Ukweli ni kwamba hakuna mpinzani anayepinga ndege kununuliwa, wala hakuna anayepinga shirika letu la ndege kufufuliwa

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Anaandika Malisa GJ,

Awali ya yote nipongeze juhudi za Rais JPM za kununua ndege kadhaa mojawapo ni Boeing 787 Dreamliner iliyopokelewa wiki jana. Hizi ni juhudi za kupongezwa na kila mtanzania, kwamba sasa serikali inamiliki ndege za usafiri wa umma.

Pamoja na juhudi hizo yapo madai kwamba kuna wapinzani wanapinga ununuzi wa ndege hizo. Haya ni madai yanayotolewa na watu waliozoea kujipendekeza kwa viongozi.

Ukweli ni kwamba hakuna mpinzani anayepinga ndege kununuliwa, wala hakuna anayepinga shirika letu la ndege la ATCL kufufuliwa. Kila mtu anapongeza juhudi hizi, lakini kupongeza hakuzuii watu kuhoji. Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD) aliwahi kusema "Kuhoji ni haki ya mtawaliwa inayolindwa kikatiba, na kujibu hoja ni haki ya mtawala. Kumzuia mtawaliwa kuhoji ni kumnyima haki yake, na kumzuia mtawala kuhojiwa ni kumnyima haki yake ya msingi inayolindwa kikatiba"

Kwahiyo watu wanaohoji kuhusu ununuzi wa ndege hizo, sio kwamba wanapinga bali wanahitaji ufafanuzi. Ni muhimu wajibiwe kwa hoja. Lazima tutofautishe kuhoji na kupinga. Mwanaharakati na mpigania uhuru wa zamani wa Rhodesia ya kusini Mchungaji Ndabaningi Thisole aliwahi kusema "Wendawazimu peke yao ndio wasioweza kutofautisha kukosoa na kupinga, na bahati mbaya tuna wendawazimu wengi wenye madaraka na vyeo."

Binafsi nimepitia hoja za wapinzani zinazowafanya waambiwe wanapinga ununuzi wa ndege. Nimepata hoja zifuatazo;

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]; Watu wanahoji kwanini tununue ndege kwa fedha taslimu? Hoja hii imetolewa na kaka yangu Sam Ruhuza. Alisema Biashara ya usafiri wa anga mara nyingi ndege hununuliwa kwa mikataba. Mashirika makubwa kama KLM, Quatar Airways etc hayanunui ndege kwa cash. Kwanini sisi tununue cash? Ndege hii imenunuliwa kwa dola milioni 225 ambayo ni sawa na Bilioni 500 za kitanzania. Kwanini tusingelipa nusu, ili pesa nyingine zitumike kwenye shughuli nyingine za maendeleo, halafu nusu inayobaki ilipwe na ndege yenyewe kupitia mapato yake? Hii hoja haijajibiwa. Majibu yanayotolewa ni kwamba wapinzani wanapinga ununuzi wa ndege. Aibu.!

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]; Watu wanahoji kwanini tununue ndege wakati kuna huduma muhimu za kijamii hatuna? Hoja hii hii imetolewa na Comrade Julius S. Mtatiro. Kuna maeneo nchi hii watu wanakunywa maji kwa kushare na mifugo, kuna vituo vya afya havina watumishi, unakuta mtu ni "Medical Attendant" lakini ana act kama mganga mfawidhi wa kituo. Wanafunzi hawana mikopo wengi wamekatiza masomo, watu wanakufa kwa kukosa madawa, ajira hakuna etc.

Je kulikuwa na umuhimu wa kuacha yote haya na kukimbilia kununua ndege? Vipaumbele vyetu kama taifa ni vipi? Je tupo tayari kuona watu wanakufa kwa kukosa "panadol" lakini tunayo ndege? Je ni kweli kwamba tunathamini zaidi maendeleo ya vitu kuliko maendeleo ya watu? Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa hoja, sio kusema wapinzani wanapinga kila kitu.

[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG]; watu wanahoji kwanini ndege zinunuliwe na serikali na sio ATCL kuwezeshwa ili ijiendeshe yenyewe? Rais hajaiwezesha ATCL kujitegemea. Anachofanya ni serikali kununua ndege kisha kuikodishia ATCL. Yani ndege zote 4 zilizonunuliwa hadi sasa, hakuna hata moja inayomilikiwa na ATCL. Zote zinamilikiwa na serikali then ATCL wanakodi kufanyia biashara.

