KijanaHuru
JF-Expert Member
- Jan 7, 2017
- 1,822
- 2,290
habari ya leo, poleni na majukumu na pilikapilika za kutwa,
Nishaona baadhi ya maswali mbalimbali hapa jf watu tukiulizana juu ya taifa la Israel kwamba je ndio hao walipo hapo sasa Israel? Au sio hao?
Tumekuwa na majibu tofauti tofauti kabisa juu ya hili, pia katika baadhi ya hoja nishawahi kuahidi yakuwa nitajitahidi kuleta hapa maelezo kwa mujibu wa Biblia hawa watu wako wapi na ni akina nani waliopo sasa?
nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunipa nafasi hii na mimi leo naenda kueleza kwa kufuata Neno la Mungu(Biblia) natumia kitabu hiki sababu ndio nakielewa zaidi na nimekisoma zaidi huenda kuliko vitabu vingine.
Nikiulizwa kuwa Israeli ya sasa ndio Israeli Inayotajwa na Biblia basi ni kwaherufi Kubwa jibu ni HAPANA yaani BIG NO Israeli yasasa sio taifa lile ambalo tumekuwa tukilisoma katika vitabu vya dini japo ardhi ni yenyewe ila naomba uelewe yakuwa wakaaji wa ile ardhi ni wavamizi tu, wala sio ardhi yao ile.
Kuna baadhi ya watu watakuwa wanashanaa sana ninapoliongelea hili hiyo nikutokana na jinsi ambavyo wamekuwa wakikaririshwa Neno la Mungu pasipo kulielewa vyema.
japo sijisifu kuwa mimi nalielewa vyema ila nikutokana na waumini wengi tunapenda sana kumezeshwa na kutafuniwa kuliko kutafuna wenyewe.
Sasa naanza kuitetea hoja yangu kwa namna hii
Kwanza kabisa nilazima tuweze kuelewa jambo moja linaloitwa ESCHATOLOGY, eschatology hii ni elimu inayoelezea matukio ya siku za mwisho, kupitia matukio ya siku za mwisho ndio tutaweza kupata jibu zuri sana juu ya taifa la Israel, pia unaweza uka-google kwa kulielewa zaidi maana mimi nimetoa maelezo kwa ufupi tu ili uweze kujua naongelea nini(kwa wale wasiojua)
Kwa lugha nyingine tunasema ni kipindi cha kanisa hadi kufikia Millenium (utanielewa mbele nini naongelea)
Ili Uiweze kunipata vizuri naomba nikugusie mgawanyiko wa vipindi vya maisha ya mwanadamu kwa mfumo huu
1.The Age Of Innocence
-Hiki ni kipindi cha uumbaji hadi kipindi cha kuanguka kwa Mwanadamu(Anguko)
2.The Age Of Conscience
-Hiki ni kipindi cha mwanadamu Kutoka anguko hadi Gharika Kuu
3.The Age Of Goverment
-Hiki ni kipindi ambacho mwanadamu aliishi kutoka Gharika kuu hadi kipindi cha Lutu
4.The Patriarchal Age
-Hiki ni Kipindi cha Abrahamu Hadi kipindi cha Musa
5.The Age Of law
-Hiki Nikipindi cha Musa hadi Kipindi cha Yesu Kristo
6.The Age Of The Church
-Hiki Ni Kipindi kutoka Pentekoste Hadi unyakuo wa Kwanza (kunyakuliwa kwa Kanisa)
7.The Millennium Age
-Hiki ni kipindi Cha ufunuo hadi Kunyakuliwa kwa kanisa.
