Ukweli usioujua kuhusu uchaguzi wa meya jijini Arusha

Wana JF najua ni wengi wanajiuliza maswali mengi juu ya uhalali wa uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha ambao umekuwa mjadala mpaka leo. Swali wengi wanalojiuliza je uchaguzi ulikuwa halali au si halali?
Nataka niweke wazi uchaguzi ule ulikuwa halali kabisa na taratibu zilifuatwa kabisa. Kabla ya uchaguzi kufanyika kulikuwa na utata wa mjumbe mmoja wa CCM Mary Chitanda kupiga kura kwa sababu yeye si mwakilishi wa mkoa wa Arusha. Yeye ni katibu wa CCM mkoa wa Arusha lakini kwa sasa yeye ni mbunge wa viti maalum mkoani Tanga. CCM ilikuwa na wajumbe 15 ie madiwani na huyo mwenye utata 1 jumla ni 16. CDM ilikuwa na wajumbe 14 pamoja na G. Lema mbunge.
Utata huu ulipelekea kuomba ufafanuzi, na ufafanuzi ulipatikana kuwa mjumbe yule yaani Mary Chitanda alikuwa halali kwa maandishi na siyo mdomo kwa vyama vyote, hiyo ilikuwa siku ya pili baada ya kuahirisha uchaguzi jana yake.
Hilo ndiyo jambo kuu lilikuwa likibishaniwa. Sasa endapo jambo hili lilipatiwa ufumbuzi kwa maandishi inakuwaje leo hii viongozi wa CDM waendeleze malumbano jukwaani?
Ni jambo lisilofichika kwa nini Mary Chitanda asiende kupiga kura Tanga badala yake Arusha. Hilo ndilo suala la msingi kabisa lakini majibu yake vile vile kisheria hakuna kipengele kinachomkataza kupiga kura kwani bado ni kiongozi wa wanaCCM Arusha, na kuzingatia sheria haimbani CCM wakaonelea basi ni vema wakaitumia loopwhole hiyo.
Tuachane na ubishi kama sheria haimkabi basi CDM hawana haja ya malumbano. Machoni pa watu itaonekana si halali lakini mbele ya sheria inaonekana sawa. Katika uchaguzi wa urais hakuna mahakama yenye uwezo wa kutengua mara baada ya matokeo kutangazwa na tume ya uchaguzi. Hapa tunajifunza mapungufu ya sheria zetu za bongo. Hili ni jambo lisilopingika kabisa na kwa hili linahitaji mabadiliko.
Uchaaguzi umekwisha na meya keshapatikana sasa kama sheria zilikikwa basi tukapate haki yetu mahakamani na siyo kwa mashinikizo ya jukwaani.
CDM ni chama makini lakini kimepotoka kwa hili kwa ndiyo maana yake hawataki kwenda mahakamani kwa sababu wanajua hawana jipya. Kinachofanyika saizi ni propaganga ya sintofahamu ya tukio hili kwa wananchi!
Ni kweli mara baada ya kupewa taarifa ya uhalali wa Mary Chitanda CDM walitoka nje kujadili wakawaacha wajumbe wengine 17 wakiwa ndani na kipindi hicho walishasaini tayari column ya mahudhurio! Ilipoonekana wamechelewa kurudi CCM hapo ndipo walipocheza rafu kwa kuendesha uchaguzi kwani tayari walikuwa na sababu zote za kushinda kesi. Sijui ni daftari au niiteje umesaini, kisha umetoka nje kujadili basi jamaa wakaendelea ndani na uchaguzi. CDM walishituka pindi matokeo yanatangazwa na kuja ukumbini wakiongozwa na mbunge wao Lema wakaambiwa nyie si MMESUSIA uchaguzi basi endeleeni ila viongozi wamepatikana.
Huo ndiyo ukweli wa uchaguzi wa meya Arusha.
Kwa kuwa ukweli huu umejificha kauli nyingi za kulaani zilitokea na kuzidi hasa baada ya maandamano kuzuiliwa na kupeleka vifo.
Kauli za kiburi toka kwa viongozi wa CCM akiwemo Makamba zikaamsha hisia kali. CCM ni kama walikuwa wanawakebehi CDM kwa sababu walijua hawana pa kushika mahakamani na ndiyo maana wanawashinikiza viongozi wa CDM waande huko ili haki ijulikane.
Usichokijua ni hiki, kwa nini wasiende mahakamani wafungue kesi kisha waitishe maandamano ili kushinikiza haki ya kusikilizwa kesi upesi. Kukataa kwao kwa kisingizio mahakama haitatenda haki kunatilisha mashaka na waelewe kuwa mashinikizo yao hayana direct impact badala yake yanawapa changamoto viongozi wa CCM.
Mwisho naalani kwa kauli moja kuwa nguvu iliyotumika kuzima maandamano yale ilikuwa kubwa mno na viongozi wetu wa serikali waache kutumika kisiasa. La Arusha latosha kuwa funzo.
Kikwete zlisema tukio la Arusha ndiyo mwanzo na mwisho naomba iwe kweli ingawaje nasikia Mbeya vijana wake wamekwisha ua tena!!!
MD usiichangane na thread yoyote ile, iweke ili watu wajue na ku challange pale wanapoona siyo sahihi.
We ni kilaza uliyetumwa na Makamba au Kikwete. Mbona hujatuambia ni wajumbe wangapi walioshiriki kupiga kura za kumchagua huyo meya wenu wa kubumba? Quorum ilikuwa ya wajumbe wangapi? na kwa nini wajumbe wa CHADEMA wanaokaribia nusu ya wajumbe wote hawakushirikishwa katika zoezi hilo? Hoja zako zinaashiria wewe hutumii mfumo wa akili za kawaida kufikiri, labda kipo kiungo kingine unachotumia; bila shaka tumbo kama ilivyo kwa mafisadi wenzako wengine! Tunataka uongee facts na si pumba zilizooza kama ulivyofanya. Shame be unto you and your CCM. Mungu ibariki Tanzania.
 