Mfumo huu hauwezi kuwa na tija. Kwa sababu kama ni kukodisha ndege, ATCL wangeweza kukodi mahali pengine, sio lazima wakodi ndege za serikali. Hoja ya watanzania ni ATCL kumiliki ndege zake yenyewe, sio kukodisha ndege. Kwanini serikali inunue ndege then ATCL wakodi? Kwani walishindwa kukodi kwingine?

Kuilazimisha ATCL kukodi ndege za serikali ni kuongeza gharama za uendeshaji, kwa sababu ATCL watalazimika kupandisha bei ili wapate fedha za kuilipa serikali na wabaki na faida. Vinginevyo watajiendesha kwa hasara, kama ambavyo imeanza kujitokeza, ambapo mwaka jana na mwaka juzi wamepata hasara ya zaidi ya bilioni 60 (kwa mujibu wa ripoti ya bunge).

Kwahiyo ili kuondoa hasara hiyo, ingekuwa busara ndege hizo kumilikiwa na ATCL moja kwa moja. Yani serikali ingenunua ndege hizo na kuipa ATCL izimiliki moja kwa moja, au serikali ingewapa fedha ATCL wanunue ndege wenyewe ili waweze kuzimiliki.

Vinginevyo shirika hili litajiendesha kwa hasara maradufu kuliko ilivyokuwa awali. Kwa sababu katika mapato ya ATCL italazimika kupata fedha za kumlipa mmiliki wa ndege (serikali), kukidhi gharama za uendeshaji, kisha ibaki na faida. Hii ni ngumu sana hasa kwa kuwa soko la ATCL bado lina ushindani mkubwa kwa makampuni mengine ya ndege yaliyopo.

[HASHTAG]#Nne[/HASHTAG]; ni kuhusu serikali kufufua shirika la ATCL. Kufufua kitu means kitu kilikuwepo lakini kikafa/kuuawa. Kabla ya kupongeza JPM kufufua ATCL ni muhimu kujiuliza nani aliyeiua? Swali hili ni muhimu kwa sababu litasaidia isife tena.

Ukweli ni kwamba Serikali hii hii (ya CCM) inayosifiwa kufufua ATCL ndio iliyoua shirika hilo. Shirika la ndege la taifa (wakati huo likiitwa ATC) lilianzishwa mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa shirika la ndege la Afrika Mashariki, East African Airways (EAA).

Mpaka kufikia mwaka 1994 ATC ilikuwa na jumla ya ndege 8 kubwa na za kisasa. Ndege tatu kati ya hizo tulizitaifisha kutoka EAA, na nyingine tulinunua. Zilikuwepo ndege 8 aina ya Boeing 737, Boeing 747 SP, Airbus A320, Boeing 737-500 etc. Hizi zilikuwa ndege kubwa, bora na za kisasa.

Katika picha hizi nilizoambatanisha hapa chini utaona ndege mbalimbali za ATC wakati huo zikiwa ktk safari zake. Picha ya kwanza kulia ni nege ya ATC ikiwa imepaki uwanja wa ndege wa Frankfurt nchini Ujerumani mwaka 1994, na picha ya 3 kushoto ni ndege ya ATC aina ya Boeing 737 ikiwa imepaki uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo, SA mwaka 2006.

Kwahiyo sio kweli kwamba hatujawahi kuwa na ndege kama wachache wanavyojaribu kupotosha. Tulikuwa nazo nyingi na nzuri na zilifanya safari za kimataifa, lakini serikali hiihii ya CCM inayosifiwa leo ikazifilisi na kuua shirika. Watu walewale waliouwa ATCL ndio haohao wanaosifiwa kufufua shirika hilo leo. Futuhi.!!

Mwaka 2002 serikali iliingia mkataba (wa kijinga) na shirika la ndege la Afrika Kusini (SAA) wa dola milioni 20, na kuiwezesha SAA kumiliki 49% ya mali za ATC zikiwemo ndege. Dola milioni 20 ni kama shilingi bilioni 45 za kitanzania. Kwahiyo kwa Bilioni 45 tu SAA wakamiliki 49% ambayo ni kama nusu ya mali zote za ATC. Hapa ndipo jina lilipobadilishwa kutoka ATC kuwa ATCL.

