Ukweli ni kwamba pamoja na nia nzuri ya Rais Magufuli, sasa hivi Tanzania ni kama uwanja wa fujo

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nadhani wengi tulimuunga mkono Raisi Magufuli juu ya nia nzuri ya kurekebisha hali ya nchi yetu, katika masuala ya uongozi, uchumi na uwajibikaji. Lakini inafikia mahali tujiulize kama kweli hili ndilo linalofanyika. Inabidi uwe shabiki mbaya wa kisiasa au kipofu wa kifikra kutoona kwamba nchi yetu sasa imekuwa kama uwanja wa fujo karibu kila nyanja;
  • Bungeni - vurugu, mipambano, kukomoana, kunyanyasana na ukamataji wa wabunge kwa sababu zisizo za msingi, ubabe na vitisho kwa wabunge ukosefu wa nguvu za hoja na utumiaji wa nguvu za wingi (partisanship)
  • Siasa - ukosefu wa kuvumiliana na kuheshimiana, malumbano kwenye vyombo vya habari, kujibizana kwa press release, uadui unaokua kati ya vyama vya siasa, lugha za kukebehi na kukosa staha ya kiuongozi, utekaji, majaribio ya mauaji, udhibiti wa uhuru wa kuhutubia, vyama vya upinzani kuonekana wazi vikiandamwa na serikali na polisi
  • Uhuru wa vyombo habari - ufungiaji na vitisho kwa magazeti na mitandao ya kijamii, ukamataji wa kiholela wa kauli zinazoonekana kuikosoa serikali
  • Nidhamu ya kazi - nidhamu ya woga kujitokeza kwa kiasi kikubwa kwa hofu ya kutumbuliwa
  • Uwekezaji wa nje - migongano na wawekezaji (confrontation), kutofanya mambo kwa utaratibu wa kisheria
  • Utawala wa mikoani na wilayani - ubabe kama kuwekana ndani masaa 48, migongano kati ya wanasiasa na watendaji, hujuma na ufitini ili kujinufaisha kibinafsi
  • Mipaka ya kimadaraka - muingiliano ya madaraka kati ya watendaji, chama na serikali, kutia ndani uingizaji wa siasa katika vyombo vya kijeshi taasisi za kiserikali
  • Utawala wa kisheria - ukiukwaji wa makusudi wa katiba ya nchi, ukiukwaji wa kimakusudi wa maamuzi ya mahakama, uhasama kati ya wananchi na polisi na usalama wa taifa, ubabe wa vyombo vya usalama
  • Hali ya maisha - ugumu wa maisha kwa mwananchi wa kawaida, ukosefu wa ajira, uchungu na athari za maamuzi ya serikali kama bomoa bomoa, uhalifu wenye kuongezeka, hofu na kukosa furaha, mzigo wa faini za barabarani kwa makosa madogomadogo
Kwa namna fulani, naanza kuona kuwa gharama ya "kuinyosha" Tanzania inakuwa kubwa sana, ikiwa na namna fulani ya tishio la kuifanya nchi yetu iingie katika hali isiyoeleweka na kuwa uwanja wa fujo.

Sipendekezi kwamba Raisi Magufuli aache nia yake njema ya kuinyoosha Tanzania, bali swali ambalo ningependa sana raisi Magufuli ajiulize ni kwamba, je njia anazotumia "kuinyoosha" nchi amezitafakari sana kuona faida zake na hasara za muda mrefu? Je ni bora kuwa na nchi iliyonyooka "at any cost, regardless of the socio and psychological consequences"?

Je, sasa si wakati muafaka wa kutafakari namna iliyo bora zaidi ya kuinyoosha nchi kuliko njia zinazotumika kwa sasa? Kuna faida gani kuinyoosha nchi kwa ajili ya wananchi ambao kila siku wanazidi kupandwa na hasira na nmana inayotumika kuinyoosha nchi - kwamba wao wanapaswa kuwa collateral damage?