Tunapokuwa tunazungumzia Eschatology hayo mambo saba Juu n ya Muhimu mno kuyajua, kile kipengele cha sita ni ule unyakuo wa kwanza tunakuja unyakuo wa pili ambapo ndio ile tunasema The Second Coming of The Christ, kutoka hapo Mwanadamu Ataingia katika Kipindi cha The Millennium
Sasa katika kipindi hiki cha Millennium Ndio unakuja kukutana na taifa la Israel lenyewe halisia
1.The Restoration Of Israel
Kwanza Israel atarudishwa nyumbani kwake katika nchi yake ya ahadi na atarudishwa kuwa taifa tena
Mwanzo 12:1-3, Unaposoma hapo Mwanzo Unapata zile ahadi ambazo zinatolewa juu ya taifa hili sasa Angalia hapa
Kumbukumbu la Torati 4:30-31 " 30 Utakapokuwa katika dhiki kali na maneno yote haya yawe yamekupata mwishoni mwa siku hizo, basi utarudi kwa Yehova Mungu+ wako na kuisikiliza sauti yake.+ 31 Kwa maana Yehova Mungu wako ni Mungu mwenye rehema.+ Hatakutupa wala kukuharibu wala kulisahau agano+ la mababu zako ambalo aliwaapia."
kuikazia hoja hii unaweza kuanza tena kwa kusoma Kumb 4:1-6
Kuna watu wanaweza kujiuliza ama kudai kwamba haya maneno yalikuwa ni kwa wakati ule wala sio sasa naweza kukuongeza jambo hili lililofichika ambalo wengi wao hawataki mlijue wala si wachungaji wala maaskofu hawafundishwi huko vyuoni ila yapo katika vitabu tu nikwamba wao watafute kwa bidii yao tu, nikwamba kila kitabu kilikuwa kina kinaandikwa kwa lengo fulani na kwa watu fulani na kwajamii fulani kwa muda fulani(ukiweza kupata msaada kuyajua kwa kila msingi wa kitabu utapata Mengi sana yaliyofichika
Naendelea hapo hapo juu kueleza juu ya Israel kurudishwa nyumbani kwakwe katika taifa lake angalia tena hapa
2Sam 7:10 "10 Nami hakika nitachagua mahali+ kwa ajili ya watu wangu Israeli na kuwapanda,+nao hakika watakaa mahali walipo, nao hawatasumbuliwa tena; na wana wa ukosefu wa uadilifu hawatawatesa tena kama walivyofanya hapo mwanzoni,"
Amosi 9:11-15
Isaya 27:12-13
Unapoendelea kusoma maneno Amosi na Isaya hapo juubado utaona habari ama ahadi anazoahidiwa Israeli kipindi atakapokuwa anarudishwa nyumbani kwake
Sasa angalia na hapa hii ni ahadi ambayo anapewa kipindi atakapokuwa amefika Nyumbani kwake
Isaya 60:1-22 Ukisoma vizuri msitari wa pili hapo utagundua kwamba hiki ndio kipindi kile cha utawala wa muovu ambapo mataifa mengine yatapata hiyo shida lakini sio kwa Israel.
Yeremia 16:14-16 "14 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’+ asema Yehova, ‘wakati haitasemwa tena: “Kama anavyoishi Yehova aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri!.......”
Sasa endelea kusoma katika kitabu cha Ezekiel 20:34-44 ,
Warumi 11-11-27 Kuanzia hapa katika kitabu cha warumi maneno yaliyoandikwa hapa ni makubwa mno na rahisi sana kuyaelewa kiasi kwamba hata angesoma mtoto angeelewa tu. kmbuka habari zote hapa tunaangalia juu ya Israeli kuwepo utumwani na watakaporudishwa nyumbani kwao, Soma kwa msisitizo kuanzia msitari wa 17 hapo utaona vyema namna ambavyo neno linavyongea kwa wazi kabisa.
Yaani hapa katika Warumi unaona kabisa kuna mtu ambaye yupo katika unyonge na anaambiwa maneno ya faraja namna ambavyo atarudishwa tena katika miliki yake ama katika haki yake.