Lengo la kuingia ubia na SAA ilikuwa kujaribu kuona kama tutapata faida kwa sababu ATC ilikuwa ikijiendesha kwa hasara sana wakati huo. Lakini baada kufunga "ndoa" hiyo hasara ikawa maradufu. Kufikia mwaka 2005 tukawa tumepata hasara ya dola milioni 19 (kama shilingi Bilioni 40 hivi) ndani ya miaka mitatu tu. Yani tuliuza shirika kwa Bilioni 45 halafu baada ya miaka mitatu tukapata hasara ya Bilioni 40. Biashara kichaa.!!

Mwaka 2006 tukashindwa kuendelea na mkataba huo. Tukauvunja. Kilichotokea wengi mnajua. Baadhi ya ndege zetu zilizuiwa na SAA kufidia hasara. Waliosababisha hasara hiyo hawajawahi kuwajibishwa wala kuchukuliwa hatua zozote za kisheria.

Leo taifa zima linashangilia Boeing 1 na kuimba mapambio ya kuabudu kana kwamba hatujawahi kuwa na ndege kabisa, kumbe tulikuwa na Boeing nyingi za kisasa. Serikali ileile iliyoua ATCL na kufilisi ndege zote 8 zilizokuwepo ndio hiohio inayosifiwa kwa kununua ndege moja. Nimekumbuka kauli ya Mwalimu Nyerere aliyowahi kusema ujinga ni kuibiwa madini ukapewa kichupa halafu ukaondoka ukishangilia kama zuzu.

Mwaka 1994 wakati ATCL ikiwa na Boeing 8, shirika la ndege la Kenya Airways ilikuwa na Boeing 4 tu ambapo mbili zilikuwa za kukodi. Lakini leo miaka 24 baadae, Kenya Airways wana Boeing 25 sisi tumenunua Boieng moja taifa zima linasifu na kuabudu. What a shame?? Lazima tujiulize tumefikaje hapa.

Anayestahili kupongezwa katika juhudi hizi ni Rais JPM, sio serikali ya CCM ambayo ilishiriki kuua ATCL. Lakini pamoja na pongezi hizo ni muhimu ashauriwe namna bora ya kufufua shirika hilo ili yasije yakajitokeza yaleyale yaliyosababisha likafa. Nchi hii ni yetu sote, hakuna mwenye haki zaidi kuliko mwingine. Watu wanapohoji wasikejeliwe au kujibiwa kwa mipasho, wajibiwe kwa hoja. Tukosoane, tushauriane, tuelimishane kwa maslahi ya taifa. Kwa pamoja tuijenge nchi yetu.!

Malisa GJ
FB_IMG_1531573404041.jpg
 
Anaandika Malisa GJ,

Awali ya yote nipongeze juhudi za Rais JPM za kununua ndege kadhaa mojawapo ni Boeing 787 Dreamliner iliyopokelewa wiki jana. Hizi ni juhudi za kupongezwa na kila mtanzania, kwamba sasa serikali inamiliki ndege za usafiri wa umma.

Pamoja na juhudi hizo yapo madai kwamba kuna wapinzani wanapinga ununuzi wa ndege hizo. Haya ni madai yanayotolewa na watu waliozoea kujipendekeza kwa viongozi.

Ukweli ni kwamba hakuna mpinzani anayepinga ndege kununuliwa, wala hakuna anayepinga shirika letu la ndege la ATCL kufufuliwa. Kila mtu anapongeza juhudi hizi, lakini kupongeza hakuzuii watu kuhoji. Askofu Dr.Benson Bagonza (PhD) aliwahi kusema "Kuhoji ni haki ya mtawaliwa inayolindwa kikatiba, na kujibu hoja ni haki ya mtawala. Kumzuia mtawaliwa kuhoji ni kumnyima haki yake, na kumzuia mtawala kuhojiwa ni kumnyima haki yake ya msingi inayolindwa kikatiba"

Kwahiyo watu wanaohoji kuhusu ununuzi wa ndege hizo, sio kwamba wanapinga bali wanahitaji ufafanuzi. Ni muhimu wajibiwe kwa hoja. Lazima tutofautishe kuhoji na kupinga. Mwanaharakati na mpigania uhuru wa zamani wa Rhodesia ya kusini Mchungaji Ndabaningi Thisole aliwahi kusema "Wendawazimu peke yao ndio wasioweza kutofautisha kukosoa na kupinga, na bahati mbaya tuna wendawazimu wengi wenye madaraka na vyeo."