Updates:
Kuanzia sasa nitaweka kutoka magazetini habari zinazoonyesha ni jinsi gani nchi yetu Tanzania inakuwa uwanja wa fujo siku hadi siku;

  1. Mbunge Lijuakali ashikiliwa na Polisi - kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Malinyi Majura Kasika, kosa likiwa ni kuhudhuria kikao cha ndani cha Chadema nje ya jimbo lake (Mwananchi 28/09/2017)
  2. Wadau wa habari nchini wainyooshea kidole serikali - wakielezea kwamba asasi na vyombo vya habari vinaogopa kutoa taarifa zinazoikosoa Serikali kwa kuhofia usalama na vitisho vinavyotoka kwenye mamlaka (Mwananchi 29/09/2017)
  3. Msukuma ajiandaa kumlipua Kamanda - Mgogoro wa watendaji wakuu wa mkoa ambapo Mwenyekiti wa CCM Geita anatangaza kuanika uhalifu wa Kamanda wa Polisi wa Geita kwa kulipiza kisasi kitendo cha kamanda huyo kumkamata kama mhalifu kwa kumkunja suruali kiunoni (Nipashe 29/09/2017)
 
Nyumba haijatulia
Iliwahi kuwa haijatulia huko nyuma, mfano kipindi cha kufunga mikanda kwa miezi 18 baada ya vita vya Kagera. Nchi hii ilivumilia hali ambayo si rahisi watu kuvumilia. Sasa tofauti ya wakati huo na sasa, ni kwamba Nyerere, kwa hekima yake ya uongozi, alihakikisha wananchi wote wako nyuma yake.

Mie nadhani ingekuwa ni busara sana kwa Raisi Magufuli, kama alivyofanya Nyerere wakati huo, kuhakikisha kwamba katika kipindi cha mpito kuelekea kuinyoosha nchi, wanananchi wote wako nyuma yake, kutia ndani vyama vya upinzani. Ni mpango mbaya kuwagawanya wananchi kiitikadi wakati uko kwenye kampeni kubwa ya kuinyoosha nchi.

Hakuna kipindi ambacho Magufuli alipaswa awe karibu sana na wananchi na vyama vya upinzani kama hiki cha kuinyoosha nchi. Hii ni philosophy ndogo sana ya uongozi ambayo nadhani Raisi Magufuli haitambui - creating a common enemy in order to have the support of the masses.

Hupaswi kutengeneza "maadui" au migawanyiko wakati unataka kukabiliana na "common enemy". Common enemy hapa ni ufisadi, kutowajibika, kuibiwa na wawekezaji nk. Sasa haya ndio mambo ambayo Magufuli alipaswa kuya preach na kutaka support ya vyama vya upinzani na wananchi kwa ujumla - na ungekuta hata kina Tundu Lissu wanamkubali na kumsifia, kwa sababu ana-address mambo ambayo ni "common enemy".

Na Raisi Magufuli anasahau strategy muhimu sana katika kujenga nchi - "Rome was not built in one day" Anajipa mambo mengi sana kwa wakati mmoja. Anataka kumla ng'ombe kwa mkupuo, ataweza wapi kama sio kuja kuchanganyikiwa kukuta umeanza kula pembe zikakudhuru tumbo na kisha ukashindwa hata kula maini??

Mara nyingine tukiri kwamba mambo ya public administration na management ni profession. Sio siasa.
 
Nadhani wengi tulimuunga mkono Raisi Magufuli juu ya nia nzuri ya kurekebisha hali ya nchi yetu, katika masuala ya uongozi, uchumi na uwajibikaji. Lakini inafikia mahali tujiulize kama kweli hili ndilo linalofanyika. Inabidi uwe shabiki mbaya wa kisiasa au kipofu wa kifikra kutoona kwamba nchi yetu sasa imekuwa kama uwanja wa fujo karibu kila nyanja;
  • Bungeni - vurugu, mipambano, kukomoana, kunyanyasana na ukamataji wa wabunge kwa sababu zisizo za msingi, ubabe na vitisho kwa wabunge ukosefu wa nguvu za hoja na utumiaji wa nguvu za wingi (partisanship)
  • Siasa - ukosefu wa kuvumiliana na kuheshimiana, uadui unaokua kati ya vyama vya siasa, lugha za kukebehi na kukosa staha ya kiuongozi, utekaji, majaribio ya mauaji, udhibiti wa uhuru wa kuhutubia, vyama vya upinzani kuonekana wazi vikiandamwa na serikali na polisi
  • Uhuru wa vyombo habari - ufungiaji na vitisho kwa magazeti na mitandao ya kijamii, ukamataji wa kiholela wa kauli zinazoonekana kuikosoa serikali
  • Nidhamu ya kazi - nidhamu ya woga kujitokeza kwa kiasi kikubwa kwa hofu ya kutumbuliwa
  • Uwekezaji wa nje - migongano na wawekezaji (confrontation), kutofanya mambo kwa utaratibu wa kisheria
  • Utawala wa mikoani na wilayani - ubabe kama kuwekana ndani masaa 24, migongano kati ya wanasiasa na watendaji, hujuma na ufitini ili kujinufaisha kibinafsi
  • Mipaka ya kimadaraka - muingiliano ya madaraka kati ya watendaji, kutia ndani uingizaji wa siasa katika vyombo vya kijeshi taasisi za kiserikali
  • Utawala wa kisheria - ukiukwaji wa makusudi wa katiba ya nchi, ukiukwaji wa kimakusudi wa maamuzi ya mahakama, uhasama kati ya wananchi na polisi na usalama wa taifa, ubabe wa vyombo vya usalama
  • Hali ya maisha - ugumu wa maisha kwa mwananchi wa kawaida, ukosefu wa ajira, uchungu na athari za maamuzi ya serikali kama bomoa bomoa, uhalifu wenye kuongezeka, hofu na kukosa furaha, mzigo wa faini za barabarani kwa makosa madogomadogo
Kwa namna fulani, naanza kuona kuwa gharama ya "kuinyosha" Tanzania inakuwa kubwa sana, ikiwa na namna fulani ya tishio la kuifanya nchi yetu iingie katika hali isiyoeleweka na kuwa uwanja wa fujo.

