FAJES
JF-Expert Member
- Oct 29, 2017
- 715
- 627
Wanabodi heshima kwenu.
Naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye mada.
Kwanza kabisa niwashukuru sana wadau wote waliochangia kwenye uzi wangu huu uliopita, ukipenda unaweza kusoma hapa. Baada ya kusoma comments zote za wadau kwenye uzi huu na kufanya tafakuri ya kina, nimebaini na kujifunza mambo machache yafuatayo .
Kuna mstari mwembaba sana unaotofautisha kati ya utajiri wa mali na ubinafsi. Neno utajiri wa mali sina haja ya kulitolea ufafanuzi wake maana ni kitu kinachofahamika kwa walio wengi. Ila naomba niazime tafsiri ya neno 'Ubinafsi' kutoka kwenye mtandao wa wikipedia. Wanasema, Ubinafsi ni 'tabia ya kujipendea mno hata kutojali wengine na shida zao'. Unaweza kusoma mwenyewe kwa link hii (Ubinafsi). Comments za wadau zimedhihirisha pasi na shaka kwamba, ili uweze kutoboa kwenye haya maisha, yaani kwamba uweze kumiliki mali nyingi inabidi kwanza uwe mbinafsi. Maana yake ni kuwa ujijali zaidi wewe mwenyewe ikiwemo labda wazazi na mke/mme na watoto pekee bila kutazama shida za watu wengine wanaokuzunguka.
Kwa ufafanuzi zaidi ni kuwa, haijalishi jirani au ndugu yako ana shida kiasi gani, ila usijaribu kabisa kuendekeza shida za watu wengine maana utaishia kuwa maskini kwakuwa shida za watu hutazimaliza hapa duniani. Kama ni kusaidia labda usaidie kwa watu wachache sana na mara chache mno. Kiufupi usiendekeze kabisa shida za watu wengine kwenye maisha yako. Na awengine wakaenda mbali zaidi kwa kusema ikiwezekana kwenye masuala ya kiutafutaji usiishi karibu na ndugu zako. Uende ukaishi eneo lingine mbali ili kupunguza kabisa mazoea ya kuombana misaada.
Jambo hili limenisukuma kudhani ya kuwa hali hii ya kujipenda mwenyewe kwa sisi Wafuasi wa Ukristo huenda ikawa tofauti na imani hii maana kwenye Ukristo tunafundishwa kumpenda jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako. Najua wadau wengine wanaweza kusema mie ndio sifahamu tafsiri ya maandiko hayo ila katika hali ya kawaida maandiko hayo yanamanisha kumpenda jirani ama mtu mwingine aliye karibu yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Ikimaanisha kuwa ukimpenda jirani yako hutamuacha alale njaa na wala hutamuacha afariki kwa kukosa matibabu kwa kisingizio cha utafutaji wa mali na kujikusanyia mali nyingi hapa Duniani.
Kwa upande mwingiine, ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi waliofanikiwa kwenye utafutaji waliamua 'ubahili' na kujijali wao zaidi iwe sehemu ya maisha yao. Ukiwa mtoaji sana kwenye utafutaji utaishia kuwa mtu wa kawaida na huenda ikapelekea kufilisika na hao uliowasaidia wasikukumbuke utakapokuwa umeanguka chini.
Any way, naomba nisieleweke kuwa huenda hoja yangu imejikita kwenye masuala ya imani, ila kwa kuhitimisha ni kuwa, ili utoboe kwenye haya maisha kiufupi, inabidi uwe mbinafsi sana. Sasa kama ubinafsi ni hali inayoenda kinyume na imani zetu hilo ni jambo lingine ambalo linahitaji jicho la kitaalamu kiimani ila naomba kuishia hapo kwa sasa.
Naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye mada.
Kwanza kabisa niwashukuru sana wadau wote waliochangia kwenye uzi wangu huu uliopita, ukipenda unaweza kusoma hapa. Baada ya kusoma comments zote za wadau kwenye uzi huu na kufanya tafakuri ya kina, nimebaini na kujifunza mambo machache yafuatayo .
Kuna mstari mwembaba sana unaotofautisha kati ya utajiri wa mali na ubinafsi. Neno utajiri wa mali sina haja ya kulitolea ufafanuzi wake maana ni kitu kinachofahamika kwa walio wengi. Ila naomba niazime tafsiri ya neno 'Ubinafsi' kutoka kwenye mtandao wa wikipedia. Wanasema, Ubinafsi ni 'tabia ya kujipendea mno hata kutojali wengine na shida zao'. Unaweza kusoma mwenyewe kwa link hii (Ubinafsi). Comments za wadau zimedhihirisha pasi na shaka kwamba, ili uweze kutoboa kwenye haya maisha, yaani kwamba uweze kumiliki mali nyingi inabidi kwanza uwe mbinafsi. Maana yake ni kuwa ujijali zaidi wewe mwenyewe ikiwemo labda wazazi na mke/mme na watoto pekee bila kutazama shida za watu wengine wanaokuzunguka.
Kwa ufafanuzi zaidi ni kuwa, haijalishi jirani au ndugu yako ana shida kiasi gani, ila usijaribu kabisa kuendekeza shida za watu wengine maana utaishia kuwa maskini kwakuwa shida za watu hutazimaliza hapa duniani. Kama ni kusaidia labda usaidie kwa watu wachache sana na mara chache mno. Kiufupi usiendekeze kabisa shida za watu wengine kwenye maisha yako. Na awengine wakaenda mbali zaidi kwa kusema ikiwezekana kwenye masuala ya kiutafutaji usiishi karibu na ndugu zako. Uende ukaishi eneo lingine mbali ili kupunguza kabisa mazoea ya kuombana misaada.
Jambo hili limenisukuma kudhani ya kuwa hali hii ya kujipenda mwenyewe kwa sisi Wafuasi wa Ukristo huenda ikawa tofauti na imani hii maana kwenye Ukristo tunafundishwa kumpenda jirani yako kama unavyoipenda nafsi yako. Najua wadau wengine wanaweza kusema mie ndio sifahamu tafsiri ya maandiko hayo ila katika hali ya kawaida maandiko hayo yanamanisha kumpenda jirani ama mtu mwingine aliye karibu yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Ikimaanisha kuwa ukimpenda jirani yako hutamuacha alale njaa na wala hutamuacha afariki kwa kukosa matibabu kwa kisingizio cha utafutaji wa mali na kujikusanyia mali nyingi hapa Duniani.
Kwa upande mwingiine, ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi waliofanikiwa kwenye utafutaji waliamua 'ubahili' na kujijali wao zaidi iwe sehemu ya maisha yao. Ukiwa mtoaji sana kwenye utafutaji utaishia kuwa mtu wa kawaida na huenda ikapelekea kufilisika na hao uliowasaidia wasikukumbuke utakapokuwa umeanguka chini.
Any way, naomba nisieleweke kuwa huenda hoja yangu imejikita kwenye masuala ya imani, ila kwa kuhitimisha ni kuwa, ili utoboe kwenye haya maisha kiufupi, inabidi uwe mbinafsi sana. Sasa kama ubinafsi ni hali inayoenda kinyume na imani zetu hilo ni jambo lingine ambalo linahitaji jicho la kitaalamu kiimani ila naomba kuishia hapo kwa sasa.