Ukweli usioujua kuhusu uchaguzi wa meya jijini Arusha

Mzee wa Rula, kutokana na kichwa cha habari hapo juu, mbona baadhi ya matukio hujayaeleza, nadhani ingekuwa busara ungeweka na kisa cha Bwana Lema na wengineo kupigwa na polisi kwani ilikuwa ni sehemu ya huo uchaguzi
 
Mzee wa Rula hapo umeweka rula inapotakiwa tena ni rula yenye pima maji.

kama madiwani wa CDM walisaini daftari/kitabu cha mahudhurio basi uchaguzi ulikuwa halali. Lakini nawasiwasi kuwa aliyeanzisha thread hii hasemi ukweli; yawezekana ametumwa na Makamba ili kukatisha tamaa wananchi ktk kudai haki yao. Kama kweli CDM walisaini mahudhurio basi ushahidi uwekwe hapa.
 
Huna hoja, nadhani unataka kuleta sanaa kwenye jumba la sanaa!!!

Umejichanganya tena? Ulitaka apeleke sanaa wapi kama si kwenye jumba la sanaa, maana ndo mahali pake ati!
Mzee wa Rula uwelewa wako umethibitisha ulichokiandika!
 
Afadhari kuongoza mbwa 100 kuliko mwana ccm 1 kwani viongozi wao 99m percent ni wabinafsi wasiojali watantania.
 
Sijatumika na sitatumika ila huo ndiyo ukweli ninaioufahamu. Kama huamini CDM hawawezi kwenda mahakamani mpaka kiama. Ukiona CDM hawaendi mahakamani jua mimi ni mkweli katika hili. Kwamba walitakiwa kukutana Olasiti Garden ni jambo la kushangaza, mimi nafahamu hawa jamaa walikuwa Equator Hotel iliyopo opposite na halmashauri.




Hapa mnatuchanganya, kuna mmoja kati yenu hakutakuwa kuwa among Great thinker kwa kuwa analeta information za uongo!
 
Hivi ni sheria gani ambayo inataka mahudhurio ya vikao vya halmashauri yawe 2/3?

Mtu anayejua kifungu cha sheria hiyo atujulishe ili kusaidia mjadala.
 
