Habari wadau.
Nipo sehemu moja napata moja moto.. kuna jamaa katusua kapanda cheo kazini huko auditing firm moja kubwa , yupo early 30s anadai muda wa kuoa umefika, anadai lazima aoe mwanamke mwenye kipato kama chake ama amzidi yeye mwanaume kipato.. maana watu wanapenda sana kuvuna wasichopanda.. yeye anaona bora achunwe na mwanamke mwenye hela kuliko kuchunwa na mwanamke maskini.
Pia, nikajaribu kuwaza harusi nazoziona za walionizunguka, unakuta kama bwana harusi ni mtoto wa tajiri kama kimei anafunga ndoa na binti wa tajiri mwenzake kama matemba wa victoria oil.. nawaza dada zangu mimi maskini na ndoto zao za kuolewa na wenye pesa zitatimia kweli? ama wanaume kina sisi wa uswazi kuoa wanawake wenye pesa zitatimia kweli?
Ushauri wa wazi kama unataka maisha mazuri kwenye ndoa yako ni lazima wewe mwenyewe uwe na uwezo wa kujipa hayo maisha mazuri kabla hujaoa ama kuolewa, kwa sababu hakuna anaesaini mkataba husio na win win situation zama hizi kisa mapenzi
Nipo sehemu moja napata moja moto.. kuna jamaa katusua kapanda cheo kazini huko auditing firm moja kubwa , yupo early 30s anadai muda wa kuoa umefika, anadai lazima aoe mwanamke mwenye kipato kama chake ama amzidi yeye mwanaume kipato.. maana watu wanapenda sana kuvuna wasichopanda.. yeye anaona bora achunwe na mwanamke mwenye hela kuliko kuchunwa na mwanamke maskini.
Pia, nikajaribu kuwaza harusi nazoziona za walionizunguka, unakuta kama bwana harusi ni mtoto wa tajiri kama kimei anafunga ndoa na binti wa tajiri mwenzake kama matemba wa victoria oil.. nawaza dada zangu mimi maskini na ndoto zao za kuolewa na wenye pesa zitatimia kweli? ama wanaume kina sisi wa uswazi kuoa wanawake wenye pesa zitatimia kweli?
Ushauri wa wazi kama unataka maisha mazuri kwenye ndoa yako ni lazima wewe mwenyewe uwe na uwezo wa kujipa hayo maisha mazuri kabla hujaoa ama kuolewa, kwa sababu hakuna anaesaini mkataba husio na win win situation zama hizi kisa mapenzi