Ukweli unabaki kuwa mabadiliko yalitikisa sana mwaka 2020. Jamii ikachangamkia na kuchemka kwa sababu ya joto la mabadiliko. Kiasi kwamba mpaka CCM wakaamua kudandia train la mabadiliko mpaka tukampata raisi tuliyenaye.
Kwa uchambuzi yakinifu kabisa ni kwamba
1.Wanamabadiliko wengi walikuwa vijana ambao walijitokeza kumpigia kura Lowassa na tunategemea pia watakuwa na nguvu bado na watajitokeza kupiga tena kura. Na inavyoonekana bado hawajashawishika na raisi aliye madarakani kwa hiyo kura zao bado zitapigwa UKAWA.
2.Kipo kizazi kipya cha wapiga kura kitakacho ibukia 2020. Hiki ni kizazi cha dot. com yaani wapenda mitandao ambayo utawala uliopo unaomba malaika waizime. Na hawa pia wana damu ya upinzani dhidi ya sera za kijima na kijamaa na kwa asilimia kubwa hawajashawishika na siasa za chama tawala.
3. Wengi wa waliompigia kura raisi ni watu wazima na wazee ambao ndani ya mwaka mmoja tu wamechoka na wengine wamekata tamaa kwa staili ya utawala wake. Kwa hiyo katika hawa baadhi hasa hawatapiga kura na wengine watabadilika na kurudi upande wa pili.
4. Wapo wasio na vyama na wengine ni UKAWA ambao walimpigia kura kwa kujaribu tu wakiamini kwamba kwa kariba yake basi ataleta mabadiliko tofauti na utawala wa nyuma na wengine waliona yeye ni bora kuliko Lowassa waUKAWA. Baadhi yao sasa wameshamgeuka na wanaona walikosea mwaka 2015.
5. Wapo wale (ndani ya serikali na CCM) ambao utawala huu umeawaumiza, kuwadhalilisha na hata kusababisha vidonda katika maisha yao na hawa pia hawawezi kurudia maamuzi ya mwaka 2015.
6. Wapo wafanya biashara ambao kutokana na sera hizi za awamu hii biashara zao tena halali kabisa zimeathirika na wengine wamefikia hatua ya kufunga biashara. Hawa pia hawataweza kumpa tena kura.
Sasa unaweza kujiuliza CCM watapata wapi wapiga kura wapya ukitia maanani kwamba wapiga kura wao kwa asilimia kubwa ni watu wazima na wazee ambao inawezekana kufikia 2020 wakaona ni usumbufu kujipanga katika foleni ya kupiga kura?
Kama CCM mnaamini kura zenu zitaongezeka je, zitatoka katika kundi lipi? Wapiga kura wenu wapya ni akina nani?
Mnafikiri mnaweza kushinda kwa njia halali 2015?
UKAWA anzeni kupigania tume huru ya uchaguzi. Kura nyingi ni zenu 2020.
Kwa uchambuzi yakinifu kabisa ni kwamba
1.Wanamabadiliko wengi walikuwa vijana ambao walijitokeza kumpigia kura Lowassa na tunategemea pia watakuwa na nguvu bado na watajitokeza kupiga tena kura. Na inavyoonekana bado hawajashawishika na raisi aliye madarakani kwa hiyo kura zao bado zitapigwa UKAWA.
2.Kipo kizazi kipya cha wapiga kura kitakacho ibukia 2020. Hiki ni kizazi cha dot. com yaani wapenda mitandao ambayo utawala uliopo unaomba malaika waizime. Na hawa pia wana damu ya upinzani dhidi ya sera za kijima na kijamaa na kwa asilimia kubwa hawajashawishika na siasa za chama tawala.
3. Wengi wa waliompigia kura raisi ni watu wazima na wazee ambao ndani ya mwaka mmoja tu wamechoka na wengine wamekata tamaa kwa staili ya utawala wake. Kwa hiyo katika hawa baadhi hasa hawatapiga kura na wengine watabadilika na kurudi upande wa pili.
4. Wapo wasio na vyama na wengine ni UKAWA ambao walimpigia kura kwa kujaribu tu wakiamini kwamba kwa kariba yake basi ataleta mabadiliko tofauti na utawala wa nyuma na wengine waliona yeye ni bora kuliko Lowassa waUKAWA. Baadhi yao sasa wameshamgeuka na wanaona walikosea mwaka 2015.
5. Wapo wale (ndani ya serikali na CCM) ambao utawala huu umeawaumiza, kuwadhalilisha na hata kusababisha vidonda katika maisha yao na hawa pia hawawezi kurudia maamuzi ya mwaka 2015.
6. Wapo wafanya biashara ambao kutokana na sera hizi za awamu hii biashara zao tena halali kabisa zimeathirika na wengine wamefikia hatua ya kufunga biashara. Hawa pia hawataweza kumpa tena kura.
Sasa unaweza kujiuliza CCM watapata wapi wapiga kura wapya ukitia maanani kwamba wapiga kura wao kwa asilimia kubwa ni watu wazima na wazee ambao inawezekana kufikia 2020 wakaona ni usumbufu kujipanga katika foleni ya kupiga kura?
Kama CCM mnaamini kura zenu zitaongezeka je, zitatoka katika kundi lipi? Wapiga kura wenu wapya ni akina nani?
Mnafikiri mnaweza kushinda kwa njia halali 2015?
UKAWA anzeni kupigania tume huru ya uchaguzi. Kura nyingi ni zenu 2020.