Endelea kusoma Tena Matendo 15:13-16
Hapo tumeangalia namna ambavyo Israel atarudishwa nyumbani kwake
2.Kutakaswa Kwa Israel(The Cleansing Of Israel)
Kwanza Kumbuka yakuwa sababu kubwa ya Israel kuwekwa utumwani nikwamba walilaaniwa kwa kumkataa Yesu Kwanini walimkataa?
Sababu kubwa mojawapo nikwamba kipindi hicho Warumi ndio walikuwa wakishikilia dola ya kipindi hicho, Yesu anapokuja wao walijua yakuwa atawaongoza kupindua utawala wa waroma, Lakini Yesu hakuja kwa Vita kama ambavyo wao walijua ndio maana wakamkataaa Yesu na walishazoea kuwa kila Nabii ambaye Mungu alikuwa akimuinua katikati yao basi alikuwa ni mpiganaji japo kwa Yesu haikuwa hivyo sasa Kwahiyo wakamkataa Yesu na Wakamsurubisha Sasa hii dhambi wataanza kusamehewa kwanza na baadaye watakuja kuondolewa laana ile ya kuwa watumwa kwa mataifa mengine
Ezekieli 36:24-28
Naomba niishie hapo tu Kwasasa Japo kamtiririko haka nikarefu mno point ilikuwa nikuonyesha kwamba katika kipindi cha mwisho Taifa la Israeli ndio linatarudishwa Nyumbani kwake.
kwa Maana Hiyo Israeli Halali Hadi sasa Hayupo Nyumbani Kwake Kabisaa, Aliyepo sasa wala siye Yeye
Yale mambo yakusema atakayembariki nami nitambariki na atakaye mlaani nami nitamlaani kwasasa hayana Nguvu maana yule sio Mhusika ila hii itakuja kuhusika mara baada ya Unyakuo wa Kwanza.
Nimefupisha sana pole kama sitaeleweka lakini kuna msingi upo ambao unaweza kukuongoza kwa kujisomea zaidi na zaidi ili kujipa maariofa na kuelewa zaidi
Maswali yanakaribishwa
Nishaona baadhi ya maswali mbalimbali hapa jf watu tukiulizana juu ya taifa la Israel kwamba je ndio hao walipo hapo sasa Israel? Au sio hao?
Tumekuwa na majibu tofauti tofauti kabisa juu ya hili, pia katika baadhi ya hoja nishawahi kuahidi yakuwa nitajitahidi kuleta hapa maelezo kwa mujibu wa Biblia hawa watu wako wapi na ni akina nani waliopo sasa?
nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunipa nafasi hii na mimi leo naenda kueleza kwa kufuata Neno la Mungu(Biblia) natumia kitabu hiki sababu ndio nakielewa zaidi na nimekisoma zaidi huenda kuliko vitabu vingine.
Nikiulizwa kuwa Israeli ya sasa ndio Israeli Inayotajwa na Biblia basi ni kwaherufi Kubwa jibu ni HAPANA yaani BIG NO Israeli yasasa sio taifa lile ambalo tumekuwa tukilisoma katika vitabu vya dini japo ardhi ni yenyewe ila naomba uelewe yakuwa wakaaji wa ile ardhi ni wavamizi tu, wala sio ardhi yao ile.
Kuna baadhi ya watu watakuwa wanashanaa sana ninapoliongelea hili hiyo nikutokana na jinsi ambavyo wamekuwa wakikaririshwa Neno la Mungu pasipo kulielewa vyema.
japo sijisifu kuwa mimi nalielewa vyema ila nikutokana na waumini wengi tunapenda sana kumezeshwa na kutafuniwa kuliko kutafuna wenyewe.
