Ukwiukwaji wa Haki za Binaadamu Tarime: Waziri Mkuu aomba Msamaha...

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,582
Katika Kipindi cha Maswali na ya papo kwa papo leo kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Tarime. Mhe. Charles Mwera, ameuliza swali kuhusu vitendo vya udhalilishaji, unyanyasaji na uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu kulikofanya na polisi mkoa wa kipolisi wa Tarime, cha kuwalazimisha kina mama kuvua nguo zao zote mpaka za ndani, na kuwalazimisha kuwanyonya hao polisi sehemu zao za siri!

Waziri Mkuu alioneshwa kushtuka na kuguswa sana tukio hilo la Tarime. Kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu Pinda, ameomba msamaha kwa niaba ya Serikali kwa yaliyotokea kama ni kweli yametokea, pili ameitisha kikao cha dharura kati ya Mwera, Waziri wa mambo ya ndani na wahusika wengine, kikao hicho kitafanyika asubuhi hii hii baada ya kipindi cha maswali na majibu.

My Take:
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kupokea hoja ya upinzani na sio tuu kuifanyia kazi promptly, bali pia kuiombea msamaha jamii husika na umma kwa jumla.

Huu ni ustaarabu wa ziada wa Mhe. Pinda, anayo sifa ya ziada iitwayo 'humility', ndio maana kwenye mauaji ya albino, ni kiongozi pekee ambaye chozi lilimtoka.

Huu unaweza kuwa ni utamaduni mpya wa serikali kukubali hoja za msingi za wapinzani na kuzifanyia kazi promptly.
 
Heshima kwako Pasco,

Nimeisoma habari hii kwa masikitiko makubwa sana,lakini pia nimefarijika kusikia waziri mkuu alivyorespond yamkini hatua sahihi zitachukuliwa dhidi ya polisi waliofanya kitendo cha kinyama kiasi hicho.

Nadhani Tarime ni kanda maalumu [mkoa wa kipolisi] labda polisi wamechukulia sababu za kuanzishwa kwa mkoa wa kipolisi Tarime ni sababu tosha ya kufanya ushenzi dhidi ya raia.Nategemea polisi wote waliohusika watafukuzwa kazi na kuchuliwa hatua nyingine zaidi za kisheria.

Napenda kumpa pole mbunge wa Tarime na wakaazi wote wa Tarime kwa mateso na manyanyaso wanayopata.
 
Kuna mambo yakifanyika mtu unashindwa kuamini kama yanafanyika tanzania hii. Hili tukio la Tarime kwa kweli limetuumiza watu wengi. Hawa polisi wetu mbona kuna wakati wanakuwa kama vichaa? Unawezaje kumvua mwana mama nguo zote na kumlazimisha anyonye nyeti za mwanaume mbele ya kadamnasi? Jamani tuko Tz au Somalia? Ukatili huo na manyanyaso hayo hayavumiliki. Serikali ichukue hatua kwa kweli.
 
...I am reserving my praises first for the PM untill I hear some heads rolling! This was the most inhumane someone could do to our Mothers.
 
We Pasco, mama yako ananyonya askari halafu unaombwa msamaha unafurahia! namna gani hapa!
 
We Pasco, mama yako ananyonya askari halafu unaombwa msamaha unafurahia! namna gani hapa!
Shalom, hivi nimeonyesha nimefurahi?
Unaweza kutofautisha kufurahi na appreciation?.
Mimi ni appreciate humility ya Pinda ambayo, hata rais wako hana, na waziri Masha ndio kabisa. Polisi wamefanya mambo mabayo, maovu na ya ajabu kuliko haya and no one showed any humility japo angalau kusema pole tuu an samahani. Pinda limemgusa kasema pole.

Ukiondoa Nyerere alipoomba msamaha kiutu uzima na kwa kusema " kufanya kosa sio kosa, kosa kurudia kosa, na kukubali kuwa huko nyuma tulifanya makosa, kiongozi gani kati viongozi wetu wakuu amewahi kuomba msamaha wowote hadharani?.

Madudu mangapi yamefanywa na polisi bila hata watu kupewa pole, nimesikia kifuta machozi kwa wale waliouwawa Pemba, kilitoka mwaka jana, ni Sh. 50,000 kwa kila familia!, Brother Ditto (RIP), alipomditto yule dereva wa daladala pale Lugalo kwa ditto, serikali ilikimbiza ubani wa 1,000,000 kwa mjane, na VC kumtembelea kumpa pole. Hata wale wachimba madini wa Zombe, umewahi sikia hata pole, au ubani, ua serikali kuomba msamaha kwa yaliyotokea?.

