Hivi Msigwa ni mchungaji wa aina gani. Anayetapeli hadi wajane??!??????.
.
Tarehe za viambatanisho mbona utata mtupu maggid ......... sometimes ni vizuri kukaa kimya. Umenikumbusha yule mwandishi mwenzio aliyekuja kulalama hapa akidai yeye sio shoga bali anazushiwa tu........michango aliyopata humu JF mpaka leo simsikii tena!
https://www.jamiiforums.com/celebri...-pili-wa-pascal-mayalla-maisha-binafsi-4.html
Ngoja tumsubiri Mchungaji Msigwa naye aje aseme yake kwani kwa ushahidi uliotolewa na Mjenga, pesa kiasi cha Shs. millioni moja kilihamishiwa kwenye account yake.
Je alizifikisha? Mchungaji njoo usafishe jina lako.
Tiba
utata uko wapi mpsea 19/9/2012 na CRDB tarehe 4/10/2012.
Sasa mbona hujatoa conclusion ya kufuta upotoshwaji wa kuchafua majina ya watu?
Ungemaliza kwa kusema kuwa hakuna mtu aliyetafuna fedha za Familia ya Mwangosi, si Peter Msigwa wala Lukosi.
Kwenye maandishi yako umeishia kujidefend wewe binafsi pasi na kuwasafisha wenzio.
Alipofariki David Mwangosi. Ulishupalia sana, ukageuka kuwa msemaji wa polisi na waandishi wa habari wa Iringa.
Umoja wa waandishi wa habari wa lringa,waligoma kuandika habari za kipolisi mkoa wa lringa wakishinikiza kamanda Kamuhanda awajibike.
Ulivyo mnafiki Majid ukajitokeza kuwapiga wenzio na kuwa kibaraka wa Kamuhanda.
Ukaona haitoshi ukaanza kufanya PR eti kwa kuchangisha rambirambi ambazo kimsingi mpaka leo bado hujaziwakilisha.
Mbali na kuunga mkono kauli ya Chagonja kuwa David Mwangosi kadondokewa na kitu chenye ncha na ukataka jamii iamini hivyo
Mungu si Athuman, tukapata picha za mnato alivyouliwa Mwangosi, lakini ulipinga tena.
Laana ya kupinga kifo cha mwangosi na kula rambirambi zake. Daima mzimu wa Mwangosi hautokoma kukuandama daima. Una laana katubu kwanza.
Kweli walimu wana kazi....
Inakuwaje same amount amtumie Msigwa kwa Mpesa halafu aiingize tena CRDB? Walau hiyo pay-in-slip ingesainiwa na Msigwa tungeelewa......na gap ya hizo tarehe wewe sio utata kwako?
Sasa km Uliingiza hela ktk Account ya huyo mjane moja kwa moja ingawaje ulipewa maagizo umpatie mchungaj msigwa kwanini usitokeze na kumwambia kwa ujasiri huyo mwehu Lukosi kuwa aache ujinga?UKWELI WANGU KUHUSU UTATA RAMBIRAMBI ZA MJANE WA MWANGOSI...
......
Hitimisho: Ukweli wangu ndio huo. Hakuna hata senti moja ya rambirambi kwa mjane wa marehemu Mwangosi iliyopotea mikononi mwangu. Na chini hapo ni risiti ya CRDB ikionyesha fedha zote zilizochangwa na nilizoziingiza kwenye akaunti ya Itika Mwangosi, mjane wa marehemu Mwangosi. Ushahidi wa majina ya waliochangia na kiasi walichochanga pia upo.
Nimeyaweka haya hadharani kwa nia njema ili kuzuia upotoshaji na hali ya kuchafuana majina kama ningeamua kubaki kimya.
Nawashukuru nyote mnaoendelea kuniamini hata mnaposikia yenye kuzushwa juu yangu.
Wenu Katika Ujenzi wa Nchi Yetu.
Maggid Mjengwa.
Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio