Ukweli usemwe: Intelijensia ya CHADEMA is super and unique. Maamuzi magumu ni yale tu!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,174
25,446
Kitendo cha kuwabaini 'wasaliti' ndani ya vyama vya siasa ni kitendo kikubwa. Ni ukweli kuwa kikulacho ki nguoni mwako. Lakini,kujua kuwa kikulacho kiko sehemu gani ya nguo ni jambo la mfano. Kumjua unayekula,unayelala,unayekunywa na unayeishi naye kuwa si mwenzio si mchezo.

Kuanzia mwaka 2013,CHADEMA ilijitikisa na kujisafisha. Wengine huita kujivua gamba. Iliwabaini wasio waaminifu chamani mwao na kuwashughulikia kinidhamu. Waliokumbwa na mtikiso huo ni Zitto Kabwe,Prof. Kitila Mkumbo,Samson Mwigamba, Alberto Msando,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba,kutaja wachache.

Kufikia sasa,pamoja na propaganda na maneno yote ya wakati huo,wote hao ni wanachama wa CCM isipokuwa Zitto ambaye ni Kiongozi wa ACT Wazalendo. Wote sasa ni wapinzani wa waziwazi wa CHADEMA. Baada ya kubainika,sasa ni dhahiri.

Mara tu baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa,Patrobas Katambi naye 'akashtukiwa' kuwa hayupo kichama. Akawa anapewa taarifa na kushirikishwa kwa mipaka. Akawa 'anatengwa'. Leo,amejiunga na CCM.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Intelijensia ya CHADEMA is super and unique. Inaona mbali kwa darubini kali!
 
IMG_20171121_153720.jpg
 
Katambi tulishambaini kuwa ni "TOGWA" na alipewa uenyekiti wa BAVICHA taifa kimkakati na aliposhindwa kazi tuliyomtuma kwa siku za mwanzo tu tulimpiga teke tukawapa majukumu Sosopi na katibu mkuu wa BAVICHA taifa. Zitto alizungukwa na mamluki tukamuonya hakusikia ila ameshajifunza.Tutamrudisha kundini mwakani baada ya kusafisha wale wote waliokuwa wakimuhadaa!
 
Katambi tulishambaini kuwa ni "TOGWA" na alipewa uenyekiti wa BAVICHA taifa kimkakati na aliposhindwa kazi tuliyomtuma kwa siku za mwanzo tu tulimpiga teke tukawapa majukumu Sosopi na katibu mkuu wa BAVICHA taifa. Zitto alizungukwa na mamluki tukamuonya hakusikia ila ameshajifunza.Tutamrudisha kundini mwakani baada ya kusafisha wale wote waliokuwa wakimuhadaa!
huyo sosopi mtakuja kumkataa muda si mrefu.
 
Bado wengine nao wanajiandaa kumfuata shetani. Maji na Mafuta havichangamani.
 
Pamoja na kuwa yote uliyoyaongea ni kweli, lakini sidhani kama ni intellijensia ya Chama imefanya na kuona hayo.

Mkuu, ndege wafananao huruka pamoja. Baada ya wote hao kufukuzwa uanachama baada ya kubainika kuwa na Ukaribu na Z. Z. Kabwe, hakukua kuna namna nyingine zaidi ya kumfata yule waliyokua karibu yake na kuunda Chama chao.

Kwa bahati mbaya sana, walitegemea Chama chao kitanyanyuka kwa haraka mithili ya swala aliyeona simba.

Ndipo sasa wakaamua kugeukia upande mwingine ambayo ulionekana kuwa na angalau kwao.
 
Katambi tulishambaini kuwa ni "TOGWA" na alipewa uenyekiti wa BAVICHA taifa kimkakati na aliposhindwa kazi tuliyomtuma kwa siku za mwanzo tu tulimpiga teke tukawapa majukumu Sosopi na katibu mkuu wa BAVICHA taifa. Zitto alizungukwa na mamluki tukamuonya hakusikia ila ameshajifunza.Tutamrudisha kundini mwakani baada ya kusafisha wale wote waliokuwa wakimuhadaa!

Hapa G Sam nakuunga mkono mara elfu hilo la kumsamehe Zitto na kumrejesha cdm. Kwangu mimi Zitto ni mara mia ukimuweka Lowassa na Sumaye pamoja. Zitto ni mwana mpotevu ila sasa ameujua ukweli ni kumsamehe na kumpa nafasi ya kugombea urais kwani amejiandaa na ana damu ya upinzani. Kutenda kosa si kosa ...
 
Katambi tulishambaini kuwa ni "TOGWA" na alipewa uenyekiti wa BAVICHA taifa kimkakati na aliposhindwa kazi tuliyomtuma kwa siku za mwanzo tu tulimpiga teke tukawapa majukumu Sosopi na katibu mkuu wa BAVICHA taifa. Zitto alizungukwa na mamluki tukamuonya hakusikia ila ameshajifunza.Tutamrudisha kundini mwakani baada ya kusafisha wale wote waliokuwa wakimuhadaa!
Sosopi ndio anatakiwa kupewa kiti
 
Kitendo cha kuwabaini 'wasaliti' ndani ya vyama vya siasa ni kitendo kikubwa. Ni ukweli kuwa kikulacho ki nguoni mwako. Lakini,kujua kuwa kikulacho kiko sehemu gani ya nguo ni jambo la mfano. Kumjua unayekula,unayelala,unayekunywa na unayeishi naye kuwa si mwenzio si mchezo.

Kuanzia mwaka 2013,CHADEMA ilijitikisa na kujisafisha. Wengine huita kujivua gamba. Iliwabaini wasio waaminifu chamani mwao na kuwashughulikia kinidhamu. Waliokumbwa na mtikiso huo ni Zitto Kabwe,Prof. Kitila Mkumbo,Samson Mwigamba, Alberto Msando,Juliana Shonza na Mtela Mwampamba,kutaja wachache.

Kufikia sasa,pamoja na propaganda na maneno yote ya wakati huo,wote hao ni wanachama wa CCM isipokuwa Zitto ambaye ni Kiongozi wa ACT Wazalendo. Wote sasa ni wapinzani wa waziwazi wa CHADEMA. Baada ya kubainika,sasa ni dhahiri.

Mara tu baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa,Patrobas Katambi naye 'akashtukiwa' kuwa hayupo kichama. Akawa anapewa taarifa na kushirikishwa kwa mipaka. Akawa 'anatengwa'. Leo,amejiunga na CCM.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Intelijensia ya CHADEMA is super and unique. Inaona mbali kwa darubini kali!
Upuuzi mtupu!
Kuondoka kwake kumekuuma mkuu, haina ubishi!
 
88 Reactions
Reply
Back
Top Bottom