Sasa naanza kuitetea hoja yangu kwa namna hii
Kwanza kabisa nilazima tuweze kuelewa jambo moja linaloitwa ESCHATOLOGY, eschatology hii ni elimu inayoelezea matukio ya siku za mwisho, kupitia matukio ya siku za mwisho ndio tutaweza kupata jibu zuri sana juu ya taifa la Israel, pia unaweza uka-google kwa kulielewa zaidi maana mimi nimetoa maelezo kwa ufupi tu ili uweze kujua naongelea nini(kwa wale wasiojua)
Kwa lugha nyingine tunasema ni kipindi cha kanisa hadi kufikia Millenium (utanielewa mbele nini naongelea)
Ili Uiweze kunipata vizuri naomba nikugusie mgawanyiko wa vipindi vya maisha ya mwanadamu kwa mfumo huu
1.The Age Of Innocence
-Hiki ni kipindi cha uumbaji hadi kipindi cha kuanguka kwa Mwanadamu(Anguko)
2.The Age Of Conscience
-Hiki ni kipindi cha mwanadamu Kutoka anguko hadi Gharika Kuu
3.The Age Of Goverment
-Hiki ni kipindi ambacho mwanadamu aliishi kutoka Gharika kuu hadi kipindi cha Lutu
4.The Patriarchal Age
-Hiki ni Kipindi cha Abrahamu Hadi kipindi cha Musa
5.The Age Of law
-Hiki Nikipindi cha Musa hadi Kipindi cha Yesu Kristo
6.The Age Of The Church
-Hiki Ni Kipindi kutoka Pentekoste Hadi unyakuo wa Kwanza (kunyakuliwa kwa Kanisa)
7.The Millennium Age
-Hiki ni kipindi Cha ufunuo hadi Kunyakuliwa kwa kanisa.
Tunapokuwa tunazungumzia Eschatology hayo mambo saba Juu n ya Muhimu mno kuyajua, kile kipengele cha sita ni ule unyakuo wa kwanza tunakuja unyakuo wa pili ambapo ndio ile tunasema The Second Coming of The Christ, kutoka hapo Mwanadamu Ataingia katika Kipindi cha The Millennium
Sasa katika kipindi hiki cha Millennium Ndio unakuja kukutana na taifa la Israel lenyewe halisia
1.The Restoration Of Israel
Kwanza Israel atarudishwa nyumbani kwake katika nchi yake ya ahadi na atarudishwa kuwa taifa tena
Mwanzo 12:1-3, Unaposoma hapo Mwanzo Unapata zile ahadi ambazo zinatolewa juu ya taifa hili sasa Angalia hapa
Kumbukumbu la Torati 4:30-31 " 30 Utakapokuwa katika dhiki kali na maneno yote haya yawe yamekupata mwishoni mwa siku hizo, basi utarudi kwa Yehova Mungu+ wako na kuisikiliza sauti yake.+ 31 Kwa maana Yehova Mungu wako ni Mungu mwenye rehema.+ Hatakutupa wala kukuharibu wala kulisahau agano+ la mababu zako ambalo aliwaapia."
kuikazia hoja hii unaweza kuanza tena kwa kusoma Kumb 4:1-6
Kuna watu wanaweza kujiuliza ama kudai kwamba haya maneno yalikuwa ni kwa wakati ule wala sio sasa naweza kukuongeza jambo hili lililofichika ambalo wengi wao hawataki mlijue wala si wachungaji wala maaskofu hawafundishwi huko vyuoni ila yapo katika vitabu tu nikwamba wao watafute kwa bidii yao tu, nikwamba kila kitabu kilikuwa kina kinaandikwa kwa lengo fulani na kwa watu fulani na kwajamii fulani kwa muda fulani(ukiweza kupata msaada kuyajua kwa kila msingi wa kitabu utapata Mengi sana yaliyofichika
Naendelea hapo hapo juu kueleza juu ya Israel kurudishwa nyumbani kwakwe katika taifa lake angalia tena hapa
2Sam 7:10 "10 Nami hakika nitachagua mahali+ kwa ajili ya watu wangu Israeli na kuwapanda,+nao hakika watakaa mahali walipo, nao hawatasumbuliwa tena; na wana wa ukosefu wa uadilifu hawatawatesa tena kama walivyofanya hapo mwanzoni,"
Amosi 9:11-15
Isaya 27:12-13
Unapoendelea kusoma maneno Amosi na Isaya hapo juubado utaona habari ama ahadi anazoahidiwa Israeli kipindi atakapokuwa anarudishwa nyumbani kwake
Sasa angalia na hapa hii ni ahadi ambayo anapewa kipindi atakapokuwa amefika Nyumbani kwake
Isaya 60:1-22 Ukisoma vizuri msitari wa pili hapo utagundua kwamba hiki ndio kipindi kile cha utawala wa muovu ambapo mataifa mengine yatapata hiyo shida lakini sio kwa Israel.
