Uchaguzi 2020 Ukweli ni kwamba Uchaguzi 2020 ni wa upande mmoja, hakuna ushindani, tunakwenda kutimiza matakwa ya Katiba tu

Dam55

JF-Expert Member
Oct 8, 2015
5,592
11,831
Kwa kifupi kabisa ni kwamba tunakwenda kwenye Uchaguzi ambao mshindi tayari anajulikana. Ninasema haya kwasababu zifuatazo.

1. Kukubalika kwa Rais Magufuli kwa watanzania walio wengi (hili liko wazi na halina ubishi) Watanzania wanampenda sana huyu mtu na hawapo tayari aondoke Ikulu mapema.

2. Upinzani haujajiandaa kushika dola (hawako serious na uchaguzi) hawana hoja zenye mashiko hoja pekee iliyo baki ni Udikteta, wanafanya siasa kutegemea matutio ya ccm (kwakifupi wanayumbishwa na siasa za ccm) mfono mzuri ni jinsi wanavyojikita kwenye mgogoro wa Membe na ccm wenzake.

3. Siasa za uongo za upinzani na kutafuta huruma kwa wananchi kitu ambacho hakina msaada kwao mfano mzuri ni tukio la hivi karibuni la kusingizia serikali kumshambulia MH Mbowe, wakifanya makosa na kukamatwa kwa mujibu wa sheria basi hudai wameonewa au kutekwa ilhali wamakamatwa kwa mujibu wa sheria.

4. Hawana mgombea sahihi mwenye ushawishi mkubwa na anayekubalika na watanzania ambaye anaweza kumtikisa Magufuli, mfano mzuri ni Chadema walio tia nia wote si watu serious wa kwenda kupambana na Magufuli kuanzia Peter Msigwa hadi Tundu Lissu kwa akili tu yakawaida hawa watu niwachanga mno kwa Rais Magufuli.

5. Migogoro ndani ya vyama pinzani ambayo inawagawa wao wenyewe mfano mzuri ni wimbi kubwa la wabunge, madiwani na wanachama wengine wanaohama kutoka Chadema na CUF kwenda vyama vingine, mbaya zaidi badala ya vyama hivi kukaa kutathimini siasa za ndani za vyama vyao ili kufanya marekebisho badala yake wanakuja na tuhuma kuwa wanachama wao wananunuliwa.

Mwisho niseme tu kwamba mwaka huu tunakwenda tu kukamilisha matakwa ya kikatiba kumpa Rais Magufuli nafasi ya kutawala miaka mingine 5 lakini hatuwezi kusema kuwa ni uchaguzi wa ushindani, huu ndio ukweli hata kama utapingwa kwasababu ukweli mara nyingi huwa unaumiza.

Tujipange kwa uchaguzi wa 2025 panapo majaliwa ila kwa huu wa 2020 ccm wamesha shinda tayari wakuu, ila kwasababu siasa ni ajila, kipaji na ni sehemu ya maisha basi natuendelee tu kupiga porojo na kujifurahisha.
 
Magufuli hana sifa za kushinda kwa kushindana kwenye box la kura. Fuatilia hata alipokuwa mbunge alikuwa anashinda vipi. Alichofanya sasa hivi ni kuzuia vyama vya upinzani kutokufanya siasa, kisha ikatumika propaganda kuwa anakubalika sana. Wakati huo huo amebana vyombo vya habari vimtangaze. na kumpamba yeye tu.

Kwenye box la kura ya tumeona hujuma, uhayani na ukatili wa wazi ili CCM watangazwe washindi. Na yote hayo ni kwa maagizo yake. Hizo ni tabia za midictator wote, kubana watu, na kulazimisha vyombo vya habari kueneza propaganda kuwa wanakubalika sana.
 
Magufuli hana sifa za kushinda kwa kushindana kwenye box la kura. Fuatilia hata alipokuwa mbunge alikuwa anashinda vipi. Alichofanya sasa hivi ni kuzuia vyama vya upinzani kutokufanya siasa, kisha ikatumika propaganda kuwa anakubalika sana. Wakati huo huo amebana vyombo vya habari vimtangaze. na kumpamba yeye tu.

Kwenye box la kura ya tumeona hujuma, uhayani na ukatili wa wazi ili ccm watangazwe washindi. Na yote hayo ni kwa maagizo yake. Hizo ni tabia za midictator wote, kubana watu, na kulazimisha vyombo vya habari kueneza propaganda kuwa wanakubalika sana.
Imani hii ndio itawapoteza wapinzani kama hawatashtuka mapema.
 
Imani hii ndio itawapoteza wapinzani kama hawatashtuka mapema.

