Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,794
Nimechukua muda wa kutosha kusoma kitabu kinachotoboa siri za utapeli wa TB Joshua kinachoitwa "The TB Joshua I Know-Deception of the Age Unmasked" kilichoandikwa na Bi. Hephzibah Bisola Johnson ambaye alikuwa mtumishi wake wa karibu sana kwa muda wa miaka 14.
Infact Bisola alikuwa right-hand person wake aliyekwenda naye kila mahali. Pia nimesikiliza video clips 32 zinazomhusu TB Joshua; nimesoma articles mbalimbali zinazohusu sakata hili; nimesikiliza mahojiano mbalimbali ya watu waliotajwa kwenye kitabu cha Bi Bisola Johnson; nimefuatilia Tweets na page zao za social media; nimesoma maelezo ya watoto wa marehemu waliokufa au kupotea wakiwa ndani ya Sinagogi la TB Joshua bila ndugu kupata maelezo ya kueleweka; nimesikiliza maelezo ya watu maarufu wakiwemo wacheza mpira na wacheza filamu waliowahi kutekwa na uongo wa TB Joshua na kisha kujikuta wakimpa fedha nyingi bila sababu yoyote. Wacheza mpira waliotajwa ni pamoja na Nwankwo Kanu aliyewahi kuichezea timu ya Arsenal na Emmanuel Amunike aliyekuwa kocha wa Timu yetu ya Taifa Stars.
Nimefuatilia pia taarifa zinazohusu kesi zinazomkabili TB Joshua Afrika Kusini zilizofunguliwa na wazazi wa mabinti wadogo waliopelekwa kwake kwaajili ya kuombewa na kisha kufanya nao mapenzi; Nimefuatilia comments na maandiko ya watu wanaomtetea; Nikarudi pia kutazama clip za mahubiri na uponyaji katika Sinagogi lake; n.k, n.k. Ili kujumuisha naomba niseme yafuatayo:
1. Anaendelea kuamini kuwa TB Joshua ni Nabii wa kweli. Na kwamba anafanya miujiza ya kweli, basi ajue anafanya hivyo at his or her own risk! Kama ulienda kwake ukapona, basi ujue ni imani yako tu... siyo TB Joshua. Endelea kumuamini Mungu wako aliyekuponya.
2. Zile kauli za 'wametumwa wamchafue..' hapa hazina mashiko hivyo usikimbilie kijifunika na blanketi hilo.. Tulia. Omba hekima ya Mungu. Kumbuka Hypnosis (yaani kupumbazwa) is real.
2. Kama una maji yake, sticker, mafuta, au chochote chake, ni afadhali utupe tu. Inawezekana unaendelea kujiunganisha na roho usizozijua.
3. Nawashauri wakristu wenzangu tuache kupenda miujiza kupita kiasi hadi kufikia kupumbazwa nayo. Tutulie, na kumtafuta Mungu katika Roho na Kweli. Siyo katika watu, miti, mapango, wala mahekalu...
Kwa anaetaka kusoma kitabu hicho kinapatikana Amazon.
The level of detail in this book is scary. Na mwandishi amesema yuko tayari kupelekwa mahakamani na TB Joshua kama aliyoyasema ni ya uongo. Bi Johnson ameanza kwa kuwataka radhi watu wote na kusema maneno haya: "Please forgive me oo. We did these atrocities together with him oo. I was part of it oo." Ila sasa ametubu na anaamini Yesu Kristo ameshamsamehe. Hivyo anawiwa kuwasaidia watu wengine wasiendelee kupotea.
Pia unaweza kusikiliza mahojiano youtube.
Sent using Jamii Forums mobile app
Infact Bisola alikuwa right-hand person wake aliyekwenda naye kila mahali. Pia nimesikiliza video clips 32 zinazomhusu TB Joshua; nimesoma articles mbalimbali zinazohusu sakata hili; nimesikiliza mahojiano mbalimbali ya watu waliotajwa kwenye kitabu cha Bi Bisola Johnson; nimefuatilia Tweets na page zao za social media; nimesoma maelezo ya watoto wa marehemu waliokufa au kupotea wakiwa ndani ya Sinagogi la TB Joshua bila ndugu kupata maelezo ya kueleweka; nimesikiliza maelezo ya watu maarufu wakiwemo wacheza mpira na wacheza filamu waliowahi kutekwa na uongo wa TB Joshua na kisha kujikuta wakimpa fedha nyingi bila sababu yoyote. Wacheza mpira waliotajwa ni pamoja na Nwankwo Kanu aliyewahi kuichezea timu ya Arsenal na Emmanuel Amunike aliyekuwa kocha wa Timu yetu ya Taifa Stars.
Nimefuatilia pia taarifa zinazohusu kesi zinazomkabili TB Joshua Afrika Kusini zilizofunguliwa na wazazi wa mabinti wadogo waliopelekwa kwake kwaajili ya kuombewa na kisha kufanya nao mapenzi; Nimefuatilia comments na maandiko ya watu wanaomtetea; Nikarudi pia kutazama clip za mahubiri na uponyaji katika Sinagogi lake; n.k, n.k. Ili kujumuisha naomba niseme yafuatayo:
1. Anaendelea kuamini kuwa TB Joshua ni Nabii wa kweli. Na kwamba anafanya miujiza ya kweli, basi ajue anafanya hivyo at his or her own risk! Kama ulienda kwake ukapona, basi ujue ni imani yako tu... siyo TB Joshua. Endelea kumuamini Mungu wako aliyekuponya.
2. Zile kauli za 'wametumwa wamchafue..' hapa hazina mashiko hivyo usikimbilie kijifunika na blanketi hilo.. Tulia. Omba hekima ya Mungu. Kumbuka Hypnosis (yaani kupumbazwa) is real.
2. Kama una maji yake, sticker, mafuta, au chochote chake, ni afadhali utupe tu. Inawezekana unaendelea kujiunganisha na roho usizozijua.
3. Nawashauri wakristu wenzangu tuache kupenda miujiza kupita kiasi hadi kufikia kupumbazwa nayo. Tutulie, na kumtafuta Mungu katika Roho na Kweli. Siyo katika watu, miti, mapango, wala mahekalu...
Kwa anaetaka kusoma kitabu hicho kinapatikana Amazon.
The level of detail in this book is scary. Na mwandishi amesema yuko tayari kupelekwa mahakamani na TB Joshua kama aliyoyasema ni ya uongo. Bi Johnson ameanza kwa kuwataka radhi watu wote na kusema maneno haya: "Please forgive me oo. We did these atrocities together with him oo. I was part of it oo." Ila sasa ametubu na anaamini Yesu Kristo ameshamsamehe. Hivyo anawiwa kuwasaidia watu wengine wasiendelee kupotea.
Pia unaweza kusikiliza mahojiano youtube.
Sent using Jamii Forums mobile app