Ulaji wa mafuta wa Crown v6 2.5l 12km/l

ili neno "kwahiyo" wanaopenda kutumia wengi ni watu wasio jiamini na duniani kuna kiumbe mmoja tu ambaye hajiamini ambaye ni ha ha ha ha ladies and gentlemen
Kwahiyo unashangaa nini? Na hili ni jukwaa la nini?
 
Niwaambie sasa, niliwahi fanya research ndogo kuhusu gari aina ya Toyota Progress Engine CC 2400, nilichofanya baada ya kukabidhiwa tu na Muuzaji nikaipiga full Tank lita around 60, nikatembea nayo muda wa siku tatu then nikarud nayo petrol station nikajaza tena full tank nikapiga hesabu lita nilizotumia kwa siku zile 3. Then nikachukua utofauti wa kilometa wa siku nakabidhiwa gari na siku ile ya tatu niliyoweka tena mafuta nikagundua kuwa kwa kila lita 1 katika zile siku 3 nimetembea km 6.5. Na huu ndo ulaji halisi wa gari zote za CC 2400 hadi 2900 km gari itatembea chini ya km 80 kwa saa Muda mwingi.
Mkuu,ni kweli kabisa. Verossa,Brevis,Crown,Mark X,Grande Mark II,Harrier VVTi 2362 cc,Rav4 VVTi 2362 CC,zote hizo range ya matumizi ya mafuta ni kilometa 6.4-7.0 tu kwa lita. Tena magari mengine inasoma hapo,6-6.8 kwenda7
 
Wadau kila mara napitia page ya enhance auto,,Kwakua nazipenda crown, najaribu kuangalia ulaji wake wa mafuta naona wameendika 12km/l,,Pamoja na web page zingine,,
Je ni kweli kwetu hapa tanzania ni hivyo? Na kama ni hivyo mbona naona crown nyingi sana zinauzwa bado ili hali zimeingizwa nchini siku chache, Nina imani wengi wanaziuza sababu ya unywaji uliokubhu wa mafuta.
Wenye experience na ulaji wa crown ukiacha wa kwenye notes za mtandaoni tushare jamani,,,
Tusije kukurupuka halafu nasisi baada ya muda turudi mitandaoni kuuza!
Mkuu ulaji wa mafuta kwa Gari una factor nyingi.. Ila kwa haraka haraka tu hiyo 12km/l wanaongelea uendeshaji kwenye safari ndefu na sio mjini/kwenye foleni ambapo Mara nyingi unatembelea Gia ndogo.. Kama unendeshea Dar ulaji wa crown unacheza kati ya 6.5-8km/l ambacho ni kawaida kabisa kwa Gari nyingi.. Mfano GX 110 grand kwa uendeshaji wa hapa mjini inatumika 7-8km/l ila ukisafiria safari ndefu inatumika 12-13km/l.
 
Lakini tukumbuke ulaji wa wastani ni 8km/l kwa magari mengi ambapo nadhani hata hio crown kama inakula sana wese haitoshuka chini ya hapo.
Crown ulaji wake wa town trip ukicheki autodata.net imeandikwa ni 7.87km/l wabongo wengi wapo rough kwenye acceleration yani mtu anataka kuvuka taa za karume anakanyaga mafuta rpm inafika mpaka kwenye 4, kwanza hii gari ukibadili setting inakuonesha ulaji wake wa mafuta i.e 8.5km/l pia inakuonesha kwa mafuta yaliopo kwenye tank gari inatembea km ngapi Mungu akisaidia huyu mnyama mweusi lazima niwe nae
 
Tatizo lingine ni pale mtu ananunua gari anataka aweke mafuta ya 10,000-20,000 halafu atembee nalo wiki nzima au kilomita zaidi ya 100 A/C ipo on revs za 3-4 rpm hapo lazima aulize kuhusu ulaji wa mafuta bila shaka
 
Aisee fanya kweli bablai, mie najipanga mdo mdo ila tutafika tu huko.

Crown ulaji wake wa town trip ukicheki autodata.net imeandikwa ni 7.87km/l wabongo wengi wapo rough kwenye acceleration yani mtu anataka kuvuka taa za karume anakanyaga mafuta rpm inafika mpaka kwenye 4, kwanza hii gari ukibadili setting inakuonesha ulaji wake wa mafuta i.e 8.5km/l pia inakuonesha kwa mafuta yaliopo kwenye tank gari inatembea km ngapi Mungu akisaidia huyu mnyama mweusi lazima niwe nae
 
Tatizo lingine ni pale mtu ananunua gari anataka aweke mafuta ya 10,000-20,000 halafu atembee nalo wiki nzima au kilomita zaidi ya 100 A/C ipo on revs za 3-4 rpm hapo lazima aulize kuhusu ulaji wa mafuta bila shaka
wanayumba
 
Mkuu ukinunua Crown ni sawa na umefunga nayo ndoa,ni hazifai kwa consuption ya mafuta
Tena ikiwa V6 hio ni ndoa hata kuuza huiuzi labda utauza bei ya bodaboda
Crown ikiwa Highway unaenda zaidi ya speed 110 hapo utaiona geji ya mafuta inavyopuliza
Kwa swala la Luxury,Full Options pia barabarani zinatulia,Hapo kwa Crown ni kiboko
Lkn kwa upande wa mafuta ndio ni kichef chefu hazifai
Pia
Brevis
Mark II GX 110 Grand
Mark II GX 100
Hizo zote hazifai kwasbb ni V6 kwa mafuta unaweza ukaiacha gari barabarani,hususa kwa town unatembelea gea kubwa kwasbb ya Jam hapo kila baada ya siku 2 lazma mafuta ya 40 elf yatahitajika ndio taa ya petrol izimike ktk gej ya mafuta‍♂️
Kwa uhakika ingia App ya Kupatana utazikuta hizo gari zikiwa bado safi kabisa lakini bei zake zinavyouzwa hazizidi Milion4‍♂️
Bila shaka wewe ulikimbia umande
 
Back
Top Bottom