Narudia tena, madictator wote hujenga mazingira ya kuogopwa, kwa kutumia makundi ya watu wasiojulikana kwa backup ya vyombo vya dola. Huzuia vyama au taasisi zozote zinazowakosoa, kisha kupitia mwanya huo hulazimisha kuonyesha wanapendwa sana ili kuhadaa umma. Lakini linapokuja suala la uchaguzi ambapo wananchi watadhibitisha kupendwa kwao, hufanya hujuma, ukatili na uhayawani wa wazi ili kutangazwa washindi.

Mambo yote yanayofanyika hivi sasa yapo wazi kwa kila mtu kuyaona. Wote tunaona kundi la watu wasiojulikana likiteka watu bila hatua zozote. Tunaona vyama vya upinzani na vyombo vya habari vikizuiwa kufanya kazi zake. Huku kiongozi akishurutisha kukubalika na kutangazwa ili kuhadaa umma kama anakubalika sana. Uzuri ni kuwa wananchi walishaamka kwenye hizo hadaa za kijinga, na wanajua kila kitu vizuri.
 
Punguza hasira kabla huja comment.
Mkuu kama anakubalika kihivyo kwa Watanzania walio wengi na hata pia ndani ya chama chake, mbona inatumika kila njia kumzuia mtia nia mwingine kuja kushindanishwa naye kwa kificho cha kuzidi kuishi kwa mazoea ya kiutamaduni?

Hili ni takwa la kikatiba na pia uhitaji wa wakati wa sasa wa kutaka kupanua uwanja wa demokrasia ndani ya chama hiki kinachojinasibu kwa ukongwe barani Afrika. Mbona ANC kutokana na ukongwe wao wanaruhusu jambo hili kufanyika bila hiyana? Tumeshuhudia Rais Ramaphosa akishindanishwa na mtia nia na akaibuka kidedea.

Viongozi wetu wasiogope, waanze kuiga haya mambo mazuri kwa wakongwe wenzao barani Afrika na kwingine ulimwenguni ktk vyama rafiki.
 
Dam55,

Hata mimi kwa kuangalia chaguzi zilizopita na mizengwe ya kunyang'anya ushindi wazi wazi hata pale wapinzani waliposhinda,naamini hakuna ushindi kwa upinzani.Sasa ikiwa ni hivyo nchi maskini kama hii kwanini tunakwenda kupoteza fedha nyingi sana na wakati kwa madhumuni ya kutimiza matakwa ya katiba tu.

Kwani nani tunayemuogopa hata tupoteze uchumi ambao tangu hapo uko taabani. Si tuwaambie tu mwaka huu hatuna uchaguzi. Viongozi waliopo wataendelea mpaka mwaka 2025 isipokuwa Mungu akiwachukua.
 
Dam55,

Hata mimi kwa kuangalia chaguzi zilizopita na mizengwe ya kunyang'anya ushindi wazi wazi hata pale wapinzani waliposhinda,naamini hakuna ushindi kwa upinzani.Sasa ikiwa ni hivyo nchi maskini kama hii kwanini tunakwenda kupoteza fedha nyingi sana na wakati kwa madhumuni ya kutimiza matakwa ya katiba tu.

Kwani nani tunayemuogopa hata tupoteze uchumi ambao tangu hapo uko taabani. Si tuwaambie tu mwaka huu hatuna uchaguzi. Viongozi waliopo wataendelea mpaka mwaka 2025 isipokuwa Mungu akiwachukua.
Mizengwe gan hiyo
 
Mkuu kama anakubalika kihivyo kwa Watanzania walio wengi na hata pia ndani ya chama chake, mbona inatumika kila njia kumzuia mtia nia mwingine kuja kushindanishwa naye kwa kificho cha kuzidi kuishi kwa mazoea ya kiutamaduni?

Hili ni takwa la kikatiba na pia uhitaji wa wakati wa sasa wa kutaka kupanua uwanja wa demokrasia ndani ya chama hiki kinachojinasibu kwa ukongwe barani Afrika. Mbona ANC kutokana na ukongwe wao wanaruhusu jambo hili kufanyika bila hiyana? Tumeshuhudia Rais Ramaphosa akishindanishwa na mtia nia na akaibuka kidedea.

Viongozi wetu wasiogope, waanze kuiga haya mambo mazuri kwa wakongwe wenzao barani Afrika na kwingine ulimwenguni ktk vyama rafiki.
Wewe kwanini hutaki wao waendelee kuishi kwa taratibu na utamaduni wao kama chama?
Mbona Uchaguzi wa Zanzibar ushindani upo?
 
Back
Top Bottom