Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,582
Katika Kipindi cha Maswali na ya papo kwa papo leo kwa Waziri Mkuu, Mbunge wa Tarime. Mhe. Charles Mwera, ameuliza swali kuhusu vitendo vya udhalilishaji, unyanyasaji na uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu kulikofanya na polisi mkoa wa kipolisi wa Tarime, cha kuwalazimisha kina mama kuvua nguo zao zote mpaka za ndani, na kuwalazimisha kuwanyonya hao polisi sehemu zao za siri!
Waziri Mkuu alioneshwa kushtuka na kuguswa sana tukio hilo la Tarime. Kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu Pinda, ameomba msamaha kwa niaba ya Serikali kwa yaliyotokea kama ni kweli yametokea, pili ameitisha kikao cha dharura kati ya Mwera, Waziri wa mambo ya ndani na wahusika wengine, kikao hicho kitafanyika asubuhi hii hii baada ya kipindi cha maswali na majibu.
My Take:
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kupokea hoja ya upinzani na sio tuu kuifanyia kazi promptly, bali pia kuiombea msamaha jamii husika na umma kwa jumla.
Huu ni ustaarabu wa ziada wa Mhe. Pinda, anayo sifa ya ziada iitwayo 'humility', ndio maana kwenye mauaji ya albino, ni kiongozi pekee ambaye chozi lilimtoka.
Huu unaweza kuwa ni utamaduni mpya wa serikali kukubali hoja za msingi za wapinzani na kuzifanyia kazi promptly.
Waziri Mkuu alioneshwa kushtuka na kuguswa sana tukio hilo la Tarime. Kwa mara ya kwanza, Waziri Mkuu Pinda, ameomba msamaha kwa niaba ya Serikali kwa yaliyotokea kama ni kweli yametokea, pili ameitisha kikao cha dharura kati ya Mwera, Waziri wa mambo ya ndani na wahusika wengine, kikao hicho kitafanyika asubuhi hii hii baada ya kipindi cha maswali na majibu.
My Take:
Hii ni mara ya kwanza kwa serikali kupokea hoja ya upinzani na sio tuu kuifanyia kazi promptly, bali pia kuiombea msamaha jamii husika na umma kwa jumla.
Huu ni ustaarabu wa ziada wa Mhe. Pinda, anayo sifa ya ziada iitwayo 'humility', ndio maana kwenye mauaji ya albino, ni kiongozi pekee ambaye chozi lilimtoka.
Huu unaweza kuwa ni utamaduni mpya wa serikali kukubali hoja za msingi za wapinzani na kuzifanyia kazi promptly.