Wana JF najua ni wengi wanajiuliza maswali mengi juu ya uhalali wa uchaguzi wa meya wa jiji la Arusha ambao umekuwa mjadala mpaka leo. Swali wengi wanalojiuliza je uchaguzi ulikuwa halali au si halali?
Nataka niweke wazi uchaguzi ule ulikuwa halali kabisa na taratibu zilifuatwa kabisa. Kabla ya uchaguzi kufanyika kulikuwa na utata wa mjumbe mmoja wa CCM Mary Chitanda kupiga kura kwa sababu yeye si mwakilishi wa mkoa wa Arusha. Yeye ni katibu wa CCM mkoa wa Arusha lakini kwa sasa yeye ni mbunge wa viti maalum mkoani Tanga. CCM ilikuwa na wajumbe 15 ie madiwani na huyo mwenye utata 1 jumla ni 16. CDM ilikuwa na wajumbe 14 pamoja na G. Lema mbunge.
Utata huu ulipelekea kuomba ufafanuzi, na ufafanuzi ulipatikana kuwa mjumbe yule yaani Mary Chitanda alikuwa halali kwa maandishi na siyo mdomo kwa vyama vyote, hiyo ilikuwa siku ya pili baada ya kuahirisha uchaguzi jana yake.
Hilo ndiyo jambo kuu lilikuwa likibishaniwa. Sasa endapo jambo hili lilipatiwa ufumbuzi kwa maandishi inakuwaje leo hii viongozi wa CDM waendeleze malumbano jukwaani?
Ni jambo lisilofichika kwa nini Mary Chitanda asiende kupiga kura Tanga badala yake Arusha. Hilo ndilo suala la msingi kabisa lakini majibu yake vile vile kisheria hakuna kipengele kinachomkataza kupiga kura kwani bado ni kiongozi wa wanaCCM Arusha, na kuzingatia sheria haimbani CCM wakaonelea basi ni vema wakaitumia loopwhole hiyo.
Tuachane na ubishi kama sheria haimkabi basi CDM hawana haja ya malumbano. Machoni pa watu itaonekana si halali lakini mbele ya sheria inaonekana sawa. Katika uchaguzi wa urais hakuna mahakama yenye uwezo wa kutengua mara baada ya matokeo kutangazwa na tume ya uchaguzi. Hapa tunajifunza mapungufu ya sheria zetu za bongo. Hili ni jambo lisilopingika kabisa na kwa hili linahitaji mabadiliko.
Uchaaguzi umekwisha na meya keshapatikana sasa kama sheria zilikikwa basi tukapate haki yetu mahakamani na siyo kwa mashinikizo ya jukwaani.
CDM ni chama makini lakini kimepotoka kwa hili kwa ndiyo maana yake hawataki kwenda mahakamani kwa sababu wanajua hawana jipya. Kinachofanyika saizi ni propaganga ya sintofahamu ya tukio hili kwa wananchi!
Ni kweli mara baada ya kupewa taarifa ya uhalali wa Mary Chitanda CDM walitoka nje kujadili wakawaacha wajumbe wengine 17 wakiwa ndani na kipindi hicho walishasaini tayari column ya mahudhurio! Ilipoonekana wamechelewa kurudi CCM hapo ndipo walipocheza rafu kwa kuendesha uchaguzi kwani tayari walikuwa na sababu zote za kushinda kesi. Sijui ni daftari au niiteje umesaini, kisha umetoka nje kujadili basi jamaa wakaendelea ndani na uchaguzi. CDM walishituka pindi matokeo yanatangazwa na kuja ukumbini wakiongozwa na mbunge wao Lema wakaambiwa nyie si MMESUSIA uchaguzi basi endeleeni ila viongozi wamepatikana.
Huo ndiyo ukweli wa uchaguzi wa meya Arusha.
Kwa kuwa ukweli huu umejificha kauli nyingi za kulaani zilitokea na kuzidi hasa baada ya maandamano kuzuiliwa na kupeleka vifo.
Kauli za kiburi toka kwa viongozi wa CCM akiwemo Makamba zikaamsha hisia kali. CCM ni kama walikuwa wanawakebehi CDM kwa sababu walijua hawana pa kushika mahakamani na ndiyo maana wanawashinikiza viongozi wa CDM waande huko ili haki ijulikane.
Usichokijua ni hiki, kwa nini wasiende mahakamani wafungue kesi kisha waitishe maandamano ili kushinikiza haki ya kusikilizwa kesi upesi. Kukataa kwao kwa kisingizio mahakama haitatenda haki kunatilisha mashaka na waelewe kuwa mashinikizo yao hayana direct impact badala yake yanawapa changamoto viongozi wa CCM.
Mwisho naalani kwa kauli moja kuwa nguvu iliyotumika kuzima maandamano yale ilikuwa kubwa mno na viongozi wetu wa serikali waache kutumika kisiasa. La Arusha latosha kuwa funzo.
Kikwete zlisema tukio la Arusha ndiyo mwanzo na mwisho naomba iwe kweli ingawaje nasikia Mbeya vijana wake wamekwisha ua tena!!!
MD usiichangane na thread yoyote ile, iweke ili watu wajue na ku challange pale wanapoona siyo sahihi.

