mtoto wa Kiafrika ambaye atakuwa raia moja kwa moja sasa labda ukataka kumpa jina la KitanZania sheria za Ulaya haziruhusu, yaani lazima umuite mtoto jina la hiyo nchi!

Na ndiyo maana Mario Baloteli ambaye wazazi wake asilia walikuwa ni wahamiaji haramu ktk Ghana kutokana na ugumu wa maisha ikabidi wamkabidhi mtoto wao kwa familia ya Kiitaliano, sasa ikawa ili aweze kuwa Muitalino ni lazima awe na jina la Kiitaliano na ndiyo hapo alipopoteza jina lake la Kiafrika na kupewa Mario Baloteli!

Na ndiyo maana hata Marekani, Wamarekani weusi wote hakuna mwenye jina la Kiafrika ingawaje walipoondoka Afrika walikuwa na majina yao ya kiafrika, sasa yalienda wapi??

Wazungu wote Wamarekani mpaka leo hii jina lake linaashiria nchi yake asilia ambako wazazi wake walitoka huko Ulaya, na hawajabadilisha!

Je kuna cha kujifunza hapa??? Kama wazungu hawaruhusu kumuitta mtoto wako jina la Kiafrika ni kwa nini sisi tunaita watoto wetu majina ya Kizungu? Unakuta mtoto kazaliwa Tanzania anitwa Michelle, John, Michael, George, Christoph, Ahmad, Mohamad, kwa nini tusitumie majina yetu???

Si kweli mkuu!!

Mimi nimezaa na kujukuu huku Marekani. Watoto wangu wote nimewazaa hapa (mke wangu na mimi tukiwa wa-Tanzania) na watoto wote tumewapa majina ya kiTanzania, tena yale ya kikabila kabisa. Wamerekani walikwaa ndimi zao weee mpaka sasa wanayatamka vizuri tu.

Wajukuu wetu wote wamezaliwa hapa hapa Marekani. Wazazi wao ni waMarekani na hao wajukuu wote wana majina ya kimatumbi, tena yale konk kabisa.

Kumpa mtoto jina unalotaka ni chaguo lako mwenyewe popote pale duniani. Nina marafiki wa kiAfrika waliozagaa dunia nzima na ni kama tumeambizana, watoto na wajukuu wao (sio wote) wamewapa majina ya kiAfrika.

Wamarekani weusi wanashindwa kutoa majina asilia ya kiAfrika kwa kuwa wengi hawajui kwao ni wapi. Wengi wao wanatumia ubini wa waliowaweka utumwani (slave names).

Unajua, mimi nilipozaliwa (katika familia ya kikatoliki) wazazi wangu waliamini kuwa mkristu huwezi kumpa mtoto wako jina la kimatumbi. Ilikuwa ni kama lazima vile umpe mtoto jina lenye asili ya mashariki ya kati au kirumi (Mathews, Luka, Maria, Juventus, n.k.).

Hivyo hivyo kwa wale wanaozaliwa katika Uislamu wazazi wao watawaita majina ya Kiarabu (Salim, Farida, Seif). Ni nadra sana kukuta mtoto wa kiTanzania aliezaliwa katika dini akapewa (akasilimishwa au akabatiizwa kutumia) jina la kimatumbi.

Huu nao ni utumwa wa kifikra wa aina fulani.

Tafakari.
 
Back
Top Bottom