G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Kama wewe umewahi kupigiwa simu na mheshimiwa sana mkuu sana Rais Magufuli basi unaelewa jinsi ambavyo anaweza kufanya jambo lolote yeye kama yeye. Hawa hapa wamekiri kwa wenzetu kuwa walihamia CCM baada ya kupokea simu ya Rais Magufuli akiwashawishi kwa vyeo.
Hata kama hawana nia ya kuhama ila Rais akishakupigia simu akikutaka ufanye jambo fulani basi unakuwa huna namna. Ukweli pia baadaye utadhihiri kwani watarudi kwenye kambi zao zilizowalea.
1. David Kafulila
2. Julius Mtatiro
3. James Ole Milya
Hao wengine; Waitara alishawishiwa na Paul Makonda. Waliobaki wengine ni kazi ya Polepole. Likubwa wanaloaminishwa ni ubunge wa awamu mbili utakaokoma mwaka 2025. Hali hiyo imewafanya baadhi yao kuchukua mikopo mikubwa ya malipo ya muda mrefu wa zaidi ya robotatu bilioni kwani wana uhakika wa kudumu miaka 7 ijayo ndani ya Bunge "Bubu" la Tanzania.
Pamoja na hao pia kuna baadhi ya wabunge wa upinzani ambao wanasumbuliwa sana kama Ester Bulaya. Huyu angekuwa na roho nyepesi basi Chadema angekuwa ameiacha wa kwanza kabisa. Hali hiyo imemfanya kuaminiwa sana na wabunge wenzake wa Chadema.
Baada ya hili wimbi. Wapinzani imara wataonekana haijalishi amehamia au kukulia Chadema. Wale watarudi na ukweli huu ninaouweka hapa leo watakuja kuusema miaka kadhaa ijayo.
Tuombe uzima.
Hata kama hawana nia ya kuhama ila Rais akishakupigia simu akikutaka ufanye jambo fulani basi unakuwa huna namna. Ukweli pia baadaye utadhihiri kwani watarudi kwenye kambi zao zilizowalea.
1. David Kafulila
2. Julius Mtatiro
3. James Ole Milya
Hao wengine; Waitara alishawishiwa na Paul Makonda. Waliobaki wengine ni kazi ya Polepole. Likubwa wanaloaminishwa ni ubunge wa awamu mbili utakaokoma mwaka 2025. Hali hiyo imewafanya baadhi yao kuchukua mikopo mikubwa ya malipo ya muda mrefu wa zaidi ya robotatu bilioni kwani wana uhakika wa kudumu miaka 7 ijayo ndani ya Bunge "Bubu" la Tanzania.
Pamoja na hao pia kuna baadhi ya wabunge wa upinzani ambao wanasumbuliwa sana kama Ester Bulaya. Huyu angekuwa na roho nyepesi basi Chadema angekuwa ameiacha wa kwanza kabisa. Hali hiyo imemfanya kuaminiwa sana na wabunge wenzake wa Chadema.
Baada ya hili wimbi. Wapinzani imara wataonekana haijalishi amehamia au kukulia Chadema. Wale watarudi na ukweli huu ninaouweka hapa leo watakuja kuusema miaka kadhaa ijayo.
Tuombe uzima.