Binafsi nimepitia hoja za wapinzani zinazowafanya waambiwe wanapinga ununuzi wa ndege. Nimepata hoja zifuatazo;

[HASHTAG]#Mosi[/HASHTAG]; Watu wanahoji kwanini tununue ndege kwa fedha taslimu? Hoja hii imetolewa na kaka yangu Sam Ruhuza. Alisema Biashara ya usafiri wa anga mara nyingi ndege hununuliwa kwa mikataba. Mashirika makubwa kama KLM, Quatar Airways etc hayanunui ndege kwa cash. Kwanini sisi tununue cash? Ndege hii imenunuliwa kwa dola milioni 225 ambayo ni sawa na Bilioni 500 za kitanzania. Kwanini tusingelipa nusu, ili pesa nyingine zitumike kwenye shughuli nyingine za maendeleo, halafu nusu inayobaki ilipwe na ndege yenyewe kupitia mapato yake? Hii hoja haijajibiwa. Majibu yanayotolewa ni kwamba wapinzani wanapinga ununuzi wa ndege. Aibu.!

[HASHTAG]#Pili[/HASHTAG]; Watu wanahoji kwanini tununue ndege wakati kuna huduma muhimu za kijamii hatuna? Hoja hii hii imetolewa na Comrade Julius S. Mtatiro. Kuna maeneo nchi hii watu wanakunywa maji kwa kushare na mifugo, kuna vituo vya afya havina watumishi, unakuta mtu ni "Medical Attendant" lakini ana act kama mganga mfawidhi wa kituo. Wanafunzi hawana mikopo wengi wamekatiza masomo, watu wanakufa kwa kukosa madawa, ajira hakuna etc.

Je kulikuwa na umuhimu wa kuacha yote haya na kukimbilia kununua ndege? Vipaumbele vyetu kama taifa ni vipi? Je tupo tayari kuona watu wanakufa kwa kukosa "panadol" lakini tunayo ndege? Je ni kweli kwamba tunathamini zaidi maendeleo ya vitu kuliko maendeleo ya watu? Hoja hii inapaswa kujibiwa kwa hoja, sio kusema wapinzani wanapinga kila kitu.

[HASHTAG]#Tatu[/HASHTAG]; watu wanahoji kwanini ndege zinunuliwe na serikali na sio ATCL kuwezeshwa ili ijiendeshe yenyewe? Rais hajaiwezesha ATCL kujitegemea. Anachofanya ni serikali kununua ndege kisha kuikodishia ATCL. Yani ndege zote 4 zilizonunuliwa hadi sasa, hakuna hata moja inayomilikiwa na ATCL. Zote zinamilikiwa na serikali then ATCL wanakodi kufanyia biashara.

Mfumo huu hauwezi kuwa na tija. Kwa sababu kama ni kukodisha ndege, ATCL wangeweza kukodi mahali pengine, sio lazima wakodi ndege za serikali. Hoja ya watanzania ni ATCL kumiliki ndege zake yenyewe, sio kukodisha ndege. Kwanini serikali inunue ndege then ATCL wakodi? Kwani walishindwa kukodi kwingine?

Kuilazimisha ATCL kukodi ndege za serikali ni kuongeza gharama za uendeshaji, kwa sababu ATCL watalazimika kupandisha bei ili wapate fedha za kuilipa serikali na wabaki na faida. Vinginevyo watajiendesha kwa hasara, kama ambavyo imeanza kujitokeza, ambapo mwaka jana na mwaka juzi wamepata hasara ya zaidi ya bilioni 60 (kwa mujibu wa ripoti ya bunge).

Kwahiyo ili kuondoa hasara hiyo, ingekuwa busara ndege hizo kumilikiwa na ATCL moja kwa moja. Yani serikali ingenunua ndege hizo na kuipa ATCL izimiliki moja kwa moja, au serikali ingewapa fedha ATCL wanunue ndege wenyewe ili waweze kuzimiliki.

Vinginevyo shirika hili litajiendesha kwa hasara maradufu kuliko ilivyokuwa awali. Kwa sababu katika mapato ya ATCL italazimika kupata fedha za kumlipa mmiliki wa ndege (serikali), kukidhi gharama za uendeshaji, kisha ibaki na faida. Hii ni ngumu sana hasa kwa kuwa soko la ATCL bado lina ushindani mkubwa kwa makampuni mengine ya ndege yaliyopo.

