Kanjwinjwi
JF-Expert Member
- Jun 22, 2017
- 256
- 342
Correction: Malimao na tangawizi, nyungu havitibu malaria wala typhoid bali vinasaidia kutibu CoronaNyungu haitibu corona msijidangamye. Ikikupata kama immune system yako ni ndogo lazima uende.
Mimi nimeugua wiki mbili. Nilianza na nyungu lakini hali ilikuwa mbaya zaid. Nimekula michanganyiko ya malimao tangawizi, pilipili etc. Hali ikaendelea kuwa mbaya tu. Mpaka mdomo na koo likawa chungu kisa kula madawa yasiyokuwa na dose.
Nilichofanya ni kupima magonjwa yote. Nikakutwa na malaria na typhoid. Nikayatibu kwa kumaliza dose zote. Nikala matunda ya kuimprove immune system Kama mananasi, machungwa na parachichi.
Mafuta ya mawese hayakukosa katika chakula nilichokuwa nikila. Nikaacha kulala lala nikapiga mazoez na kuendelea na kazi nyingne ndogo ndogo.
Nilirecover bila hata mwenyewe kujua. Mke wangu naye akafatia. Nkamwambia achane na nyungu afanye kama nilivyofanya yani yeye alipona within days.
Ukiumwa typhoid na malaria nenda hospital kama ulivyofanya na sio kila ukijiskia kuumwa ni Corona magonjwa mengine bado yapo hayajaenda likizo