Ndio maana nikaapreciate hii humility ya Pinda, inaweza ikawa ni mwanzo wa utamaduni japo sio wa kuwajibika serikali, bali kuonyesha concern na ku act first which is "a good thing" na sio kufurahi kama unavyodhani.
 
Pamoja na kuomba msamahaa, hao askari wamechukuliwa hatua gani mpaka sasa?
 
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kupokea hoja ya upinzani na sio tuu kuifanyia kazi promptly, bali pia kuiombea msamaha jamii husika na umma kwa jumla.

Huu ni ustaarabu wa ziada wa Mhe. Pinda, anayo sifa ya ziada iitwayo 'humility', ndio maana kwenye mauaji ya albino, ni kiongozi pekee ambaye chozi lilimtoka.

Huu unaweza kuwa ni utamaduni mpya wa serikali kukubali hoja za msingi za wapinzani na kuzifanyia kazi promptly.

Pasco ndugu yangu Oktoba sio mbali sana, kitu chochote negative kinaeza kuwa na athari kubwa kwa wapiga kura. Kumbuka Gordon Brown aliponzwa na neno bigot, ikabidi arudi kuomba msamaha kwa yule mama na msamaha ukaonyeshwa live ili watu waone waziri mkuu wao anajali.

hii yote i kubemebeleza kura oktoba 2010, yaani ingekuwa kwenye boxing tungesema wamebanwa kwenye kona.
 
Pamoja na kuomba msamahaa, hao askari wamechukuliwa hatua gani mpaka sasa?

Nadhani kikao hicho cha pamoja PM, Mwema na Lau ndo kitaamua kuwa wapigwe risasi, wafukuzwe kazi, wapelekwe mahakamani au watoroshwe, hii ni Tanzania. where the obvious does not happen and the unexpected always happens.
 
Muda wa kura umekaribia...kila mmoja sasa anajitahidi kuwa mwema...angalieni kwa makini. hata hivyo tunahitaji actions zaidi kuliko msamaha hewa...
 
Katika Kipindi cha Maswali na ya papo kwa papo leo kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Tarime. Mhe. Charles Mwera, ameuliza swali kuhusu vitendo vya udhalilishaji, unyanyasaji na uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu kulikofanya na polisi mkoa wa kipolisi wa Tarime, cha kuwalazimisha kina mama kuvua nguo zao zote mpaka za ndani, na kuwalazimisha kuwanyonya hao polisi sehemu zao za siri!

Waziri Mkuu alioneshwa kushtuka na kuguswa sana tukio hilo la Tarime. Kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu Pinda, ameomba msamaha kwa niaba ya Serikali kwa yaliyotokea kama ni kweli yametokea, pili ameitisha kikao cha dharura kati ya Mwera, Waziri wa mambo ya ndani na wahusika wengine, kikao hicho kitafanyika asubuhi hii hii baada ya kipindi cha maswali na majibu.

My Take:
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kupokea hoja ya upinzani na sio tuu kuifanyia kazi promptly, bali pia kuiombea msamaha jamii husika na umma kwa jumla.

Huu ni ustaarabu wa ziada wa Mhe. Pinda, anayo sifa ya ziada iitwayo 'humility', ndio maana kwenye mauaji ya albino, ni kiongozi pekee ambaye chozi lilimtoka.

Huu unaweza kuwa ni utamaduni mpya wa serikali kukubali hoja za msingi za wapinzani na kuzifanyia kazi promptly.
Hizi Response zimekaa kisiasa zaid...
Waziri Masha akiulizwa hili atasema pia hajui..
 
Shalom, hivi nimeonyesha nimefurahi?
Unaweza kutofautisha kufurahi na appreciation?.
Mimi ni appreciate humility ya Pinda ambayo, hata rais wako hana, na waziri Masha ndio kabisa. Polisi wamefanya mambo mabayo, maovu na ya ajabu kuliko haya and no one showed any humility japo angalau kusema pole tuu an samahani. Pinda limemgusa kasema pole.

Ukiondoa Nyerere alipoomba msamaha kiutu uzima na kwa kusema " kufanya kosa sio kosa, kosa kurudia kosa, na kukubali kuwa huko nyuma tulifanya makosa, kiongozi gani kati viongozi wetu wakuu amewahi kuomba msamaha wowote hadharani?.

Madudu mangapi yamefanywa na polisi bila hata watu kupewa pole, nimesikia kifuta machozi kwa wale waliouwawa Pemba, kilitoka mwaka jana, ni Sh. 50,000 kwa kila familia!, Brother Ditto (RIP), alipomditto yule dereva wa daladala pale Lugalo kwa ditto, serikali ilikimbiza ubani wa 1,000,000 kwa mjane, na VC kumtembelea kumpa pole. Hata wale wachimba madini wa Zombe, umewahi sikia hata pole, au ubani, ua serikali kuomba msamaha kwa yaliyotokea?.

Ndio maana nikaapreciate hii humility ya Pinda, inaweza ikawa ni mwanzo wa utamaduni japo sio wa kuwajibika serikali, bali kuonyesha concern na ku act first which is "a good thing" na sio kufurahi kama unavyodhani.
Alikuwa wapi hadi aje aombe msamaha bungeni tena baada ya kuulizwa!!!!!tusidanganywe na hawa jamaa....tofauti ya Pinda na viongozi wengine ni kwamba Pinda anajua Wa TZ wanataka nini,thats why hata majibu yake yako so smoothe,ila inatusaidia nini kuomba msam,aha tena mpaka uulizwe!!!!in maana alikuwa hajui, ila atlest tunashukuru..angekuwa Masha angejibu "Tunalichunguza hilo na tutalitolea tamko"
 
Pasco ndugu yangu Oktoba sio mbali sana, kitu chochote negative kinaeza kuwa na athari kubwa kwa wapiga kura. Kumbuka Gordon Brown aliponzwa na neno bigot, ikabidi arudi kuomba msamaha kwa yule mama na msamaha ukaonyeshwa live ili watu waone waziri mkuu wao anajali.

hii yote i kubemebeleza kura oktoba 2010, yaani ingekuwa kwenye boxing tungesema wamebanwa kwenye kona.
Ngambo Ngali, nakubaliana na wewe kuelekea Octoba, wazee watawaamkia vijana, watoa pesa watatoa pesa na kutanguliza asante, badala ya mpokeaji kushukuru na mengine mengi.

Ila naomba nimtete Pinda, jamaa ni kweli ana humility, humble na down to earth sio kwa ajili ya kuombea kura. Ndio maana hata kusikika hasikiki sana katika mikiki mikiki ya kuelekea 2015.
 
Ngambo Ngali, nakubaliana na wewe kuelekea Octoba, wazee watawaamkia vijana, watoa pesa watatoa pesa na kutanguliza asante, badala ya mpokeaji kushukuru na mengine mengi.

Ila naomba nimtete Pinda, jamaa ni kweli ana humility, humble na down to earth sio kwa ajili ya kuombea kura. Ndio maana hata kusikika hasikiki sana katika mikiki mikiki ya kuelekea 2015.

Pasco, kama ni hivyo nakubaliana nawe kwenye second take yako kuwa Mheshimiwa PM ana humility ya Ziadan aya hali ya juu, ni kiongozi aliyejiweka chini ya watu, myenyekevu, anajali shida za watu, lakini maskini hakuna anayemsikiliza.
 
Miaka ya sabini kuna madudu yaliyofanyika usukumani yanayofananafanana na haya. Pengine Pinda anaweza kujifunza kutokana na hatua zilizochukuliwa na serikali ya kipindi kile. RPC, RSO walihukumiwa kifungo miaka 7 baada ya kusota rumande zaidi ya miaka 3.

Huu ni uovu mkubwa ambao hauwezi kufanywa na askari wa chini bila baraka za wakuu wao. Kama huyo kamanda wa kanda maalum bado yuko ofisini, huo msamaha unaoombwa na Pinda itakuwa mzaha na kejeli kwa waliofanyiwa uovu huo!
 
My take:
a) Kuomba msamaha haitoshi na kiongozi hatakiwi kuomba msamaha bila kutuambia hatua zinazochukuliwa kwa wahusika.
b) Mwema umechukua muda sana kutupa feedback ya uchunguzi wako na hatua zilizochukuliwa, WHY WHY WHY? Kuvua watu nguo na unyama huo unahitaji siku ngapi kufanyiwa uchunguzi wakati hadi watoto wadogo wameona?
c) Fanya uchunguzi wa askari wako mara kwa mara, kuna wagonjwa wa akili, wavuta bange, wala unga, ukizingatia wengi waliingia baada ya kufeli shule. Wasio na maadili watafutie sababu-OUT!
 
Back
Top Bottom