Ukweli mkali: Yatokeayo sasa Bungeni na kwingineko ni 'laana' ya uchaguzi mkuu wa 2020

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Umekuwa msimamo wangu popote ninaposema au kuandika kuwa mwaka 2020 hakukuwa na uchaguzi mkuu. Kulikuwa na uchafuzi mkuu wa Tanzania. Kulikuwa tu na kutimiza lengo la kuwaondoa 'kivyovyote vile' wapinzani Bungeni. Lengo kuu lilikuwa ni kunyamazisha sauti za upinzani ndani ya Bunge kwa nguvu na maarifa yoyote yale. Hakukuwa na uchaguzi wowote huru au usio huru. Kulikuwa na uchafuzi na uteuzi.

Katika kufanikisha hilo lengo kuu, watu waliteswa;walijeruhiwa;waliminywa na hata wengine kuikimbia nchi. Wananchi walibanwa kwenye kona ya kuona CCM tu wakitamba kama dume la simba bila upinzani wowote. Safu kandamizi ilisukwa kuanzia NEC hadi chini kabisa vituoni. CCM tukashinda kwa kishindo kuliko cha nyundo na kushangilia huku wapinzani wetu wakilia. Mungu akatuona. Akaanza kutuadhibu.

Adhabu kutokana na machozi, jasho na damu ya watanzania uchaguzini. Adhabu kuhusu kuuharibu uchaguzi mkuu makusudi kwa kutimiza lengo la kuufuta upinzani nchini Tanzania. Adhabu ilipoanza, tukaanza kuweweseka. Kwanza, tukalazimisha uwepo upinzani Bungeni ule ule ambao tulitaka usiwepo. Tukalazimisha Wabunge 19 waitwe wa CHADEMA na wa ACT waingie Bungeni kwa mbwembwe.

Haikuishia hapo. Sasa Wabunge wetu wanaparurana kilaana wenyewe kwa wenyewe. Eti, wanawapambanisha na kuwatofautisha Mwendazake Magufuli na Rais Samia. Eti, Wabunge wanademka na kuchemka kumponda mmoja na kumpenda mwingine. Eti Wabunge wetu wa CCM wanaunda kambi kalikali kama mbilimbi. Wanaunda pande kama kande. Wabunge wetu wanaweweseka na kuhangaika kwa laana ya 2020.

Amini nawaambia, hakuna Mbunge wa sasa anayeufurahia ubunge wake. Wabunge wetu hawana amani kama zamani. Wanateswa na dhamira zao na majuto yamekuwa akilini mwao. Wabunge wetu wanatamani kusema Bunge livunjwe lakini hawawezi. Wanatamani tuanza upya kama Taifa kidemokrasia lakini hawathubutu. Wanaishia kupambana wenyewe kwa wenyewe. Karma is real!

Mama, waache Wabunge wademke hadi hamu yao iwatoke!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Masasi, Mtwara)
 
Wewe ni zee jinga sana, ulidhani watanzania ni vilaza hadi wateue mtetezi wa mashoga?
 
Wasipoitwa vinara wa makundi hayo na kupewa kalipio Kali na Chama pale Lumumba au Chimwaga, huenda makundi hayo yakaleta mpasuko wa chama though hautakuwa mkubwa kama ule wa 2015.
 
Nimeona comment mtu anaongelea mashoga, wewe kama si shoga yanakuhusu je? Mashoga ndo mastaa wa nchi hizo unazoziita mabeberu ambazo mlienda kununua ndege. Kwanini hamkwenda China ambako nako kuna mashoga ila wanajificha.

Mtu aliyekuwa anamtukuza mungu wake kila kukicha, akadiriki kusema corona ni mafua kama mengine, aliona walivyoanza kuporomoka wenzake, rafiki zake wakaponea chupu na yeye akaondoka kwa kisingizio cha moyo kushindwa kufanya kazi.

Kile kifaa kilihitaji oxygen toka kwenye mapafu ambayo yalishafail na bado tukadanganywa. Je, kwanini yeye mcha mungu wake achukuliwe na mashoga wabaki? Tunachanganya mada na kuanza kuleta uchafu usiohusu mambo ya bali ni kitu cha mtu mmoja mmoja.
 
Kuna watu wanataka bunge livunjwe lakini wanasahau kurejea kwenye katiba nini kitatokea bunge likivunjwa.

Bunge likivunjwa inabidi uitishwe uchaguzi mkuu ambapo itabidi tufanye na uchaguzi mkuu wa rais.

Hoja ya kuvunjwa bunge ni ngumu kutekelezeka kwa mazingira yetu.
 
Kwa kweli Mungu hayuko pamoja na wanaodhulumu! kwa maana hii hakuna kitakachokuwa katika serikali hii na kila kitakachoshikwa kitageuka kuwa chungu na maumivu zaidi!
Mifano mingi tumeanza kuiona; mabasi mwendo kasi, ATCL, Wizi wa kupitiliza n.k.
Mbaya zaidi tunaoumia ni wote kwa makosa ya CCM na washirika wao! Na kwa vile ni zao la laana hawataweza kurekebisha ingawa Mungu amewapa nafasi ya kurekebisha! "Summum bukummum umuyyun fahum laa yarjiuun"!
Hakuna kitakachokuwa zaidi ya kufitiana wenyewe kwa wenyewe!
 
Kuna watu wanataka bunge livunjwe lakini wanasahau kurejea kwenye katiba nini kitatokea bunge likivunjwa.

Bunge likivunjwa inabidi uitishwe uchaguzi mkuu ambapo itabidi tufanye na uchaguzi mkuu wa rais.

Hoja ya kuvunjwa bunge ni ngumu kutekelezeka kwa mazingira yetu.
Kwa kadiri ya Katiba yetu hii mbaya, Rais akivunja Bunge, tunaenda kwenye uchaguzi wa wabunge. Kama endapo theluthi mbili ya wabunge wa zamani watachaguliwa, Rais anajiuzulu, mnaenda kwenye uchaguzi wa Rais.

Lakini kwa wabunge hawa wa sasa, hakuna muujiza wa theluthi 2 kurudi. Zaidi ya 50% wataishia hapo kwenye kura za maoni. Na 50% ya wale 50% watakaopita kwenye kura za maoni, watadondoka kwenye uchaguzi.

Lakini sioni dalili ya Bunge kuvunjwa. Kikubwa kitakachotokea, ni mmoja baada ya mwingine kupokea mapigo ya laana ya dhuluma, ambayo yatakuwa mabaya kuliko hata Bunge lingevunjwa.

Sioni mwisho mzuri kwa Ndugai.

Wabunge wengi walio wanyofu lakini walioingizwa kwenye uchafubwa uchaguzi ulioasisiwa na marehemu, wanajutia, na wangefarijika sana, hata leo hii Bunge lingevunjwa.
 
Sasa kwanini tuendelee kuishi na hiyo laana miaka mitano? bunge livunjwe.

Ianzishwe pettition tuweke sign zikifika milioni 2 bunge livunjwe.
 
Back
Top Bottom