Mzee wa Rula, makala yako haina kituchochote kipya hayo unayosema ndiyo wananchni wanalalamikia hayohayo; Kupiga kura wakati wengine wanatafuta ufumbuzi wa kujua uhalali wa Huyo kitanda kupiga kura wakati si Mjumbe katika baraza la madiwani wa Arusha Mjini! kwanini wasisubiri warudi wao wakapiga kura alafu wanaporudi wewe unasema mwenyewe kuwa CCM ilikuwa inawakebi CDM Kukebei maana yake nini? (Elezea mwenyewe) Pia unasema utata uliperekea kuomba ufafanuzi sasa kwanini Msisubiri na wenzenu wapate ufafanuzi ili Uchaguzi ufanyike kihalali na kwa amani? Bwana Rula pia Makala yako aisema ufafanuzi uliombwa wapi na kwa nani na ufafanuzi upi ulitolewa husemi hilo! huoni kuwa hukuwa na haja ya kuharisha haraka kuwa Uchaguzi ulikuwa huru! we mwenyewe unasema Kulikuwa na Utata, Ufafanuzi Ukaombwa kwa barua, then CCM wakapiga kura wakati wenzao wanajadili huo utata nje Rula vipi hapo oanisha maneno yako kabla, maana utaonekana hauna Rula unatumia mkono kupiga mstari!

Nakushauri uangalie mkanganyiko huo wa maneno alafu utwambie huru na haki inatoka waka katika lindi la Utata kama huo na wakati utata unashughulikiwa walioleta utata wana piga kura harakaharaka; Tumia Rula yako Vizuri
 
Mzee Wa rula

Nimefurahi sana ulivyo panga maneno yako na kutuaminisha kuwa CDM ndio wenye matatizo katika uchaguzi huu wa meya lakini nimeshindwa kabisa kukuelewa kwanini unatumia akili nhyingi kupotosha uma ambao hauwezi kupotoka hata kidogo.......Mfano mdogo umesema CDM baada ya kuombwa ufafanuzi wa lijibiwa na kuona kama hawajaridhika wakatoka nje ya ukumbi kwenda kujadili hapo ndipo mkurugenzi akaendelea na uchaguzi akisema CDM wame susa

Swali lakujiuliza ninani alisema CDM wamesusa?

Unasema marry Chatanda ni mbunge wa kuteuliwa huko Tanga na nikatibu wa CCM Arusha na aliingia kwenye uchaguzi kama mjumbe halali wa CCM akitumia logic ya kuwa Mbunge wa kuteuliwa

Swali Sheria ya uchaguzi wa meya inasema mbunge wa kuteuliwa mahalipopote anahaki ya kuchagua meya wa mahali pengine?

Unasema CCM wali tumia fauro kidogo baada ya CDM kutoka nje ya ukumbi na wakachaguana kwa kudai CDM wamesusa

Swali hiyo fauro kidogo haina impact katika taratibu za uchaguzi? na kama inaimpact ninani atalaumiwa?

Umesema CCM walitumia maneno ya kejeri na kiburi na wa kasema wako sahihi juu ya uchaguzi ule na kuwataka CDM kwenda mahakamani kama wanaona taratibu hazijafuatwa.

Swali Unaonaje mtu ambaye amekukosea anakulazimisha uende mahakamani ...unadhani haki itapatikana hapo na kama itapatikana itapatikana baada ya mdaa gani?

