Ukweli uwe mbele: 'Walioaminiwa sana' na Mwendazake wakichunguzwa, madudu hayatatazamika. Kuungwa kwao mkono na Mwendazake kilikuwa kichaka hatari

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Mambo yameanza kunoga. Deusdedith Kakoko wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ametiwa nguvuni na yuko chini ya TAKUKURU kwa mahojiano na uchunguzi. Sote tunajua kuwa Mwendazake alikuwa akimwamini na kumtetea sana Kakoko. Alikuwa akimsifu na kumpa 'sapoti' ya kutosha na kutisha. Rangi halisi ya Kakoko wa Bandari imeanza kuonekana. Rangi ya kutisha, ufisadi wa kutisha.

Kakoko alikuwa Mungumtu pale Bandari. Amewachafua na kuwafukuza wote waliokuwa na uwezo wa kikazi kuliko yeye waliokuwa Mameneja wa Bandari katika mikoa mbalimbali hapa Tanzania. Mfano ni Bwana Salama aliyekuwa Meneja wa Bandari kule Kigoma. Alimchafua na kumfukuza kazi pamoja na ufanyakazi wake uliotukuka ulioongeza hata faida na kuimarisha Bandari ya Kigoma. Kwasasa Bwana Salama anapambana na kesi yake Tume ya Utumishi.

Kakoko ni mfano tu ya waliojificha kwenye kuaminiwa na Mwendazake na kufanya ufisadi/wizi/dhulma kubwa. Muda wa kuwashughulikia umefika. Muda wa kuwachunguza umewadia. Muda wa kuchoma kichaka chao ni huu. Wamefanya mengi sana mabaya kuzihusu fedha za umma na fedha za watu binafsi. Wametesa watumishi na wananchi wa kawaida. Nawataja baadhi: Makonda, Sabaya, Chalamila na Dotto James.

Kuaminiwa na Mwendazake kulikuwa ndiyo kisingizio chao. Nasema hivi, wale wote waliokuwa wakiaminiwa sana na Mwendazake wachunguzwe. TAKUKURU tafadhalini wasaidieni watanzania kujua ukweli kuwahusu hao na wengine watakaotajwa na wananchi. Tunahitaji kusafisha nchi yetu ili tusonge mbele bila kelele. Mafisadi washughulikiwe kwa kuonekana. Mafisadi wawajibike.

Propaganda na uongo ndizo zilizokuwa nguzo za Serikali ya Mwendazake!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Tuliwahi andika humu kuwa huwezi kupambana na rushwa na ufisadi kama vyombo vya habari hasa vya uchunguzi, Bunge na Whistleblowers hawako huru.

Watu, kwa ujinga na ushabiki, walikuwa wanaifananisha awamu ya Magu na ya Kikwete katika swala zima la rushwa na ufisadi bila kuzingatia ukweli kuwa, enzi za Kikwete, Bunge, Vyombo vya habari na Whistleblowers walikuwa na uhuru wa kuanika madudu ya serikali na watendaji wake.

Mashabiki wa Jiwe wataishia kwa aibu na fedheha sana kipindi hiki.
 
Hii kuanza kutaja majina randomly inanikumbusha Makonda alivyokua anataja majina ya mashoga na drug dealers baadaye Dudubaya akawa mtaja majina wa Makonda.

Anyway, ndiyo nchi yetu ilivyoamua.
 
Tuliwahi andika humu kuwa huwezi kupambana na rushwa na ufisadi kama vyombo vya habari hasa vya uchunguzi,Bunge na Whistleblowers wamezibwa midomo...
Unataka kusema nini? Kipindi kile mnaoneshana madole ya kati BUNGENI ndio kipindi ambacho rushwa haikuwepo!
 
Kipimo cha nguvu ya mama kipo hapa na kwa PM! Akifanikiwa kuving'oa hivi visiki viwili, nitaamini kweli ana nguvu.
Chief Kwamba unaamini Madame President hajapewa same authority na katiba kama waliyogewa waliopita mpaka adeal na hao wawili?
 
Mambo yameanza kunoga. Deusdedith Kakoko wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ametiwa nguvuni na yuko chini ya TAKUKURU kwa mahojiano na uchunguzi. Sote tunajua kuwa Mwendazake alikuwa akimwamini na kumtetea sana Kakoko. Alikuwa akimsifu na kumpa 'sapoti' ya kutosha na kutisha. Rangi halisi ya Kakoko wa Bandari imeanza kuonekana. Rangi ya kutisha...ufisadi wa kutisha....
Kwenye hiyo list umemsahau na Hapy wa Iringa ambaye aliwaambia wazee wetu wastaafu waliolitumikia taifa kama viongozi kuwa watawavunja vunja.
 
Tuliwahi andika humu kuwa huwezi kupambana na rushwa na ufisadi kama vyombo vya habari hasa vya uchunguzi,Bunge na Whistleblowers wamezibwa midomo...
Una manung'uniko gani kwa Magufuli ikiwa ulitamani aje Rais dikteta mwenye uchungu na nchi yake?
 
Tuliwahi andika humu kuwa huwezi kupambana na rushwa na ufisadi kama vyombo vya habari hasa vya uchunguzi, Bunge na Whistleblowers hawako huru.

Watu, kwa ujinga na ushabiki, walikuwa wanaifananisha awamu ya Magu na ya Kikwete katika swala zima la rushwa na ufisadi bila kuzingatia ukweli kuwa, enzi za Kikwete, Bunge, Vyombo vya habari na Whistleblowers walikuwa na uhuru wa kuanika madudu ya serikali na watendaji wake.

Mashabiki wa Jiwe wataishia kwa aibu na fedheha sana kipindi hiki.
Kwako shida sio kutafuta njia ya kulimaliza tatizo, kwako muhimu ni kuwa updated na vyombo vya habari kuhusu taarifa za maendeleo ya tatizo, usiite wenzio wajinga bila kujijua vizuri wewe uko upande gani, unaweza kuwa uko two steps ahead ya ujinga wao.

Hao whistleblowers unaowasema walianika madudu wakati wa Kikwete, now niambie, ni viongozi wangapi wa CCM unaowajua sasa hivi wako magerezani wakitumikia vifungo vya rushwa na ufisadi?

CCM ni ile ile, ufisadi, rushwa, and everything viko pale pale, tofauti ni wapigaji tu na zama zao, hata huyu mnaemshangilia leo wataibuka wapigaji wake wakati ukifika, kuendelea kushangilia fulani ndani ya CCM amekutwa na hatia juu ya hayo kwangu sioni cha kushangaza, zaidi nawashangaa nyie mnaoshangaa hayo.

Huu ni wakati wa kuidai Katiba Mpya kwa nguvu zote, sio kuendelea kupoteza muda kushangilia wizi unaofanywa serikalini karibia kila awamu, hao mwishowe hulindana.
 
Back
Top Bottom