Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

aisee umenichekesha sana, inaonekana kuna vingi vitamu kumbe hatujavionja tu!

ngoka nijaribu kuongezea kidogo kuhusu huyo mwalimu wako...........

very rough,
baadae alipata ukuu wa shule katika shule moja inaitwa nahukahuka,
baadae akahamia shule flani inaitwa mtua (bado yupo) kama mwalimu wa kawaida,
mkulima mzuri wa nyanya na mbogamboga zingine.....haoni hatari kujitwisha tenga la mchicha/nyanya kichwani na kutembeza!
Kweli unamjua Mr Mwazembe..Yule jamaa namkubali hanaga mambo ya aibu,enzi hizo analima bustani mahiwa alikuwa anaweza kujitwisha tenga akaenda nyangao kupeleka pilipili oho au kabichi
 
Jamaa nimeamua kumkaushia Tu..sipendagi ligi,tena kaungana na Peramiho yetu wakawa wawili wananipinga,wakati Mimi nayajua nje ndani maeneo ya mikoa ya Lindi na Mtwara

Mkoa wa Lindi sehemu km Nyangao,mahiwa,namupa,sehemu za Rondo,Namangale,Baadhi ya vitongoji vya mtama,Nachingwea na baadhi ya vijiji vya Ruangwa vyenye wakristo wengi km luagalala,namahema NK panya wanalika vizuri tu
Cc Chige
 
Yule sio panya... Tuelewane hapo kwanza. Kuanzia Wayao, Wamakua, Wamatumbi, Wamakonde na makabila mengi ambayo nimekutana nayo wanakula huyo kiumbe. Na walaji wengi ni wakulima.
Kwamba "yule sio panya", usitake ku-complicate mambo!! Kuhusu hayo makabila uliyotaja, ukitoa Wayao na Wamakua, na sana sana Wamakua, narudia, hayo makabila mengine sio kweli!! Panya wanaliwa na watu wa Masasi ambako wenyeji wa huko sio Wamatumbi wala Wamakonde! Wamatumbi wapo Kilwa, na hawali panya!! Wamakonde wapo wilaya za Mtwaar mjini, Vijijini, Newala, na Tandahimba! Wenyeji wa hizo wilaya, majority ni Waislamu.

Kwa watu mnaopita huko juu juu ndio mnashindwa kutofautisha, lakini Wamakonde wenyewe na wenyeji wa huko wanajua kutofautisha kati ya Wamakonde na Wamawiya! Hawa Wamawiya ndio huwa hawachagui nyama, na wengi wao wanatokea Msumbiji!!!
Shida yenu vijana ni kubisha tu hata kama kitu hukijui. Mie ni mkulima na nimelima maeneo hayo na siku hizi makabila yamechanganyika sana tofauti na zamani. Kusini yote nimevuruga sijui utaniambia nini. Nimelala sana maporini, naomba nisiongee sana sababu naweza kuta nabishana na mtu ambae anaifahamu kwa kupitia google. Na hao unaosema ni waislamu sana wa kusini huko wanagonga kitimoto kama hawana akili nzuri hususani ya kitomoto pori.

Unabishana na mtu ambaye yupo Mtandi sahizi akiwa ametoka Kibo muda huu.
Sio kweli!!!
 
Satoh Hirosh yupo sahihi panya wanaliwa sana hata mkoa wa Lindi maeneo yenye wakristo wengi.
Basically, ulaji wa panya kule hauna uhusiano na dini bali na kabila!! Na kama hoja ni dini, kwa Lindi ni wilaya ya Nachingwea ndiko unaweza kukuta Wakristo wengi, na majority ni Wamwera na hawali panya!! kutokana na ukaribu wa Masasi na Nachingwea, ndipo unaweza kukuta baadhi ya watu huko wanakula panya lakini sio kwa sababu ni Wakristo bali ni Wamakua wa Masasi!!! Kwenye posts zangu nimetaja Waislamu kwa sababu we all know Waislamu ndio wenye ku-complicate mambo yanayohusu misosi!!
 
