Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

Sio kweli!! Ni Masasi peke yake ndiko panya wanakoliwa kwa wingi! Hakuna sehemu yoyote Lindi unakoweza kuta panya wanaliwa kwa wingi, na ukiona watu wanakula panya basi huyo ni mwenyeji wa Masasi! Ni kama Zanzibar ukute mtu au baadhi ya watu wanakula kitimoto halafu u-conclude kwamba ni jambo la kawaida sana Zanzibar kuona watu wanakula kitimoto!

Ukikuta mahali Lindi wanakula panya basi ni kama kukuta Zanzibar watu wanakula kitimoto!! Pia sio rahisi ukute panya wanaliwa kwa wingi wilaya zingine za hata mkoa wa Mtwara mbali na Masasi kwa sababu, ukitoa Masasi, wilaya karibu zote Mtwara zimejaa Waislamu!!

Hili nalifahamu vizuri kwa sababu nimezunguka sehemu mbalimbali za mkoa wa Lindi na Mtwara kuanzia mwezi March hadi June.
Mkuu nilichokieleza ni kweli kabisa

Kuna sehemu mkoa wa Lindi panya wanakula vizuri Tu..au naongopa mkuu Viprealestate
 
Wewe muongo!!! Ukitoa wilaya ya Masasi (ambayo ndiyo inachanganya na Namtumbo), maeneo mengine uliyotaja yote sio kweli. Mahali kama Newala ukikuta panya basi ni kwa uchache, na watakuwa wanaliwa na wenyeji wa Masasi, au labda watu wa Msumbiji ambao wao ndio ula hadi Chatu, lakini Mmakonde wa kawaida, ambao wengi ni Waislamu, huwezi kukuta wanakula panya au chatu!
Na hata hvyo namtumbo inapakana na wilaya ya tunduru si masasi wilaya ya masasi inapakana na wilaya ya NANYUMBU ambayo makao yake makuu yapo m MANGAKA

Huyo jamaa n muongo anatulisha matango pori

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Sio kweli!! Ni Masasi peke yake ndiko panya wanakoliwa kwa wingi! Hakuna sehemu yoyote Lindi unakoweza kuta panya wanaliwa kwa wingi, na ukiona watu wanakula panya basi huyo ni mwenyeji wa Masasi! Ni kama Zanzibar ukute mtu au baadhi ya watu wanakula kitimoto halafu u-conclude kwamba ni jambo la kawaida sana Zanzibar kuona watu wanakula kitimoto!

Ukikuta mahali Lindi wanakula panya basi ni kama kukuta Zanzibar watu wanakula kitimoto!! Pia sio rahisi ukute panya wanaliwa kwa wingi wilaya zingine za hata mkoa wa Mtwara mbali na Masasi kwa sababu, ukitoa Masasi, wilaya karibu zote Mtwara zimejaa Waislamu!!

Hili nalifahamu vizuri kwa sababu nimezunguka sehemu mbalimbali za mkoa wa Lindi na Mtwara kuanzia mwezi March hadi June.
Satoh Hirosh yupo sahihi panya wanaliwa sana hata mkoa wa Lindi maeneo yenye wakristo wengi.
 
Wewe muongo!!! Ukitoa wilaya ya Masasi (ambayo ndiyo inachanganya na Namtumbo), maeneo mengine uliyotaja yote sio kweli. Mahali kama Newala ukikuta panya basi ni kwa uchache, na watakuwa wanaliwa na wenyeji wa Masasi, au labda watu wa Msumbiji ambao wao ndio ula hadi Chatu, lakini Mmakonde wa kawaida, ambao wengi ni Waislamu, huwezi kukuta wanakula panya au chatu!
Yule sio panya... Tuelewane hapo kwanza. Kuanzia Wayao, Wamakua, Wamatumbi, Wamakonde na makabila mengi ambayo nimekutana nayo wanakula huyo kiumbe. Na walaji wengi ni wakulima.

Shida yenu vijana ni kubisha tu hata kama kitu hukijui. Mie ni mkulima na nimelima maeneo hayo na siku hizi makabila yamechanganyika sana tofauti na zamani. Kusini yote nimevuruga sijui utaniambia nini. Nimelala sana maporini, naomba nisiongee sana sababu naweza kuta nabishana na mtu ambae anaifahamu kwa kupitia google. Na hao unaosema ni waislamu sana wa kusini huko wanagonga kitimoto kama hawana akili nzuri hususani ya kitomoto pori.

Unabishana na mtu ambaye yupo Mtandi sahizi akiwa ametoka Kibo muda huu.
 