Baada yakujiuliza mashali haya hebu hebu jiulize mwenyewe unamaana gani kupotosha umma ilihali unajua ukweli?
 
kama quorum haikutimia, sheria inasemaje?? kikao kuahirishwa we ***** tukueleze kama hujui, siyo kuendelea na kikao. Maana maazimio yake hayakubaliki kisheria kwa kuwa quorum haikutimia.
 
Katika katiba ya Tanzania au taratibu za NEC hakuna cheo kinachoitwa mbunge wa kuteuliwa/viti maalum wa mkoa fulani.

Ukitaka kulielewa vizuri suala hili inabidi uanzie hapo.

Chatanda sio mbunge wa kuteuliwa wa mkoa wa Tanga. Ni mbunge wa kuteuliwa wa CCM.

Kama kuna cheo cha mbunge wa kuteuliwa wa mkoa basi pia kutawa na wabunge wa viti maalum wa NGO, au wabunge wa viti maalum wa walemavu au wabunge wa viti maalum wa vyuo vikuu au wabunge wa kuteuliwa wa wafanyakazi nk. Maana hayo pia yalikuwa makundi ndani ya CCM.

Je kama kuna wabunge wa viti maalum wa mikoa, nani wanawakilisha mikoa hiyo kwa upande wa CHADEMA? Nani wanawakilisha mikoa mbalimbali kwa upande wa CUF.

Chatanda aliteuliwa na CCM kupitia kundi la mikoa kwa mkoa wa Tanga. Huo ndio ulikuwa mwisho wa mkoa wake. Majina yalipopelekwa NEC yalipelekwa kama wateule wa CCM. Uamuzi wa kuteua baadhi ya viti kwa kutumia kigezo cha mikoa ulikuwa ni wa CCM. Mbali ya mikoa pia kuna makundi mengine kama NGO, Wafanyakazi, viti maalum, vijana nk.

CHADEMA nao walikuwa na utaratibu wao ambao ulifuata uzoefu katika siasa pamoja na elimu zao.

Tukielielewa hilo, mabo mengine inakuwa rahisi kuyaelezea.
 
.....]CCM Mary Chitanda kupiga kura kwa sababu yeye si mwakilishi wa mkoa wa Arusha. [/B]Yeye ni katibu wa CCM mkoa wa Arusha lakini kwa sasa yeye ni mbunge wa viti maalum mkoani Tanga. ..


Mzee wa Rula nisaidie kwa hili Marry Chatanda Arusha si mwakilishi wa wananchi bali mwajiriwa wa CCM kama katibu. Tanga ni mwakilishi wa wananchi. Napenda kuamini kuwa Chatanda anaweza kupiga kura huko Tanga sababu yeye ni mwakilishi lakini kwa Arusha ainiingii akilini kabisa.

Sidhani kama maelezo ya kuwa anaishi Arusha ni kigezo cha kushiriki kama diwani kwenye council. Je tutasemaje kwa wabunge wengi wa kuteuliwa wanaoishi Dar na familia zao je ni halali wao pia kushiriki kama madiwani ktk halmashauri za Ilala, Kinondoni na au temeke?
 
Logic iliyotumika ni ubunge wa viti maalumu na ndiyo maana kuna mbunge wa viti maalumu mmoja wa CDM nae angepiga kura ambaye nae alizua mvutano kwa kuwa alikuwa hajaapa. Lakini hilo lilipatiwa ufumbuzi kuwa ni halali kupiga kura. Mbunge wa viti maalumu wa CCM ndiye Mary Chitanda ambaye ni mbunge wa Tanga lakini ni katibu mkuu wa CCM. Sasa CCM wakamleta huku Arusha ili aje apige kura kwa sababu sheria haimkatazi kufanya hivyo kwani bado ni kiongozi wa CCM mkoa hivyo alikuwa na haki. Hii ilitokana baada ya kuona hali ni tete Arusha.

It was the thechnical know how ambayo CCM walitumia kwa yule mbunge wa CDM kutoapishwa. Hivyo hii mada yako yote ni ya kipuuzi tu
 
Pamoja na maelezo yako yakishabiki polisi hawakuwa na sababu ya kuua maana walitembea umbali wa kilomita moja na waandamanaji bila tatizo walipoona wanakaribia kufika uwanjani polisi wa kutuliza ghasia wakaanzisha ghasia nchi hii si ya ccm wala nani wananchi wa leo hawako tayari kuburuzwa kwa vyovyote vile.
 