Yeremia 16:14-16 "14 “‘Kwa hiyo, tazama! siku zinakuja,’+ asema Yehova, ‘wakati haitasemwa tena: “Kama anavyoishi Yehova aliyewaleta wana wa Israeli kutoka katika nchi ya Misri!.......”
Sasa endelea kusoma katika kitabu cha Ezekiel 20:34-44 ,
Warumi 11-11-27 Kuanzia hapa katika kitabu cha warumi maneno yaliyoandikwa hapa ni makubwa mno na rahisi sana kuyaelewa kiasi kwamba hata angesoma mtoto angeelewa tu. kmbuka habari zote hapa tunaangalia juu ya Israeli kuwepo utumwani na watakaporudishwa nyumbani kwao, Soma kwa msisitizo kuanzia msitari wa 17 hapo utaona vyema namna ambavyo neno linavyongea kwa wazi kabisa.
Yaani hapa katika Warumi unaona kabisa kuna mtu ambaye yupo katika unyonge na anaambiwa maneno ya faraja namna ambavyo atarudishwa tena katika miliki yake ama katika haki yake.
Endelea kusoma Tena Matendo 15:13-16
Hapo tumeangalia namna ambavyo Israel atarudishwa nyumbani kwake
2.Kutakaswa Kwa Israel(The Cleansing Of Israel)
Kwanza Kumbuka yakuwa sababu kubwa ya Israel kuwekwa utumwani nikwamba walilaaniwa kwa kumkataa Yesu Kwanini walimkataa?
Sababu kubwa mojawapo nikwamba kipindi hicho Warumi ndio walikuwa wakishikilia dola ya kipindi hicho, Yesu anapokuja wao walijua yakuwa atawaongoza kupindua utawala wa waroma, Lakini Yesu hakuja kwa Vita kama ambavyo wao walijua ndio maana wakamkataaa Yesu na walishazoea kuwa kila Nabii ambaye Mungu alikuwa akimuinua katikati yao basi alikuwa ni mpiganaji japo kwa Yesu haikuwa hivyo sasa Kwahiyo wakamkataa Yesu na Wakamsurubisha Sasa hii dhambi wataanza kusamehewa kwanza na baadaye watakuja kuondolewa laana ile ya kuwa watumwa kwa mataifa mengine
Ezekieli 36:24-28
Naomba niishie hapo tu Kwasasa Japo kamtiririko haka nikarefu mno point ilikuwa nikuonyesha kwamba katika kipindi cha mwisho Taifa la Israeli ndio linatarudishwa Nyumbani kwake.
kwa Maana Hiyo Israeli Halali Hadi sasa Hayupo Nyumbani Kwake Kabisaa, Aliyepo sasa wala siye Yeye
Yale mambo yakusema atakayembariki nami nitambariki na atakaye mlaani nami nitamlaani kwasasa hayana Nguvu maana yule sio Mhusika ila hii itakuja kuhusika mara baada ya Unyakuo wa Kwanza.
Nimefupisha sana pole kama sitaeleweka lakini kuna msingi upo ambao unaweza kukuongoza kwa kujisomea zaidi na zaidi ili kujipa maariofa na kuelewa zaidi
Maswali yanakaribishwa