Nadhani mtoa post anawazungumzia Ndezi ambao nahisi kama jina lingine ndio Panya pori. Na kuna mdau amezungumzia wale wanaokula wadudud kwenye magamba ya miti, wadudu wale wanaitwa Sondo.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Asee nimeishi Sana kilwa hasa maeneo ya kipatimo masoko pande nakiu nanjirinji kiranjeranje kinjumbi chumo kibata sijawah ona watu wakila chatu au panya si kweli

Panya wanaliwa maeneo ya masasi mangaka Tena mangaka au nanyumbu n maeneo machache Sana


Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Umeishi lakini hujalima..... Watu wanaokula hawa viumbe huwa ni wakulima na sio majumbani.

Ila watu mnashangaza hapa, yawezekana mnadhani viumbe hawa wanauzwa mabuchani. Tembeeni mashambani huko muone watu wanakula vitu gani.

Mie nimeshuhudia wati wakila chatu Mafia sehemu wanaita Utende. Jiulize ni kina nani waliokua wakila hao chatu? Usije ukasema waburushi sijui hawali nimekaa miaka 8 huko sijaona. Suala la kuona ni binafsi sana.

Hata huko Meatu, Shinyanga, Kibiti, Mwanza, Morogoro, Mwanza wanakula hawa viumbe na kote nimeshuhudia watu wakila. Ukitaka kuona show ya hayo mambo tembelea wakulima.
 
Nilikula panya Lusaka tena downtown kabisa wanauzwa kwenye masinia a wale wadudu jamii ya washa washa watam balaa
 
Kama ni hao wa shambani hata mi nimekula sana utotoni huko mkoani. Kuna mwingine panyabuku, kuna mnyama makazi yake ni chini kwa chini anapendelea sehemu mliyolima viazi vitamu na haoni mchana (jina lake kwa kiswahili sijui, najua kwa lugha yangu tu)
 
Nilikula panya Lusaka tena downtown kabisa wanauzwa kwenye masinia a wale wadudu jamii ya washa washa watam balaa
hata hao jamii ya washawasha nimekula, kuna funza wanene wa kwenye miti nimepiga, ndege fulani wana rangi nyeupe na nyeusi hawaliwi kule mkoani mimi nimepiga, paka anayetembea usiku tu anakula kuku nimepiga, hao panzi ndio sana tu.
 
Hebu nieleze vizuri hapo kwenye UPUPU kuwa msosi .
Kuna upupu wa porini(unawasha) na upupu tunaita wa nyumbani(hauwashi),huu wa nyumbani sasa ndio unaoliwa,unapandwa(mbegu zipo)shambani na kuvunwa ukikomaa na kukauka.Unapikwa na kumwagwa maji mara kadhaa then unachunwa maganda yake na kupikwa tena mpaka uive,hapo unakua tayari kwa kuliwa.Unaweza kula kama ulivyo kwa kunyunyuzia chumvi kama chipsi kavu au unaweza kuungaaka na viongo vingine kama nyanya na vitunguu then ukala au ukafanya mboga.Mostly upupu unatumika kama kifungua kinywa na ni biashara nzuri sana wilaya ya masasi(kuuza upupu usiopikwa kwa wapikaji,kuuza upupu uliopikwa kww walaji)

Ule wa porini kuna baadhi wanauandaa pia na kula,maandalizi yake si ya kitoto,unaweza chomoka ulimi ukikosea.
 
Kuna kisa kimoja cha mwalimu wangu juu ya ulaji wa panya..
nimesoma kusini mkoa wa Lindi shule moja inaitwa mahiwa high school

Mwalimu wangu wa geography aliitwa Mr mwazembe jitu la miraba minne kutoka mbeya alibahatika kupata binti wa pale kijijini,.Ruti za shuleni kwenda kijijini Kwa mchumba wake zilikuwa nyingi sn.

Km unavyojua mikoa ya Lindi na Mtwara ulaji wa panya ni kitu cha kawaida sn,Kwa hiyo mke wa ticha alikuwa mlaji mzuri sn wa panya.Km ilivyo kawaida ya wabongo,ticha alidharau sn watu wanokula panya,lkn Yule dada (demu wake) alikuwa mlaji wa panya..siku moja ticha akaamua kujaribu kuonja..asee Radha aliyokutana nayo,kuanzia siku hiyo akageuka kuwa ndiyo kinara wa walaji panya

Ticha akaenda mbali zaidi,akawa na mtu wake maalumu anachukua panya kwa bili,kisha analipia mwisho wa mwezi mshahara ukitoka..
Mwazembe ni Mnyiha, Wanyiha wanakula panya pia. Labda ticha mwanzon alikuwa anavunga tu.
 
Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
ajabu yake, wanakula sana panya lakini panya wewe hawaishi. hata hivyo, siwadharau kwasababu katika maisha yangu ilishawahi kutokea sehemu fulani nilipokuwepo wanakula panya, na nilikula hadi nikawazoea kama chakula cha kawaida kabisa. wala sio kitu cha ajabu.
 
25 Reactions
Reply
Back
Top Bottom