Dosari ya Msingi ni uhalali wa Mary Chatanda. Nimeangalia kwenye website ya CCM, wakati wanapitisha majina ya wagombea wa viti maalum.

Mary Chatanda aliteuliwa na CCM katika Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya pili) Mkoa wa Tanga.

Ni wazi basi uwakilishi wake ungepasika kuwa wa Watu wa Tanga na si Arusha.

Malumbano mengine yanakuja kutokana na wale wanaosimamia na kutoa miongozo ya Chaguzi hizo kuwa wateuliwa wa Watawala walioko madarakani, na hivyo kulinda maslahi ya kisiasa ya chama cha watawala hao.

Angalia: Website Rasmi ya Chama Cha Mapinduzi - CCM

WanaCCM Waliopendekezwa Kugombea Nafasi ya Viti Maalum Tanzania
(i) Viongozi Wakuu wa UWT
1.Ndg Sophia Mnyambi Simba (Mwenyekiti)
2.Ndg Amina Nassoro Makilagi (Katibu Mkuu)
(ii) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya kwanza)
Mara 3.Ndg. Gaudentia Mugosi Kabaka
Tanga 4.Ndg. Ummi Ally Mwalimu
Mtwara 5.Ndg. Agness Elias Hokororo
Manyara 6.Ndg. Martha Jachi Umbulla
Shinyanga 7.Ndg. Lucy Thomas Mayenga
Kusini Pemba 8.Ndg. Faida Mohamed Bakari
Dodoma 9.Ndg. Felista Alois Bura
Kaskazini Unguja 10. Ndg. Kidawa Hamid Saleh
Ruvuma 11. Ndg. Stella Martine Manyanya
Mwanza 12. Ndg. Maria Ibeshi Hewa
Mbeya 13. Ndg. Hilda Cynthia Ngoye
Kigoma 14. Ndg. Josephine Johnson Genzabuke
Simiyu 15. Ndg. Esther Lukago Midimu
Kaskazini pemba 16. Ndg. Maida Hamad Abdalla
Kusini Unguja 17. Ndg. Asha Mshimba Jecha
Dar es Salaam 18. Ndg. Zarina Shamte Madabida
Arusha 19. Ndg. Namalok Edward Sokoinei
Tabora 20. Ndg. Munde Tambwe Abdallah
Kagera 21. Ndg. Benardetha Kasabago Mushashu
Geita 22. Ndg. Vick P. Kamata
Njombe 23. Ndg. Pindi Hazara Chana
Lindi 24. Ndg. Fatuma Abdallah Mikidadi
Morogoro 25. Ndg. Getrude Rwakatare
Kilimanjaro 26. Ndg. Betty E. Machangu
Singida 27. Ndg. Diana Mkumbo Chilolo
Mjini Magharibi 28. Ndg. Fakharia Shomari Khamis
Pwani 29. Ndg. Zaynabu Matitu Vulu
Rukwa 30. Ndg. Abia Muhama Nyabakari
Katavi 31. Ndg. Pudenciana Kikwembe
Iringa 32. Ndg. Lediana Mafuru Mng'ong'o


(iii) Kundi la Vijana T/Bara (nafasi tatu) 33. Ndg. Sarah Msafiri Ally
34. Ndg. Catherine V. Magige
35. Ndg. Ester Amos Bulaya
36. Ndg. Neema Mgaya Hamid
(iv) Kundi la Vijana T/Zanzibar (nafasi 2) 37. Ndg. Tauhida Galos Cassian
38. Ndg. Asha Mohamed Omari
(v) Kundi la NGO's (nafasi 2)
39. Ndg. Rita Louis Mlaki
40. Ndg. Anna Margreth Abdallah
(vi) Kundi la Vyuo Vikuu (nafasi 2)
41. Dkt. Fenella E. Mukangara
42. Ndg. Terezya Lwoga Huvisa
(vii) Wanawake wenye Ulemavu (nafasi 2)
43. Ndg. Al-Shaymaa Kwegir
44.Ndg. Margreth Mkanga
(viii) Kundi la Wafanyakazi (nafasi 2)
45. Ndg. Angellah Jasmin Kairuki
46.Ndg. Zainab Rashid Kawawa