Sipendekezi kwamba Raisi Magufuli aache nia yake njema ya kuinyoosha Tanzania, bali swali ambalo ningependa sana raisi Magufuli ajiulize ni kwamba, je njia anazotumia "kuinyoosha" nchi amezitafakari sana kuona faida zake na hasara za muda mrefu? Je ni bora kuwa na nchi iliyonyooka "at any cost, regardless of the socio and psychological consequences"?

Je, sasa si wakati muafaka wa kutafakari namna iliyo bora zaidi ya kuinyoosha nchi kuliko njia zinazotumika kwa sasa? Kuna faida gani kuinyoosha nchi kwa ajili ya wananchi ambao kila siku wanazidi kupandwa na hasira na nmana inayotumika kuinyoosha nchi - kwamba wao wanapaswa kuwa collateral damage?
Fear creates hate
 
Kulifikia tatizo na kulitatua kuna njia nyingi sana, na kila mtu anaweza kutumia njia yake kutatua tatizo..
Unaweza kulitatua tatizo ukaacha athari au ukatatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo na kuacha athari kubwa.

Tatizo la Taifa letu la Tanzania ni matatizo mchanganyiko ambayo yanasumbua karibu kila mtanzania, Ila tatizo kuu ni Uchumi mbovu na umasikini kwa watanzania, bila shaka ukitatua tatizo hili unaweza ukawa umetatua matatizo mengi sana.

Ni jukumu letu sasa kuamua ipi ni njia sahihi katika wakati huu wa karne ya 21 katika kutatua matatizo yetu..
 
Mi naona JPM aendelee tu kukamua hadi majipu yote yatoe damu, hapo ndo kidogo viini vitakua vimetoka pia. Magufuli go go gooo.
 
