Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,058
- 22,755
Naam, walimmiminia risasi thelathini na nane (38) na kumi na sita (16) kati ya hizo zikatua mwilini mwake.
Naam, zilikuwa ni risasi za kumwangusha tembo na waliondoka hapo wakijua kazi waliyotumwa imemalizika.
Waliondoka hapo kwa haraka ya kufikisha habari njema hii kwa waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu kubwa.
Walijua ujira na pongezi kubwa zilikuwa zikiwasubiri kwa kutekeleza kwa ufanisi mkubwa jukumu walilopewa.
Hapana shaka wakiwa njiani walijipongeza wakiwa na uhakika wa mapokezi makubwa yanayowasubiri.
Je kwa nini pamoja na yote hayo, waliomimina risasi wanaonekana kuteseka kuliko aliyemiminiwa risasi? Toa maoni...
Naam, zilikuwa ni risasi za kumwangusha tembo na waliondoka hapo wakijua kazi waliyotumwa imemalizika.
Waliondoka hapo kwa haraka ya kufikisha habari njema hii kwa waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu kubwa.
Walijua ujira na pongezi kubwa zilikuwa zikiwasubiri kwa kutekeleza kwa ufanisi mkubwa jukumu walilopewa.
Hapana shaka wakiwa njiani walijipongeza wakiwa na uhakika wa mapokezi makubwa yanayowasubiri.
Je kwa nini pamoja na yote hayo, waliomimina risasi wanaonekana kuteseka kuliko aliyemiminiwa risasi? Toa maoni...