[HASHTAG]#Nne[/HASHTAG]; ni kuhusu serikali kufufua shirika la ATCL. Kufufua kitu means kitu kilikuwepo lakini kikafa/kuuawa. Kabla ya kupongeza JPM kufufua ATCL ni muhimu kujiuliza nani aliyeiua? Swali hili ni muhimu kwa sababu litasaidia isife tena.

Ukweli ni kwamba Serikali hii hii (ya CCM) inayosifiwa kufufua ATCL ndio iliyoua shirika hilo. Shirika la ndege la taifa (wakati huo likiitwa ATC) lilianzishwa mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa shirika la ndege la Afrika Mashariki, East African Airways (EAA).

Mpaka kufikia mwaka 1994 ATC ilikuwa na jumla ya ndege 8 kubwa na za kisasa. Ndege tatu kati ya hizo tulizitaifisha kutoka EAA, na nyingine tulinunua. Zilikuwepo ndege 8 aina ya Boeing 737, Boeing 747 SP, Airbus A320, Boeing 737-500 etc. Hizi zilikuwa ndege kubwa, bora na za kisasa.

Katika picha hizi nilizoambatanisha hapa chini utaona ndege mbalimbali za ATC wakati huo zikiwa ktk safari zake. Picha ya kwanza kulia ni nege ya ATC ikiwa imepaki uwanja wa ndege wa Frankfurt nchini Ujerumani mwaka 1994, na picha ya 3 kushoto ni ndege ya ATC aina ya Boeing 737 ikiwa imepaki uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo, SA mwaka 2006.

Kwahiyo sio kweli kwamba hatujawahi kuwa na ndege kama wachache wanavyojaribu kupotosha. Tulikuwa nazo nyingi na nzuri na zilifanya safari za kimataifa, lakini serikali hiihii ya CCM inayosifiwa leo ikazifilisi na kuua shirika. Watu walewale waliouwa ATCL ndio haohao wanaosifiwa kufufua shirika hilo leo. Futuhi.!!

Mwaka 2002 serikali iliingia mkataba (wa kijinga) na shirika la ndege la Afrika Kusini (SAA) wa dola milioni 20, na kuiwezesha SAA kumiliki 49% ya mali za ATC zikiwemo ndege. Dola milioni 20 ni kama shilingi bilioni 45 za kitanzania. Kwahiyo kwa Bilioni 45 tu SAA wakamiliki 49% ambayo ni kama nusu ya mali zote za ATC. Hapa ndipo jina lilipobadilishwa kutoka ATC kuwa ATCL.

Lengo la kuingia ubia na SAA ilikuwa kujaribu kuona kama tutapata faida kwa sababu ATC ilikuwa ikijiendesha kwa hasara sana wakati huo. Lakini baada kufunga "ndoa" hiyo hasara ikawa maradufu. Kufikia mwaka 2005 tukawa tumepata hasara ya dola milioni 19 (kama shilingi Bilioni 40 hivi) ndani ya miaka mitatu tu. Yani tuliuza shirika kwa Bilioni 45 halafu baada ya miaka mitatu tukapata hasara ya Bilioni 40. Biashara kichaa.!!

Mwaka 2006 tukashindwa kuendelea na mkataba huo. Tukauvunja. Kilichotokea wengi mnajua. Baadhi ya ndege zetu zilizuiwa na SAA kufidia hasara. Waliosababisha hasara hiyo hawajawahi kuwajibishwa wala kuchukuliwa hatua zozote za kisheria.

Leo taifa zima linashangilia Boeing 1 na kuimba mapambio ya kuabudu kana kwamba hatujawahi kuwa na ndege kabisa, kumbe tulikuwa na Boeing nyingi za kisasa. Serikali ileile iliyoua ATCL na kufilisi ndege zote 8 zilizokuwepo ndio hiohio inayosifiwa kwa kununua ndege moja. Nimekumbuka kauli ya Mwalimu Nyerere aliyowahi kusema ujinga ni kuibiwa madini ukapewa kichupa halafu ukaondoka ukishangilia kama zuzu.

Mwaka 1994 wakati ATCL ikiwa na Boeing 8, shirika la ndege la Kenya Airways ilikuwa na Boeing 4 tu ambapo mbili zilikuwa za kukodi. Lakini leo miaka 24 baadae, Kenya Airways wana Boeing 25 sisi tumenunua Boieng moja taifa zima linasifu na kuabudu. What a shame?? Lazima tujiulize tumefikaje hapa.

