Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

Kuna kisa kimoja cha mwalimu wangu juu ya ulaji wa panya..
nimesoma kusini mkoa wa Lindi shule moja inaitwa mahiwa high school

Mwalimu wangu wa geography aliitwa Mr mwazembe kitu la miraba minne kutoka mbeya alibahatika kupata binti wa pale kijijini,.Ruti za shuleni kwenda kijijini Kwa mchumba wake zilikuwa nyingi sn.

Km unavyojua mikoa ya Lindi na Mtwara ulaji wa panya ni kitu cha kawaida sn,Kwa hiyo mke wa ticha alikuwa mlaji mzuri sn wa panya.Km ilivyo kawaida ya wabongo,ticha alidharau sn watu wanokula panya,lkn Yule dada (demu wake) alikuwa mlaji wa panya..siku moja ticha akaamua kujaribu kuonja..asee Radha aliyokutana nayo,kuanzia siku hiyo akageuka kuwa ndiyo kimara wa walahi panya

Ticha akaenda mbali zaidi,akawa na mtu wake maalumu anachukua panya kwa bili,kisha analipia mwisho wa mwezi mshahara ukitoka..
Chezea atoro wewe
 
Panya wa porini wana proteins nyingi sana. Ni nyama nzuri tu kwa matumizi ya binadamu kama ilivyo ndezi.

Ni utamaduni hasa wa wamakua kutoka Wilaya ya Masasi mkoa wa Mtwara. Panya ni watamu sana.

Ahsante.
 
Mkuu vipi mzunguko wa pesa Lindi na Mtwara upo? Kuna fursa gani zinapatikana huko?
 
Kuna kisa kimoja cha mwalimu wangu juu ya ulaji wa panya..
nimesoma kusini mkoa wa Lindi shule moja inaitwa mahiwa high school

Mwalimu wangu wa geography aliitwa Mr mwazembe kitu la miraba minne kutoka mbeya alibahatika kupata binti wa pale kijijini,.Ruti za shuleni kwenda kijijini Kwa mchumba wake zilikuwa nyingi sn.

Km unavyojua mikoa ya Lindi na Mtwara ulaji wa panya ni kitu cha kawaida sn,Kwa hiyo mke wa ticha alikuwa mlaji mzuri sn wa panya.Km ilivyo kawaida ya wabongo,ticha alidharau sn watu wanokula panya,lkn Yule dada (demu wake) alikuwa mlaji wa panya..siku moja ticha akaamua kujaribu kuonja..asee Radha aliyokutana nayo,kuanzia siku hiyo akageuka kuwa ndiyo kimara wa walahi panya

Ticha akaenda mbali zaidi,akawa na mtu wake maalumu anachukua panya kwa bili,kisha analipia mwisho wa mwezi mshahara ukitoka..
Umemaliza mwaka gani Mahiwa Mkuu.
 
Nimesoma o level pale Kaka
Nimemaliza 2011..Bila Shaka Kwa hili swali lako unapajua mahiwa
Napajua mkuu,ingawa sijasoma hapo ila nilikuwa na mdogo wangu,akawa anasoma Advance hapo Mahiwa High school,kamailiza six 2011. Nikawa namtembelea nyakati za likizo.
 
Habar zingine zinahitaj moyo kuzisoma,mnavyozisifia panya nimechefukwa mno adi nahis kutapika,ila nimejifunza kitu apo
 
Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
Unajua Mungu kaumba viumbe wawili wawili wenye kama kufanana fanana hivi.

Panya wa nyumbani na panya wa porini wanafanana haoo.

Binadamu na tumbili wanafanana hao.

Kenge na mamba wanafanana hao.

Paka na chui hufanana hao.

Tandu na jongoo hufanana hao.

Nyoka na mkunga hufanana haoo.(kuna watu wanakula mkunga nyoka hawali)

Pwngine panya wa porini sio panya ila walipewa jina la panya na watu fulani kswa kuona wamefanana na wale wa nyumbani na kuwafanya wote kuwa panya.

Pengine hata mkunga angepewa jina la nyoka laiti tungelichelewaa kidogo na ingekuwa kumla mkunga inasemwa uamemla nyokaaa
 
Safari yenye takribani kilomita 600+ hadi Mkoani Mtwara wilaya ya Masasi kijiji cha Nangoo napata fursa ya kuifahamu jamii ya watu wa mikoa hii japo kwa uchache.

Nikiwa eneo hilo nilipata fursa ya kufahamu baadhi ya tamaduni za kule, baadhi tu kama vile Unyago na aina ya vyakula ambavyo vipo tofauti na vingine.

Achana na kufanya Upupu kama ni chakula ila hili la ulaji panya lilinivutia zaidi, Panya!! Ukuaji wangu umenikuza nikiamini Panya ni sehemu ya wadudu waharibifu wa kwenye nyumba za watu au mashambani.

Biashara ya kitoweo hiki kule Kusini siyo ya kificho, ni biashara ya wazi inayotembezwa kama bidhaa nyingine tu ya kawaida. Panya wanawekwa kwenye mtungo wa mti au kupangwa fungu kwa idadi fulani na kufungwa na kamba.