(ix) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya pili)
Kusini Pemba 47.Ndg. Mwanakhamis Kassim Said
Lindi 48.Ndg. Riziki Said Lulida
Ruvuma 49.Ndg. Devotha Mkuwa Likokola
Morogoro 50.Ndg. Christina Ishengoma
Dodoma 51.Ndg. Mariam Salum Mfaki
Tabora 52.Ndg. Margreth Simwanza Sitta
Pwani 53.Ndg. Subira Khamis Mgalu
Iringa 54.Ndg. Rita E. Kabati
Singida 55.Ndg. Martha Moses Mlata
Kaskazini Pemba 56.Dkt. Maua Abeid Daftari
Kagera 57.Ndg. Elizabeth Nkunda Batenga
Shinyanga 58.Ndg. Azza Hillal Hamad
Mbeya 59.Ndg. Mary Machuche Mwanjelwa
Geita 60.Ndg. Josephine T. Chengula
Kaskazini Unguja 61.Ndg. Bahati Ali Abeid
Kusini Unguja 62.Ndg. Kiumbwa Makame Mbaraka
Rukwa 63.Ndg. Roweete Faustine Kasikila
Mtwara 64.Ndg. Anastazia Wambura
Tanga 65.Ndg. Mary Pius Chatanda
Mara 66.Ndg. Rosemary Kasimbi Kiligini
Dar es Salaam 67.Ndg. Mariam Nassor Kisangi
Mwanza 68.Ndg. Kemilembe Julius Lwota
Mjini Magharibi 69.Ndg. Asha Abdalla Juma
Katavi 70.Ndg. Anna Richard Lupembe
Simiyu 71.Ndg. Tinner Andrew Chenge
Njombe 72.Ndg. Rosemary Staki Senyamule
Kilimanjaro 73.Ndg. Shally Josepha Raymond
Arusha 74.Ndg. Halima Mohamed Mamuya
Manyara 75.Ndg. Dora Heriel Mushi
Kigoma 76.Ndg. Amina Butoye Kanyogoto

(x) Kundi la Vijana – Tanzania Bara (nafasi 3) 77.Ndg. Happyness Elias Lungiko
78.Ndg. Kaslida Jeremia Mgeni
79.Ndg Mboni Mohamed Mhita
(xi) Kundi la Vijana – T/Zanzibar (nafasi 1) 80.Ndg. Rabia Abdallah Hamid
(xii) Kundi la Vyuo Vikuu 81.Ndg. Rukia S. Mselem
(xiii) Kundi la Walemavu 82.Ndg. Hidaya Mjaka Ali
(xiv) Kundi la Kapu – (nafasi 18) 83.Ndg. Janet Maurice Masaburi
84.Ndg. Sifa Amani Swai
85.Catherine Peter Nao
86.Ndg. Moshi Kondo Kinyogoli
87.Ndg. Janath Mussa Kayanda
88.Ndg. Zulfa Abdalla Said
89.Ndg. Asha Ramadhani Baraka
90.Ndg. Aziza Sleyum Ally
91.Ndg. Mwaka Abdurahamani Ramadhani
92.Ndg. Esther Kabadi Nyawazwa
93.Ndg. Fatuma Hassan Toufiq
94.Ndg. Mwantum Haji
95.Ndg. Florence E. Kyendesya
96.Ndg. Aisha Matembe
97. Ndg. Raya Talib Ali
98.Ndg. Rukia Masasi
99.Ndg. Nemburis Kimbele
100.Ndg. Fatuma Hamza Mohamed