Anayestahili kupongezwa katika juhudi hizi ni Rais JPM, sio serikali ya CCM ambayo ilishiriki kuua ATCL. Lakini pamoja na pongezi hizo ni muhimu ashauriwe namna bora ya kufufua shirika hilo ili yasije yakajitokeza yaleyale yaliyosababisha likafa. Nchi hii ni yetu sote, hakuna mwenye haki zaidi kuliko mwingine. Watu wanapohoji wasikejeliwe au kujibiwa kwa mipasho, wajibiwe kwa hoja. Tukosoane, tushauriane, tuelimishane kwa maslahi ya taifa. Kwa pamoja tuijenge nchi yetu.!

Malisa GJ


Mimi nitajibu la kwanza, kukodisha kitu unalipia kidogokidogo lkn kuna riba ambayo ni kubwa na mwisho wa siku utaishia kulipia zaidi ya bei halisia, hivyo kama unayo fedha taslimu ni bora ulipe kuliko ulipie kidogo kidogo, hiyo iko hata kwenye magari kuna tofauti kati ya leasing na kulipia gari cash!

Pia kuna mambo mengine mengi kwenye kukodi ndge kwa kuwa umeikodi ina maana hiyo ndege siyo yako na ina masharti, najua kwenye magri kwa mfano ukichukuwa kwa leasing gari linakuwa siyo lako umekodishwa tu na unapewa mashrti kwa mfano huruhusiwi labda kutembea na gari kwa zaidi ya km 10 000/mwaka, likipata ajali na kuharibika utaendelea kulipia ingawaje gari hauna na mambo mengine mengi, hivyo kwenye Ndege kukodi haiwezi kuwa tofauti tena na zaidi.

Hivyo kukodi ndege kama ilivyo kwenye Gari inalipa tu kama Shirika la Ndege likiwa ni kubwa kama hayo KLM-AirFrance kama ilivyo leasing inalipa tu kwa watu wenye makampuni lkn kwa mtu binafsi kama una fedha taslimu ni bora ulipe mara moja na umiliki kitu chako, vivyo hivyo kwa Shirika changa kama letu kukodi ndege hailipi kabisa isitoshe tumetoka huko kwani ATC tangu kuanzishwa kwake ilikuwa inakodi Ndege lkn ilikufa na bado tukaendelea kulipia gharama siajabu na ndo maana mpaka leo hii bado tuna madeni!
 
Mpaka sasa tunaambiwa tumeshatumia shilingi bilioni 1,495(kwa mujibu wa Halima Mdee akinukuu bajeti za wizara husika tangu 2015/2016) kufufua hili shirika alafu hata mahesabu ya shirika hayaeleki ila watu kwa uzuzu wanashangilia.

Hata CAG nae ukaguzi wa hili shirika kwenye ripoti yake ya hivi karibuni sijui kama aliongea chochote.

Kwa kifupi,tunarudi kule kule tulikotoka muda si mrefu maana huu usiri si wa bure.
 
Chadema Kwa kujikweza eti wanahoji ndege ? Wanaacha kuhoji Chama chao Kwa nini kinakaribia kufikia miaka 30 Bado hakina ofisi ya makao makuu ya kueleweka .Makao makuu utafikiri Banda la kufugia kuku pamoja Na mabilioni ya ruzuku na ya wafadhili waliyoyapokea na hela wanazowakamua Kila mwezi wabunge miaka yote.Charity begins at home
 
Chadema Kwa kujikweza eti wanahoji ndege ? Wanaacha kuhoji Chama chao Kwa nini kinakaribia kufikia miaka 30 Bado hakina ofisi ya makao makuu ya kueleweka .Makao makuu utafikiri Banda la kufugia kuku pamoja Na mabilioni ya ruzuku na ya wafadhili waliyoyapokea na hela wanazowakamua Kila mwezi wabunge miaka yote.Charity begins at home
Hapa ndio nashindwa kabisa kuwaelewa hawa wazungusha mikono.
 
Chadema Kwa kujikweza eti wanahoji ndege ? Wanaacha kuhoji Chama chao Kwa nini kinakaribia kufikia miaka 30 Bado hakina ofisi ya makao makuu ya kueleweka .Makao makuu utafikiri Banda la kufugia kuku pamoja Na mabilioni ya ruzuku na ya wafadhili waliyoyapokea na hela wanazowakamua Kila mwezi wabunge miaka yote.Charity begins at home
Hizo ni kodi zetu na sio hela za CCM.
 
