Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,557
- 217,844
Unapohamia ccm leo ufahamu kwamba unaunga mkono juhudi zote za kuficha taarifa za Shambulizi la mauaji ya Tundu Lissu , yaani unaunga mkono Lissu kunyimwa matibabu ili afe kwa kukosa huduma baada ya kushambuliwa , Ni kweli kwamba kila mmoja anayo haki ya kuhamia chama akipendacho , bali ni lazima tukumbuke kwamba ukipenda jongoo basi usisahau kuupenda na mti wake , ni lazima ukubali utaratibu mpya wa kutoruhusiwa kusalimia mgonjwa wa upinzani , ni lazima ukubali kwamba wapinzani ndio maadui wa nchi hii na hawaruhusiwi kufanya siasa za majukwaa , na wakithubutu watandikwe mabomu au risasi za moto
Kwahiyo basi wote wanaohamia ccm leo wamekubali kufichwa kwa CCTV CAMERA ya majengo ya waheshimiwa kule Dodoma ili kuficha taarifa , wamekubali Alphonce Mawazo asizikwe kwa vile Geita kuna kipindupindu , wamekubali kwamba upinzani ni uhaini , na ni lazima wakubali pia kwamba Mbowe na genge lake ndio walimuua Akwilina , ni lazima pia wakubali kwamba unyama wote wanaotendewa wapinzani ni halali yao maana wanatumwa na mabeberu .
Hivyo basi ndugu wananchi mnapaswa sasa kuwatambua wahusika kutokana na matendo yao ya sasa , na si yale yaliyopita maana wakati tunaoishi ni huu na ujao , hatutaishi tena jana wala juzi.
Mungu ibariki Tanzania
Kwahiyo basi wote wanaohamia ccm leo wamekubali kufichwa kwa CCTV CAMERA ya majengo ya waheshimiwa kule Dodoma ili kuficha taarifa , wamekubali Alphonce Mawazo asizikwe kwa vile Geita kuna kipindupindu , wamekubali kwamba upinzani ni uhaini , na ni lazima wakubali pia kwamba Mbowe na genge lake ndio walimuua Akwilina , ni lazima pia wakubali kwamba unyama wote wanaotendewa wapinzani ni halali yao maana wanatumwa na mabeberu .
Hivyo basi ndugu wananchi mnapaswa sasa kuwatambua wahusika kutokana na matendo yao ya sasa , na si yale yaliyopita maana wakati tunaoishi ni huu na ujao , hatutaishi tena jana wala juzi.
Mungu ibariki Tanzania