UPATIKANAJI NA UANDAAJI WA PANYA
Mwanzo nilidhani ni rahisi tu kupata Panya kwasababu ni kawaida kuwakuta kwenye nyumba zetu za kawaida kumbe la hasha! Siyo kila panya ni kitoweo.

Panya wa Porini Vs Panya wa Nyumbani.

Ikae akilini mwako kuwa kule wametofautisha Panya kwa aina hizo mbili, sasa taarifa ikufikie wale Panya wa Porini ambao kwa kawaida wanapatikana mashambani huko hasa ndio maalumu kwajili ya Kitoweo. Muda wangu wote kule sijashuhudia Panya wa nyumbani wakifanywa kitoweo bali uuliwa na kutupwa kama ilivyo sehemu nyingine.

Panya wa Porini wanapatikana kwenye mashimo huko shamba na kuna utaalamu katika uwindaji wake. Sasa tutazame namna wanaandaliwa Panya hadi kuwa Kitoweo.

Wakishapatikana wanaondolewa uhai wao kwa kupigwapigwa chini, hatua inayofuata ni kuwasafisha/ kuwaandaa kwa kuweka viungo kama chumvi na pilipili kiasi halafu unawabanika jikoni kwa moto wa wastani.

Ni kama tu unavyobanika Kuku au vile wamasai wanavyoweka Nyama kwenye Mtungo na kubanika. Baada ya zoezi hilo hatua inayofuata ni kuwafunga mafungu au kuuza mmoja mmoja tayari kwa kitoweo.

JE, INASHANGAZA?
Hapana bali inavutia, hata mimi mwanzo kila nilipojaribu kuonesha kuwashangaa nao walinishangaa kwanini nina washangaa basi tukawa tunashangaana.

Hoja yao wanasema huo ni utamaduni wao na uheshimiwe ni kitu kilichobadili mtazamo wangu juu yao, wanasema mbona ipo jamii inakula Mbwa kitu ambacho kule kusini siyo utamaduni wao kabisa. Mwingine aliniambia wapo watu wa Mkoa fulani wanakula panzi, bahati nzuri kwao waliamua kukipa thamani kitoweo chao.

FAHAMU
Siyo watu wote wa Kusini wanakula Panya HAPANA, wapo wengine ni tofauti kabisa na hawajawahi kula hata mara moja. Nafikiri hii ni kawaida tu kwenye mambo mengi.

Siku zangu 37 za kuishi kusini nilijifunza mengi sana, watu wake ni wema na wakarimu wanaojali zaidi wageni kuliko wenyewe kwa wenyewe. Huu ni udhaifu toka kwao.

Mwisho.
Katika safari yako ya siku 35,ulibahatika kupiga kitoweo hicho mara ngapi ndugu,na ulikionaje,ulikifurahia ama?
 
Niongezee nyama kidogo mkuu.

Kwanza kabisa panya hupatikana Kwa wingi kuanzia mwezi wa sita Hadi wa kumi ,kipindi ambacho wakulima wameshavuna mahindi na ufuta mashambani.Panya wanaovunwa kipindi hiko huwa wananona na huwa na mafuta mengi sn Kwa sababu hula mabaki ya vyakula vilivyopo mashambani Kama mahindi,mtama,muhogo na ufuta

Wawindaji wa panya huangalia mashimo yaliyo na njia nyingi zilizo bize,na mashimo ndani ya hayo huwa na panya kuanzia 50 Hadi 100+

Maandalizi:

Panya hupangwa kwenye fimbo ndefu,fimbo moja wanaweza kupangwa hata panya 10 kisha Moto mkubwa huwashwa kisha zile fimbo zenye panya huwekwa kwenye Moto Kwa ajili ya kubabua manyoya

Baada ya manyoya kubabuliwa na kubaki na ngozi laini isiyo na manyoya,Moto unapunguzwa na kubakia Moto wa wastani kisha panya hubanikwa..hatua hii panya huwa wananona na kutoa mafuta mengi sn kiasi cha kumfanya mtu kutokwa na mate Kwa uchu

Baada ya kazi ya kubanikwa kumalizika hutolewa kwenye zile fimbo walizotundikwa na kupangwa mafungu Tyr Kwa kuuza

Mnunuaji wa panya akigika nyumbani anawatoa utumbo kisha huwaunga..kumbuka mapishi ya panya ni tofauti na samaki,panya hawahitaji mchuzi mwingi,mapishi yake ni Kama losti ya maini au nyama

Mboga ikishakamilika inakuwa Tyr kuliwa..tofauti na wakosoaji wengi kwa watu wanaokula panya,nyama ya panya ni tamu sn na mtu yeyote akijaribu Kula panya aliyeandaliwa vizuri hawezi kuacha Kula nyama ya panya

Kuna kisa kimoja cha mwalimu wangu wa geography kutoka kanda Fulani ambaye alikuja kugeuka mlaji mzuri sn wa panya nitakielezea...
Duuu aisee wewe jamaa wa Nyumbani kabisaaa!!!
Mwezi wa Tisa nakuja Masasi Kwenye msimu wa korosho naomba uniandalie panya kadhaa nitawapokea hapo ndanda
 
Back
Top Bottom