Nadhani wengi tulimuunga mkono Raisi Magufuli juu ya nia nzuri ya kurekebisha hali ya nchi yetu, katika masuala ya uongozi, uchumi na uwajibikaji. Lakini inafikia mahali tujiulize kama kweli hili ndilo linalofanyika. Inabidi uwe shabiki mbaya wa kisiasa au kipofu wa kifikra kutoona kwamba nchi yetu sasa imekuwa kama uwanja wa fujo karibu kila nyanja;
  • Bungeni - vurugu, mipambano, kukomoana, kunyanyasana na ukamataji wa wabunge kwa sababu zisizo za msingi, ubabe na vitisho kwa wabunge ukosefu wa nguvu za hoja na utumiaji wa nguvu za wingi (partisanship)
  • Siasa - ukosefu wa kuvumiliana na kuheshimiana, uadui unaokua kati ya vyama vya siasa, lugha za kukebehi na kukosa staha ya kiuongozi, utekaji, majaribio ya mauaji, udhibiti wa uhuru wa kuhutubia, vyama vya upinzani kuonekana wazi vikiandamwa na serikali na polisi
  • Uhuru wa vyombo habari - ufungiaji na vitisho kwa magazeti na mitandao ya kijamii, ukamataji wa kiholela wa kauli zinazoonekana kuikosoa serikali
  • Nidhamu ya kazi - nidhamu ya woga kujitokeza kwa kiasi kikubwa kwa hofu ya kutumbuliwa
  • Uwekezaji wa nje - migongano na wawekezaji (confrontation), kutofanya mambo kwa utaratibu wa kisheria
  • Utawala wa mikoani na wilayani - ubabe kama kuwekana ndani masaa 24, migongano kati ya wanasiasa na watendaji, hujuma na ufitini ili kujinufaisha kibinafsi
  • Mipaka ya kimadaraka - muingiliano ya madaraka kati ya watendaji, kutia ndani uingizaji wa siasa katika vyombo vya kijeshi taasisi za kiserikali
  • Utawala wa kisheria - ukiukwaji wa makusudi wa katiba ya nchi, ukiukwaji wa kimakusudi wa maamuzi ya mahakama, uhasama kati ya wananchi na polisi na usalama wa taifa, ubabe wa vyombo vya usalama
  • Hali ya maisha - ugumu wa maisha kwa mwananchi wa kawaida, ukosefu wa ajira, uchungu na athari za maamuzi ya serikali kama bomoa bomoa, uhalifu wenye kuongezeka, hofu na kukosa furaha, mzigo wa faini za barabarani kwa makosa madogomadogo
Kwa namna fulani, naanza kuona kuwa gharama ya "kuinyosha" Tanzania inakuwa kubwa sana, ikiwa na namna fulani ya tishio la kuifanya nchi yetu iingie katika hali isiyoeleweka na kuwa uwanja wa fujo.

Sipendekezi kwamba Raisi Magufuli aache nia yake njema ya kuinyoosha Tanzania, bali swali ambalo ningependa sana raisi Magufuli ajiulize ni kwamba, je njia anazotumia "kuinyoosha" nchi amezitafakari sana kuona faida zake na hasara za muda mrefu? Je ni bora kuwa na nchi iliyonyooka "at any cost, regardless of the socio and psychological consequences"?

Je, sasa si wakati muafaka wa kutafakari namna iliyo bora zaidi ya kuinyoosha nchi kuliko njia zinazotumika kwa sasa? Kuna faida gani kuinyoosha nchi kwa ajili ya wananchi ambao kila siku wanazidi kupandwa na hasira na nmana inayotumika kuinyoosha nchi - kwamba wao wanapaswa kuwa collateral damage?
Anko tunarudisha nidhamu ilopotea ndo maaana unaona vurugu. Watakaa Sawa tu soon!,


Magu songa mbele
 
Ukimkosoa hadharani unaitwa mchochezi. Lengo lako si kuijenga Tanzania bali ni kuiharibu. Tumechoshwa na mauaji na kamatakamata.
 
Aendelee kukaza watanzania tunahitaji kunyooshwa hasa mimi naona bado.

Uvivu unatakiwa ututoka tuchape kazi na kupunguza udaku.

Go go go Mr.President,kufika nchi ya ahadi sio lelemama.
 
Kulifikia tatizo na kulitatua kuna njia nyingi sana, na kila mtu anaweza kutumia njia yake kutatua tatizo..
Unaweza kulitatua tatizo ukaacha athari au ukatatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo na kuacha athari kubwa.

Tatizo la Taifa letu la Tanzania ni matatizo mchanganyiko ambayo yanasumbua karibu kila mtanzania, Ila tatizo kuu ni Uchumi mbovu na umasikini kwa watanzania, bila shaka ukitatua tatizo hili unaweza ukawa umetatua matatizo mengi sana.

Ni jukumu letu sasa kuamua ipi ni njia sahihi katika wakati huu wa karne ya 21 katika kutatua matatizo yetu..

Good analysis Mkuu. Ndio maana nina wasiwasi sana na anachofanya raisi Magufuli, pamoja na kwamba ana nia nzuri. Hata Hitler alikuwa na nia nzuri na Ujerumani, aka thrive kwenye support aliyopata toka kwa baadhi ya Warumani na kuwapuuza hata kuwaua walioona anakosea - pamoja na nia yake nzuri. Kiongozi mzuri unatakiwa uwe flexible, kuna wakati inabidi urudi kwenye drawing board, sio kuwa persistent na njia yako ambayo akili yako inakuambia ndiyo inayofaa.