Wakati wewe unayajua maeneo ya huko nje ndani, tena kwa kutembelea tu mimi ni mtu wa huko!! NImekuuliza, Lindi sehemu au wilaya gani? Tuanze hapo kwanza!
Chige unataka nn mkuu..mbn comment yangu imejitosheleza kujibu swali lako

Hebu funguka pengine sijaielewa hoja yako..lkn km ni kuhusu Lindi wanaliwa sehemu gani panya Tyr nimejibu
 
Kuna upupu wa porini(unawasha) na upupu tunaita wa nyumbani(hauwashi),huu wa nyumbani sasa ndio unaoliwa,unapandwa(mbegu zipo)shambani na kuvunwa ukikomaa na kukauka.Unapikwa na kumwagwa maji mara kadhaa then unachunwa maganda yake na kupikwa tena mpaka uive,hapo unakua tayari kwa kuliwa.Unaweza kula kama ulivyo kwa kunyunyuzia chumvi kama chipsi kavu au unaweza kuungaaka na viongo vingine kama nyanya na vitunguu then ukala au ukafanya mboga.Mostly upupu unatumika kama kifungua kinywa na ni biashara nzuri sana wilaya ya masasi(kuuza upupu usiopikwa kwa wapikaji,kuuza upupu uliopikwa kww walaji)

Ule wa porini kuna baadhi wanauandaa pia na kula,maandalizi yake si ya kitoto,unaweza chomoka ulimi ukikosea.
Umenikumbusha mbali sana shule ya msingi Nanjoka Tunduru ukupiga upupu na maji asubh unaweza usile mpaka mchana unashibisha balaaa
 
Basically, ulaji wa panya kule hauna uhusiano na dini bali na kabila!! Na kama hoja ni dini, kwa Lindi ni wilaya ya Nachingwea ndiko unaweza kukuta Wakristo wengi, na majority ni Wamwera na hawali panya!! kutokana na ukaribu wa Masasi na Nachingwea, ndipo unaweza kukuta baadhi ya watu huko wanakula panya lakini sio kwa sababu ni Wakristo bali ni Wamakua wa Masasi!!! Kwenye posts zangu nimetaja Waislamu kwa sababu we all know Waislamu ndio wenye ku-complicate mambo yanayohusu misosi!!
Mkuu naijua hiyo Wilaya pengine kuliko unavyoijua.

Wamwera wa Marambo, upande mwingine Mitumbati, Farm 2 ...17 , Mtila kuelekea Mnero wanagonga hiyo kitoweo kama wamakua.
Pia Ruangwa na baadhi ya vijiji vilivyokuwa vya Lindi vijijini kutoka Nanganga kuelekea Ruangwa wanakula panya sana tu. Maeneo ya Namakuku, Mkowe, .... e.t.c.

Wamakonde wa kitanzania wa Chiumbati na maeneo jirani wanakula panya kama kawaida.

Ukweli wamakua wanakula sana panya, na tembo(ndovu) kuliko makabila mengine ya kusini. Wanaongoza wamakonde wa Msumbiji wale wakristo.
 
Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
Bwana weweeee, kwani hujuwi habari bila picha kuwa hainogi tuuuuu!
 
Kwamba "yule sio panya", usitake ku-complicate mambo!! Kuhusu hayo makabila uliyotaja, ukitoa Wayao na Wamakua, na sana sana Wamakua, narudia, hayo makabila mengine sio kweli!! Panya wanaliwa na watu wa Masasi ambako wenyeji wa huko sio Wamatumbi wala Wamakonde! Wamatumbi wapo Kilwa, na hawali panya!! Wamakonde wapo wilaya za Mtwaar mjini, Vijijini, Newala, na Tandahimba! Wenyeji wa hizo wilaya, majority ni Waislamu.

Kwa watu mnaopita huko juu juu ndio mnashindwa kutofautisha, lakini Wamakonde wenyewe na wenyeji wa huko wanajua kutofautisha kati ya Wamakonde na Wamawiya! Hawa Wamawiya ndio huwa hawachagui nyama, na wengi wao wanatokea Msumbiji!!!

Sio kweli!!!
Kwa details hizi, we lazima utakuwa Chinga sema unajifanyisha tu kwamba eti ulitembelea huko
 
25 Reactions
Reply
Back
Top Bottom