(i) Kiongozi Mkuu wa UWT 1. Ndg. Asha Bakari Makame (Makamu Mwenyekiti)
(ii) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya kwanza)
Mjini Magharibi 2. Ndg. Amina Iddi Mabrouk
Kusini Pemba 3. Ndg. Shadya Moh'd Suleiman
Kusini Unguja 4. Ndg. Salma Mussa Bilali
Kaskazini Pemba 5. Ndg. Bihindi Hamadi Khamis
Kaskazini Unguja 6. Ndg. Panya Ali Abdalla
(iii) Kundi la Vijana nafasi mbili (2) 7. Ndg. Wanu Hafidh Ameir
8. Ndg. Viwe Khamis Abdallah
(iv) Kundi la Vyuo Vikuu (Nafasi ya kwanza) 9. Ndg. Mgeni Hassan Juma
(v) Kundi la Walemavu (Nafasi ya Kwanza) 10. Ndg. Raya Sleimani Hamadi
(vi) Kundi la nafasi mbili (2) kila Mkoa (nafasi ya pili)
Mjini Magharibi 11. Ndg. Mwanaidi Kassim Mussa
Kusini Pemba 12. Ndg. Zainab Omar Moh'd
Kaskazini Unguja 13. Ndg. Mwanajuma Kassim Mkame
Kusini Unguja 14. Ndg. Nashide Hijja Abdullah
Kaskazini Pemba 15. Ndg. Sharifa Humuod Rashid
(vii) Kundi la Vijana nafasi tatu (3) 16. Ndg. Asha Juma Khamis
17. Ndg. Riziki Khamis Pembe
18. Ndg. Nadra Gulam Rashid
(viii) Kundi la Vyuo Vikuu (Nafasi ya pili) 19. Ndg. Sabaha Salehe Ali
(ix) Kundi la Walemavu (Nafasi ya pili) 20. Ndg. Mwantatu Mbarak Khamis




Imetayarishwa...
23:45:18 14.08.2010
Source:
Website Rasmi ya Chama Cha Mapinduzi - CCM

Accessed 16 January 2011 11:23 am
 
Katika katiba ya Tanzania au taratibu za NEC hakuna cheo kinachoitwa mbunge wa kuteuliwa/viti maalum wa mkoa fulani.

Ukitaka kulielewa vizuri suala hili inabidi uanzie hapo.

Chatanda sio mbunge wa kuteuliwa wa mkoa wa Tanga. Ni mbunge wa kuteuliwa wa CCM.

Kama kuna cheo cha mbunge wa kuteuliwa wa mkoa basi pia kutawa na wabunge wa viti maalum wa NGO, au wabunge wa viti maalum wa walemavu au wabunge wa viti maalum wa vyuo vikuu au wabunge wa kuteuliwa wa wafanyakazi nk. Maana hayo pia yalikuwa makundi ndani ya CCM.

Je kama kuna wabunge wa viti maalum wa mikoa, nani wanawakilisha mikoa hiyo kwa upande wa CHADEMA? Nani wanawakilisha mikoa mbalimbali kwa upande wa CUF.

Chatanda aliteuliwa na CCM kupitia kundi la mikoa kwa mkoa wa Tanga. Huo ndio ulikuwa mwisho wa mkoa wake. Majina yalipopelekwa NEC yalipelekwa kama wateule wa CCM. Uamuzi wa kuteua baadhi ya viti kwa kutumia kigezo cha mikoa ulikuwa ni wa CCM. Mbali ya mikoa pia kuna makundi mengine kama NGO, Wafanyakazi, viti maalum, vijana nk.

CHADEMA nao walikuwa na utaratibu wao ambao ulifuata uzoefu katika siasa pamoja na elimu zao.

Tukielielewa hilo, mabo mengine inakuwa rahisi kuyaelezea.

Iwapo wabunge ni wawakilishi wa wananchi katika chombo cha kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa sheria hizo, haiingii akilini kuwa kuna mbunge anaenda tu bungeni bila kuwakilisha kundi fulani la watanzania kutokana na sehemu yao wanayotoka, jinsia yao, au kundi lao maalum.

unataka kutuambia kuwa Mary Chatanda hana uwakilishi wa kundi lolote, na anaweza kesho kuhamishiwa Pemba akawa kwenye baraza la madiwani Pemba? Hivi mabaraza ya madiwani ya hivi stability yake itakuwa wapi? haiingii akilini kabisaaaaaaaaaa.

Hapo ni kupindisha sheria kukidhi mahitaji ya watawala. Ni sehemu ya siasa chafu za CCM.

Katiba mpya iondoe loopholes kama hizi zinazotuvuruga.
 
Back
Top Bottom