Mmeanza kubadili gia hewani!

Nyie ndio mlikuwa mnapinga Kwanini Tununue
Ndege wakati Wananchi wanahitaji Maji Na huduma za Afya?, Leo Boeing limetua tumeanza kuona kina Zitto Kabwe wamekata Tiketi Na kuanza kutumia usafiri huo mnakuja
Na ngonjera Mpya
 
Asante sana Mkuu Malisa..
Wakati hizo hoja zako zikijibiwa hapa..
Pia tuelezwe ipo wapi 1.5Tril ambayo CAG hakuiona kwenye ukaguzi wake kwenye Mwaka wa fedha ulioisha..
Maana tunadanganywa na kulaghaiwa kwa hizi ndege wakati kuna upotevi mkubwa wa kiasi hiki cha pesa za walipa kodi wa Nchi hii..
Where is our 1.5Tril?
[HASHTAG]#Jizi[/HASHTAG].
 
Tunahoji kodi zetu.Hizo ndege hazijanunuliwa na hela ya CCM.
Na Mimi nahoji Kwa nini chadema hamjajenga ofisi ya kueleweka ya makao makuu miaka yote wakati mumekula kodi yangu kupitia ruzuku mnayopewa .Kodi yangu iliyomo kwenye ruzuku mnayopewa mnapeleka wapi? Hadi hata ofisi ya makao makuu ya maana hamna? Naomba serikali iwafutie ruzuku
 
Na Mimi nahoji Kwa ni chadema hamjajenga ofisi ya kueleweka ya makao makuu miaka yote wakati mumukula kodi yangu kupitia ruzuku mbayopewa kodi yangu iliyomo kwenye ruzuku mnayopewa mnapeleka wapi? Hadi hata ofisi ya makao makuu ya maana hamna? Naomba serikali iwafutie ruzuku
Kamata kitu yako.
IMG_20180709_223625.jpg
 
Na Mimi nahoji Kwa ni chadema hamjajenga ofisi ya kueleweka ya makao makuu miaka yote wakati mumekula kodi yangu kupitia ruzuku mnayopewa .Kodi yangu iliyomo kwenye ruzuku mnayopewa mnapeleka wapi? Hadi hata ofisi ya makao makuu ya maana hamna? Naomba serikali iwafutie ruzuku
Mbona nyie tangu uhuru mnaendesha nchi kwa kutegemea misaada?
 
Mbona nyie tangu uhuru mnaendesha nchi kwa kutegemea misaada?
CCM
Misaada tunaitumia vizuri ona ofisi za CCM nchi nzima zilivyo safi Na za nguvu nyie misaada mnapeleka kunywea bia za Kilimanjaro lager badala ya kujenga ofisi za kueleweka ikiwemo makao makuu
 
Hakuna mafuta ya kupaka kubadili rangi ya mpingo. Unapokuwa hukubaliani na majibu ya anaeulizwa swali, Kuhoji kwako ndio kunageuka kupinga, sababu maswali yote yanayoulizwa na mapendekezo yanayotolewa, yanapotolewa majibu na serikali mtu akaendeleza propaganda za kusimamia haki yake ya kuhoji! Huko sio kuhoji tena ni kupinga.

Mara kadhaa Rais/serikali bungeni wametolea majibu ya maswali yote hayo mpaka juzi wakati wa kupokea ndege. Ndani ya upinzani hakuna anayekuwa tayari kusikiliza/kukubaliana na hotuba wala ufafanuzi wa serikali/Rais, kiasi cha kutaka hata kukwamisha bajeti, kutoka au kutopiga kura. Huko sio kuhoji tu bali na kupinga ndani ayake.
Maswali ya kwanini cash, kwanini kufufua kilicho kufa, Kwanini ATCL ikodishiwe na serikali kwa mtu aliyejifanya hakuwahi kusikia majibu yake asikilize hotuba ya Magufuli ya kupokea BOIENG 787-8 asione kichefuchefu kusikia asiyopenda kusikia.
Na kama kunawanaodhani kwa kununuliwa ndege hizi zimekwamisha huduma za msingi kwa wananchi wenye pesa zao, majibu yake tutayapata 2019/2020 kwa matokeo ya kura za Serikali za mitaa na Urais sababu wakati huo Twaweza watakua watazamaji
 
Back
Top Bottom