Raisi Magufuli anapaswa kuwa humble na kukubali kwamba kuna baadhi ya approach zake katika kuinyoosha nchi sio tu hazifai, bali hazileti mafanikio na sana sana zinakuwa na matokeo mabaya kwa ujumla.

Japo hatujui nani alihusika, hakuna mtu mwenye akili ambaye atabisha kwamba kupigwa risasi kwa Tundu Lissu ni matokeo ya kujihusisha kwake na siasa katika awamu ya raisi Magufuli. Na ukweli mchungu ambao watu hawataki kuusema ni kwamba katika awamu zote za uongozi zilizopita isingekuwa rahisi kufikia hali ya kupigana risasi waziwazi hivyo kwa ajili tu ya siasa - na hapo sijagusia Kibiti. Hivyo ni wazi kwamba raisi Magufuli anapaswa kujiuliza kama njia zake, hata kama anahisi zitakuwa na positive impact ya muda mrefu, kama negative impact ya sasa ina-justify kuzikomalia. Na tunajuaje impact zinazoonwa kama ni short term hazitakuwa za long term kiasi hata ku-overshadow benefits anazotarajia?

Hebu jiulize, kuna ubaya gani kukomalia kwa kila namna ufisadi, wafanyakazi hewa, vyeti feki, uwajibikaji, huku ukiwa umeruhusu wapinzania kuendelea na siasa zao za mitaani kama kawaida? Au unadhani Watanzania ni wajinga sana kiasi kwamba hawatajua kama wanadanganywa na hotuba za wanasiasa pale wanapoona juhudi halisi za raisi wa nchi na chama chake cha siasa? Kwa namna fulani, kusema unawazuia wanasiasa kwenda kuhubiri uongo kwa wananchi is an insult to the intelligence of Tanzanians, hata kama si wote wana PhD kama wewe.
 
Tatizo linaloleta fujo ni kutofata utawala wa sheria...... Basi,

Utawala bora,demokrasia,ukifata utawala wa sheria,demokrasia,na ukawa na nia ya kujenga mifumo ya nchi na si kujijenga wewe na kikundi chako,nchi inatulia tu

Katika giza la kutofata utawala wa sheria maiti zinaokotwa baharini,watanzania wenzetu hawakupata haki ya kusikiliza ushahidi dhidi yao na wao kutoa ushahidi ,wameuwawa in cold blood katika maeneo ya siri,wamepewa adhabu ambazo hazijaandikwa kwenye sheria-kuuwawa,kutupwa baharini na kufungwa jiwe zito,

Katika hali hiyo watu wameingia clouds na mabunduki,watu wamemwonyesha bastola nape,watu wamempiga risasi lissu,spika anawafungia mabinti,halima na easter kwa ubabe,spika anasema hakuna jaji atawarudisha bungeni,spika anasema anaweza kumzuia zitto asiongee bungeni milele,watu wanaambiwa wakibisha hawatasurvive
 
Kulifikia tatizo na kulitatua kuna njia nyingi sana, na kila mtu anaweza kutumia njia yake kutatua tatizo..
Unaweza kulitatua tatizo ukaacha athari au ukatatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo bila kuacha athari..
Katika kutatua tatizo pia kunaweza kukawa na njia ambazo sio sahihi na zikashindwa kutatua tatizo na kuacha athari kubwa.

Tatizo la Taifa letu la Tanzania ni matatizo mchanganyiko ambayo yanasumbua karibu kila mtanzania, Ila tatizo kuu ni Uchumi mbovu na umasikini kwa watanzania, bila shaka ukitatua tatizo hili unaweza ukawa umetatua matatizo mengi sana.

Ni jukumu letu sasa kuamua ipi ni njia sahihi katika wakati huu wa karne ya 21 katika kutatua matatizo yetu..
Dawa ya ufisadi ni kuondoa umasikini,ukipiga vita ufisadi huku unaharibu uchumi,unatengeneza njaa,mwenye njaa kuwa fisadi ni rahisi sana

Uchumi ndio dawa ya kila kitu,hata maeneo ya watu masikini ndio yamejaa uhalifu,si masaki,oyersterbay,

Hata vita ya kupambana na ufisadi inahitaji uchumi mzuri ili uwalipe wapambanaji,uimarishe taasisi kwa mifumo ya kiteknolojia

UFISADI NI DALILI TU,kama homa,ugonjwa wenyewe ni UMASIKINI
 
Back
Top Bottom